Ukiombwa pesa ya soda unatoa shilingi ngapi?

Ukiombwa pesa ya soda unatoa shilingi ngapi?

😂😂😂😂😂 wengine huomba “hela ya soda” lakini ukweli ni kwamba hajala hivyo anaomba pesa ili apate mlo. Mimi inategemea muombaje kaombaje, lakini kwa kujua muombaje anaweza kuwa anaomba pesa ya kula mara nyingi hutoa elfu 10.

Juzi nilikua zangu nmekaa sehemu nakula rost ya kitimoto na Red Wine , wakati naendelea kula pale ghafla akatokea dada mmoja ambae ni jirani yangu lakini hatuna mazoea kivile, nikamsalimia akaitika, nikamkaribisha aje kula (Kama mnavyojua wabongo unamkaribisha tuu mtu kimazoea mda mwingine hatumaanishi)

Akavuta kiti akakaa, nashangaa anamuita muhudumu "Muuudumu niletee Glass na tishuuu! "nikashangaa sana, Wine yangu nilitaka ninywe mwenyewe sasa imepata muhuni tunaipiga mande!, nikasema sio tabu, Glass ikaletwa tukawa tunakunywa huku tunapiga story.

Kiukweli Dada aliniboa sana, ananiletea story nyingi, mara aniambie "hapa kuna vyumba ujuee"

Kiukweli mimi sipendi mtu aniongeleshe sana hua nasikia kama kichwa kinauma.

Nilimaliza kula, nikapiga glass moja ya mwisho, nikanawa, nikamuita muhudumu nikalipa bili, nikamuaga yule dada nikamuacha na chupa ya wine pale anywe.

Nashangaa naondoka ananishika mkono eti anataka nimuachie hata ya soda, nikasema sio shida, kwakua nilikua na chenchi nikampa 500 ya Coin akanywe hiyo soda, alitoa macho kama kapigwa shoti, kwa mawazo yake sijui alijua nitampa shingapi.

Mambo mengine bana.
 
600 ya pepsi big, akiamua kununua ya jero, 100 ataitafutia matumizi mbadala.
 
😂😂😂😂😂 wengine huomba “hela ya soda” lakini ukweli ni kwamba hajala hivyo anaomba pesa ili apate mlo. Mimi inategemea muombaje kaombaje, lakini kwa kujua muombaje anaweza kuwa anaomba pesa ya kula mara nyingi hutoa elfu 10.
Sio kwamba anakuwa hajala. Ila hela ya soda muombaji anaweza kuwa kamaanisha wine, sasa elfu 10 wine gani labda ile tamu ya kikristo (altar wine)
 
Juzi nilikua zangu nmekaa sehemu nakula rost ya kitimoto na Red Wine , wakati naendelea kula pale ghafla akatokea dada mmoja ambae ni jirani yangu lakini hatuna mazoea kivile, nikamsalimia akaitika, nikamkaribisha aje kula (Kama mnavyojua wabongo unamkaribisha tuu mtu kimazoea mda mwingine hatumaanishi)

Akavuta kiti akakaa, nashangaa anamuita muhudumu "Muuudumu niletee Glass na tishuuu! "nikashangaa sana, Wine yangu nilitaka ninywe mwenyewe sasa imepata muhuni tunaipiga mande!, nikasema sio tabu, Glass ikaletwa tukawa tunakunywa huku tunapiga story.

Kiukweli Dada aliniboa sana, ananiletea story nyingi, mara aniambie "hapa kuna vyumba ujuee"

Kiukweli mimi sipendi mtu aniongeleshe sana hua nasikia kama kichwa kinauma.

Nilimaliza kula, nikapiga glass moja ya mwisho, nikanawa, nikamuita muhudumu nikalipa bili, nikamuaga yule dada nikamuacha na chupa ya wine pale anywe.

Nashangaa naondoka ananishika mkono eti anataka nimuachie hata ya soda, nikasema sio shida, kwakua nilikua na chenchi nikampa 500 ya Coin akanywe hiyo soda, alitoa macho kama kapigwa shoti, kwa mawazo yake sijui alijua nitampa shingapi.

Mambo mengine bana.
Inategemea ntu -na- ntu, , low class nampa Jero, Middle Class nampa buku bee na high class nampa Msimbazi
 
Siku ukijua kwanini kuna watu wanasema

1. Nakuja na kibajaji changu , halafu akaja na vitz

2. Nimejenga kibanda changu, ukienda kwake unakuta ana mjengo akitaka kupanda chumbani kwake anatumia lift

3. Akikwambia narudi dakika sifuri tu, nisubiri, halafu anarudi baada ya nusu saa

4. Nina njaa kali, halafu kwenye akaunti ana 10M plus ipo ipo tu haina kazi maalum

Siku ukielewa hiyo kauli, utaelewa na kauli ya kuomba soda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom