The Best Of All Time
JF-Expert Member
- Aug 30, 2022
- 2,968
- 6,839
Kila nikiangalia nyuzi mbalimbali naona ukavu katika kila eneo la maisha ya mtu, ukavu kwenye mahusiano, ukavu kwenye suala la utafutaji wa pesa, wengine ni wagonjwa na wengine wamesongwa na msongo wa mawazo maishani mwao, hawaoni muelekeo. Wengi wanalia kwasababu ya usaliti katika mahusiano na ndoa.
Ila Daudi katika kitabu cha Zaburi asema hivi
Zaburi 107:35
[35]Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji,
Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
Ni muda sasa umkabidhi Mungu awe mshika usukani wa maisha yako, mahusiano yako , utafutaji wako na afya yako, na atageuza ukavu katika Kila eneo la maisha yako kuwa sehemu nyevu , yenye baraka, yenye furaha na amani. Mwamini Mungu, atakuletea mtu sahihi kwenye maisha yako, kazi sahihi na wazo sahihi ya jinsi ya kujikwamua kiuchumi. Usimwamini mwanadamu wala maneno wanayoandika humu ya kuwakatisha tamaa na kuwakejeli kama Daudi anayosema humu.
Zaburi 146:3
[3]Msiwatumainie wakuu,
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
Nawatakia Dominika njema.
Tumsifu Yesu Kristu.
Bwana Yesu asifiwe, watu wa Mungu.
Nawatakia Jumapili njema.
Ila Daudi katika kitabu cha Zaburi asema hivi
Zaburi 107:35
[35]Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji,
Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
Ni muda sasa umkabidhi Mungu awe mshika usukani wa maisha yako, mahusiano yako , utafutaji wako na afya yako, na atageuza ukavu katika Kila eneo la maisha yako kuwa sehemu nyevu , yenye baraka, yenye furaha na amani. Mwamini Mungu, atakuletea mtu sahihi kwenye maisha yako, kazi sahihi na wazo sahihi ya jinsi ya kujikwamua kiuchumi. Usimwamini mwanadamu wala maneno wanayoandika humu ya kuwakatisha tamaa na kuwakejeli kama Daudi anayosema humu.
Zaburi 146:3
[3]Msiwatumainie wakuu,
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
Nawatakia Dominika njema.
Tumsifu Yesu Kristu.
Bwana Yesu asifiwe, watu wa Mungu.
Nawatakia Jumapili njema.