rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
Nimekuwa nikifuatilia jamii forum ambayo sio maarufu sana hapa Africa kusini,
Nitakayoyasema hapa naomba nieleweke nimeshawishika sana baada ya kufatilia sana
Hii thread inayoendelea hapa jamvini kuhusu watanzania waishio nje ya nchi,
Nimeishi nchi kumi na moja za kiafrica pekee, sijawahi kutoka nje ya Africa japo nina visa ya china ambayo niliamua kutokusafiri kwa sababu zangu binafsi zikiwemo mahesabu ya kibiashara.
Nimeishi hapa ni miaka 15 sasa,nimeishi miji yote mikubwa hapa ikiwemo Pretoria,Johannesburg,na capetown.
Kwanza kabla sijatoa yaliyo moyoni naomba niwarudishe nyuma kama wiki zilizopita kuna mtu alitoa thread hapa akisema watanzania tunafanya biashara ndogondogo kama za saloon na bar,aliongezea eti watanzania hawawezi biashara kubwa,
Naomba kumweleza huyo member ya kwamba anajidanganya,hapa south Africa kuna watanzania wengi sana wenye biashara kubwa kama za business consultant, building construction, super market kubwa,hospital,ict na nyingine nyingi,
Sio kweli kwamba watanzania hawawezi biashara kubwa,inawezekana huyo jamaa hajasafiri ,nafikiri kusafiri ni jambo la muhimu sana kwa sababu unapata kitu kinaitwa exposureambayo inakufungua macho na kuona mbali sana.
Sipendi kueleza mengi hapa kuhusu maisha lakini ndugu zangu kama unaona mtu kashindwa kurudi ujue mambo sio mazuri,
Watanzania tuna kitu kinaitwa home sick,kama mtu mambo mazuri anakimbilia home chapchap,
Kuna watu wako hapa miaka mingi na niliwakuta lakini hawajarudi home kwa sababu mambo sio mambo na wamekataa tamaa kabisa
Wengine wamebadili majina kwa sababu hali ni mbaya kwelikweli,
Mlio hapo Tanzania naomba msidanganyike kukimbilia nchi nyingine,bora ukomae hapo,
Nikiwaona jamaa zangu niliowaacha hapo miaka ya 90 wako mbali sana,wana vinyumba vyao vizuri,wanajiamini katika maisha,kikubwa zaidi wana familia,
Tunaoishi nje wengi asilimia kubwa maisha mabovu,naomba msidanganyike!
Tutaonana.
Nitakayoyasema hapa naomba nieleweke nimeshawishika sana baada ya kufatilia sana
Hii thread inayoendelea hapa jamvini kuhusu watanzania waishio nje ya nchi,
Nimeishi nchi kumi na moja za kiafrica pekee, sijawahi kutoka nje ya Africa japo nina visa ya china ambayo niliamua kutokusafiri kwa sababu zangu binafsi zikiwemo mahesabu ya kibiashara.
Nimeishi hapa ni miaka 15 sasa,nimeishi miji yote mikubwa hapa ikiwemo Pretoria,Johannesburg,na capetown.
Kwanza kabla sijatoa yaliyo moyoni naomba niwarudishe nyuma kama wiki zilizopita kuna mtu alitoa thread hapa akisema watanzania tunafanya biashara ndogondogo kama za saloon na bar,aliongezea eti watanzania hawawezi biashara kubwa,
Naomba kumweleza huyo member ya kwamba anajidanganya,hapa south Africa kuna watanzania wengi sana wenye biashara kubwa kama za business consultant, building construction, super market kubwa,hospital,ict na nyingine nyingi,
Sio kweli kwamba watanzania hawawezi biashara kubwa,inawezekana huyo jamaa hajasafiri ,nafikiri kusafiri ni jambo la muhimu sana kwa sababu unapata kitu kinaitwa exposureambayo inakufungua macho na kuona mbali sana.
Sipendi kueleza mengi hapa kuhusu maisha lakini ndugu zangu kama unaona mtu kashindwa kurudi ujue mambo sio mazuri,
Watanzania tuna kitu kinaitwa home sick,kama mtu mambo mazuri anakimbilia home chapchap,
Kuna watu wako hapa miaka mingi na niliwakuta lakini hawajarudi home kwa sababu mambo sio mambo na wamekataa tamaa kabisa
Wengine wamebadili majina kwa sababu hali ni mbaya kwelikweli,
Mlio hapo Tanzania naomba msidanganyike kukimbilia nchi nyingine,bora ukomae hapo,
Nikiwaona jamaa zangu niliowaacha hapo miaka ya 90 wako mbali sana,wana vinyumba vyao vizuri,wanajiamini katika maisha,kikubwa zaidi wana familia,
Tunaoishi nje wengi asilimia kubwa maisha mabovu,naomba msidanganyike!
Tutaonana.