UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

UKAWA nendeni Mahakamani kesho 15/10/2015

Uko sahihi kabisa Mkuu. Ni vema UKAWA wachukue hatua sasa kabla hawajachelewa.

Mimi nakuunga mkono ila ninavyowaelewa ukawa wanaweza kuzembea jambo hilo hadi mwisho na likaleta maafa hiyo tarehe 25/10/'15. Jambo la kupuuzia mambo kwa viongozi wa ukawa niliuona wakati wa uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani uliohusisha kuachiana majimbo kwa vyama washirika . Kwa uzembe tu lilipojitokeza tatizo la wagombea wawili wawili kujitokeza kwenye baadhi ya majimbo na kata viongozi wa juu walingangana tu makao makuu badala ya kwenda kutatua migogoro hiyo kuepusha kugawa kura na kuruhusu ccm kushinda. Hakika hili litawagharimu sana ukawa kwa kukosa majimbo.Maovu yanayoweza kufanywa na ccm wakiachwa wenyewe ni mengi na haitakuwa mara yao ya kwanza kufanya mbinu chafu kwa lengo la kukibakiza chama na serikali yake madarakani.Chaguzi za nyuma zote zilizohusisha upinzani zinaonyesha hivyo. Vinginevyo huo ushindi utapokonywa wazi wazi.
 
Umeshaambiwa piga kura sepa unalinda kura kwani wewe ni wakara sasa mjifanye wabishi upige kura ukae kituoni uone kitakacho kutokea unavunjwa miguu unasekwa ndani tii sheria bila shuruti vinginevyo utaona vyombo vyadola vinavyo fanya kazi yake

We ma.vi!! id yako ni wakulichomeka au ni wakulichomekewa?
 
Last edited by a moderator:
wana UKAWA wote tuamke mapema zaidi.. ili tupige KURA mapema. halafu saa 10 jion tuwahi kurudi kupata matokeo vituoni tulikopigia KURA.

Sasa kurudi kwako saa kumi jioni kwa lengo la kuyajua tu matokeo huku mamluki wameshavamia kituo na kuingiza kura haramu au wameshamtoa nje ya chumba cha kura wakala wako na kufanya yao inakusaidia nini? Inatakiwa hata kama ni kula mnaenda wachache na kuwaacha wengi wakilinda mamluki kuingia vituoni na kupenyeza kura zao nanyi mnarudi fasta wenzenu nao waende.Mara ngapi magari haswa haya tinted yanaingia vituoni na mabaunsa na kutoa vipigo kwa wakala mwenye msimamo au kuwashawishi kwa rushwa na wakikataa wanapata vipondo? Sheria ya uchaguzi iliyopo vitabuni ni kwa mpiga kura kuwa umbali wa mita mia mbili toka kituoni na viongozi wa ukawa wanatakiwa wakafungue haraka malalamiko mahakama kuu tena chini ya sheria ya dharura kuhusu wapiga kura na wanachama wao kutishiwa na wasioruhusiwa kutafsiri sheria.
 
SIO KWELI, Kukaa mita 100, au 200 au 350 ni UVUNJAJI WA SHERIA! tafuta ukweli na ukweli utakuweka huru.

Ukweli na katiba/sheria ni vitu viwili tofauti. Nakuuliza tena sheria inayosimamia uchaguzi inasema watu wakae umbali gani baada ya kupiga kura?
 



mkuu hata mi nawashngaa hawa jamaaa, sasa kila mfuasi wa chama akibaki kituoni si kutakuwa na VURUGU...

Yaani hawa jamaa pamoja na kuwa na mawakala wao bado wanawaza kuibiwa tu

Sheria inayosimamia uchaguzi ndivyo inayosema, haijalishi nani atashangaa. Iko wazi kabisa, ukishamaliza kupiga kura ondoka eneo hilo na ukae umbali wa 100M utakapoamua kwenda ni juu yako ilimradi usogee huo umbali na usivunje sheria. Hawa wanasheria wanaosema ukishapiga kura nenda nyumbani wanayatoa wapi? Nakubali ni ushauri mzuri lakini waweke wazi kwamba hayo ni mapendekezo yao na sio sheria, tena wasisitize atakae kaa huo umbali uliotajwa havunji sheria.
 
Nasema watakaobaki vituoni baada ya kupiga kura na wapigwe virungu!

Hakuna haja ya kupiga watu.....elimu....elimu...elimu.Waelimishwe na wata elewa tu.kwani ukiwapiga na wao wakarudishia yanatokea MAPIGANO na huenda vifo vikatokea na baada ya hapo uhasama wa milele na mahakamani
 
Ukweli na katiba/sheria ni vitu viwili tofauti. Nakuuliza tena sheria inayosimamia uchaguzi inasema watu wakae umbali gani baada ya kupiga kura?

kisheria hautakiwi ubaki eneo la kupigia kura baada ya kupiga kura. ni kipindi cha "tension" kwahiyo ni bora kukaa mbali.

miaka iliyopita watu walishauri baada ya kura watu wabaki ndani ya nyumba mpaka matokeo yatoke.
 
Mode funga hii thread. Imeshapitwa na matukio. Kesi iko mahakamani. Unajaza quota ya JF bure.
 
Sio suala la kumwamini wakala au kutomwamini, sheria ya uchaguzi inasemaje baada ya kupiga kura, kama inaruhusu watu kukaa umbali usiopungua mita 100, hao wanaozuia wanatumia kigezo gani?

katika kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura Na. 343 kinasema nanukuu


“Hakuna mtu atakayefanya Mkutano siku ya kupiga kura au; ndani ya jengo lolote ambamo upigaji kura katika uchaguziunaendelea, au mahali popote ndani ya eneo la mita miambili yajingo hilo, kuvaa au kuonyesha kadi ya picha yoyote, upendeleoau nembo nyingine inayoonesha kuunga mkono mgombea Fulanikatika uchaguzi”


Mwisho wa kunukuu.


Aidha, kifungu cha 103 (1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali zaMitaa, Sura ya 292 kinasema, Nanukuu:


“hakuna mtu atakayeruhusiwa, katika jengo lolote ambalo upigajikura katika uchaguzi unaendelea, au njia yoyote inayotumiwa naumma ndani ya umbali wa mita mia tatu ya mlango wowote wakuingilia katika jengo, atavaa au kuonyesha kadi, upendeleo au 4 nembo yoyote inayoashiria kumuunga mkono mgombea Fulanikatika uchaguzi”

Mwisho wa kunukuu.
 
katika kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura Na. 343 kinasema nanukuu


“Hakuna mtu atakayefanya Mkutano siku ya kupiga kura au; ndani ya jengo lolote ambamo upigaji kura katika uchaguziunaendelea, au mahali popote ndani ya eneo la mita miambili yajingo hilo, kuvaa au kuonyesha kadi ya picha yoyote, upendeleoau nembo nyingine inayoonesha kuunga mkono mgombea Fulanikatika uchaguzi”


Mwisho wa kunukuu.


Aidha, kifungu cha 103 (1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali zaMitaa, Sura ya 292 kinasema, Nanukuu:


“hakuna mtu atakayeruhusiwa, katika jengo lolote ambalo upigajikura katika uchaguzi unaendelea, au njia yoyote inayotumiwa naumma ndani ya umbali wa mita mia tatu ya mlango wowote wakuingilia katika jengo, atavaa au kuonyesha kadi, upendeleo au 4 nembo yoyote inayoashiria kumuunga mkono mgombea Fulanikatika uchaguzi”

Mwisho wa kunukuu.

Mkuu, kwani kwa wengi wetu ni mara ya kwanza tunapiga kura? Watu wanajivua tu ufahamu!
 
Back
Top Bottom