Ukimya wa CCM na Lusinde

Ukimya wa CCM na Lusinde

Sijaona tofauti ya Lusinde na Lema; wote wametukana labda chadema ni wakweli waanze na lema!
 
Hata siku moja mwendawazimu hawezikubali kuwa ni mwenda wazimu.
 
Komandoo Salmin Amour au Komandoo Hamza Kalala? Kama Ni Salmin naona ashakuwa mgambo...hana lake tena kwisha habari yake. Ndo faida ya siasa za kibabe.
Ni Komandoo Salmin na mhasimu wake mkubwa Maalim Seif...
 
Mie nilimsikiliza mpaka sasa nasikia kichefuchefu.Lusinde hana nidhamu hata kidogo.Ni mchafu wa mdomo kupitiliza.Ni kweli matusi yake hayaandikiki kila mmoja ajisikilizie mwenyewe
 
Mods naomba muitenganishe hiyo post ya petition na hii
 
Mimi nawashangaa watanzania mbona hampigi debe gazeti kama ijumaa lifutwe
 
Ombwe la uongozi halipo kwenye serikali ya CCM bali pia hata kwenye chama kinachotawala. Ningetarajia mwenyekiti wa CCM au yeye mwenyewe au kupitia kwa katibu wa Chama walaani hayo matusi yaliyotolewa na Lusinde na kusema kwamba hayo yalikuwa ni mambo yake binafsi na wala hakutumwa na Chama. Lakini kukaa kimya bila kukemea maana yake ni kwamba aliyoyasema Lusinde ni maelekezo ya chama chake. Kama alivyosema mmoja wa wana JF hapa, hayo matusi yatakuwa mtaji wa kisiasa kwa CDM kwenye chaguzi zijazo.

Mukama yuko wapi? Hata kwenye kampeni sikumsikia, angekuwa Makamba tayari angekuwa amesafisha hali ya hewa!!!

Tiba
 
Mie nilimsikiliza mpaka sasa nasikia kichefuchefu.Lusinde hana nidhamu hata kidogo.Ni mchafu wa mdomo kupitiliza.Ni kweli matusi yake hayaandikiki kila mmoja ajisikilizie mwenyewe

Kweli mkewe anashida, kaolewa najinsia moja mh, mwanaume gani anamdomo kuliko waimba mipasho atakua shoga walaah.
 
Suala la Lusinde limerudishwa kwenye kamati ya maadili ya chama!

Hawana cha kumfanya, kwa sababu TOT sasa imepoteza mwelekeo huku Hadija Kopa kapoteza muelekeo kwenye mipasho. Sasa lusinde ndo kachukua nafasi ya TOT na Hadija Kopa, so na yeye wakimpiga stop sijui nani tena mwingine atakayechukua nafasi yake. Lazima wamlinde
 
Bado nafikiri tuna serous conditioning na CCM ... hatuuoni na kuukubali ukweli ulioko wazi kabisa.. Why discuss about Lusinde in this whole issue!! Lusinde?? Hakusimama pale akiwakilisha familia au kampuni yake!!

Muondoe Lusinde Leo pale kwa sababu ya alichokifanya ... Nani kakuambia utakuwa umeangamiza yale MATUSI pale CCM!!? The seed is still there, soon will manifest another Lusinde tena aliyepiga sugu ... kwa kuwa MBEGU ni CCM yenyewe!

Kwa namana yoyote CCM isaidiwe, IPEWE MSAADA WA DHATI kwa kuchukuliwa hatua kali, yenyewe HAIJIWEZI!!

Pamoja na Maumivu yatakayokuwepo ... CCM itashikuru kwa Upendo wa kweli utakao kuwa Imepewa kwa hatua hizo ... Yenyewe haijiwezi!!
 
CCM haiko serious...vinginevyo ungekuta wameshamuwajibisha ipasavyo...na ataendelea kupeta tu mtaani na mdomo wake mchafu kama choo cha stendi
 
Livingstone Lusinde ana bahati ya kuzaliwa, yule mtu ana elimu ya chekechea, zaidi ya hapo hata elimu ya kimazingira haimsaidii chochote! Zaidi sisiemu aibu yao wenyewe kumwamini mtu wa aina ile kumnadi mgombea mbele ya ushindani kama huu wa leo.
 
CCM hawawezi kutoa tamko lolote kwani wameishiwa sera, miaka hamsini ya uhuru hawajafanya lolote, kwahiyo matusi ndio imekuwa sera yao.
 
Sijaona tofauti ya Lusinde na Lema; wote wametukana labda chadema ni wakweli waanze na lema!

Nafikiri ingekuwa vizuri kama ungetuwekea uthibitisho kama huo, vinginevyo utaishia kutukanwa tu.
 
Jamani hakukuwa na namna nyingine ya kuua tuhuma za Ben zaidi ya kumtoa kafara ya 'Mh.' Lusinde kwa kumdanganya ajiabishe kwa kutumia maneno yasiyofaa mbele ya watoto na watu wazima.

Kwa hiyo habari ya Ben juu ya "Mwalimu" ndiyo inawekwa kapuni, si mnaona anavyoshupaliwa 'Mh'.Lusinde.
 
siamini kuwa magamba watakaa kimya kwa hili......NASUBIRI KWA HAMU KUSHUHUDIA KESI YA UDHALILISHAJI ITAKAYOFUNGULIWA NA VIONGOZI WA CHADEMA,WATETEZI WA HAKI ZA WATOTO,NA AKINA MAMA MAKINI NDANI YA TAIFA LETU...HII NI AIBUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU SI KWA CCM TU BALI KWA KILA MWENYE BABA NA MAMA aka WAZAZI
 
Back
Top Bottom