Ujenzi wa miji na majiji bora: Tufanye nini kuboresha majiji yetu hapa Tanzania?

HENRY14

JF-Expert Member
May 13, 2021
2,340
4,386
Habari zenu wanaJF na wadau wa jukwaa la ujenzi.

Nimesoma mada nyingi humu kuhusu ujenzi wa makazi. Makazi yakizidi tunajikuta na miji na hatimaye majiji. Kama ilivyo kwa nyumba abayo ikipangiliwa vibaya 'livability' yake inakuwa ngumu, basi miji na majiji ni hivyo hivyo.

Kama mkazi wa Dar na mdau/mpenzi wa ujenzi na tasnia ya ubunifu/usanifu majengo, nimekuwa nikiangalia jinsi miji yetu ya Tanzania inavyokua, kwa fano Dar lenyewe. Siwezi kusema nimeitazama kitaalam sana ila naweza kusema nimejifunza machache, likiwemo suala la kwamba maendeleo ya maeneo yanayofanywa na wananchi ni kwa kasi kubwa kuliko wataalam wa mipango miji na huduma za jiji zinavyopangwa au kupatikana. Kwa maana vijiji na miji vinaanzishwa na wananchi na baadae huduma na miundombinu inapelekwa na serikali. Nazungumzia barabara bora, maji, umeme, shule, hospitali, nyumba za ibada, viwanja vya wazi vya starehe na michezo, n.k. Kwa mfano huu nimeona kuwa mwishowe tunajikuta tunajenga jiji lisilo bora kwa vigezo kadhaa.

Nimeona mada hii inaweza kuchambuliwa kwa namna tofaut, ila nimeona nianze na 'livability'(urahisi au ubora wa kuishi jiji husika), kwa maana naamini hili huenda ndilo jambo kuu la ujenzi wa miji. Hii ni 'big picture' na swali langu litakuwa ni "je, jiji letu liko 'livable'?" na "je, tunaweza kuliboreshaje?" na ni wapi tumepatia vema na kustahili kuwa mfano kwa majiji mengine?

Kama tutaweza kujadili suala hili, ningependa pia kuwashirikisha video chache za 'inspiration' kutoka kwenye miji mingine. Nianze na hii survey ya Most Livable cities ya 2014 iliyofanywa na shirika la habari la Monocle. Tumaini langu ni kuwa tutajifunza na kulinganisha na sisi tulipo na kujiuliza ni nini tufanye tubereshe majiji yetu.

NB: Nimeandika summary ila ya sec. 20 za hii video ila mimi mbovu wa kutafsiri kiingereza hivyo nitaweka kama ilivyo, baadae nitajitahidi kuiweka kwa kiswahili.

Quality of Life Cities: Vancouver, Tokyo & Copenhagen:




Summary

The most livable cities in the world get the essentials right:

Reliable public transport

Good Schools

Low crime

But they attain a more subjective excellence too. They must be cities which people would want to live and work. Cities that not only make it easy to get to the office, but have life in them too. These are steered by individuals who constantly look at other cities to improve, and they change and adapt, as any great city must, without losing sight of their strengths.

Karibuni.
 
Ni kuunda mamlaka ya upimaji mipango miji,ardhi na ramani kama Ilivyo Tarura, Tanroads,Ruwasa nk

Moja ya jukumu lake kuu ni kupanga miji na Vijiji na ipewe nguvu za kisheria na chanzo cha uhakika cha pesa hapo mambo yatakaa sawa
 
Ni kuunda mamlaka ya upimaji mipango miji,ardhi na ramani kama Ilivyo Tarura, Tanroads,Ruwasa nk

Moja ya jukumu lake kuu ni kupanga miji na Vijiji na ipewe nguvu za kisheria na chanzo cha uhakika cha pesa hapo mambo yatakaa sawa
Nilidhani kitu kama hicho kipo tayari.
 
Uzi mzuri kabisa. Kiujumla kama mtu ambaye nimebahatika kuishi Dar, Jiji letu siyo livable na hata quality ya maisha iko chini sana. Na hili linawahusu wenye uwezo na wasio nao. Mfano, niliwahi kuishi Mbezi Beach. Kila asubuhi au jioni najitahidi nitembee. Lakini ni vigumu kupata side walk ya kutembea kwa mguu. Ukitoka Masana mpaka Mbuyuni zile barabara za pembeni ni kama zimekufa. Ingawa ni za waenda kwa miguu, wanaozitumia ni bodaboda. ukijichanganya utagongwa.

Designers wa barabara nyingi Dar, hawakuwahi kuwafikiria watembea kwa miguu au watumia basikeli au usafiri mwingine usio gari. Unaweza kwenda Masaki au Mbezi unakuta Nyumba ya millions, lakini nje ya geti kuna madimbwi balaa au barabara haipitiki.

Kiufupi, miji yetu bado sana. Kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu, maendeleo yanafuata watu..not vice versa. Yaani kila mtu anafanya chake na kama ukiweza kuonyesha kwamba una thamani kwa mwanasiasa, chochote kibovu wahusika watakikalia kimya. Refer: Issue ya Machinga. siku hizi watu wanapika vyakula maji machafu wanamwaga barabarani....na usisahau kwamba wanapofanyia biashara machinga ni sehemu mahsusi kwa waenda kwa miguu.
 
Uzi mzuri kabisa. Kiujumla kama mtu ambaye nimebahatika kuishi Dar, Jiji letu siyo livable na hata quality ya maisha iko chini sana. Na hili linawahusu wenye uwezo na wasio nao. Mfano, niliwahi kuishi Mbezi Beach. Kila asubuhi au jioni najitahidi nitembee. Lakini ni vigumu kupata side walk ya kutembea kwa mguu. Ukitoka Masana mpaka Mbuyuni zile barabara za pembeni ni kama zimekufa. Ingawa ni za waenda kwa miguu, wanaozitumia ni bodaboda. ukijichanganya utagongwa.

Designers wa barabara nyingi Dar, hawakuwahi kuwafikiria watembea kwa miguu au watumia basikeli au usafiri mwingine usio gari. Unaweza kwenda Masaki au Mbezi unakuta Nyumba ya millions, lakini nje ya geti kuna madimbwi balaa au barabara haipitiki.

Kiufupi, miji yetu bado sana. Kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo juu, maendeleo yanafuata watu..not vice versa. Yaani kila mtu anafanya chake na kama ukiweza kuonyesha kwamba una thamani kwa mwanasiasa, chochote kibovu wahusika watakikalia kimya. Refer: Issue ya Machinga. siku hizi watu wanapika vyakula maji machafu wanamwaga barabarani....na usisahau kwamba wanapofanyia biashara machinga ni sehemu mahsusi kwa waenda kwa miguu.
Kweli kabisa. Jiji liko vibaya kwa mambo mengi mno. Naona umeleta jambo kubwa la kuwa sisi wananchi wenyewe hatuko poa kifikra na kimatumizi ya hata hiyo miundombinu finyu tuliyonayo. Mfano suala la wamachinga na mama lishe kwenye njia za waenda kwa miguu pia linasbabisha mitaro ya maji ya mvua kujaa taka taka. Mvua zikinyesha matokeo yake ni mafuriko, hali ambayo ingeepukika kirahisi tu watu wasingetupa takataka mitaroni na kuiziba.
 
Back
Top Bottom