Ukiona choo ndotoni usikitumie

Ukiona choo ndotoni usikitumie

Mkuu heading ni hiyohiyo "ukiona choo ndotoni usikitumie".

Sasa ndiyo nikakuuliza kwani ndani ya ndoto huwa tuna utashi ama maamuzi ya kufanya?

Ninavyoelewa ni kuwa ndoto huratibu yenyewe pa kwenda na cha kufanya.

Wewe huletewa tu matokeo ya ndoto ilikokwenda na ilichoenda kufanya.

Sasa kuikontro cha kufanya ilikokwenda wakati wewe haupo, ilikuacha usingizini ni vigumu.
Tuna utashi na ndoto japo si asilimia mia moja... Ndio maana kuna baadhi huwa tunakemea ama kustuka usingizini
Hii nazungumzia ukikiona choo ndotoni... Hili si jambo la kawaida...
Unakiona choo kisha unavutika kukitumia.. Si kwamba umebanwa na haja la hasha unakiona ndotoni kisha unataka kukitumia
 
Mshana Jr swali fikirishi Je unawezaje ku-control mpk usikitumie choo wakati ndoto inapotokea mhusika unakuwa huna uwezo wa ku-control unachoota au je mtu unaweza kuzuia ndoto wakati inatokea wakati unakuwa katika un-conscious mind?
Tuna utashi na ndoto japo si asilimia mia moja... Ndio maana kuna baadhi huwa tunakemea ama kustuka usingizini
Hii nazungumzia ukikiona choo ndotoni... Hili si jambo la kawaida...
Unakiona choo kisha unavutika kukitumia.. Si kwamba umebanwa na haja la hasha unakiona ndotoni kisha unataka kukitumia
 
Mkuu Mshana Jr naomba tafsiri ya hii kitu.

Kuna ndoto imekuwa inanitatiza na mara nyingi imekuwa ikijirudia rudia.Ni hivi:si mara moja au mara mbili nimekuwa nikiota nimeokota pesa nyingi au ninachimba chimba kwenye mchanga na kisha nakutana na noti za kufa mtu.Ila katika ndoto zote hizo,fedha hizo (noti) huwa zinakuwa zimeloa maji, au zinachuruzika maji.

Na ndoto hizo hutokea pale ninapokuwa nina mchongo unahisiana na pesa,yaani kabla pesa hiyo sijaipata au tayari nimeipata ndoto hizo huibuka.Ila nikiwa sina mchongo wowote mbeleni huwa sipati ndoto hizo.Je,zinamaanisha nini?
 
Ni kweli kwamba unapokuwa kwenye ndoto unauwezo wa kufanya maamuzi kulingana na tukio unaloota kama kukubali,kukataa,kufurahi,kuchukia,kuogopa,kutokuogopa,kuamini au kutokuamini.
Kifupi matukio ya kwenye ndoto yatatokea kama kwenye uhalisia yanavyotokea. Maisha ni mapambano uki give-up inakula kwako, ukikomaa unashinda na kwenye ndoto ukikomaa unashinda
 
Mkuu Mshana Jr naomba tafsiri ya hii kitu.

Kuna ndoto imekuwa inanitatiza na mara nyingi imekuwa ikijirudia rudia.Ni hivi:si mara moja au mara mbili nimekuwa nikiota nimeokota pesa nyingi au ninachimba chimba kwenye mchanga na kisha nakutana na noti za kufa mtu.Ila katika ndoto zote hizo,fedha hizo (noti) huwa zinakuwa zimeloa maji, au zinachuruzika maji.

Na ndoto hizo hutokea pale ninapokuwa nina mchongo unahisiana na pesa,yaani kabla pesa hiyo sijaipata au tayari nimeipata ndoto hizo huibuka.Ila nikiwa sina mchongo wowote mbeleni huwa sipati ndoto hizo.Je,zinamaanisha nini?
Nitarejea kwako kwa kutulia
 
Sikutaka kuileta mada hii mapema bali wakati huu.... Nina sababu maalum.... Baada ya muda mchache ujao tutaenda kulala, wala tusitambue yanayoendelea ulimwenguni... Mwili wa utashi utapumzika... Mwili wa roho uta take cover...!
Roho ni 'nafsi huru ' itafanya itakayo na kuenda itakako.. Taarifa utazipata kupitia ndotoni....
Ndoto taarifa
Ndoto maono
Ndoto mvurugano
Unapoona/ unapoota choo ndotoni kuna tafsiri kama tatu... Moja lazima iwe sahihi... Makinika... Usikitumie kwanza...

Choo ni uchafu... Hakuna anayependa uchafu.. Ukiona mtu anapenda uchafu ana walakini
Choo kinanuka... Hakuna anayependa harufu mbaya.. Ukiona mtu anapenda harufu mbaya ana walakini...!
Choo si kitu cha kuonekana hadharani... Kina sehemu yake ya kutunzwa... Ukikiona choo ndotoni si ishara njema(hapa ni kwa tafsiri ya kinyesi)
Choo ni mlango wa kuzimu ( hapa choo ni kile kibebeo cha uchafu wa kinyesi toka kwa mwanadamu)... Choo cha mnyama hakina kinyaa kama cha mwanadamu kwakuwa mnyama ni hayawani...

Epuka kutumia choo ndotoni kwakuwa kama hujajisaidia kitandani basi kuna jambo bays linakutafuta....
Utaepukaje wakati uko ndoni na akili zako zinakuwa siyo za mtu aliye macho ila ni za ndotoni? Je kama akiwa msichana mzuri amevua nguo napo ufanyeje? Je kama ukiona rundo la pesa kwenye gunia pembeni ya barabara ufanyeje? Uziache kweli?!
 
Ni kweli kwamba unapokuwa kwenye ndoto unauwezo wa kufanya maamuzi kulingana na tukio unaloota kama kukubali,kukataa,kufurahi,kuchukia,kuogopa,kutokuogopa,kuamini au kutokuamini.
Kifupi matukio ya kwenye ndoto yatatokea kama kwenye uhalisia yanavyotokea. Maisha ni mapambano uki give-up inakula kwako, ukikomaa unashinda na kwenye ndoto ukikomaa unashinda
Siyo kweli kabisa huwezi kufanya mambo hayo ukiwa ndotoni yaani kutumia akili ya kawaida ukiwa macho na akili ya ndotoni. Ukiona unaweza kufanya hivyo ujue hiyo siyo ndoto au uko macho
 
Duh mbona wengine ndoto zetu hatuwezi kucontrol?

Au mimi sijui kuota vizuri teh!
Ni kweli kwamba unapokuwa kwenye ndoto unauwezo wa kufanya maamuzi kulingana na tukio unaloota kama kukubali,kukataa,kufurahi,kuchukia,kuogopa,kutokuogopa,kuamini au kutokuamini.
Kifupi matukio ya kwenye ndoto yatatokea kama kwenye uhalisia yanavyotokea. Maisha ni mapambano uki give-up inakula kwako, ukikomaa unashinda na kwenye ndoto ukikomaa unashinda
 
Tuna utashi na ndoto japo si asilimia mia moja... Ndio maana kuna baadhi huwa tunakemea ama kustuka usingizini
Hii nazungumzia ukikiona choo ndotoni... Hili si jambo la kawaida...
Unakiona choo kisha unavutika kukitumia.. Si kwamba umebanwa na haja la hasha unakiona ndotoni kisha unataka kukitumia
Okay Nimekusoma. Nakumbuka kuna siku niliota jamaa ananiita nikawa nagoma kabisa kumfuata mpk nikashtuka jasho linanitoka
 
Sikutaka kuileta mada hii mapema bali wakati huu.... Nina sababu maalum.... Baada ya muda mchache ujao tutaenda kulala, wala tusitambue yanayoendelea ulimwenguni... Mwili wa utashi utapumzika... Mwili wa roho uta take cover...!
Roho ni 'nafsi huru ' itafanya itakayo na kuenda itakako.. Taarifa utazipata kupitia ndotoni....
Ndoto taarifa
Ndoto maono
Ndoto mvurugano
Unapoona/ unapoota choo ndotoni kuna tafsiri kama tatu... Moja lazima iwe sahihi... Makinika... Usikitumie kwanza...

Choo ni uchafu... Hakuna anayependa uchafu.. Ukiona mtu anapenda uchafu ana walakini
Choo kinanuka... Hakuna anayependa harufu mbaya.. Ukiona mtu anapenda harufu mbaya ana walakini...!
Choo si kitu cha kuonekana hadharani... Kina sehemu yake ya kutunzwa... Ukikiona choo ndotoni si ishara njema(hapa ni kwa tafsiri ya kinyesi)
Choo ni mlango wa kuzimu ( hapa choo ni kile kibebeo cha uchafu wa kinyesi toka kwa mwanadamu)... Choo cha mnyama hakina kinyaa kama cha mwanadamu kwakuwa mnyama ni hayawani...

Epuka kutumia choo ndotoni kwakuwa kama hujajisaidia kitandani basi kuna jambo bays linakutafuta....
Duuh aisee,ndoto nijuavyo mimi unakuwa unconsciously,sasa sijui utawezaje kuzuia ikitokea,utakata gogo tu😂😂😂
 
Binadamu wa siku ni wabishi sana kwa sababu taarifa na maarifa vinapitakana kirahisi sana kwa mwenye kuhitaji kujua.
Uwanja wa taarifa na Mwanga wa maarifa ni mkubwa zaidi kuliko ilivyokuwa enzi za teknolojia duni na zama za giza.
Kuna ukweli ndani yake...

Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...


Cc: mahondaw
 
Utaepukaje wakati uko ndoni na akili zako zinakuwa siyo za mtu aliye macho ila ni za ndotoni? Je kama akiwa msichana mzuri amevua nguo napo ufanyeje? Je kama ukiona rundo la pesa kwenye gunia pembeni ya barabara ufanyeje? Uziache kweli?!
kila kimoja kinajitegemea kuna mmoja aliota anaogelea kuamka kajikojolea chapachapa
 
Duuh aisee,ndoto nijuavyo mimi unakuwa unconsciously,sasa sijui utawezaje kuzuia ikitokea,utakata gogo tu
Hivi hili neno unconscious maana yake halisi inajulikana vizuri kweli? Maana yake ni kupoteza fahamu yani unakuwa hujitambui
 
Shida ni kwamba nitakumbuka hii post nikiwa ndotoni??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom