Hivi nyie mnaowaza kuibiwa kura, mawakala wenu wanafanya kazi gan ndan ya kituo
Kama tatizo ni kuwa Ukawa wana mawakala , na tegemea na CCM vile vile wana mawakala.
Kuna haja gani ya Polisi tena?
Hivi nyie mnaowaza kuibiwa kura, mawakala wenu wanafanya kazi gan ndan ya kituo
Hasa vijijini ambapo watu hawajazoea kuona polisi wenye silaha. Mfumo mzima wa NEC umetengenezwa kuibeba CCM. Kwa kweli Chadema (UKAWA) wana udhaifu mkubwa wa kutishia kwa mdomo bila kutumia mahakama na vyombo vingine vilivyopo kisheria. Si kazi ya tume, Rais au polisi kutafsiri sheria. Hiyo ni kazi ya mahakama.Mkuu mawakala wanaweza tishwa.... wanaweza nunuliwa.... tumeyaona haya na kuyasikia wafuasi mahili wa upinzania kununuliwa.....
Hasa vijijini ambapo watu hawajazoea kuona polisi wenye silaha. Mfumo mzima wa NEC umetengenezwa kuibeba CCM. Kwa kweli Chadema (UKAWA) wana udhaifu mkubwa wa kutishia kwa mdomo bila kutumia mahakama na vyombo vingine vilivyopo kisheria. Si kazi ya tume, Rais au polisi kutafsiri sheria. Hiyo ni kazi ya mahakama.
Tatizo ni kwamba wengi wanadhani kwa kufanya hivi itasaidi 'goli la mkono' huku wakisahau kuwa wizi wa kura umefanyika karibia chaguzi zote zilizotangulia na mambo yalikuwa yakiwaendea vizuri waibaji wa kura. Kufanikiwa kwao kuiba kura ilikuwa ni kwa sababu walikuwa na watu 'smart' na wenye IQ za juu lakini katika kuvutana mikono na kuingizana wajomba, mama wadogo nk kwenye system safari hii walio nje nao wanaonekana kuwa even smarter kuzidi waliomo ndani na ndio maana hata wengine wakaropoka kabla uchaguzi hata haujafanyika.Kikwete alishawahi kumletea nani kiroba cha sembe...labda ile sembe nyingine inayozungumzwa kuwa mwanae ni supplier, importer na exporter mkubwa wa mazao ya 'nafaka'.
Kila mtu anayajua maisha yake, kwani siku zote wewe ndio unawalisha?
Wewe Chaggadema naona una hamu sana ya KURITHI Nafasi ya Joyce Mukya KOMAA!Manyoya mpaka ndukum
Wanajamvi,
Hili suala la kubaki vituoni baada ya kupiga kura linaanza leta ukakasi sasa, leo Mh. Raisi kaliongelea na kusisitiza watakaobaki vituoni watashughulikiwa. Nimemsikia mhe. Kinana na IGP pia wakiliongelea na mbaya zaidi kwenye magroup yote wana CCM wamefurahia sana tamko la leo la mh. Raisi ambae pia ni Amiri jeshi mkuu katika nchi ambayo Tume ya Uchaguzi haiko huru, tumeona wakurugenzi wa tume wakibadilishwa chini ya mwezi mmoja kabla ya uchaguzi kwa sababu za kikatiba/kisheria maana mhe. Raisi ana uwezo huo.
Lakini pia tuna kumbukumbu za chaguzi zilizo pita ambapo bila wananchi kuwepo eneo la tukio, sina uhakika kama mh. Wenje angepata ushindi zaidi ya mh. Masha aliye kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Hii yote inaleta Sintofahamu na kuonyesha kama ule usemi wa Nape unatimizwa kwa njia hii.
Pia nimemuona Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC akiiweka kama issue ya kubaki kwenye vituo haiko kisheria.
Je, kama suala la kubaki vituoni kwa umbali usiopungua mita 100 liko kisheria, ni kwa nini UKAWA wasiende mahakamani kesho kwa hati ya dharula kuweza pata ufafanuzi na order ya mahakama kwenye jambo hili?
Nia ni kuepusha damu za Watanzania kumwagika maana ninavyoona, tunakoelekea sio kuzuri ifikapo tarehe 25 Oktoba.
Nawakilisha.
Acheni uhuni wenu.kila mtu akibaki kituoni itakuwa fujo.wewe huelewi nini!
section 4(1) of The National election.Act Cap343, imesema ndani ya mita 200 ambapo huruhusiwi kukusanyika ,kuvaa nembo ya chama au sare za Chama, huu unaosemwa na Tume ni uongoMmezoea kubembelezwa Watanzania. . . .Kama una hakika na sheria isemavyo fine be there. . . . . Hili lilihitaji mjadala??!!
High IQ unajenga premises tu conclusion inakuja automatically. . . . . .
Kama una uhakika be there. . . .
Watu 450!
Fujo itatoka wapi?
Hakuna umeme, radio/tv zitatupaje taarifa?
Kuna haja gani ya kubandika matokeo kama hadhira haipo?
Wanajamvi,
Hili suala la kubaki vituoni baada ya kupiga kura linaanza leta ukakasi sasa, leo Mh. Raisi kaliongelea na kusisitiza watakaobaki vituoni watashughulikiwa. Nimemsikia mhe. Kinana na IGP pia wakiliongelea na mbaya zaidi kwenye magroup yote wana CCM wamefurahia sana tamko la leo la mh. Raisi ambae pia ni Amiri jeshi mkuu katika nchi ambayo Tume ya Uchaguzi haiko huru, tumeona wakurugenzi wa tume wakibadilishwa chini ya mwezi mmoja kabla ya uchaguzi kwa sababu za kikatiba/kisheria maana mhe. Raisi ana uwezo huo.
Lakini pia tuna kumbukumbu za chaguzi zilizo pita ambapo bila wananchi kuwepo eneo la tukio, sina uhakika kama mh. Wenje angepata ushindi zaidi ya mh. Masha aliye kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.
Hii yote inaleta Sintofahamu na kuonyesha kama ule usemi wa Nape unatimizwa kwa njia hii.
Pia nimemuona Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC akiiweka kama issue ya kubaki kwenye vituo haiko kisheria.
Je, kama suala la kubaki vituoni kwa umbali usiopungua mita 100 liko kisheria, ni kwa nini UKAWA wasiende mahakamani kesho kwa hati ya dharula kuweza pata ufafanuzi na order ya mahakama kwenye jambo hili?
Nia ni kuepusha damu za Watanzania kumwagika maana ninavyoona, tunakoelekea sio kuzuri ifikapo tarehe 25 Oktoba.
Nawakilisha.
Tutalinda kura. Mimi ntakuwa mstari wa mbele kati ya watakao kaa kituoni
Mkuu sheria inasemaje? Mbona huongelei experience ya Wenje na je watu 450 kweli wanaweza fanya fujo?Mkuu naomba tu nikwambie ukweli kuwa hujui unachokisema. Hivi hata ukitumia akili yako ya kawaida unaona inawezekana watu wa vyama vyote wakalinde kura kweli? Mbona mnataka kuletea hii nchi vurugu zisizo na maana? Ni kweli wewe hujui binadamu huwa hawawazi the same?
Ukikusanya watu elfu moja au hata billion moja hakuna hata mmoja kati yao atafanana mawazo na mwingine. Hao watu unaotaka wakalinde kura umehakikisha kuwa watakuwa wanawaza kama wewe yaani kulinda tu kura na wasifanye fujo?
Nyie wengine humu nishagundua ni kati ya wale wasiokuwa na huruma na nchi na familia zenu. Sasa hivi nyie mnahifadhi wakimbizi wengi wa burundi. Jaribu kuangalia wewe utakimbilia wapi halafu ndiyo uanze kushabikia huo upuuzi wako. Nakutakia uchaguzi mwema.
Acheni uhuni wenu.kila mtu akibaki kituoni itakuwa fujo.wewe huelewi nini!
Not young..I said small....kichwani. Talk about Mbowe, that's your opinion and one guy once said "opinions are like 'as...holes', everybody's got one"Sikatai "i may still be young" but a minded developed sane guy.Watch out brother,Your mind is in Mbowe's trouser pocket.
Sio suala la kumwamini wakala au kutomwamini, sheria ya uchaguzi inasemaje baada ya kupiga kura, kama inaruhusu watu kukaa umbali usiopungua mita 100, hao wanaozuia wanatumia kigezo gani?
Kuna nguchiro huwa wanapiga kura maofisini Kisha wanazileta zihesabiwe. Hao ndio wanatakiwa kuzuiliwa kuingia chumba cha kura. Mawakala wanaweza kununuliwa au hata kutishwa na wakati mwingine kusingiziwa wanaleta fujo pindu wanapo protest hujuma. Wanaitiwa Polisi, wanakuwa detained na hii inampa nafasi msimamizi wa uchaguzi ambaya ni kada tu wa CCM kuandaa matokeo anayotaka. Pia wakati mwingine kuwepo Watu nje ya kituo kunawakumbusha mawakala kuwa kununuliwa ni hatari kwao na pia kuwa kuna support nje in case maharamia wakitaka kuanzisha udhalimu wao. Purely simple.
Well, sasa wewe mtu wa UKAWA ukitaka kubaki kulinda kura yako (presumably haumwamini mtu yeyote au unaona wakala wako hana nguvu), na CCM nao na ACT nao wabaki unadhani hapo nje ya kituo PATATOSHA?