passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Habari za uzima wakuu?
Leo nimeona mtu akiposti habari kuhusu shirika la utangazaji BBC kufichua uovu wa T.B Joshua nimefurahi sana maana mama watoto aliniambia kuhusu DSTV kuiondoa chanel yake lakini sikumtilia maanani.
Leo nitawaambia stori moja ya jamaa mmoja anaitwa JAMES RANDI(Randall James Hamilton Zwingwe) huyu alizaliwa nchini Canada Toronto, mwaka tarehe 7/08/1928.
James Randi aliukuwa ni mwana mazigaombwe wa stejini, watu wengi walipenda kumuita mfichua matapeli(debunker) lakini yeye hakupendelea neno hilo na alipenda kujiita ni mchunguzi (investigator)
James Randi alifichua uovu wa jamaa mmoja alikuwa akijulikana ni mfanya miujiza kwa jina la Peter Popoff. Huyu Peter popoff alikuwa ni tapeli akishirikiana na mke wake.
Peter Popoff alikuwa na foundation ambayo watu wakifika pale wanajaza baadhi ya taarifa zao kama vile sehemu wanazotoka, maradhi yanayowasumbua, matatizo ya kifamilia na ishu zingine za kibinafsi.
sasa akiwa katika kilele cha umaarufu wake miaka ya 1980s, akaja huyu jamaa James Randi akiwaambia watu kwamba Peter Popoff ni tapeli na mwizi, baada ya James randi kufanya uchunguzi wake akiwa na timu yake makini.
Wakagundua kuwa Peter George Popoff alikuwa na kisikiliza sauti masikioni kwake (ear piece) akipokea taarifa kutoka kwa mke wake elizabeth.
Kipindi Peter Popoff akiendelea na huduma kanisani alikuwa akitaja mtu fulani na kusema mungu anamfunulia hivyo akimuita pale mbele anaanza kumwambia vitu ambavyo mtu huyo tayari kashavijaza. Hivyo mke wake Elizabeth anamwambia jinsi ya kusema na yeye anamfatisha.
Yale yale ya Peter Popoff yatajirudia kwa T.B Joshua na BBC kufichua uovu waliosema watautoa . na bado hapa Tanzania.
Ni suala la muda tu tutaelewana.
Hawa watu mpaka watoke na wao waje kufanya kazi.
Leo nimeona mtu akiposti habari kuhusu shirika la utangazaji BBC kufichua uovu wa T.B Joshua nimefurahi sana maana mama watoto aliniambia kuhusu DSTV kuiondoa chanel yake lakini sikumtilia maanani.
Leo nitawaambia stori moja ya jamaa mmoja anaitwa JAMES RANDI(Randall James Hamilton Zwingwe) huyu alizaliwa nchini Canada Toronto, mwaka tarehe 7/08/1928.
James Randi aliukuwa ni mwana mazigaombwe wa stejini, watu wengi walipenda kumuita mfichua matapeli(debunker) lakini yeye hakupendelea neno hilo na alipenda kujiita ni mchunguzi (investigator)
James Randi alifichua uovu wa jamaa mmoja alikuwa akijulikana ni mfanya miujiza kwa jina la Peter Popoff. Huyu Peter popoff alikuwa ni tapeli akishirikiana na mke wake.
Peter Popoff alikuwa na foundation ambayo watu wakifika pale wanajaza baadhi ya taarifa zao kama vile sehemu wanazotoka, maradhi yanayowasumbua, matatizo ya kifamilia na ishu zingine za kibinafsi.
sasa akiwa katika kilele cha umaarufu wake miaka ya 1980s, akaja huyu jamaa James Randi akiwaambia watu kwamba Peter Popoff ni tapeli na mwizi, baada ya James randi kufanya uchunguzi wake akiwa na timu yake makini.
Wakagundua kuwa Peter George Popoff alikuwa na kisikiliza sauti masikioni kwake (ear piece) akipokea taarifa kutoka kwa mke wake elizabeth.
Kipindi Peter Popoff akiendelea na huduma kanisani alikuwa akitaja mtu fulani na kusema mungu anamfunulia hivyo akimuita pale mbele anaanza kumwambia vitu ambavyo mtu huyo tayari kashavijaza. Hivyo mke wake Elizabeth anamwambia jinsi ya kusema na yeye anamfatisha.
Yale yale ya Peter Popoff yatajirudia kwa T.B Joshua na BBC kufichua uovu waliosema watautoa . na bado hapa Tanzania.
Ni suala la muda tu tutaelewana.
Hawa watu mpaka watoke na wao waje kufanya kazi.