Acheni uhuni wenu.kila mtu akibaki kituoni itakuwa fujo.wewe huelewi nini!
Nani ataleta fujo zaidi ya wale wenye mazoea na nia ya kuvunja sheria?
Lini watanzania walipokusanyika walifanyiana fujo kama si ccm wanaojiweka juu ya sheria?
Mipirani, misibani, makazini, nyumba za ibada, masokoni, kwenye vyombo vya usafiri n.k Watanzania wamkuwa wakikutana na kuhitimisha shughuli zao kwa amani bila fujo pamoja na tofauti zao za kivyama. Inakuwaje kwenye ushindi na upatikanaji wa viongozi wao watakaoshinda kwa wingi wakura wakatazwe kukutanika kwamba watafanyiana fujo?
Hiyo amri ya watu kutokukusanyika paomja itaendlea hadi miaka mitano ya utawala huo itakapokwisha? Kwa nini muone hatari ipo tu siku ya uchaguzi?
Ninashauri nguvu ambayo Kinana, Lubuva na Kikwete wamepanga kuitumia kuua wapinzani, (kama wanaamini kwamba vita haina macho na wao ni marehemu wtarajiwa), itumike kuwalinda hao wanaokaa mita 200 ili wakae kwa amani pasiwe na fujo. Na hao waliopangwa kutuua, wahakikishe tunasubiri matokeo na kushangilia kwa amani baada ya matangazo.
Kifo ni mara moa na watu wote nao watakufa ila huwa tunatangulizana. Ninaamini nikiuawa na kikwete, kinana na lubuva kwa sababu ya kusimamia shsria za nchi ambazo wao wamekuwa wakitamani nchi hii isiwe na sheria kabisa, nitakufa kifo cha kishujaa. Lakini hao kina kikwete, kinana, lubuva na mangu, nao watakufa siku moja. Watakufa kifo cha aina gani, Mungu anajua. Acha watuuwe kwakuwa wameamua sasa kutuua hadharani.
Labda watatuua kwa mabomu ama silaha sumu. Ninadhani gas ya sumu itawarahishia kwa kuwa tuko wengi.