Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Mkuu Field Marshall ES,

Asante sana kwa dataz toka chunguni. Na bila shaka utazidi kutujuza hapa jamvini.
Wengi wetu walikuwa wanafikiri CCJ ni feki lakini kwa sasa tumeweza kujua CCJ ni nini na kina lengo gani. Maneno ama majibu ya Msekwa kuhusu Mpendazoe kujitoa CCM kwa upande wangu nashindwa kumuelewa Msekwa na chama chake. CCM wanaona bora kuwa wanachama wengi wapumbavu na hawajali umakini ama umahiri wa mwanachama. CCM watake ama wasitake kuondoka kwa Mpendazoe ni pigo kubwa kwao tokana na ukweli kwamba tendo hilo limeonesha kwamba kuna mpasuko mkubwa ndani ya CCM na muda wowote toka sasa CCM inaweza kusambaratika.
 
Hivi hii ina uhusiano na kesi ya Muungwana kujifungia jioni mtaa wa Lumbumba?

Sina uhakika kama yana uhusiano wowote. Kwa maana nyingine kikao chao juzi sidhani kama hakuna lililoongelewa. Lazima walikuwa na taarifa na mengi yakajadiliwa.
 
Facts nilizozipata ni kwamba CCJ ni MNF na kundi la mtaa wa 6...
 
Ndo maana Makamba alipanic sana wakati anahojiwa na wapo radio jana na kutoa majibu ya ovyo ovyo sana.
Big up sana FMES kama umekubali chama hilo la CCJ mm natafuta kadi kwa udi na uvumba.
CCM tayari ni chama cha matajiri na maskini wa kutupwa ambao hawajui nn cha kufanya zaidi ya kuridhika na vikofia na flana za zidume fikra za mwenyekiti wa chama.
 
Mimi bado nina wasiwasi na ujio wa chama hiki yes it is for real in which sense even NCCR-Mageuzi was for real lakini baada ya muda mfupi ikawa si real tena nafikiri muda si mrefu tutajua CCJ is real for wananchi au for wale walio madarakani.
 
Mie binafsi nitaendelea kuwa mtazamaji wa sakatakwasababu habari za pande mbili zinanivutia. Mosi suala mpendazoe kwenda hicho chama zinaleta mtazamo wa kwamba hicho chama kiko serious na pili ubadhirifu wanaofanyiwa Pemba na Jana Dar unaleta maswali kuliko majibu but maswali yangu ni kwanini watu waanzilishi wa hicho chama wajifiche either watakuwa wanafiki au waoga wa ajira zao? Pili mbona viongoziwake hawajulikani? Mwisho mwelekeo wao wa nchi ni upi? Mie nitaendelea kukaa mbali nao tu hadi fmes na wenzie wakileta data zaidi
 
- According to the dataz, katika kikao kimoja cha NEC hivi karibuni, Spika aliuliza hivi kuhusu kamati ya Mwinyi, "eti kweli CCM tunataka kupatanisha jua na giza?"

- The more dataz ni kwamba CCJ ni matunda ya ishu moja tu, nayo ni mdudu Richimonduli, Mwenyekiti na CCM nzima wameambiwa time and time again kwenye vikao vyao, kwamba bila ya kuwashugulikia ipasavyo wahusika wa huyo mdudu kutakua na dharuba kali sana kwa chama I guess sasa ni point of no return!

Respect.


FMEs!
 
mkuu field marshall asante sana kwa dataz lakini naona ingekuwa vizuri hayo majina ya vigogo wanao husika na hiki chama au wenye mpango wa kuamia hiki chama ni vizuri ungeweka siri kwa sasa mpaka chama kitapo pata usajili kamili.

usije ukamwaga mchele tu kwenye kuku ukawafanya wenye nia mbaya na hiki chama wakapata mwanya wa kuwafanyia maovu hao vigogo watakao jiunga na hiki chama.
 
Mbona EPA hawaisemi? Kweli EPA ilikuwa KOKORO, waliingia wasiotaka na wanaotaka.

Anyway, kama Richmonduli itasaidia kuidhoofisha na hata kuiuwa CCM, itakuwa vema tu. Ila wote waliokula hela za EPA itabidi wasimame, wakiri na kuomba msamaha na hapo tuendelee kwa uwazi na ukweli hadi aje CCM mwingine maana "......that's the way life (love) goes......"
 
Ndo maana Makamba alipanic sana wakati anahojiwa na wapo radio jana na kutoa majibu ya ovyo ovyo sana.
Big up sana FMES kama umekubali chama hilo la CCJ mm natafuta kadi kwa udi na uvumba.CCM tayari ni chama cha matajiri na maskini wa kutupwa ambao hawajui nn cha kufanya zaidi ya kuridhika na vikofia na flana za zidume fikra za mwenyekiti wa chama.

Angalia bold hiyo Mkuu, kama unakipigia debe vile?? na mimi nafuata kadi mara moja Mkuuu
 
- Kwa all the tomasos ninaomba kusema hivi kwamba some of us hapa tunajaribu as much as we can kuhabarishana kwa kutumia dataz na codes na siku zote tunajaribu kuwa one step ahead of the game, wanaotupa hizi dataz believe me wanabeba a very high risk infact wengi wao simu zao ziko taped na hata zetu vile vile, sasa kuzunguka inatugharimu sana lakini tunajitolea kwa sababu we have committed ourself into this course,

- Naomba niamini kwamba tungependa sana kuweka kila kitu wazi hapa tena all the times, zamani tulikua tunaweka wazi kila kitu lakini sasa na wao wameshituka sana ndio maana siku hizi inakua vigumu sana, sasa ni suala la kuvumiliana ingawa mimi nilifkiri kidogo sio sawa na kutokua nacho kabisa yaani giza la totoro, na hasa either hapa au magazetini bongo,

- I understand kiu ya kila mmoja wetu kutaka kujua all, lakini ni lazima tuviheshimu vyanzo vyetu kwa kuangalia upepo always, halafu msi-underestimate wanaoingia hapa maana mkiwajua wengi hamtaamini, tafadhalini sana tuvumiliane sana kwenye hii ishu panapowezekana sawa pasipowezekana tusameheane, na sisi wengine tumeshapewa chanzo basi tujikite na kutafuta umalizo wa habari! Tuvumiliane jamani!

Respect.

FMEs!
 
Nshomile

Asante kwa maoni yako.

Mosi; Suala la Dr Slaa kuwa mwenyekiti wa CHADEMA au yoyote yule kushika nafasi hiyo kwa sasa tunapoelekea uchaguzi wa mwaka 2010 si kipaumbele kwa sasa kwa kuwa CHADEMA ilishafanya uchaguzi mwaka 2009 na kwa mujibu wa katiba uongozi huo utakaa kwa miaka mitano. Labda yatokee mambo tofauti kabisa ambayo hatuyaombei.

Pili; tuhuma ulizozitoa kuna dalili za matumizi mabaya ya fedha zinazomhusu Mbowe kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti ni vizuri ukazitolea maelezo ya zaida kwa kuzitaja bayana kwa vielelezo kama ambavyo CHADEMA na washirika wake walifanya tulipotoa orodha ya mafisadi: http://www.chadema.or.tz/tamko/tamko.php?id=16. Lakini zingatia kuwa kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA katibu mkuu ndiye muwajibikaji mkuu (Chief accounting officer) inapokuja suala la matumizi ya chama katika shughuli mbalimbali. Kwa kuzingatia hilo, hoja yako ya kwamba Mbowe awe katibu wakati huo huo unamtuhumu kuwa ameshindwa kusimamia fedha inajikanyaga wakati huo huo ukitaka Dr Slaa ambaye unamuamini kwa kusimamia fedha awe Mwenyekiti inajichanganya yenyewe

Tatu, kuhusu maoni yako ya kutaka Dr Slaa ateuliwe kuwa mgombea urais, nashukuru kwa maoni yako ambayo naomba nisiyatolee maoni. Ila naamini kwamba Dr Slaa akipita hapa atasoma maoni yako.

Kwa ujumla hoja yako kuu ni kutaka mabadiliko katika uongozi wa CHADEMA kama msingi wa CHADEMA kwenda mbele; naamini unaweza kuona kwa mifano kwamba toka uchaguzi wa CHADEMA ufanyike Septemba 2009 ni timu hii ya CHADEMA imeendelea kufanya kazi kwa pamoja na kwenda kwa wananchi vijijini kukijenga chama iwe ni kupitia operesheni Sangara ama njia nyingine mathalani wilaya zote za Tanga, wilaya zote za Dodoma na mikoa mingine na bado operesheni hizi zitaendelea maeneo mengine mpaka kieleweke.

Wakati CHADEMA inafanya hivyo, vitazame vyama vingine pia ndio unaweza kutoa hoja vilivyo kama CHADEMA inasonga mbele, inarudi nyuma au iko pale pale.

Baada ya kusema hayo, nisisitize kwamba sisi katika chama tuko wazi kupokea maoni na hoja zenye kujenga, na sio kupokea hoja tu; tunaomba kila mpenda demokrasia na maendeleo popote pale alipo kuchukua hatua ya kuwa sehemu ya mabadiliko anayotaka kuyaona.

Nawatakia mjadala mwema

JJ
mheshimiwa Mnyika hata MBOWE naye yupo hapa ungemwacha aje kujibu mwenyewe kama ulivyosema kwa SLAA.
 
mkuu field marshall asante sana kwa dataz lakini naona ingekuwa vizuri hayo majina ya vigogo wanao husika na hiki chama au wenye mpango wa kuamia hiki chama ni vizuri ungeweka siri kwa sasa mpaka chama kitapo pata usajili kamili.

usije ukamwaga mchele tu kwenye kuku ukawafanya wenye nia mbaya na hiki chama wakapata mwanya wa kuwafanyia maovu hao vigogo watakao jiunga na hiki chama.

- Hili lilishatokea tayari mkuu, infact hiki chama kiliunganishwa sana lile kongamano la Foundation, lakini kwenye kikao cha NEC kilichofuatia waliopakaziwa wakiongozwa na zero walimjia juu sana muungwana hadi ikabidi awaombe radhi na Makamba akaomba radhi kwa yale maneno yake kuhusu lile kongamano.

- Ahsante sana ndugu yangu, wewe unaona mbali sana wewe na kuna something unakijua, nimekusikia sana mkuu!

Respect.

FMEs!
 
Asiyejua maana haambiwi maana.Wewe subiri presidential nominee wao wakisajiliwa,Tanzania haitakuja kutosha siku hizo.

Asante mkuu lakini naona hunitendei haki. Kuuliza si ujinga bali ni katika kutaka kujua kwa lengo la kuwa pamoja katika mjadala huu.
 
Napinga mawazo yako kabisa CHADEMA ni chama cha kikabila [NGO ya Ndesamburo & Mtei] wala hakina ajenda ya kuwakomboa watanzania kuondokana na umaskini,maradhi na ujinga.Niambie ruzuku wanayopata CHADEMA imetumikaje kusaidia wananchi.Inajulikana ruzuku inatumika kulipa madeni hewa ya mwenyekiti,huu kama si ufisadi ni nini ?,tusijidai tunapigia kelele ufisadi ili hali tukipata nafasi tunaogelea kwenye ufisadi.



CHADEMA hakuna demokrasia kabisa chama kinaendeshwa kifamilia na kimekaa kama NGO zaidi kuliko chama cha siasa.Nakubali wapo baadhi ya viongozi wenye vipaji ndani ya CHADEMA lakini Bwana Mbowe si mmojawapo.
Najua wewe si mwanachama wa chadema wa shabiki wa chadema utakuwa una chama chako unachoshabikia kwa hiyo usitusemee kuhusu chama letu we hujui sisi wanachama wenyewe mbona tunaikubali sana chadema. take care
 
Asante mkuu lakini naona hunitendei haki. Kuuliza si ujinga bali ni katika kutaka kujua kwa lengo la kuwa pamoja katika mjadala huu.

mkuu field marshall asante sana kwa dataz lakini naona ingekuwa vizuri hayo majina ya vigogo wanao husika na hiki chama au wenye mpango wa kuamia hiki chama ni vizuri ungeweka siri kwa sasa mpaka chama kitapo pata usajili kamili.

usije ukamwaga mchele tu kwenye kuku ukawafanya wenye nia mbaya na hiki chama wakapata mwanya wa kuwafanyia maovu hao vigogo watakao jiunga na hiki chama.

Kidatu, nafikiri jibu kaandika Arsene Wenger. Kuandika jina la mtu kwa sasa ni hatari sana. Kuwa na subira na utamfahamu. Angalia na majibu ya Mzee FMes.
 
Back
Top Bottom