Ukienda kwa Nabii T.B. Joshua, jihadhari sana

Christo hakuja kumponya mtu dunian wala kutenda miujiza yoyote dunian ndiomaana alkuwa kila akifanya muujiza lazma awaambie wahusika msimwambie mtu,, alichokuja dunian ni kuleta mwanga wa wokovu na neema ya ukombozi tuu, na sio mengine, hayo ya uponyaji yanabaki kama tu zawadi ya kumuanin then unafunguliwa kila kitu, ata alipowaponya weng wao walimuamn kwanza ndpo kuponywa ispokuwa wale tu waliokufa maana hawakuweza kunena lolote,,,,Point ni hii chrsto anatak na anakutaka wew Kupata maarifa na mwangaza wa neno ya kwel uondoe ujinga kichwan mwako kwanza ndpo mengine yafanyikee,,kupona huja baada ya kujua kwel ni ipi, kupata maarifa mapya ya kuondoa ujinga na vifungo vya akili kuchwan,..awo mnaowaita wachungaj na manabii wanajua wanachokifanya, wao hawapo kukusaidia bali kukupumbaza na kuifanya akil yako isifunguke ubak kuwa mtumwa wa akili, na roho, pia uwe mtegemez maan mtumwa n mtu tegemezi, hvyo bas wao ukupa muujiza ambao utakufnya umtukuze mchungaj,nasio Mungu, oia ukufanya uwe mtumwa wa mchungaji kwa kumtegemea yeye,,huo Upuuzi christo ndio aliupinga,,yaan inashangaza wachungaj na manabiu uchwara wa kileo hawana wito wowote, wala unabii wowote zaid ya ushirikina,,nakazia maneno kuwa zama hiz hakuna unabii wala utume wowotee,awo woote muwapao majina makubwa makubwa wote majizi tuu hutumia ushirikina kuwaponya na kuwa hadaa,,,Mungu wa kwel anakutaka upate maarifa yakujua ww muafrikan nani hapa dunian, nn kusudio lako, Mungu wa kwel anakupa nguvu zakujiponya wew mwenywe paspo kumtegemea mtu yyte,,Shetani ndiye ana control hiz dini zote na kila aina ya iman kwakujifananisha na Mungu, ndio maana nyakat hiz hakuna waty wanaotenda maajabu kama ya manabii wa kale,,mtian mdogo tuu mfuate uyo anaejiita nabii au mponyaji akupe unabii kuhusu ugonjwa wa covid19 kwa undan wake kama ajakupiga chenga,,pili muulize undan wa historia ya israel ya kwel kwakutumia unabii na maandiko, akikujibu haya maswal kama majibu yake yalivyo fasaha bas mfuate
 
Kansa ikimrudia mtu ndo easy assumption kuwa Katenda tena dhambi?
Seriously?
Sio assumption; hiyo ni kwa mujibu wa maneno ya Yesu(Yn 5:14). Kwahiyo kama mtu alipona kansa kabisa kwa muujiza(kwa kuombewa tu) kisha baadaye ikamrudia kuna uwezekano mkubwa mtu huyo baada ya kupona aliendelea na maisha ya dhambi. Kama amedumu katika utakatifu, akaugua tena ugonjwa huo, zipo sababu nyingine(za kibiblia) kwanini watakatifu wanaugua.
 
Nikaufungua fasta nikidhani umekuja na tahadhari dhidi ya wanaokwenda kwa tapeli la kidini TBJoshua kumbe umeweka pumba tu humu... hilo la kwanza

Jambo la pili, kama ulitaka kumaanisha ujumbe uliouweka basi haikuwa na haja ya kumtaja huyo jamaa kwenye title, badala yake ungeweza tu kusema "...kwa manabii, mitume na waponyaji"
 
Yaani ningekuwa nakujua ningekupa.zawadi kwa some ulilolitoa. Shida wengi hawajui.neno wala.hawasomi neno.Mungu huponya wote bure ila gharama yake ni kuacha dhambi. Kingine na mazingira ya kupata ugonjwa binadamu anatakiwa ujihoji, utubu na kuacha dhambi.
Hivi binadamu alieumbwa dhaifu na alie venerable na ushawishi wa ibilisi anawezaje kwa utashi wake kuacha hicho unachokiita dhambi??

Et aache dhambi, kwani anatenda kwa utashi wake labda ahame duniani akaishi sayari isiyo na ushawishi wa kutenda dhambi
 
Tb Joshua is an Agent of the devil .Nakushangaa uliekuja hapa kupigia kampeni jitu jizi na tapeli km Tb Joshua. Kwanza mahubiri yake yamejaa udhalilishaji akionyesha live wanawake wanaojifungua baada ya kupokea maombi yake. Anafanya km chambo ya kuwavuta watu kupitia matukio ya kutengenezwa na kupangwa wengi wavutike.

Lakini pia hata imani yake ni ya kutia shaka.Mara awafundishe watu kufanya maombi kutumia shanga,maji na stika yenye picha yake ndo maandiko yameagiza ivo? Kibaya zaidi anauza maji,shanga na stika km bidhaa.

Wajinga wengi wasiojua kutafakari maandiko wameamini na kuishia kupigwa pesa nyingi.Tb Joshua anatumia uchawi na ujanja ujanja katika kuwateka watu. Nakushauri acha kupoteza muda na manabii wajanja wajanja km Prophet Bushiri,TB Joshua,Mwamposa,Gwajima, Suguye na wengineo utapoteza mda na pesa zako bureee.
sasa twende kwa nani bwana.
 
Utamjuaje kama nabii anatumia ulimwengu wa roho au nguvu za Yesu?
Ulimwengu wa roho unahusisha roho zote 2 nzuri na mbaya...yani roho mtakatifu na roho wachafu

hivyo ulimwengu wa roho sio sehemu mbaya kwa maana ukijenga roho njema rohoni Yesu atatuma taarifa zake kupitia roho mtakatifu kwenye ulimwengu wako wa roho.....

Ulimwengu wa roho upo mbele yetu, tukio kabla halijatokea tayari roho inakuwa na taarifa hivyo kama pamejengeka kikamilifu mbele ya Mungu, utaweza oneshwa hatari hiyo na jinsi ya kujinasua.....eg wanaoota wanaenda pata ajali alaf hawasafiri na wanasali na kweli inatokea etc....

Utajuaje manabii wakweli na waongo, ipo kwenye karama za mafundisho yao.....sikuzote mtu anaehubiri andiko la Yesu asilimia 85% atahubiri njia ya kumfuata Yesu na kujiandaa kuishi maisha nje ya haya ya duniani...huelezea njia za kumpokea kristo na wale wengine wao huhubiri mafanikio ya pesa kwa asilimia 90% na hata akihubiri kuhusu hatua za kuurithi ufalme wa milele basi atagusagusa tu......

Mungu humtumia Mtumishi wake yoyote kutenda miujiza na sio kama huyo muanzisha mada aliposema nenda kwa wahubiri maarufu, kwani umaarufu ndio hutenda miujiza?.
 
T.B. Joshua anafahamika sana ulimwenguni kutokana na maombezi anayoyafanya katika kanisa lake kubwa, lililoko Nigeria. Kwa wanaofuatilia habari za mhubiri huyo, ni wazi watakuwa ama wamesikia au kuona vipofu, viwete, viziwi na wenye magonjwa sugu wakitoa shuhuda za uponyaji baada ya kuombewa na T.B. Joshua. Sio mhubiri huyo tu anayeombea wagonjwa, wapo wahubiri wengine Kenya, South Africa, Korea ya Kusini, USA nk wanaoombea watu wenye magonjwa mbalimbali.
Kuna Mwingine Morogoro naye anajiita jina kama hilo na anafanana sana na huyo wa Nigeria sijui ni ndugu au ni branch yake!!
1621951818692.png
1621951871552.png

Kuna mhubiri fulani, Tanzania, yeye sio tu anaombea wagonjwa, amewahi kuonekana pia akiombea mtu aliyekufa, kisha mtu huyo akafufuka!
Bila kumtaja huyo mfufuaji wa Tanzania hutakuwa umetenda haki
 
T.B. Joshua anafahamika sana ulimwenguni kutokana na maombezi anayoyafanya katika kanisa lake kubwa, lililoko Nigeria. Kwa wanaofuatilia habari za mhubiri huyo, ni wazi watakuwa ama wamesikia au kuona vipofu, viwete, viziwi na wenye magonjwa sugu wakitoa shuhuda za uponyaji baada ya kuombewa na T.B. Joshua
Kuna mawaziri kadhaa toka hapa kwetu walikwenda kuombewa huko vipi mrejesho wadau
 
Mkuu Abby Newton habari. Ulichoandika hapa kinaeleza mengi ambayo hujayasema. Naomba nikuulize, Je Yesu Kristo ameshafanyika Bwana na Mwokozi wa Maisha yako? Je leo ikiwa ndio siku yako ya mwisho duniani, una shuhudiwa ndani yako Roho yako inaelekea mbinguni au jehanamu?

Mkuu Abby Newton, naomba uelewe kwamba sijakupinga kwa kila ulichoandika ILA ni vyema ukafahamu kwamba mambo ya Rohoni (utambuzi) hutambuliwa na watu wa Rohoni tu (Waliookoka). Kwahiyo Mkuu Abby Newton chukua hatua mapema ya kumpokea Kristo katika maisha yako

Ahsante
Ni sawa kuokoka ni muhimu....lakini katika maisha haya ya duniani na mazingira halisi...kuishi maisha ya kiroho bila kumkwaza Mungu ni kujidanganya.....unless kama ni tajiri ambaye unajitegemea kwa kila kitu....lakini otherwise walokole wengi ni wanafiki sababu tunaishi nao mitaani na tunaona
 
Mtu akienda kuombewa akaambiwa atoe kwanza pesa ndio aombewe, asikubali. Yesu hakuwalipisha pesa wagonjwa. Hata wanafunzi wake alipowapa mamlaka ya kupoza wagonjwa, aliwaambia amewapa mamlaka hayo bure hivyo watoe huduma hiyo bure. Sadaka tu ndio mtu anaweza kutoa, tena kwa hiari na moyo mkunjufu, sio kwa kulazimishwa.

Mhubiri yeyote anayesema “Panda Mbegu” ili uombewe, muogope kama ukoma!! Vaa viatu vyako na nenda zako nyumbani!! Yesu alitoa bure na mtumishi wa Mungu anatoa bure, ila zaka na sadaka ni muhimu kutoa.
 
Mtu akienda kuombewa akaambiwa atoe kwanza pesa ndio aombewe, asikubali. Yesu hakuwalipisha pesa wagonjwa. Hata wanafunzi wake alipowapa mamlaka ya kupoza wagonjwa, aliwaambia amewapa mamlaka hayo bure hivyo watoe huduma hiyo bure. Sadaka tu ndio mtu anaweza kutoa, tena kwa hiari na moyo mkunjufu, sio kwa kulazimishwa.
Hapo sasa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Ni sawa kuokoka ni muhimu....lakini katika maisha haya ya duniani na mazingira halisi...kuishi maisha ya kiroho bila kumkwaza Mungu ni kujidanganya.....unless kama ni tajiri ambaye unajitegemea kwa kila kitu....lakini otherwise walokole wengi ni wanafiki sababu tunaishi nao mitaani na tunaona
Walokole ni noma asee

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom