Haya yote yanatokea ni kwasababu ya utawala na uongozi wa nchi mbovu. Kama mafisadi wangethibitiwa kuibia nchi yetu tungetumia rasilimali zetu kuwasomesha watoto wetu bure na ajira ingepatikana na hao vijana wanaokwapua simu na kwenda kuuza ili wapate mlo mmoja wa siku wasingekuwepo!! Hivyo basi haya mabo ya vibaka yangepungua kwani mgawanyo wa maliasili ya Taifa ungekuwa equitable na tofauti ya matajili na maskini isingekuwa kubwa kama ilivyo sasa. Mbona wananchi hawaoneshi hasira kwa wale wanaotukwapulia mabilioni ya fedha kwa kusaini mikataba mibovu badala yake wanawaua wakwapua simu?