Ujinga utaachwa pale tutakapoacha kuhukumu watu kwa hisia na assumptions zisizo na msingi. Mtu akija JF kama mwanaume au mwanamke, jambo la msingi ni hoja aliyokuja nayo, si kumchunguza jinsia yake kwa kubahatisha.
Kama post haikupendezi, ipite tu. Kama una hoja, jibu hoja. Lakini kugeuza kila mjadala kuwa “huyu ni mwanamke anayejifanya mwanaume” au “huyu ni mwanaume anayejifanya mwanamke” ni kupoteza muda na kushusha kiwango cha mjadala.
JF ni sehemu ya mawazo na mijadala, si ofisi ya sensa ya kuhesabu wanaume na wanawake.