Ukweli kuhusu alama ya mnyama

Nyie Wa Siku ya Saba,
Bi Hellena amesha waharibu ubongo wenu wote.
Hakuna mnacho waza zaidi ya Sabato, Jumapili. Roman Cathoric, Jumamosi, Papa na Vatikani, na aya za Biblia zinazotaja maeneo hayo.
Mtu akiku Challenge kwenye mada yako basi atakuwa Mkatoriki tu.
Sasa mimi nitaongea nini na wewe ?
Toka utotoni na kanisani kwenu mmekaririshwa aya zinazozunguka maeneo hayo hayo ya Papa na Sabato.
Akili yako imeishia humohumo mwa Jumamosi na Jumapili, mada zako zote ni za Jumamosi Jumapili na Papa.
Wewe wala hujawahi kuwa Mwislamu.
Ni afadhali kuwa Mwislamu kuliko kuwa Msabato ambaye kila ukiamka anawaza chuki dhidi ya Wakatoriki na kuiabudu siku ya Jumamosi.

Stay Away From Ellen G. White.
 
Wewe wala hujawahi kuwa Mwislamu.
Na ni afadhali uwe Mwislamu kuliko kuwa Msabato, ambaye huna jipya zaidi ya kuonyesha chuki kwa Kanisa Katoriki na kuishia kuiabudu siku ya Jumamosi.
Msabato ambaye unaacha maagizo ya Yesu Kristo na kumfuata mwanamwali Ellen G White.
Ona hayo mapichapicha uliyopesti hapo ulipo ninukuu. Ndizo Biblia alizo waachia Hellena. Mnazozisoma usiku na mchana.
Mtu akikupinga kwenye hoja yako basi huyo atakuwa Mkatoriki tu.
Hakuna mnacho waza zaidi ya Papa na Sabato, na Wanyama wa kwenye Danieli.
Mimi siwezi kuzungumza na wewe ambaye Elleni amekifunga kichwa chako na kinamuwaza yeye tu.
Mpaka unafikia kujiita Msabato, bora ungejiita Upendo.
Mi nakuambia kijana achana na kuwazia Jumamosi na Papa kila kukukicha.
Elleni amewaingizia chuki ili msiweze kuabudu ktk Roho na Kweli na Moyo uliojaa Upendo, amani na utauwa.
Elleni anawatisha kila siku eti Papa atakuja kuwagonga mihuli ya 666, na kama mkikataa atawatesa vikali.
Ha...ha...ha...kweli yule dada kawakamata pabaya sana.
Kawafunga kamba zake nanyinyi mmefungika.
Nakuonya ndugu, ukitaka kuurithi Ufalme wa Mbingu.
Look for Jesus Christ and Please,
Stay Away From Ellen G. White.
 
Mbona umebaki unalialia ohoo ellen , ellen ,

Mbona nimekwambia njoo hapa jamvin tuhojiane hoja kwa hoja ,unakimbia

Unadhan kulia lia hellen hellen.iiiiii ,ndio itakusaidia

Kila nikikukamata unakimbilia ohooo nimechikua kwa hellen kwa helleennn..,

Ngoja nikwambie mimi.na silaha mbili kwa mtu kama wewe.nakutandika kwa biblia na vitabu unavyoviamini,

SIJATUMIA ANDIKO WALA QUOTATION hata moja ya EGW, hata 1

Sasa nashangaa unalia kilio kikuu, je ninhetumia Hata kidogo tu, si ungeomba NIPIGWE BAN?

NIMEKWAMBIA LAWAMA ZAKO HAZISAIDII, NJOO HAPA TUHOJIANE HOJA KWA HOJA ,MSTARI KWA MSTARI , ILI TUONE NANI YUPO WRONG
 
NAKUONA UPO ONLINE MKUU, NJOO TUHOJIHANE HOJA KWA HOJA, MSTARI KWA MSTARI

TUANZE HAPA

UFUNUO 13

1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.
2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.
3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule.
4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye?
5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili.

TWENDE KWENYE HIZO AYA 5 TU,

NAOMBA NIJIBU MASWALI HAYA KWA AYA YA 1
Nomba nisaidie Mnyama ni nini, Mnyama huyo ni nani, PEMBE ni nini, pembe kumi ni nani, zitaje ,vilemba ni nini, vilemba hivo ni nani,

Makufuru hayo ni yapi ,makufuru ni nini

Majibu yasapotiwe na biblia na historia

AYA Ya 2 ina maana gani inamaanisha nini inaposema hivo....UKITUMIA BIBLIA NA HISTORIA naomba majibu

AYA YA 3. ,Jeraha la mauti ni nini na lilitokeaje kwenye huo uislamu na ilikuwa lini, na lilipona lini

Aya YA 4 .,JOKA NI NANI, JE JOKA ALIMPA NGUVU UISLAMU KIVIPI

AYA YA 5.,MANENO GANI MAKUFURU ALIYANENA ,JE MAKUFURU NI NINI

HIYO MIEZI 42 NI NINI, JE ILIANZA LINI NA KUISHA LINI

TUANZIE HAPO KWANZA KWA AYA HIZO , TU KABLA SIJAKUSHUSHIA MZIGO
 

Nitakujibu. Lakini meanwhile, naomba usome Daniel (chapters 3, 9 and 12) halafu tafuta Quran (usome sehemu inayoongelea Khiyama). Ukimaliza niambie tuendelee.
 
Mwanaume hapaswi kulalamika mkuu si utulie ujifunze kwani kuna ubaya gani? mimi nataka nione huyo mnyama ni yupi?
 
Nitakujibu. Lakini meanwhile, naomba usome Daniel (chapters 3, 9 and 12) halafu tafuta Quran (usome sehemu inayoongelea Khiyama). Ukimaliza niambie tuendelee.
Mkuu unatakiwa ujibu maswali hili nasi tupate faida hili tujue mnyama ni mmoja au wapo wawili ?
 
Ha ha ha ha ha Nilianza kusoma kichwa cha habari nilijua tu huyu ni msabato
Nilipomalizia mwiso nikaona kweli huyu ni msabato
Tatizo lenu wasabato mnashindwa kujua hili
What Is Worship?
What Is Day?
Ila mnataka Mfanye kuwa Day is worship
kwanini mnakuwa mnajipa tafasiri za tofauti tofauti na jinsi ambavyo uhalisia upooo?

Sikia kijana Mbinguni hatuendi kwa kusali j3,j4,j5,alhamis ,ijumaa,Jumamosi na jumapili
Wenye Moyo safi ndio wataenda mbinguni
 
Mkuu unatakiwa ujibu maswali hili nasi tupate faida hili tujue mnyama ni mmoja au wapo wawili ?

Bila mtu kusoma hivyo vitabu nilivyovitaja tutaishia kubishana badala ya kujadiliana. In actual fact tunahitaji kusoma historia ya Middle East ili kupata picha halisi.

Na tunapaswa kukumbuka kuwa maarifa yaliyokuwepo mwanzoni mwa karne ya 19 sio sawa na yaliyopo leo. Miaka 100 iliyopita Biblia ilikuwa 30% (or less) historia na 70% utabiri. Leo hii utabiri ndani ya Biblia ni less than 25% na kilichobaki ni historia.
 
Sawa ila unatakiwa ujibu halafu , kuelewa inabaki kwa muuliza swali, embu mjibu yule bwana wa ufunuo kisha tupime majibu yako
 
Nitakujibu. Lakini meanwhile, naomba usome Daniel (chapters 3, 9 and 12) halafu tafuta Quran (usome sehemu inayoongelea Khiyama). Ukimaliza niambie tuendelee.
Mkuu njoo nijibu, daniel hizo sura hazihusian na quran ,

Njoo nijibu maswali yangu, UISLAM unahusihana vip na hizo aya au maswali
 
Mkuu njoo nijibu, daniel hizo sura hazihusian na quran ,

Njoo nijibu maswali yangu, UISLAM unahusihana vip na hizo aya au maswali

Kwa maswali yako haya ina maana hujapata connection kati ya Ufunuo wa Yohana, Daniel na Ezekiel. Haraka ya nini? Wewe soma nilichokuambia ili tuanze mjadala rasmi at least ukiwa umeachana na prejudice unayoonekana kuwa nayo
 
Kwa maswali yako haya ina maana hujapata connection kati ya Ufunuo wa Yohana, Daniel na Ezekiel. Haraka ya nini? Wewe soma nilichokuambia ili tuanze mjadala rasmi at least ukiwa umeachana na prejudice unayoonekana kuwa nayo
Ukiwa tayari kumjibu naomba unitag. naona sarakasi zimekuwa nyingi ndugu
 
Ukiwa tayari kumjibu naomba unitag. naona sarakasi zimekuwa nyingi ndugu

Nitakutaarifu. Hakuna sarakasi hapa ila nampa nafasi mdau ajipe nafasi ya kujisomea japo kwa ufupi niliyoyasoma ili tuanze na equal footing. Nisije nikawa najadiliana mambo ya football na mtu wa handball (maana atatafsiri football kwa mtazamo wa handball)
 
Kwa maswali yako haya ina maana hujapata connection kati ya Ufunuo wa Yohana, Daniel na Ezekiel. Haraka ya nini? Wewe soma nilichokuambia ili tuanze mjadala rasmi at least ukiwa umeachana na prejudice unayoonekana kuwa nayo
Nijibu maswali yangu, sitak. Tabia ya kuokoteza vimistar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…