Ukweli kuhusu alama ya mnyama

Ukweli kuhusu alama ya mnyama

Nitakutaarifu. Hakuna sarakasi hapa ila nampa nafasi mdau ajipe nafasi ya kujisomea japo kwa ufupi niliyoyasoma ili tuanze na equal footing. Nisije nikawa najadiliana mambo ya football na mtu wa handball (maana atatafsiri football kwa mtazamo wa handball)
Kwanini usianze kwa kujibu maswali kuhusu hiyo sura inayomuhusu MNYAMA ,kuliko kutaka kuokoteza vimistari? Ndio maana najua huwez kujibu hayo maswali kamwe,maana umeanza sarakasi,
Au maswali hujayaona?

Niambie UISLAMU UNAHUSIKAJE hapo?
 
Nitakutaarifu. Hakuna sarakasi hapa ila nampa nafasi mdau ajipe nafasi ya kujisomea japo kwa ufupi niliyoyasoma ili tuanze na equal footing. Nisije nikawa najadiliana mambo ya football na mtu wa handball (maana atatafsiri football kwa mtazamo wa handball)
Mkuu aya 5 tu unaleta sarakas , hii inaonesha ni kwavip mbaokoteza aya na kudanganya , je ningekushushia zote ?

Huu unabii 100% unalihusu kanisa la roma, ndio maana waliamua kuwaua watakatifu, ili kuficha ukweli huu, walizui pia biblia zisichapishwe na kutafsiriwa , na WILLIAM TYNDALE ALIPOAMUA kutafsir biblia , walimchoma moto

NAKUNGOJA NJOO TUHOJIHANE, ukileta mstar umeokota huku na kule , ukahitimisha et ni UISLAMU, utachekesha , maana mwingine ataibuka atasema ni urusi ,
 
Je alama ya mnyama ni nini? Kuna maelezo mengi yaliyotolewa na baadhi ya watu juu ya alama ya mnyama, wengine hudhani kuwa alama ya mnyama ni “chip” ya computa, au kadi, au kitu halisi kinachoweza kubebeka! Lakini Je Biblia inaelezea vipi kuhusu alama ya mnyama? Ngoja tuangalie Mungu anachokisema juu ya alama ya mnyama.

(NB: maneno “alama”, “muhuri”, “ishara” au “dalili” ni visawe).

Ufunuo 13:16-17 “Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa masikini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.”

Kwanini alama hii ni ya muhimu kuelewa? Kama ukitaka kuthibitisha kwamba kitu flani ni chako, au ukitaka kuonyesha kuwa wewe ni mmiliki wa kitu flani, au ukitaka kutia alama kitu flani kuwa chako, siku zote kutakuwa na vitu vitatu tofauti.

*. Jina lako.
*. Cheo chako.
*. Mahali unapomiliki.

Hivyo, kama raisi wa Tanzania akitaka kuthibitisha kwamba kitu flani kimetoka kwake lazima athibitishe kama hivi:

*. Jina = Jakaya M. Kikwete
*. Cheo = raisi
*. Anapomiliki = Tanzania

Kuna serikali mbinguni (Isa. 9:6), na alama au muhuri wa Mungu ni sheria yake. Angalia katikati ya amri kumi na utaona muhuri wa Mungu, “Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba;…” Kut. 20:11

JINA LAKE = BWANA (“Mimi ni BWANA; ndilo jina langu…” Isa. 42:8).CHEO CHAKE = MUUMBA (…BWANA…yeye aliyeziumba mbingu, na…nchi…” Isa. 42:5).ANAPOMILIKI = MBINGU NA NCHI (“Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya BWANA…” Zab. 24:1).

Hivyo, BWANA alipoziumba mbingu na nchi kwa siku sita, siku ya saba alipumzika ili kuweka alama au muhuri kwamba yeye ndiye aliyeziumba mbingu na nchi, kwa hiyo Sabato ni muhuri unaothibitisha kwamba BWANA:

Aliziumba mbingu na nchi.Alituumba sisi pamoja na vitu vingine vyote.Anamiliki mbingu na nchi, pamoja na vitu vyote vilivyomo.

Kwanini shetani anafanya bidii sana kuwaongoza watu wasiitambue Sabato? Ni kwa sababu shetani anataka kujifanya yeye kuwa kama muumba wa mbingu na nchi, hivyo anainaingiza alama yake ambayo ni kinyume na alama ya kweli ya Mungu. Sabato ni alama au muhuri wa Mungu, kwa hakika Mungu mwenye anathibitisha ukweli huu kwa kusema, “…Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote;…” Kut. 31:13. (Kumbuka! maneno ishara, muhuri, alama ni visawe, na yanaweza kutumika kwa kuyachanganya-changanya).

Njia rahisi na nyepesi ya kugundua alama ya mnyama, ni kutafuta kujua kwanza alama ya Mungu., harafu utaona kwamba alama ya mnyama ni kinyume na alama ya Mungu.

Ufunuo 7:2-3 “Nikaona malaika mwingine, akipanda kutoka mawio ya jua, mwenye mhuri wa Mungu aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale malaika wanne waliopewa kuidhuru nchi na bahari, akisema, Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao.”

Kama tulivyoona huko nyuma kwamba muhuri na alama ni visawe! Hivyo watumwa wa Mungu wanawekwa alama katika vipaji vyao vya nyuso, kipaji cha uso hapa humaanisha akili, mawazo, au nia.

Wabrania 10:16 “Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika…”

Pia Wanafisikolojia hutuambia kuwa ubongo wa mbele wa cerebrum [paji la uso] ndipo shughuri kama uamuzi, hukumu, na uhuru wa kutaka vinapofanyikia. Hivyo, Wakristo wanawekwa alama katika vipaji vya nyuso zao, pale tu wanapomkubali Yesu kuwa Mwokozi wao na kutunza amri kumi zote kwa kuhiari, au kutaka wao wenyewe bila kulazimishwa. Hii ndiyo maana muhuri au alama ya Mungu haiwekwi mkononi, kwa sababu Yesu hatawalazimisha watu kumwabudu na kuzitii amri zake. Mkono humaanisha kulazimishwa kufanya kitu furani kinyume na nia zetu.

Jeremia 38:23 “Na watawatoa wake zako, na watoto wako wote, na kuwachukua kwa Wakaldayo; wala wewe hutapona na mikono yao, bali utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babeli, nawe utakuwa sababu ya kuteketezwa kwa mji huu.”

Yesu kamwe hatatulazimisha sisi kumwabudu, kwani anapendezwa kama tutamwabudu na kutunza sheria zake zote, kwa hiari yetu bila kulazimishwa.

Ufunuo 13:15-17 “Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe. Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.”

Alama ya mnyama inawekwa katika kipaji cha uso na kwenye mkono. Hivyo wale wote wanaokubali kwa hiari yao wenyewe kumfuata mnyama na kutii amri zake, hawa wamewekwa alama kwenye paji la uso; maana wamehiari wao wenyewe bila kulazimishwa. Na wale wanaopokea alama kwenye mkono, ni wale watakaotii amri za mnyama kwa kulazimishwa bila ridhaa yao. Kwa hofu ya kifo na kushindwa kununua wala kuuza, wanaamua kumtii mnyama ili wasipoteze vitu walivyovifanyia juhudi nyingi katika maisha yao na hili ni bonge la kosa.

Kwa sababu tumeelewa kwamba kuamua kumkubali Yesu kama Mwokozi wetu na kutunza mafundisho na amri zake zote, ni sawa na kupokea alama au muhuri wa Mungu. Tunatakiwa pia tuelewe kuwa kukubali amri, mafundisho, au mapokeo ya kanisa la Romani Katoliki au kanisa lingine lolote linalofuata imani ile ile na kufundisha mapokeo yake, inamaanisha tumepokea alama ya mnyama. Pia elewa kuwa kutakuwa na wengine ambao sio Wakatoliki lakini wanafanya kila kitu ambacho mnyama anaamru kwa kuogopa kufa, au kupoteza mahitaji ya kawaida kwa kuzuiliwa kuuza wala kununua, kitu ambacho kitapelekea kukubali kufuata matakwa ya mnyama. Hawa watapokea alama ya mnyama kwenye mkono kwa sababu wamelazimishwa kinyume na matakwa yao. Wakatoliki na Wakristo wengine ambao hukubali haya “mafundisho ya wanadamu” watakuwa wamepokea alama ya mnyama kwenye vipaji vya nyuso zao kwa sababu wamekubali kwa hiari kuwa kanisa lao liko sawa kwa kubadili maandiko na kuingiza “mapokeo” au “mafundisho ya wanadamu.” Na hii ilionywa katika unabii.

Wakolosai 2:8 “Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.”

Hivyo, kama ukipokea “alama” kwa kuchagua mwenyewe, hii inamaanisha umewekwa alama kwenye kipaji cha uso. Na kama ukipokea “alama” kwa kulazimisha, hii inamaanisha umewekwa alama kenye mkono wa kulia. Lakini kumbuka.

Mathayo 16:25 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.”

Mathayo 10:39 “Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.”

Yohana 12:25 “Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.”

Tukirudi kwenye alama ya mnyama kanisa la Romani Katoliki bila ya kutambua linatimiza unabii huu kwa maelezo yafuatayo.

“Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –-H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons

“Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

Kama unabii uko sawa unaposema jumapili ni alama ya mnyama, na Mungu anasema wazi wazi.

Kutoka 31:13 “…Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.”

Ezekieli 20:12, 20 “Tena naliwapa sabato zangu, ziwe ishara kati ya mimi na wao, wapate kujua yakuwa mimi, BWANA, ndimi niwatakasaye…zitakaseni sabato zangu; zitakuwa ishara kati ya mimi na ninyi, mpate kujua yakuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.”

Maneno ishara, muhuri, na alama ni visawe, na yanaweza kutumika popote kwa kuyabadilisha-badilisha.

Hivyo, tuna uhakika wa ukweli wa Biblia kwamba Sabato ni ishara, muhuri, au alama ya Mungu. Na jumapili ni ishara, muhuri, au alama ya mnyama.

View attachment 920036
Mkuu habari!
Nimekusoma kwa uzuri na nimekupata vilivyo. Ila naomba unisaidie kupata muunganiko wa amri ya sabato na mhuri wa Mungu.

Nijuavyo amri zipo 10 lakini umechomoa ya katikati na kuifanya iwe mhuri wa Mungu. Ni vigezo gani umetumia hapa mpendwa? Na kwa nini mhuri usiwe amri zote? Pia kama ulivyonukuu Ebr 10 kwamba Mungu atatia amri zake na kuziandika na wala si amri moja. Hapa huoni kama unatuchanganya kama siyo kutudanganya?

Pili kuhusu visawe naomba ujipange upya. Maana ya neno hutegemeana na muktadha. Na ndo maana hata kwenye kamusi utakuta maana zaidi ya moja ambapo wewe utachagua ile inayoendana na mktadha (mazingira) yako ya mazungumzo. Mtu wa Mungu AROON, ni vizuri ukawa makini na kila unachokisema ili usijeonekana unadanganya kama ulivyofanya kwenye hili hapa.

Tatu umetumia aya hii kuthibitisha usemacho!

“Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

Ombi, naomba unisaidie mimi na wengine kwa kubandika huo ukurasa husika ili tuendelee kujifunza mpendwa.

Ezekiel 20:12,20 umenukuu kuwa Mungu aliwapa sabato zake kuwa ishara. Swali la msaada, kuna sabato ngapi? Kama ni zaidi ya moja je ipi ndiyo mhuri wa Mungu?

Maana ya kutakasa ni nini?
Je watu wana uwezo wa kutakasa kitu au ni Mungu peke yake?
Si Sabato ni takatifu! Kwa nini watu wanaambiwa kuzitakasa?

Asante kwa andiko zuri, nitakuja tena.
 
Mkuu aya 5 tu unaleta sarakas , hii inaonesha ni kwavip mbaokoteza aya na kudanganya , je ningekushushia zote ?

Huu unabii 100% unalihusu kanisa la roma, ndio maana waliamua kuwaua watakatifu, ili kuficha ukweli huu, walizui pia biblia zisichapishwe na kutafsiriwa , na WILLIAM TYNDALE ALIPOAMUA kutafsir biblia , walimchoma moto

NAKUNGOJA NJOO TUHOJIHANE, ukileta mstar umeokota huku na kule , ukahitimisha et ni UISLAMU, utachekesha , maana mwingine ataibuka atasema ni urusi ,

Okay. Amini ulichoamua kukiamini. Nilidhani ninawasiliana na mtu ambae yupo tayari kujifunza kitu kipya however strange it seems to them.
 
Kwakweli mleta mada pole sana naona bado hujakutana na Bwana Yesu.
Nakushauri mimi niliye mdogo ukubali Bwana Yesu akuokoe nawe upate kuhesabiwa haki kwa sheria ya imani uachane na sheria ya dhambi iletayo mauti ndani yako.
 
Okay. Amini ulichoamua kukiamini. Nilidhani ninawasiliana na mtu ambae yupo tayari kujifunza kitu kipya however strange it seems to them.
Nilijua lazima ukimbie tu, NAUHAKIKA USINGEWEZA KUTHUBUTU HATA MSTARI MMOJA TU KUUELEZEA

ningeshangaa sana kama ungejibu walau mstari mmoja ,

Ona unakimbia ,
 
Kwakweli mleta mada pole sana naona bado hujakutana na Bwana Yesu.
Nakushauri mimi niliye mdogo ukubali Bwana Yesu akuokoe nawe upate kuhesabiwa haki kwa sheria ya imani uachane na sheria ya dhambi iletayo mauti ndani yako.
Hayo maneno hata manabii waliojaa hapa tz wanasema hivo

Njoo hapa nipinge mada yangu kwa hoja , wapi nimekosea , na kipi ni sahihi,

Sio kukariri maneno na kutoa lawama ,haisadii
 
Mkuu habari!
Nimekusoma kwa uzuri na nimekupata vilivyo. Ila naomba unisaidie kupata muunganiko wa amri ya sabato na mhuri wa Mungu.

Nijuavyo amri zipo 10 lakini umechomoa ya katikati na kuifanya iwe mhuri wa Mungu. Ni vigezo gani umetumia hapa mpendwa? Na kwa nini mhuri usiwe amri zote? Pia kama ulivyonukuu Ebr 10 kwamba Mungu atatia amri zake na kuziandika na wala si amri moja. Hapa huoni kama unatuchanganya kama siyo kutudanganya?

Pili kuhusu visawe naomba ujipange upya. Maana ya neno hutegemeana na muktadha. Na ndo maana hata kwenye kamusi utakuta maana zaidi ya moja ambapo wewe utachagua ile inayoendana na mktadha (mazingira) yako ya mazungumzo. Mtu wa Mungu AROON, ni vizuri ukawa makini na kila unachokisema ili usijeonekana unadanganya kama ulivyofanya kwenye hili hapa.

Tatu umetumia aya hii kuthibitisha usemacho!

“Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

Ombi, naomba unisaidie mimi na wengine kwa kubandika huo ukurasa husika ili tuendelee kujifunza mpendwa.

Ezekiel 20:12,20 umenukuu kuwa Mungu aliwapa sabato zake kuwa ishara. Swali la msaada, kuna sabato ngapi? Kama ni zaidi ya moja je ipi ndiyo mhuri wa Mungu?

Maana ya kutakasa ni nini?
Je watu wana uwezo wa kutakasa kitu au ni Mungu peke yake?
Si Sabato ni takatifu! Kwa nini watu wanaambiwa kuzitakasa?

Asante kwa andiko zuri, nitakuja tena.
Mbona nimeeleza muhuri unatakiwa uweje ,soma vizuri maana nimeshalieleza kwenye uzi

Umesema Mungu atatia sheria yake moyoni,

Kwanza inaonesha hujasoma uzi ukauelewa, umeusoma haraka haraka,

Sijautumia huo mstari kuonesha ni sabato tu, nimeutumia huo mstari kuonesha MUHURI UNAPOWEKWA KWENYE AKILI/MOYON MUNGU ALIMAANISHA NINI, soma tena ,

Umezungumzia SABATO KUWA ZIPO NGAPI, sabato mpaka sasa IMEBAKI MOJA TU, AMBAYO IPO KWENYE AMRI KUMI,

Kipindi cha wana israeli sabato zilikuwepo nyingi , hizo sabato ziliishia msalabani, ndio zile ambazo zimesemwa wakolosai 2:16

Sabbaths days

Umesema nimenukuu kutoka chanzo cha kikatoliki, ndio nimenukuu kuthibitisha ALAMA.YA MNYAMA NI IBADA YA JUMAPILI,

Ukitaka ushahidi , ingia google angalia record ya hiyo makala utaikuta hiyo QUOTATION, tena utazipata nyingi,

SABATO NI TAKATIFU NA MUNGU AMESHAITAKASA ,

ILA UNAPOIVUNJA AU KUFANYA UJUAYO WEWE, UNAKUWA UMEINAJISI ,

NDIO MAANA MUNGU ANATUASA TUITAKASE

kupitia nabii isaya alisema tena

Isaya 58:13

If you keep your feet from breaking the Sabbath and from doing as you please on my holy day, if you call the Sabbath a delight and the LORD's holy day honorable, and if you honor it by not going your own way and not doing as you please or speaking idle words,

HAYA WEWE MUNGU ALIKUUMBA MTAKATIFU, ILA UNAPOFANYA DHAMBI UNAKUWA NAJISI

SIMPLE LIKE THAT..
 
Okay. Amini ulichoamua kukiamini. Nilidhani ninawasiliana na mtu ambae yupo tayari kujifunza kitu kipya however strange it seems to them.
Najua umefukua ukafukua ,ukakuta hauna ushahidi,

Umeona uage , kienyeji ,

Kiukweli Natangaza ANAYEBISHA KUWA MNYAMA SIO UKATOLIKI NA ALAMA YA MNAYAMA SIO IBADA YA JUMAPILI

AJITOKEZE HAPA ASEME MNYAMA NI NANI NA ALAMA YA MNYAMA NI NANI,

TUHOJIHANE HOJA KWA HOJA , MISTARI KWA MISTARI, HISTORIA KWA HISTORIA

NIMETANGAZA UWANJA NI WAZI
FB_IMG_1540529670203.jpeg
 
Najua umefukua ukafukua ,ukakuta hauna ushahidi,

Umeona uage , kienyeji ,

Kiukweli Natangaza ANAYEBISHA KUWA MNYAMA SIO UKATOLIKI NA ALAMA YA MNAYAMA SIO IBADA YA JUMAPILI

AJITOKEZE HAPA ASEME MNYAMA NI NANI NA ALAMA YA MNYAMA NI NANI,

TUHOJIHANE HOJA KWA HOJA , MISTARI KWA MISTARI, HISTORIA KWA HISTORIA

NIMETANGAZA UWANJA NI WAZI
View attachment 924185

Tatizo lako ni kuwa upo prejudiced. Ulicholishwa na kunyweshwa kimekukolea hasa hadi ukiona rangi nyekundu ulipoambiwa utaona rangi nyeupe bado unaamini kuwa umeona rangi nyeupe kwa kuwa kina Ellen White walikuambia hivyo.

Look here; kumbuka Nabii Daniel na Mtume Yohana walionyeshwa mambo yanayotokea leo wakati wanaishi kipindi ambacho tunayoyaona leo kwao wasingeweza hata kufikiria uwepo wa hayo mambo. Kwamba ni kipi walionyeshwa ndipo akili yetu mimi na wewe tunaeishi leo hii tunapaswa kujua maana maarifa yanazidi kuongezeka (kama alivyoambiwa Daniel) na uwezo wetu wa kutafsiri unazidi kuongezeka (kwa kuwa siri zilizofichika zinafunuliwa taratibu but at an increasing rate). Nakupa mfano hapa wa kile ninachokuambia hapa.

Ukisoma Daniel 9:26 kuna utabiri juu ya kuharibiwa mji wa Jerusalem na hekalu la Mungu na "jeshi la (watu wa) mfalme (mtawala) ajae". Jerusalem ilitekwa mwaka 70 AD na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi. Msingi wa dhana inayoshikiliwa na Wasabato (na baada ya watu) hadi leo hii kuwa mpinga Kristo atatokea kanisa la Romani Katoliki linatokana na tukio hilo. Lakini Daniel aliandika specifically kuwa watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE (sio mtawala aliekuwepo wakati huo au watu wa mtawala aliekuwapo wakati huo - meaning watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE). Ni kweli mji wa Jerusalem ulitekwa na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi LAKINI JENERALI TITUS alikuwa anaongoza jeshi ambalo wanajeshi wake wengi WALIKUWA NI WAARABU NA WATURUKI na sio Warumi wazawa. Soma hapa

Who Are "The People of the Prince to Come"?

Mtawala ajae ambae hao wanajeshi Waarabu na Waturuki ni watu wake ni Kanisa Katoliki?

Cc
Masoud Mshahara
 
Hebu soma hapa ona Ufunuo inavyosema

" 9 Na mwingine, malaika wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake,
10 yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo.
11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake."



KWANZA UNAELEWA HUYO MNYAMA ANAYEZUNGUMZWA HAPO NI NANI?

JE SANAMU YA MNYAMA NI NANI?[/QUOTE]
wewe dogo nipo hapa Tunduma na hao wachungaji wako wa makambi wanaokudanganya tatizo unaaamini Unavyovipostihatuyakuviona
 
Mbona nimeeleza muhuri unatakiwa uweje ,soma vizuri maana nimeshalieleza kwenye uzi

Umesema Mungu atatia sheria yake moyoni,

Kwanza inaonesha hujasoma uzi ukauelewa, umeusoma haraka haraka,

Sijautumia huo mstari kuonesha ni sabato tu, nimeutumia huo mstari kuonesha MUHURI UNAPOWEKWA KWENYE AKILI/MOYON MUNGU ALIMAANISHA NINI, soma tena ,

Umezungumzia SABATO KUWA ZIPO NGAPI, sabato mpaka sasa IMEBAKI MOJA TU, AMBAYO IPO KWENYE AMRI KUMI,

Kipindi cha wana israeli sabato zilikuwepo nyingi , hizo sabato ziliishia msalabani, ndio zile ambazo zimesemwa wakolosai 2:16

Sabbaths days

Umesema nimenukuu kutoka chanzo cha kikatoliki, ndio nimenukuu kuthibitisha ALAMA.YA MNYAMA NI IBADA YA JUMAPILI,

Ukitaka ushahidi , ingia google angalia record ya hiyo makala utaikuta hiyo QUOTATION, tena utazipata nyingi,

SABATO NI TAKATIFU NA MUNGU AMESHAITAKASA ,

ILA UNAPOIVUNJA AU KUFANYA UJUAYO WEWE, UNAKUWA UMEINAJISI ,

NDIO MAANA MUNGU ANATUASA TUITAKASE

kupitia nabii isaya alisema tena

Isaya 58:13

If you keep your feet from breaking the Sabbath and from doing as you please on my holy day, if you call the Sabbath a delight and the LORD's holy day honorable, and if you honor it by not going your own way and not doing as you please or speaking idle words,

HAYA WEWE MUNGU ALIKUUMBA MTAKATIFU, ILA UNAPOFANYA DHAMBI UNAKUWA NAJISI

SIMPLE LIKE THAT..
Dogo hayo makambi ujinga
 
Tatizo lako ni kuwa upo prejudiced. Ulicholishwa na kunyweshwa kimekukolea hasa hadi ukiona rangi nyekundu ulipoambiwa utaona rangi nyeupe bado unaamini kuwa umeona rangi nyeupe kwa kuwa kina Ellen White walikuambia hivyo.

Look here; kumbuka Nabii Daniel na Mtume Yohana walionyeshwa mambo yanayotokea leo wakati wanaishi kipindi ambacho tunayoyaona leo kwao wasingeweza hata kufikiria uwepo wa hayo mambo. Kwamba ni kipi walionyeshwa ndipo akili yetu mimi na wewe tunaeishi leo hii tunapaswa kujua maana maarifa yanazidi kuongezeka (kama alivyoambiwa Daniel) na uwezo wetu wa kutafsiri unazidi kuongezeka (kwa kuwa siri zilizofichika zinafunuliwa taratibu but at an increasing rate). Nakupa mfano hapa wa kile ninachokuambia hapa.

Ukisoma Daniel 9:26 kuna utabiri juu ya kuharibiwa mji wa Jerusalem na hekalu la Mungu na "jeshi la (watu wa) mfalme (mtawala) ajae". Jerusalem ilitekwa mwaka 70 AD na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi. Msingi wa dhana inayoshikiliwa na Wasabato (na baada ya watu) hadi leo hii kuwa mpinga Kristo atatokea kanisa la Romani Katoliki linatokana na tukio hilo. Lakini Daniel aliandika specifically kuwa watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE (sio mtawala aliekuwepo wakati huo au watu wa mtawala aliekuwapo wakati huo - meaning watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE). Ni kweli mji wa Jerusalem ulitekwa na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi LAKINI JENERALI TITUS alikuwa anaongoza jeshi ambalo wanajeshi wake wengi WALIKUWA NI WAARABU NA WATURUKI na sio Warumi wazawa. Soma hapa

Who Are "The People of the Prince to Come"?

Mtawala ajae ambae hao wanajeshi Waarabu na Waturuki ni watu wake ni Kanisa Katoliki?

Cc
Masoud Mshahara
MBONA NIMEKUULIZA MASWALI HUTAKI KUJIBU UMEBAKI UNALALAMIKA.TU,

ZAIDI UMEJITUNGIA SWALI LAKO MWENYEWE

HAYO MASWALI YANGU YAMEKUSHINDA NINI, AU HUYAONI?
 
Tatizo lako ni kuwa upo prejudiced. Ulicholishwa na kunyweshwa kimekukolea hasa hadi ukiona rangi nyekundu ulipoambiwa utaona rangi nyeupe bado unaamini kuwa umeona rangi nyeupe kwa kuwa kina Ellen White walikuambia hivyo.

Look here; kumbuka Nabii Daniel na Mtume Yohana walionyeshwa mambo yanayotokea leo wakati wanaishi kipindi ambacho tunayoyaona leo kwao wasingeweza hata kufikiria uwepo wa hayo mambo. Kwamba ni kipi walionyeshwa ndipo akili yetu mimi na wewe tunaeishi leo hii tunapaswa kujua maana maarifa yanazidi kuongezeka (kama alivyoambiwa Daniel) na uwezo wetu wa kutafsiri unazidi kuongezeka (kwa kuwa siri zilizofichika zinafunuliwa taratibu but at an increasing rate). Nakupa mfano hapa wa kile ninachokuambia hapa.

Ukisoma Daniel 9:26 kuna utabiri juu ya kuharibiwa mji wa Jerusalem na hekalu la Mungu na "jeshi la (watu wa) mfalme (mtawala) ajae". Jerusalem ilitekwa mwaka 70 AD na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi. Msingi wa dhana inayoshikiliwa na Wasabato (na baada ya watu) hadi leo hii kuwa mpinga Kristo atatokea kanisa la Romani Katoliki linatokana na tukio hilo. Lakini Daniel aliandika specifically kuwa watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE (sio mtawala aliekuwepo wakati huo au watu wa mtawala aliekuwapo wakati huo - meaning watakaouteka mji wa Jerusalem na kuharibu hekalu ni WATU WA MTAWALA AJAE). Ni kweli mji wa Jerusalem ulitekwa na Jenerali Titus wa jeshi la utawala wa Kirumi LAKINI JENERALI TITUS alikuwa anaongoza jeshi ambalo wanajeshi wake wengi WALIKUWA NI WAARABU NA WATURUKI na sio Warumi wazawa. Soma hapa

Who Are "The People of the Prince to Come"?

Mtawala ajae ambae hao wanajeshi Waarabu na Waturuki ni watu wake ni Kanisa Katoliki?

Cc
Masoud Mshahara
Mkuu mbona haumjibu maswali yake ,zaidi.unayakwepa ? Tatizo nini, nimeona umeaga kukimbia ,sasa hivi umerudi na ngonjera nyingine, watu tumekaa tunasubiri kujifunza, utusaidie hizo Aya zinahusiana vipi na uislamu, cha kushangaza ni.kama huzioni, hizo aya unazokimbilia , hata hazihusiani na uislamu, ndio maana kwakuwa umedai, mnyama ni uislamu, umepewa sura ya yohana 13 , kuhusu mnyama ,ujibu ,umeshindwa hata kujibu mstari mmoja tu? Hebu jitahidi bhana ,wewe ndio utaonekana muongo
 
I give up!
Umegoma kumjibu, au maswali yake unaogopa yatakukaanga? Mimi na bet ukijibu Natoa Laki 1 . Naimani huna uwezo hata robo wa kujibu hayo maswali ,hata kujaribu huna huo uwezo, ,maana utakamatwa tu,na ndio unachoogopa ,mmebaki kushambulia tu usabato ,mara ellen white , sijui mkojo nyie watu, watu tunataka kujifunza mnaleta ujinga
 
Mkuu mbona haumjibu maswali yake ,zaidi.unayakwepa ? Tatizo nini, nimeona umeaga kukimbia ,sasa hivi umerudi na ngonjera nyingine, watu tumekaa tunasubiri kujifunza, utusaidie hizo Aya zinahusiana vipi na uislamu, cha kushangaza ni.kama huzioni, hizo aya unazokimbilia , hata hazihusiani na uislamu, ndio maana kwakuwa umedai, mnyama ni uislamu, umepewa sura ya yohana 13 , kuhusu mnyama ,ujibu ,umeshindwa hata kujibu mstari mmoja tu? Hebu jitahidi bhana ,wewe ndio utaonekana muongo

Kuonekana muongo sio tatizo kwangu hasa baada ya kugundua aina na uwezekano wa mtu niliekubaliana nae kujadili nae (kwa lengo la kuelimishana). Kuna shida gani kwake (au kwako) kusoma nilichoshauri akisome kwanza ili nimjibu maswali yake - essentially he could have asked in a single question as almost everything is related and entwined to each other?
Nimempa link asome - na hajasoma (au kama kasoma basi hakuelewa kitu) maana vinginevyo asingeshindwa kuona kuwa baadhi ya maswali yake yanajibiwa na maelezo yangu na yaliyomo kwenye scholarly article kwenye link niliyompa. Na kama kitu kidogo hivyo kimekuwa kikubwa kwake ataelewa kweli Christian eschatology na Islamic eschatology? Bila mtu kusoma hayo japo kidogo KAMWE hataelewa kwa majira haya - japo baadae kila mtu ataelewa tu maana ni lazima mpinga Kristo afunuliwe eventually.
 
Back
Top Bottom