Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Mimi nilikuwa sijui kama usemalo ni kweli. Muhimu zaidi GANGA yajayo kusudi makabila yote yajazane ofisini.
 
sioni tatizo kwa wachaqgga kua na nafasi nyingi maofisini ukweli ni kwamba hata uende vyuoni wachaga ni wengi ii inaonyesha kua wanasoma na kwa sasa wachaga katika vyuo vya elimu ya juu wanawazidi hata wahaya katika nafasi ya pili, wanyakyusa wa tatu na watu wa kanda ya ziwa wa nne uo ndio ukweli!

kwa iyo wao wanajali sana elimu hasa wazazi wa kichaga wanpeleka wattoto wao shule makini kwa garama yoyote ile na iyo ni rasha rasha tu kwa idadi yao katika vyuo vya elimu ya juu hali itakua ngumu sana kwa makabila mengine huko mbeleni hasahasa wenzetu wa pwani watalia sana faulo play ila ukweli ndio uo.

mimi binafsi si wa makabila hayo ila na wa admire hasa wazazi wao jinsi walivyo willing kwenda extra mile ku fund elimu za watoto wao na pia wanakua wana akili binafsi mwaka niliomaliza pale mlimani walikua wengi sana na walikua wanauwezo mzuri huwezi watuhumu kua wako pale kwa upendeleo
 
Tukipita kila ofisi serikalini,binafsi,uwiiiii
wachaga tena wako post za juu jamani
inatia moyo lakini ndugu zetu tuwaachie na wengine naona watu wameanza kukasirika najua tofauti za shule ndio sababu basi msisome sana wengine tuingie huko.....wasije wakawalalia bagamoyo dunia mbaya hii..
Wakwe mmenisikia lakini

nimecheka basi,tubanane nao tuu na tukaze musuli tutafika

tena wewe thibitisha 1.makampuni ya BIA almost yote top officers utacheka.

ila nilipo mboni hawako kiivo wamejaza akina nanihii waleeee wengine wale
kila kilicho juu kilianzia chini!!
 
Hizi sentiments za kibaguzi ndio zimetufikisha hapa tulipo. Tunaelekea soko la pomoja, muungano wa sarafu na mwisho shirikisho, kama tunaelekea miaka 50 ya uhuru, wewe bado unalia na Wachagga, hao Wakenya, Waganda, Warundi nk wakiingia, si kabila lako mtaishia kuwa ma housegirls na mashamba boi!.

Dawa sio kuwaambia Wachagga wapunguze kusoma, dawa ni wewe na kabila lako msome kuliko Wachagga muwapite na kushika hizo posti za juu.

Tukiikubali hii ya Wachagga, watafuatia Wahaya, kwanini Mshomile sana, tutawafuata Wanyakyusa mwisho hadi Iringa kwa nini inaogoza kuexport ma TX wa ndani etc, etc.

Huu ni ubaguzi tuu, hauna sura, ni dhambi sawasawa na kula nyama za watu!.

asante sana umejibu hili kwa ufasaha!!
tuko njiani na karibia tunafika
 
Jamani Jamani Jamani ! Nadhani inabidi tukumbushane tulipotoka.

Back in Memory Lane............(Nyerere's Voice)

"Vinchi vidogo, vidogo hivi .. ...,
Vya watu 27 million.....,
Tunazungumza Makabila ! (silence and uproar)...,
Tunazungumza lugha ya Makabila !...
Mtuingize katika karne ya 21, Mnapanda basi la Makabila !.."

Youtube clip :


B.P 2010
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka jitihada alizofanya baba yangu mzazi kutupatia elimu ktk family yetu naelewa sasa wengi wanachosema kuwa wazee wa kichaga wanathamini sana elimu. Ilimgharimu kula mchicha chukuchuku angalau wanawe wafike F4. Aliuza ng'ombe, miti, alikopa fedha wanawe wasome. Baada ya kuzunguka sehemu mbalimbali tz nimegundua kuwa hii spirit ni adimu sana sana kwa makabila mengine.

Nilipokuwa Versity nilishangaa jinsi ambavyo wachaga walikuwa wanawapeleka puta wenzao watokao makabila mengine. Kwanza, tulipoingia 1st yr, zile kozi za computer wao waliona kama kumfundisha mwanafunzi wa F4 kuhesabu a, e, i, o, u. Ndugu zao, wajomba, shangazi, wazazi wao wana mwanga wa elimu tayari, wengine wana computer nyumbani hata zaidi ya moja. Wakati wewe unajifunza kushika mouse mwenzako yuko mbaaaali kweli kweli.

Swala si kusoma tu darasani na kuwa na cheti, exposure ina nafasi kubwa sana sana. Kama dada yangu ni mhasibu, ni rahisi kunishawishi nisome uhasibu, kwani anafahamu mtandao wa kupata kazi. Huwezi kulinganisha na jamaa ya Mwanafunzi ambaye yeye ndiye msomi kwenye familia yao na hakupata ushauri nasaha kabla ya kuchagua kozi ya kusoma. Kuwa na mtandao ni kitu muhimu sana haswa ktk dunia hii ya utandawazi. Swala si upendeleo tu, ingawa siwezi kupinga moja kwa moja kuwa upo, bali kuwa na taarifa sahihi hilo nalo ni jambo la msingi sana.

Kabla ya kusema kuna upendeleo fanya uchunguzi kwanza ya mazingira yote yanayoruhusu kabila moja liwe dominance.
 
ETI NINI...? MNASEMA WAMESOMA...? NA WANASIFA KUWAZIDI WENGINE......?
haya majajiji wa JF AMUENI....! CHIEF WA TANROADS AITWAYE MREMA......! ANA SIFA STAHILI....?
 
NGOOJA NGOOJA! FANYA UTAFITI. MREMA SI MCHAGGA. Mnashangaa? Ni mtu wa Arusha. Fanyeni utafiti tafadhali.
ETI NINI...? MNASEMA WAMESOMA...? NA WANASIFA KUWAZIDI WENGINE......?
haya majajiji wa JF AMUENI....! CHIEF WA TANROADS AITWAYE MREMA......! ANA SIFA STAHILI....?
 
Hawa wachagga ndio waliotufikisha hapa tulipo wachoyo,wapenda mali kuliko uzalendo hawa ndio walio pewa mashirika wakayazika mbele za uso wetu angalia walipokuja kushika tanesco,Bima,Benki ya Taifa,Mbuga za wanyama,Uvuvi,misitu,madini,kilimo hawafai kabisa kusogezwa mahari popote ndio walio wengi katika nafasi za TRA unaona mwenyewe misamaha ya kodi inavyo jitokeza ndio wezi wakuu wa viwanja vya wazi wachafuzi wakubwa wa mazingira makontena mijini biashara za barabarani mioto na uchafu mwingi mwingi ni wao ni sawa na mafia hawa
 
Benk ya crdb mwanza waliifilisi wao sasa pesa za epa zote zilipita crdb wakati benki zinazoongozwa na wazungu walikataa pesa hizo hawafai wachaga kabisa katika vyanzo vya fedha
 
tatizo siyo wachaga nk...tatizo ni mtu kutokuwepo kwenye mtandao unaoongoza nchi. kwa bahati hao ndg wamefanikiwa kuwa katika mtandao wa viongozi na ndg zao. kwa mfano mashirika mengi yamejaa watoto wa wakubwa kwa kigezo hicho cha kusoma. ukweli ni kwamba kuna tabaka la wakubwa na vizazi vyao ndio watakaopata kazi nzuri mpaka atakapotokea nabii fulani kutuokoa. meanwhile tuendelee kuvumilia tu au uchukue chako mapema.
 
Kuwepo au kutokuwepo kwa Ukabila kunatoka na mwamko wa Elimu katika mikoa Tajwa......Chukua mfano mdogo K'Njaro kuna VYUO VIKUU vifuatavyo 1.Muccobs 2.Mwenge 3.Kcmc 4. Masoka na Vyo vya ualimu vya kutosha tu mabavyo ukivijumlisha unapata idadi inakua less or Equal na shule za SEKONDARI mkoa wa KIGOMA....Huko huko atokako kaka yangu mbunge Machachari ZK.....Sasa hapo tutegemee nini??????
 
Hawa wachagga ndio waliotufikisha hapa tulipo wachoyo,wapenda mali kuliko uzalendo hawa ndio walio pewa mashirika wakayazika mbele za uso wetu angalia walipokuja kushika tanesco,Bima,Benki ya Taifa,Mbuga za wanyama,Uvuvi,misitu,madini,kilimo hawafai kabisa kusogezwa mahari popote ndio walio wengi katika nafasi za TRA unaona mwenyewe misamaha ya kodi inavyo jitokeza ndio wezi wakuu wa viwanja vya wazi wachafuzi wakubwa wa mazingira makontena mijini biashara za barabarani mioto na uchafu mwingi mwingi ni wao ni sawa na mafia hawa

Bima ilijaa Wanyakyusa ilipokuwa inaongozwa na Nsekela na Mwaikambo. Matatizo ya Bima yalianza miaka hiyo. Kwahiyo usiwalaumu Wachaga.

Pia kuhusu hawa Wanyakyusa, tunazungumzia kabila gani? Tunazungumzia pia Waluguru na Wapogoro ambao ni ndugu zao? Wanyakyusa walitoka Morogoro na nimesikia kwamba wengi wao hata leo kule Rungwe na Mbeya wanajiita Walugulu. Wengine wanasema ni Wapogolo (nimeambiwa hakuna herufi ya "r" katika lugha ya Kinyakyusa). Lakini pia wanajiita Wanyakyusa ingawa wanasema ni Walugulu na Wapogolo. Ebu nifafanulie hapa. Hata leo kuna Wanyakyusa wengi sehemu za Morogoro ingawa wengi wao walihamia kusini magharibi sehemu za Rungwe na Malawi labda karne nyingi zilzopita.
 
Nilikuwa sijachangia hii topic ingawa nimeiona siku nyingi. Ni kweli wachaga wamesoma lakini ukabila wanaufanya pale penye maslahi, mfano vyeo na nafasi nyingine, hili liko wazi zaidi na hili lilifikia kileleni enzi kwenye utawala wa Mkapa.

Na kama wasingefanya, nobody would have noticed them given ukubwa na nchi hii na makabila yalivyokuwa mengi na diversity na balancing Mwalimu aliyoifanya hasa kwa kusomesha kila kabila bila ubaguzi.

Lakini pia, kila utawala nchi hii, ukiondoa awamu ya kwanza, unakuja na upuuzi wake wa kibaguzi, kwa mfano, awamu ya sasa ni uislamu, hata vibonde kibao wanapata kazi nyeti zinazohitaji umahiri na utendaji demanding kwa misingi ya udini..

HII NDIYO REGIME TULIYOMO, lakini je tutendelea hivyo mpaka lini. Wote hao wana-take advantage ya makabila madogo kama la kwangu na mengine makubwa ambayo hayakubahatika kupelekewa shule za wamisionari. Now, is that Tanzania we need, ndivyo Mwalimu alikuwa akifanya? Tunachezea shilingi ******, ndicho ninachokiona..it may not last forever.

Kila tunapo-deviate kwenye misingi ya Mwalimu, i see a potential danger. Tusidhani sisi ni invicible wa machafuko, nono..ni suala la muda, this country may be up in flames before we know it! Let's not open pandora's box as we will pay dearly! Kina Rwanda na wengine tunaowacheka, inaweza kuwa zamu yao kutucheka!
 
tuipendenchiyetu, karibu na tunafurahi kuwa umeweza hatimaye kuamua kuchangia badala ya kuwa mtazamaji tu.

a. Katika maendeleo yote ya elimu hadi hivi sasa, Makabila hayo yamerudi nyuma au yameendelea mbele?

b. Ili kuweza kufikia uwiano, je tuamue kuyafunga breki, kwa mfano kusitisha kwa miaka mitano kuchukua wanafunzi wa elimu ya juu toka makabila hayo?

c. Tukiamua kufanya hivyo, tuhakikishe kuwa hawaendi kusoma nje ya nchi pia kwa muda huo?

d. Je, tunapopokea CV ya mtu au kumchagua mtu tukiona jina la "Kagaruki", "Mwakipesile" au "Lyimo" tuwaengue moja kwa moja?

e. Kwenye ofisi ambazo zimejaa watu wa makabila hayo tuzipangue na kuwaaingiza watu wa makabila mengine ilimradi isionekane wamejaa watu wa kabila moja?

f. Tukishaanza kufanya hivyo na tukagundua kuwa watu warefu ndio wengi zaidi, tuanze kuhakikisha watu wafupi nao wanaingizwa? tukifanya hivyo tukagundua kuwa wengi wanaofanya kazi maofisini wanatumia mikono ya kulia, tuanze kutafuta watumiaji wa mikono ya kushoto? na tukimaliza hivyo na kugundua kuwa wengi waliojariwa ni wanaume, tuwapunguze ili tuongeze wanawake? Tukishamaliza hivyo na kugundua kuwa wanawake wengi waliojariwa ni waislamu, tuwaombe wastaafu ili wawapishe wakristu? tukifanya hivyo na kugundua kuwa wakristo hao wengi ni wakatoliki tuwatake wawamegee nafasi hizo waprotestanti?.. ni jinsi gani tutasitisha zoezi hilo la kibaguzi?


Baelezeeeeeeee MM, nami kesho ntabaelezeapo
 
Mwanakijiji asante sana kwa maelezo yako marefu, mazuri na yenye kusisimua, but kwa kiasi fulani hapo niko kinyume kidogo na wewe kwa jinsi unavyojaribi kupinga kwa nguvu zote kuwa hakuna ukabila. Ukabila upo kwenye taasisi nyingi za serikali na unakuwa tena kwa kasi ya ajabu tukatae au tukubali lakini huo ndiyo ukweli.

Nakubaliana na wewe kuwa hayo makabila matatu ndiyo yaliyotangula kwenda shule na kuelimika, lakini kwa sasa kuna makabila mengi hata wazaramo wengi wameenda shule na kuelimika vizuri, lakini kilichopo sasa hivi ni kuwa haya makabila matatu kwa kuwa walitangulia kwenda shule na kushika nafasi nyingi kubwa na nyeti, imekuwa ni rahisi sana kwao kuwavuta wakwao hata kama wanasifa pungufu kuliko makabila mengine. Hiyo yote ni kwa kuwa wao ndiyo wenye mamlaka ya kuajiri pia.

Mwanakijiji wewe uko marekani japo kuwa uko karibu sana na media za bongo na kufanya utafiti mwingi but yanayoendelea ndani ya hizo taasisi sidhani kama unayafahamu kiundani zaidi. Nashauri tuache ushabiki bali twende na ukweli halisi.
 
samvulechole... hakuna hoja ambayo ni ngeni hapa.. madai ya makabila hayo kupendelewa hayakuanza leo! tangu mara tu baada ya uhuru kulikuwa na tuhuma hizo hizo.. so.. there is nothing there..! Hata hivyo hatari unayoweza kuleta siyo ukabila bali ubaguzi, kuwa kama mtu anatoka kwenye makabila hayo basi asipewe nafasi fulani kwa vile watu fulani wanadhani kuna ukabila! Nitakupa mfano, kuna wanasheria watatu wote ni maprofesa... kuna Prof. Mwakalindile (Sheria, uzoefu miaka 30), Prof. Mtimba (mmakua, uzoefu miaka 10, sheria), na Prof. Chanda (Mzigua, sheria uzoefu miaka 5). Assuming maeneo ya fani zao ni sawa, ceteris paribus Rais anataka kumteua mshauri wa kisheria.. nani apewe kwa haki? Wengi watasema prof. Mwakalindile! Sasa kwa kufanya hivyo hata hivyo kuna wanyakyusa wawili tayari hapo ikulu ambao wameshapata nafasi zao, je tumnyime Mwakalindile kwa vile itaonesha ukabila?

Kabla hatujafikia hapo pa kudai ukabila tujiulize: "Kwanini inaonekana kuna wasomi wengi wa makabila hayo matatu Wachaga, Wahaya, na Wanyakyusa"? Je, tupunguze wanafunzi wanaotoka kwenye makabila hayo na kuwapa nafasi watu wa makabila mengine ili kuleta uwiano (parity)? Je tukiamua kufanya hivyo hatutakuwa tunaanza ubaguzi wa kikabila?

Tarehe 9 Disemba 1968 Nyerere alitumia siku ya Jamhuri kuzungumzia "Vitu ambavyo ni lazima Tuvisahihishe", vitu ambavyo baada ya uhuru havikwenda vilivyotarajiwa. Alizungumzia ukabila; kwanza alisema hivi:

"the man who talks about tribalism being practised without having any evidence for his statement is often a man who wants to stir up tribalism. Even if that is not his purpose, the result can be just the same. People will begin to think that there is tribalism, and, once people begin to think in these terms, then tribalism has begun to enter tinto our society"

Kuhusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachaga kupata nafasi nyingi katika serikali, Mwalimu alisema hivi miaka karibu 30 iliyopita:

"..the work of the civil servants and people in the parastatal organizations does require education..it so happened that the Tanzanians who had the opportunity for higher education under the colonialists were mostly Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa. And because most of the education was provided by missionaries, most of these people are also Christians. That was our inheritance. These conditions will change, but they have not changed yet. And for these reasons, when we get rid of the Europeans who were doing responsible jobs, and give these jobs to Tanzanians, the people who get them come mostly from one or other of these three tribes".

Akaongeza pia,

"Therefore, if you ask me why Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa have most of the jobs which require higher education, the answer is very obvious. They were the ones who received higher education during colonial times. I'd say: investigate the position in politics where a man is not asked about his educational qualifications. Look at the Parliament, the National Executive and Central Committee of TANU, and at the Cabinet. How many Wanyakyusa, Wahaya, or Wachagga are members? You will find that perhaps there aren't any, or there are one or two. This is the truth"

kwa umahiri wake wa maneno JKN akatoboa ukweli huu

"Anyone who refuses to accept a very obvious truth like this, and says that the reason is tribalism, must provide us with the evidence for his statement. If he cannot provide any evidence, we must conclude either that he is a fool, or that he is strirring up tribalism deliberately. He is the sort of (a) person who begs work on a tribal basis, and when he is refused because he does not have the capabilities, he pretends he was refused on tribal grounds."

Akasema pia ni jukumu la serikali kusaidia sehemu ambazo bado ziko nyuma kielimu. Na alimaliza kwa kusema:

".. if a Mchagga, a Mhaya, or a Mnyakyusayoung man were refused work simply because of his tribe - when he is capable and there is no other Tanzanian with the qualifications - then we would be practising a very stupid and very evil kind of tribalism such as that which caused the establishment of Biafra. I beg you, my brothers, avoid ANYTHING WHICH COULD BRING OUR COUNTRY INTO THIS KIND OF DISGRACE" (emphasis mine)
(From: Uhuru na Maendeleo pp 76,77)

so what say you?

asante kwa nukuu hizo hata asiyelewa akisoma nukuu za mwalimu zinajitosheleza. Tukisema enzi za mwalimu haaaaaaaaaa haziishi.
 
Najua hii topiki haitokuwa poplar na baadhi ya watu humu ndani na hata wenye website lakini potelea mbali

Je ni kweli wizara hizo zimejaa makabila ya Wachagga,Wanyakyusa na wahaya?

mimi nilikuwa siamini mpaka pale NILIPO ambiwa kuwa kuna UKABILA wa hali ya juuu kule Ikulu NA vile vile namba mbili kwa UKABILA ni TRA je kuna ukweli katika haya?

Japo kuna watu wanasema kuwa ni udini lakini sumu ambayo hatuko tayari hata kuijadili ni hii ya ukabila na ndio inayoturudisha nyuma je mnakubaliana nayo?




-JAMBO FORUMS WHERE WE DARE TALK OPENLY

Tupieni jicho na Tume ya Mawasiliano.
:smile-big:
 
Swali alilouliza Mwanakijiji bado halijajibiwa.

Ni kweli au ni uongo, Hakuna jibu la hili swali, so far!

Ila maoni yangu ni kwamba kama kuna wanaoona kwamba ni tatizo, na kwamba limewaathiri kwa kiasi fulani, wajitokeze, kwa sababu na vigezo na vielelezo ...; Mahakamani, vyombo vya habari .....

Nasema UWAZI, UWAZI UWAZI tu ndo unaweza kukomesha vitendo vya ubaguzi kama vipo na kuwafanya wanao-propagate hayo waone aibu. Siyo vya ukabila tu bali hata vya udini, jinsia, rangi, maumbile, - anything up-professional , (toa vielelezo) n. k.

Isije ikawa wapo wanaotaka awepo mtu wao ili "na sisi tule", au na sisi ni zamu yetu n. k.

Nafikiri kuna tabia pia ya kutojiamini na uwezo mdogo wa ku-network kati yetu WaTZ across mipaka hiyo ya kikabila na kidini n.k. Labda kwa sababu wengine tumekulia vijijini na inakuwa vigumu kuwazoea watu uliokutana nao ukubwani. Kwa wale waliozaliwa na kukulia mijini, hili swala la boundaries litakuwa dogo sana, unless kama wazazi wali-propagate huo upuuzi. Leo tunaona watu wanaoana across makabila, watoto wanaotokana nao watakuwa ni WaTZ tu!

Mungu Ibariki Tanzania!
 
Back
Top Bottom