Hivi CCM wameshatoa tamko lolote kuhusiana na mbunge wao Livingston Lusinde kuporomosha mitusi kule Arumeru?
Sahau. Kwenye matuzi yake alianza hivi: "CCM Oyeeee." Wasikilizaji wakaitikia "Oyeeeeeeeeeeeee." Kabla ya kumwaga matuzi akasema "Mheshimiwa Mwenyekiti wa chama, Waheshimiwa viongozi wenzangu na Wanachama wenzangu." Kama alikuja kivyake pale pale (hakutumwa) kwa nini ali-wamention hawa? Na kama walimtuma wanaweza kweli kumchukulia hatua?
Lakini Bob, huoni kwamba huyu jamaa ndo anaweza kuizamisha meli ya CCM 2015? Au wewe bado unataka CCM iendelee tu kutawala?
Mimi nimeanza kuhisi kuwa alikuwa na baraka zote za chama na ndiye alikuwa 'designated bomb thrower'....
Hawawezi kutoa tamko lolote kwa sababu matusi ndiyo sera yao; hivi wewe hujawahi kumsikia Mkapa akiporomosha matusi? Tofauti ni kuwa Lusinde anajua matusi mengi kuliko Mkapa, yaani anajua kutangaza sera za CCM vizuri kuliko Mkapa. Je unakumbuka mzee Makamba naye alivyokuwa akitoa matusi makavu makavu? je unamkumbuka Ditopile alivyokuwa nay akitoa matusi ya wazi wazi? Je CCM iliwafanya nini? Utamshangaa Lusinde hapo tu, lakini yeye ataendelea kudunda ndani ya CCM kwa vile ndiye mtendaji mzuri.
At Least Kibajaj amenikumbusha kampeni za akina Madevu na Komandoo miaka ya tisini
Ukimsikiliza vizuri bila ghazabu, wala ushabiki wa kichama, utagundua kama alikuwa akijibu hoja zilizowahi kutolewa awali na upande mwingine katika kampeni hiyo!
Wapenzi wengine visimu vyetu havina uwezo kufungua yotube tusikie. Mwenye uwezo aandike hayo matusi wote tujue. Ili tusaidiane kumhukumu.