Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Hatimaye shujaa wa Taifa hili, Tundu Lissu amewasili nyumbani Tanzania akiwa mzima wa afya, baada ya kutokuwepo hapa nchini kwa takribani miaka 3, akiwa nje ya nchi kwa matibabu ya majeraha makubwa sana aliyoyapata, takribani miaka 3 iliyopita, baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 16, zilizolengwa kwenye gari lake huko Dodoma na watu ambao wamebatizwa jina la "watu wasiojulikana"
waliokuwa na nia ya kumwuua.
Mapokezi makubwa sana aliyopokea shujaa huyo wa Taifa hili, hakika ni tukio la kihistoria.
Tumejionea maelfu kwa maelfu wakiusindikiza msafara huo wa shujaa wetu, tena bila ya ulinzi wowote wa Polisi, bila ya kusikia malalamiko yoyote toka kwa mwananchi yeyote ya kuibiwa kitu chake chochote au kujeruhiwa, katika muda wote wa masaa kadhaa ya msafara huo.
Tendo moja limethibitika katika ujio huo wa Tundu Lissu, kuwa wananchi wa Tanzania ni watu wapenda amani sana na hawana fujo wasipochokozwa na Jeshi la Polisi.
Kumbuka kuwa Jeshi la Polisi hapo awali lilipiga "mkwara mzito" kuwa ni marufuku kwa wananchi hao kwenda kumpokea mpendwa wao Tundu Lissu, ambaye wamem-miss mno, kwa kile walichodai kuwa kusanyiko hilo ni batili ambalo halijaombewa kibali kwao, kwa hiyo litaleta vurugu na kusababisha usalama wa watu hao kuwa shakani.
Tukumbuke pia wananchi wengi walikuwa na hamu mno ya kumwona shujaa wao amerudi akiwa mzima wa afya, baada ya kipindi cha takribani miaka 3 akiwa nje ya nchi kwa matibabu.
Kwa hiyo lilikuwa tegemeo la wananchi hao kuwa Jeshi hilo lisingepiga marufuku wananchi hao kwenda kumpokea huyo shujaa wao na badala yake Jeshi hilo liweke ulinzi kwenye msafara huo
Hata hivyo nilishukuru sana Jeshi hilo la Polisi, kwa kufanya uamuzi wa busara sana katika "dakika za majeruhi" kwa kuamua kutotumia nguvu kuwazuia wananchi hao walioamua wenyewe kwenda kumpokea mpendwa wao.
Ndipo hapo nikapata somo kuwa kumbe vurugu zote ambazo huwa tunaziona kwenye mikusanyiko yoyote huwa zinasababishwa na Jeshi hilo la Polisi kutaka kutumia nguvu kubwa ya kuzuia mikusanyiko hiyo ambayo ni wananchi hao huwa wanakuwa hawajavunja kipengele chochote cha Katiba ya nchi, kwa kuwa mikusanyiko ya wananchi inaruhisiwa kwa mujibu wa Katiba hiyo.
Mfano halisi ni namna Taifa hili lilivyompoteza mwanafunzi mdogo kabisa kwa umri, ambaye alikuwa hana hatia yoyote, Akwilina Akwiline, aliyepigwa risasi za moto na Polisi na kufa papo kwa papo wakati mmojawapo aliyekuwa miongoni ya Polisi hao waliokuja kuzima maandamano hayo ya amani ya wanachadema, kufyatua risasi "kizembe" miaka michache iliyopita wakati Jeshi hilo likitaka kuvunja maandamano hayo kwa nguvu, wakidai yalikuwa haramu na hayakuombewa kibali Polisi
Niwasihi Jeshi letu la Polisi watekeleze wajibu wao kwa weledi na kwa mujibu wa Katiba ya nchi na wasikubali kupokea maagizo haramu toka kwa watawala waliopo wa CCM.
Kwa kufanya hivyo ndivyo tutakavyoweza kudumisha amani na utulivu katika Taifa hili ambalo mara nyingi wanasiasa wetu wamekuwa wakiinadi nchi yetu kuwa ni "kisiwa" cha amani ambayo nchi yetu imejaaliwa.
Mungu ibariki Tanzania
waliokuwa na nia ya kumwuua.
Mapokezi makubwa sana aliyopokea shujaa huyo wa Taifa hili, hakika ni tukio la kihistoria.
Tumejionea maelfu kwa maelfu wakiusindikiza msafara huo wa shujaa wetu, tena bila ya ulinzi wowote wa Polisi, bila ya kusikia malalamiko yoyote toka kwa mwananchi yeyote ya kuibiwa kitu chake chochote au kujeruhiwa, katika muda wote wa masaa kadhaa ya msafara huo.
Tendo moja limethibitika katika ujio huo wa Tundu Lissu, kuwa wananchi wa Tanzania ni watu wapenda amani sana na hawana fujo wasipochokozwa na Jeshi la Polisi.
Kumbuka kuwa Jeshi la Polisi hapo awali lilipiga "mkwara mzito" kuwa ni marufuku kwa wananchi hao kwenda kumpokea mpendwa wao Tundu Lissu, ambaye wamem-miss mno, kwa kile walichodai kuwa kusanyiko hilo ni batili ambalo halijaombewa kibali kwao, kwa hiyo litaleta vurugu na kusababisha usalama wa watu hao kuwa shakani.
Tukumbuke pia wananchi wengi walikuwa na hamu mno ya kumwona shujaa wao amerudi akiwa mzima wa afya, baada ya kipindi cha takribani miaka 3 akiwa nje ya nchi kwa matibabu.
Kwa hiyo lilikuwa tegemeo la wananchi hao kuwa Jeshi hilo lisingepiga marufuku wananchi hao kwenda kumpokea huyo shujaa wao na badala yake Jeshi hilo liweke ulinzi kwenye msafara huo
Hata hivyo nilishukuru sana Jeshi hilo la Polisi, kwa kufanya uamuzi wa busara sana katika "dakika za majeruhi" kwa kuamua kutotumia nguvu kuwazuia wananchi hao walioamua wenyewe kwenda kumpokea mpendwa wao.
Ndipo hapo nikapata somo kuwa kumbe vurugu zote ambazo huwa tunaziona kwenye mikusanyiko yoyote huwa zinasababishwa na Jeshi hilo la Polisi kutaka kutumia nguvu kubwa ya kuzuia mikusanyiko hiyo ambayo ni wananchi hao huwa wanakuwa hawajavunja kipengele chochote cha Katiba ya nchi, kwa kuwa mikusanyiko ya wananchi inaruhisiwa kwa mujibu wa Katiba hiyo.
Mfano halisi ni namna Taifa hili lilivyompoteza mwanafunzi mdogo kabisa kwa umri, ambaye alikuwa hana hatia yoyote, Akwilina Akwiline, aliyepigwa risasi za moto na Polisi na kufa papo kwa papo wakati mmojawapo aliyekuwa miongoni ya Polisi hao waliokuja kuzima maandamano hayo ya amani ya wanachadema, kufyatua risasi "kizembe" miaka michache iliyopita wakati Jeshi hilo likitaka kuvunja maandamano hayo kwa nguvu, wakidai yalikuwa haramu na hayakuombewa kibali Polisi
Niwasihi Jeshi letu la Polisi watekeleze wajibu wao kwa weledi na kwa mujibu wa Katiba ya nchi na wasikubali kupokea maagizo haramu toka kwa watawala waliopo wa CCM.
Kwa kufanya hivyo ndivyo tutakavyoweza kudumisha amani na utulivu katika Taifa hili ambalo mara nyingi wanasiasa wetu wamekuwa wakiinadi nchi yetu kuwa ni "kisiwa" cha amani ambayo nchi yetu imejaaliwa.
Mungu ibariki Tanzania