Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Ujio wa CCJ: Yote unayotaka kujua

Hata mimi niliiona hii kauli.Lakini si ya kutilia mashaka sana kwani maneno mengi aliyotumia yanashabihiana n maneno ya viongozi waCHADEMA yaani wale amabo ni WAPINZANI kweli.

CCJ ikitwa chama mbadala what is a big Deal?si hta CHADEMA ni chama mbadala?

Pia nadhani mantiki ya kujiita chama mbadala ni kuondoa ile dhana ya kwamba wapinzani ni wakosoaji tu bila kutoa solution mbadala

?????????
 
-mimi nilishatoa wazo hili tangu mwanzo.pia kama watazuiwa kushiriki uchaguzi mkuu basi wapange kuunga mkono harakati za CHADEMA kwani ndicho chama wanachoshabihiana nacho kimtazamo na kimalengo

Napinga mawazo yako kabisa CHADEMA ni chama cha kikabila [NGO ya Ndesamburo & Mtei] wala hakina ajenda ya kuwakomboa watanzania kuondokana na umaskini,maradhi na ujinga.Niambie ruzuku wanayopata CHADEMA imetumikaje kusaidia wananchi.Inajulikana ruzuku inatumika kulipa madeni hewa ya mwenyekiti,huu kama si ufisadi ni nini ?,tusijidai tunapigia kelele ufisadi ili hali tukipata nafasi tunaogelea kwenye ufisadi.

Mkuu,thanks

Ila umetumia nguvu nyingi sana kutoa hii hoja,si hatari namna hiyo ndugu

Hapana sijatumia nguvu nyingi,nabonyeza key board tu mkuu wangu,ila sipendi kuona watanzania wakidanganywa tena na CHADEMA.

Nimependekeza CHADEMA kwa kuwa CHADEMA ni central party.Watawez kuungana na CHADEMA zaidi kuliko NCCRambao ni conservatives au kuliko TLP isiyo eleweka.

Vyama viko vingi sana kinachonikera ni kujaribu kuwadanganya watu kwamba CHADEMA tu ndio chama cha upinzani.Bungeni kuna UDP,CUF na CHADEMA ungesema washirikiane na vyama vyote vya upinzania ningekuelewa sana.Historia inaonyesha CHEDEMA haiko kabisa maeneo ya pwani kama ilivyo kwa CUF kule Bariadi wapo UDP wakiunganisha nguvu ya vyama vyote vya upinzani bila shaka wataweza kutupa watanzania kitu cha maana.

Ukifuatilia kwa umakini sera za CHADEMA na yale ambayo CHADEMA wamekuwa wakiyasimamia basi utaona hata wale watu waliojiunga na CCJ kama huyu Fred mpendazoe amekuwa inspired na vitailiyoasisiwa na wanachadema.Still naamini CHADEMA imekuwa na nguvu kubwa bungeni katika kuiwajibisha serikali na katika kutoa suluhisho mbadala la janga la uongozi wa Taifa letu

Ndiyo mana unaona hata CCM iliamua kuiga mambo mengi ya CHADEMA na kuyaweka ktk utekelezaji ingawa walitekeleza kw kufeli kwa kuwa waliiga vitu wasivyo na ujuzi navyo na hawaviamini moyoni mwao

Kuhusu Hoja ya Mbowe na Zitto,mbona basi Zitto alikubali na kuendelea kuwa ndani ya hicho chama?Hoja hii tu haiwezi kuzuia CCJ kuungana na CHADEMA ikiwa watazuiwa kushiriki uchaguzi mkuu ili kupanua wigo wa kuiwajibisha serikali bungeni

CHADEMA hakuna demokrasia kabisa chama kinaendeshwa kifamilia na kimekaa kama NGO zaidi kuliko chama cha siasa.Nakubali wapo baadhi ya viongozi wenye vipaji ndani ya CHADEMA lakini Bwana Mbowe si mmojawapo.
 
Mtu anaweza kuongea anachokiisi sawa kwake....kaongea kamaliza
 
Napinga mawazo yako kabisa CHADEMA ni chama cha kikabila [NGO ya Ndesamburo & Mtei] wala hakina ajenda ya kuwakomboa watanzania kuondokana na umaskini,maradhi na ujinga.Niambie ruzuku wanayopata CHADEMA imetumikaje kusaidia wananchi.Inajulikana ruzuku inatumika kulipa madeni hewa ya mwenyekiti,huu kama si ufisadi ni nini ?,tusijidai tunapigia kelele ufisadi ili hali tukipata nafasi tunaogelea kwenye ufisadi.



CHADEMA hakuna demokrasia kabisa chama kinaendeshwa kifamilia na kimekaa kama NGO zaidi kuliko chama cha siasa.Nakubali wapo baadhi ya viongozi wenye vipaji ndani ya CHADEMA lakini Bwana Mbowe si mmojawapo.

Ok,kumbe ugomvi wako ni wewe Vs mbowe sio?

Ofcourse,nikitoa mawazo una haki ya kuyapinga mkuu,mawazo yangu sio msahafu.Ila hebu jaribu kutunga hoja badala ya kurusha tuhuma tu bila uthibitisho.haya masuala ya NGO na family business yametolewa ufafanuzi sana ndugu yangu.Hata hivyo naona huna na hutoi fursa ya kueleweshwa

Bado nasimamia hoja yangu,kwamba CCJ wakae chini waunganishe nguvu na CHADEMA ikiwa watakataliwa kushiriki uchaguzi mkuu.CHADEMA ndicho chama chenye mwanga na ndicho chama chenye rekodi na experinece nzuri ya kupambana na ufisadi,na kupigania raslimali za Taifa hili
 
Jana wakati Mh. Fred Mpendazoe akitangaza kujitoa kwenye chama cha CCM alieleza kwamba, nukuu,

"CCJ siyo Chama cha Upinzani bali ni Chama Mbadala"

Nimejaribu kuitafakari kauli hii kwa makini lakini sijapata mantiki yake vizuri. Maswali ninayojiuliza bilas majibu ni haya:

1: Mpendazoe kusema hivyo anamaanisha kwamba vyama vya upinzani vilivyopo havifai au jina la "Upinzani" halifai?

2: CCJ itafanya mambo yanayolandana na ya CCM?

Wana JF mniweke wazi
Kuhusu neno upinzani, ni kweli limekuwa likitumiwa na CCM kwa propaganda chafu za kisiasa dhidi ya vyama mbadala.Mbadala linatoa ujumbe mzito kuwa kuna viongozi wengi wapambanaji na wanachama wa CCM watakikimbia chama hiki na kujiunga na CCJ na hivyo kukiimarisha na kuwa mbadala wa CCM. Ni ujumbe unaoashiria kudhoofika kwa CCM kisiasa na nafasi yake kuchukuliwa na CCJ.
 
CCJ wasikurupuke kama NCCR walivyofanya 1995, wafanye maandalizi vizuri ili chama kipate msingi wa kueleweka.

Iwapo watategemea opportunist wanaotoka CCM baada ya kukosa nafasi watajikuta wanafulia baada ya kipindi kifupi sana.
I agree with you in a way. CCJ wasiwe na papara, wachuje vizuri safu yao ya uongozi. Hata katika ofisi zao wahakikishe wanaweka watu waadilifu ambao hawataona wamepata mahali pa kula. Pia wale watakaokuwa viongozi wa CCJ wawe tayari kuachia ngazi pale ambapo itaonekana wana dosari hizi na zile. Kwa maana nyingine wasiwe na uchu wa kutaka kuhodhi madaraka ndani ya chama. Wakifanya hivyo wanaweza wakajenga chama makini.
 
Not a big deal. Whatever a good wording might be, as long as you are not "ruling" you are the opposition, full stop. Go to any country in this world and that is the definition.
 
Itakuwa jambo jema ikiwa wapambanaji wa CCJ baada ya kujiengua kutoka CCM wakashirikiana katika uchaguzi 2010 ili kupata wabunge wengi. Washirikiane katika kampeni nchi nzima. Pia waachiane majimbo pale ambapo upande mmoja unanguvu kuliko mwingine. Kwa hiyo nina wahimiza wabunge wote wa CCM wanaotaka maendeleo katika nchi yetu waondoke CCM, waingie CCJ na kisha waimarishe kambi ya upinzani

Imenipa taabu kidogo dhamira yako sioni kiuganishi katika maelezo yako ya Chadema na CCJ au ndio staili ya uandishi wetu wa kuuza gazeti
 
It minz ni chama cha kutuzuga ili tuachane na vyama vya ukweli, kama chama knakiri kimeanzishwa na vigogo wa ccm means itakuwa kubadili chupa bat mvinyo ni uleule, kwa kutoka kwao ccm hakumaanishi waeshakuwa wasafi, watueleze wametufanyia nini walipokuwa huko then ndo watupe sababu " critical" za kutoka sio majibu mepesi , kama ishu ni maadili yamepotea zaidi ya miaka 20 walikuwa wanasubiri nini.
 
Hivi huwa najiuliza CCM ni Chama Cha Mapinduzi. Hayo Mapinduzi walimpindua nani? Au ndo wananchi walipinduliwa? Na wapinduliwa wakakubali kukaa kimya baada ya kupinduliwa! Ni wakati muafaka waweke vizuri jina la chama chao====CCM- Chama Cha Mafisadi. Kwani Mashetani nini?
I think, it was just to accomodate ASP revolutionary thinking by then.
 
Nilipata kusikia CCJ haitashiriki uchaguzi mkuu 2010 mpaka kipate usajili wa kudumu Mpendazoe anajipa matumaini ya kujenga chama mbadala wakati hajui kama atashiriki katika uchaguzi asishangae CCJ kupata usajili baada ya Oktoba 2010. Usinunue mbeleko kabla mtoto hajazaliwa
 
Imenipa taabu kidogo dhamira yako sioni kiuganishi katika maelezo yako ya Chadema na CCJ au ndio staili ya uandishi wetu wa kuuza gazeti
Una maana gani? sentensi yako haieleweki kabisa.
 
CHADEMA wabaki na machopa yao hawana sera.


Inaonyesha jinsi usivyo na haya kutak kupotosha umma hapa,unatumia kigezo gani kusema CHADEMA haina sera?

Acha Rhetorics ndugu yangu,it's obvious you are not there for solution.Hivi nikikwekea sera za CHADEMA hapa utasema nini?si utaaibika tu ndugu yangu?wacha nisikusulubishe zaidi ,hebu gonga hapa
http://www.chadema.or.tz/nyaraka/index.php
 
Back
Top Bottom