UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

Kwan nchi nzima imesongamana kama dar?? Kuna maeneo mengi sana ya wazi maeneo mengineyo ya Tanzania mkuu wangu. Hata mkisema suala la sheria za serikali za mitaa....zimeshindwa kuua vijiwe vya bangi leo ndo mtazuia watu kukaa tena wakisubir matokeo ya uchaguz?? Hapana.

Ujue Vitu Vingine Inabidi Tuwe Tunafikiria Kidogo,mkuu Wewe Unapiga Kura Saa Ngapi Na Matokeo Yanatangazwa Saa Ngap?
 
Ujue Vitu Vingine Inabidi Tuwe Tunafikiria Kidogo,mkuu Wewe Unapiga Kura Saa Ngapi Na Matokeo Yanatangazwa Saa Ngap?

Tutasubiri matokeo ya kituo husika na sio ya nchi nzima mkuu....kwan watahesabu wiki nzima kituo kimoja??
 
Acheni uhuni wenu.kila mtu akibaki kituoni itakuwa fujo.wewe huelewi nini!
Bavicha wakibaki vituoni kulinda kura, nao UVCCM watakuwa na haki kubaki vituoni kulinda kura.
Hapo itakuwa mbabe ndo anashinda.
 
Sasa mkuu mawakala kuhongwa kirahisi ni organizational problem kwa nini mnataka kuleta vurugu?
Narudia wakati wa upigaji wa kura rudini nyumbani. Jioni upigaji kura ukimalizika rudini kusikiliza matokeo. Mkiweka kibaraza mnaleta Voters' intimidation yaani mnatishia wapiga kura wengine.
Mbona kinaeleweka?

hao wapiga kura si watoto wadogo unless ni mamluki ndio wataogopa kwenye kupiga kura kuna nini cha kumuogopesha mtu na kwa nini mlin'gan'ganie hili nyinyi mmezuiwa kubaki mita mia 200! kwahiyo ni wazi ndio zile njia zenu za wizi sisi sote ni watu wazima tuna akili ni tuna haki sio kwamba alie kiongozi ana haki zaid au yuko juu ya sheria ni bora kuheshimiana tutakuwa wa maana kuliko kila wakati kufanya upuuzi mpya kwa ajili ya kun'gang'ania madaraka
 
Wanajamvi,

Hili suala la kubaki vituoni baada ya kupiga kura linaanza leta ukakasi sasa, leo Mh. Raisi kaliongelea na kusisitiza watakaobaki vituoni watashughulikiwa. Nimemsikia mhe. Kinana na IGP pia wakiliongelea na mbaya zaidi kwenye magroup yote wana CCM wamefurahia sana tamko la leo la mh. Raisi ambae pia ni Amiri jeshi mkuu katika nchi ambayo Tume ya Uchaguzi haiko huru, tumeona wakurugenzi wa tume wakibadilishwa chini ya mwezi mmoja kabla ya uchaguzi kwa sababu za kikatiba/kisheria maana mhe. Raisi ana uwezo huo.

Lakini pia tuna kumbukumbu za chaguzi zilizo pita ambapo bila wananchi kuwepo eneo la tukio, sina uhakika kama mh. Wenje angepata ushindi zaidi ya mh. Masha aliye kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Hii yote inaleta Sintofahamu na kuonyesha kama ule usemi wa Nape unatimizwa kwa njia hii.

Pia nimemuona Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC akiiweka kama issue ya kubaki kwenye vituo haiko kisheria.

Je, kama suala la kubaki vituoni kwa umbali usiopungua mita 100 liko kisheria, ni kwa nini UKAWA wasiende mahakamani kesho kwa hati ya dharula kuweza pata ufafanuzi na order ya mahakama kwenye jambo hili?

Nia ni kuepusha damu za Watanzania kumwagika maana ninavyoona, tunakoelekea sio kuzuri ifikapo tarehe 25 Oktoba.

Nawakilisha.

104.-(1) No person shall, within any buildings where; voting in anelection is in progress or at any place within the radius or two hundredmeters of any such building, wear or display any card, symbol, favour orother emblem indicating support for a particular candidate in the election.(2) Any person acting in contravention of this section shall be guiltyof an offence and shall be liable on conviction to a fine not exceeding twohundred shillings.
 
Tutasubiri matokeo ya kituo husika na sio ya nchi nzima mkuu....kwan watahesabu wiki nzima kituo kimoja??

Mwaka Huu,pombe Ya Siasa Kweli Imewalevya Watu..
Sasa Mkuu Matokeo Si Jioni Lakini?Iweje Wewe Upige Kura Saa 1 Halafu Usubiri Hadi Saa 10,wakati Unaweza Kwenda Na Kurudi Muda Muafaka Wa Matokeo Kutangazwa Au Wakati Wanahesabu Kura?
 
Mnajihis tu unazan ccm wao hawawez kuibiwa kura? Mme kalili kuibiwa kura za ukawa tu ondoen akili za kijinga kias hiko "piga kura kisha nenda lwenu
 
NIMEPOKEA NCHI MIKONONI MWA RAIS WA CCM LAZIMAAAA NIIKABIDHI KWA RAIS WA CCM. Napata mashaka na huyu mtu kwamba hata kura zctoshe lazma. naunganisha na goal la mkono!!!!!
 
Well, sasa wewe mtu wa UKAWA ukitaka kubaki kulinda kura yako (presumably haumwamini mtu yeyote au unaona wakala wako hana nguvu), na CCM nao na ACT nao wabaki unadhani hapo nje ya kituo PATATOSHA?

Patatosha. And by the way, hatutakuwa tumevaa jezi za vyama vyetu maana ni kosa kisheria. Na naturally, si kila mtu atabaki. lakini ni lazima wabaki watu wa kutosha kuhakikisha vituo vinakuwa free of intrusion by "caterers" wanaoleta kura kwenye "hot-pots" za "chakula" na chupa za chai!
 
wana UKAWA wote tuamke mapema zaidi.. ili tupige KURA mapema. halafu saa 10 jion tuwahi kurudi kupata matokeo vituoni tulikopigia KURA.
 
No person can be punished by the law except for breach of the law. Any declaration that contravens the law is illegal. We have the rule of law not the rule of men because man can be arbitrary and abuse his powers for his/her own interest. Just comply to the law and your safe.
 
Hivi nyie mnaowaza kuibiwa kura, mawakala wenu wanafanya kazi gan ndan ya kituo


mkuu hata mi nawashngaa hawa jamaaa, sasa kila mfuasi wa chama akibaki kituoni si kutakuwa na VURUGU...

Yaani hawa jamaa pamoja na kuwa na mawakala wao bado wanawaza kuibiwa tu
 
Aiseeh lakini wanasiasa hasa ccm. Hivi mtu akipiga kura then akakaa hizo mita 100 akasubiria matokeo yakatangazwa halali akashangilia akaenda kwake kuna shida gani!
 
Back
Top Bottom