Ujasusi - Umoja namba 97

Kazi nzuri mkuu, ni simulizi inayoreflect maisha halisi kabisa juu ya billionare clubs and secret societies zinazoongoza serikali za nchi zetu na hizi major and merger projects za space.
 
SEHEMU YA 64

BETRAYAL(USALITI)
Sura ya mtu wa kwanza kuiona kabisa katika kundi hilo ilikuwa ni sura ya raisi mstaafu bwana Athumani Ndalu , jambo hilo lilinishangaza sana kwa yeye kuwa mahali hapo , lakini sura nyingine ambayo nilikuwa nikiifahamu katika kundi hilo ilikuwa ni sura ya waziri mkuu bwana Hamduni Saidi Rajabu kwanini nishangae uwepo wa hawa watu hapa ndani ni kwasababu kuu moja kwanza hawakuwa wamealikwa katika mkutano wa BIBTWAG kama mimi nilivyo alikwa kwani ndani ya taifa la Tanzania niliekuwa nimehudhuria mkutano huo mkuu ilikuwa ni mimi tu .
Watu wawili walokuwa wamebakia wote hawakuwa raia wa Tanzania lakini nilikuwa nikiwajua vyema kutokana na umaarufu wao katika maswala ya kisiasa, wa kwanza alikuwa ni mwanaume aliafahamika kwa jina la Coelo Snart huyu alikuwa ni waziri mkuu wa uingereza na wapili alikuwa ni waziri wa teknolojia wa marekani bwana Marc Snider .
Basi pamoja na kusawijika kwangu nilikaa kwenye kiti ambacho kiliandaliwa na ilionesha ni kama vile nilikuwa nikisubiriwa mimi kwani baada ya kukaa waliingia wahudumu na wakaweka glass za wine na chakula kikawekwa .
“ Karibu sana bwana Henry Mushi “
“ Asante sana mheshimiwa ni heshima kwangu kujumuika na wewe katika chakula cha usiku sikuwahi kuwaza kuipata hii nafasi “ ni wakati nikiitikia ukaribisho kutoka kwa waziri mkuu wa uingerereza na akatabasamu huku akiinua glass yake ya wine na kuiweka chini .
“ Mheshimiwa henry nadhani umeshangazwa sana na uwepo wetu mahali hapa mimi na mheshimiwa waziri mkuu “
“ Ndio mheshimiwa mstaafu nimeshangaa sana maana najua nimewaacha Tanzania “.
“ Ni kweli hawa hawakuwepo wala kualikuwa kwenye mkutano wa BIBTWAG lakini hawa ni moja ya wanajumuia ya BIBTWAG wakihudumu kama mawakala wetu wan je “ aliongea bwana Marc snider .
“ Hongera sana kwa kupanda daraja kutoka C kuja B hii ni mafanikio makubwa sana kwako ambayo umeyafikia na ni bahati kubwa sana kwako , kwani sio kawaida kuvuka kutoka daraja moja kwenda lingine katika hudhurio lako la kwanza “.
“ Hata mimi nimeshangazwa sana na jambo hilo na mpaka sasa sijajua sababu ya kuvuka kutoka kwenye daraja C kuja daraja B “..
Waziri mkuu wa uingereza aliinua glass yake juu na kuwaangalia wenzake na kisha wote waliinua glass zao juu , na mimi nikafata hivyo hivyo .
“ Karibu sana bwana Henry katika kundi B lakini tunakupongeza pia kwa kuchaguliwa kuwa raisi mtarajiwa wa Tanzania .. cheers “ aliongea waziri mkuu na kuzidi kunifanya nishangae Zaidi .
“ Mheshimiwa sijakuelewa ulivyomaanisha kwamba kuwa raisi wa Tanzania “ niliongea nikiwa na wasiwasi mara baada ya kushusha glass yangu chini na marc snider alimwangalia mstaafu ndalu na kumpa ishara .
“ Mheshimiwa Henry nadhani unakumbuka kikao chetu tulichokaa nchini Kenya ?”
“ Ndio nakumbuka “.
“ Kama ni hivyo basi nadhani nakumbuka maeneno yangu tlioongea juu yaw ewe kuwa raisi wa Tanzania , swala la sisi kuwa hapa ni kwa ajili ya mustakabali wa taifa la Tanzania na kikao hiki ni maalumu kwa kuzungumza ni kwa namna gani tunakwenda kulikomboa taifa la Tanzania katika umasikini uliokithiri na unaoendelea kukithiri chini ya utawala wa mheshimiwa Bendera “ aliongea mheshimiwa Ndalu na kisha alitoa tablet na kunipa kwa kuninyooshea .
“ Hio ni orodha ya wawekezaji ambao wana mpango wa kuwekeza ndani ya nchi yetu ya Tanzania lakini pia ukienda chini Zaidi utaona orodha nyingine ya wawekezaji ambao walijitoa katika kuwekeza ndani ya taifa la Tanzania mara baada ya mheshimiwa ndalu kuchukua madaraka , kwa maneno marahisi ni kwamba taifa letu kwa sasa linaangamia na hatua za haraka zinatakiwa kuchukuliwa na ndio maana mimi na waziri mkuu tupo mahali hapa “. Alingea na kisha akanyamaza .
“ Bwana Henry nadhani umesoma katiba ya kusanyiko la BIBTWAG na malengo yake kwa ujumla , lakini pia nadhani umeona ni namna ilivyokuwa ngumu kwa mwanachama kutoka ngazi moja kwenda nyingine lakini leo hii uko hapa , nataka kukuambia kwamba jambo hili halijatokea kwa bahati mbaya wewe ni mtu muhimu sana pengine kuliko mtu yoyote ndani nya taifa la Tanzania , kwa maneno marahisi tu sisi tunakutambua kama raisi wa Tanzania “ Aliongea Bwana Marc snider na kunifanya nijihisi hali flani ya msisimko lakini uliojaa woga .
Baada ya kuongea maneno ambayo yaliniingia akilini kwa kiasi kikubwa sana , na hata tamaa ya kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ikanianza kunivaa , japo jambo hilo sikujua linaenda kufanyika kwa namna ipi ,lakini nilijihisi kabisa kwamba mimi ninafaa kuongoza taifa la Tanzania .
Basi baada ya kuongea maneno kadhaa , hatimae waziri mkuu alitoa tena faili na kunikabidhi mkononi wakati huo tulikuwa tushamaliza kula na wote waliniangalia wakati napokea faili hilo .
“Mheshimiwa makamu wa raisi tunataka kukuambia hao ni viongozi wa juu wa taifa la Tanzania ambao wanakuunga mkono wewe kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania “ aliongea waziri mkuu na mimi nilianza kiupitia faili lile lililokuwa na majina ya watu pamoja na sahihi zao , wengi wao walikuwa ni viongozi wakubwa wa chama tawala , tena kilichonishangaza Zaidi ni wale watu ambao mheshimiwa raisi Bendera alikuwa akiwaamini sana , lakini pia jambo la kutisha pia ni kwamba mkuu wa majeshi pia sahihi yake ilikuwepo katika orodha hio .
“ Mheshimiwa Henry nadhani ushaona ni kwa namna gani unaungwa mkono na viongozi wa juu juu ya wewe kuchukua Nchi , hivyo kwanzia sasa imebaki kauli yako moja tu ya wewe kukubali kuwa raisi ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania “ aliongea raisi mstaafu Mheshimiwa Ndalu .
Nilikaa kimya nikitafakari maana ilikuwa maamuzi magumu ambayo ningeweza kuyafanya na isitoshe nikisema ndio nataka kuwa raisi wa jamhuri ya muungano inamaana ningekuwa namsaliti mheshimiwa Bendera ambae kwangu ni Zaidi ya ndugu .
Akili yangu ilianza kuwaza huku na huku nikiwaza nifanye maamuzi gani kwa wakati huo , wale viongozi waliokuwa pale wote walikuwa wakiniangalia , lakini mimi nilikuwa mbali kimawazo mno , nilijikuta nikianza kuanza kuwaza harakati zangu zote za kiuongozi , jinsi nilivyokuja kufahamiana na mheshimiwa bendera mpaka akaja kuwa rafiki yangu mkubwa ,, harakati zote a mimi kuwa raisi zilianza kuja katika kumbukumbu zangu , mawazo ya mke wangu nayo hayakuniacha salama kabisa , nilianza kukumbuka namna ambavyo mke wangu alivyonidanganya , niliwaza namna ambavyo pia rafiki yangu Bendera alivyonidanganya , nilijikuta pia nikija kuwaza usaliti walioufanya siku chache zilizopita moyo ulianza kuuma , ule upendo niliokuwa nao juu ya Bendera ulianza kugeuka chuki , nilianza kuwaza labda mke wangu anampendea Bendera kwasababu ni raisi , mawazo hayakuniacha salama .
“ Mheshimiwa Henry maamuzi natakiwa kuyafanya sasa hivi kwani viongozi wako hawa wanatakiwa kuwa ndani ya Tanzania muda mchache ujao hivyo hakuna muda wa kupoteza ,, tunataka kujua kama upo tayari kuwa raisi wa Tanzania “ ilikuwa ni kauli kutoka kwa waziri mkuu wa uingereza ilionigutusha .
“ Kabla ya kutoa maamuzi yangu naomba kuuliza swali kwanza “ niliongea kwa wasiwasi na wote waliniruhusu niulize swali langu
“ Ni njia gani itatumia ili mimi kuwa raisi ?”
“ Mheshimiw Henry hilo lisikusumbue kabisa , muda ukifika tutakuambia ni namna gani swala hilo litaweza kufanikiwa na wewe kuingia pale ikulu “ alijibu Marc snider
“ Okey niko tayari “ niliongea kwa wasiwasi lakini nikiwa nimemaanisha kile nilicho ongea na wote walitoa tabasamu na kunipongeza kwa uamuzi wangu wa kishujaa huku wakiahidi kwamba sitokuja kujutia kwa uamuzi nilioufanya siku hio .
Basi baada ya kutoa maamuzi yale na mimi nilisaini ile karatasi na kuwa mmoja ya watu ambao tunataka raisi Bendera aachie madaraka huku mimi nikiwa nimpokee , sikujua ni kwa namna gani jambo hilo lilikuwa linaenda kufanikishwa lakini maamuzi nilikuwa nishayatoa na hakukuwa na swala lingine ambalo ningeweza kufanya na kuyabadilisha maamuzi yangu .
Basi siku hio bada ya kukutana na viongozi wale , sikurudi tena kwenye ile boti ya kwanza na nilikuwa mwanachama kamili wa BIBTWAG kundi B nilionyeshwa chumba cha kulala na kwa bahati nzuiri ni kwamba kila kitu changu kilikuwa kishaletwa na hata mimi jambo hilo lilinishangaza lakini nilijua mambo humo ndani yanaenda kisomi , baada ya kuingia ndani ya chumba hicho ch kifahari kilichokuwa na kila kitu , aliingia mhudumu na kunipa maelekezo , na moja ya maelekezo yalionifurahisha ni kuwasha tv na kuchagua mrembo ambae ningepnda ausindikize usiku wangu kwa siku hio .
Walikuwa ni warembo haswa waliokuwa wakionekana katika runinga hio na mimi sikuleta ajizi , kwenye maisha yangu nilivyokuwa mdogo nilikuwa nina ndoto ya kulala na Red indian wanawake waliokuwa wakipatikana brazili ,, hivyo nilichagua mwanamke mmoja wa kibrazili mrembo mwenye kalio kubwa na ndani ya madakika tu mrembo huyo aliingia ,, ebwana eh aisee sikukosea katika uchaguzi wangu kabisa… maana alikuwa mrembo haswa , mwili wote ulinisisimka ,sikuwaza tena ndoa yangu , sikuwaza tena jambo ninalofanya nilikuwa nikimsaliti mke wangu , ila nilivhokuwa nikiwaza kwa wakati huo ilikuwa ni ngono tu .
Siku iliofuata ililukuwa ndio kilele cha mkutano wa BIBTWAG kiufupi hata kule hotelini hatukurudi tena kwani baada ya kutoka ndani ya meli ile ya kifahari … nilipanda ndege ya kurejea nchini Tanzania kuendelea na majukumu yangu ya kiuongozi kama makamu wa raisi .
Wakati wa kutoka niliwasiliana na mke wangu kabisa kwamba nakuja m lakini pia niliwasiliana na mwanangu Patrick ambae alikuwa nchini marekeani.
Baada ya masaa kadhaa nilikuwa ndani ya jiji la Dar es salaam katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius kambrage nyerere.
Mke wangu ndio aliekuja kunipokea akiwa ameambatana Na baadhi ya viongozi, lakini pia mke wa mheshimiwa Bendera alikuwepo uwanjani hapo
“ Karibu sana Tanzania mume wangu “ ilikuwa ni sauti ninayoipenda kuisikia ya mke wangu ikinikaribisha , na nilikumbatiana nae japo kila nilivyokuwa nikimwangalia na kukumbuka ile video roho iliniuma .
Basi siku iliofata niliweza kuwasiliana Na mheshimiwa raisi kwani alikuwa ikulu ya Dodoma na nilimwambia nimerudi salama na pia alinipongeza kwa safari yangu.
Basi siku hio asubuhi , alikuja mke wangu na kuniambia kuwa kuna mgeni wangu anahitaji kuonana na mimi na sikuwa na ajizi ,, nilimwambia mke wangu ampeleke katika ofisi yangu ndogo ya hapo nyumbani kwa ajili ya kuonana nae .
Nilijiandaa na kutoka ili kwenda kuonana na mgeni ambae mke wangu alikuwa ameniambia kuwa amekuja … baada ya kuingia ndani ya ofisi yangu ndogo sehemu ambayo nilimuelekeza mke wangu ampeleke huyo mgeni kwa ajili ya kukutana nae , ndipo nilipomuona kijana mmoja wa makamoo alienipa mgongo alikuwa na nyweli zake fupi alizonyoa kwa mtindo wa kileo huku akiwa amevalia suti .. niliingia ndani kabisa ya ofisi yangu na kusalimiana na kijana huyp na kama nilivyodhania alikuwa ni kijana mdogo kabisa wa makamo si chini ya miaka therathini kwenda juu , alikuwa na mkoba wake wa rangi nyeusi , alikuwa amependeza sana na naweza kusema kwamba kijana wangu Patrick ni mtu wa kupendeza , lakini kwa kijana huyo alikuwa amependeza Zaidi na alionekana kuwa mtu wa fasheni .
“ Karibu sana kijana “ niliongea huku nikimpa mkonoo tukiwa wote tumesimama
“ Asante sana muheshimiwa “
“ Jisikie huru , karibu sana “ nilimkaibisha na mimi nikakaa nay eye akakaa … alionekana kujiamini sana .
“ Kwa majina naitwa deusi ndimbo mimi ni mtanzania ninae ishi nchini marekani , nipo hapa nchini kama mwakilishi wa U-97 “ utambulisho huo ulinifanya nishangae hasa hapo kwenye neno U-97 .
“ Umoja namba tisini na saba ?” niliuliza kwa kuhamanika
“ Ndio muheshimiwa mimi ni agent wa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA “.
ITAENDELEA .

INAENDELEA
SEHEMU YA 65
DAMIANI RETURN(KURUDI KWA DAMIANI )
“ Nadhani muheshimiwa ushalisikia hili jina na kwa mshangao wako inaashiria unaufahamu vyema umoja huu ?”
“ Ndio nimeshangaa na naujua vyema umoja huo , na kwa hapa Tanzania tushaufuta kwani ulikuwa ni umoja unaohusika na madawa ya kulevya , lakini imenishangaza kijana kujitambulisha kwa ujasiri , ilihali mimi unajua ni kiongozi wa nchi na pia nilihusika katika kuufuta umoja huo hapa nchini “.
“Robo ya uliioongea muheshimiwa ni ya kweli , lakini robo tatu zote sio sahihi “ aliongea kijana kwa kujiamini huku akiwa ameweka uso wake wa tabasamu na hali yake ya kujiamini ilinifanya nishangae Zaidi .
“ Unataka kumaanisha nini “
“ Kwanza kama nilivyojitambulisha mimi ni wakala wa UMOJA NAMBA TISINI NA SABA na nipo nchini hapa kwa kazi maalumu na uwepo wangu ndani ya nchi hii umetokana na maamuzi yako ya kishujaa uliofanya “
“ Unamaanisha nini kuhusu maamuzi yangu ya kishujaa nilio fanya , ni maamuzi gani hayo ,maana sina kumbuklumbu na hayo unayo ongea na ni vyema kama utaenda moja kwa moja katika hoja yako kwani nina majukumu mengi “niliamua kuweka uso wa siriasi kwani kitendo cha kijana huyu kujionyesha kujiamini lakini pia kuongea maneno kunizunguka zunguka kulinikera ila niliweka sura ya kikazi Zaidi na sikutaka kuonesha kwamba nimekerwa na maneno yake , lakini nilitaka kumuonesha kwamba sipendi hoja zake za kuzunguka .
“ kama nilivyokuambia mheshimiwa kwamba ni robo tu umefanikiwa kuelezea UMOJA NAMBA TISINI NA SABA , basi itakuwa vyema Zaidi kukuelezea robo nyingine ya ukweli juu ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA nadhani ukishajua robo hio utanielewa nimekuja nchini kwa kzi gani “
“ Niambie robo zote tatu za ukweli huo “
“Mamlaka niliokuwa nayo muheshimiwa ni kukueleza robo nyingine ya lakini nusu ya ukweli itakayo baki ni jukumu la mtu mwingine kukueleza “
“Okey sawa Bwana Deusi unaweza kunieleza hio robo ya ukweli “ niliongea hivyo kwani na mimi nilikuwa msomi na nilikuwa nikielewa itifaki za mashirika makubwa duniani na hata ningekaza vipi kijana huyo asingeniambia ukweli wote .
“Kwanza kabisa muheshimiwa nataka uelewe kwamba umoja huu haujaondka hapa Tanzania na hilo ni swala ambalo haliwezekani bali mmeupa nguvu Zaidi hilo ni la kwanza la pili umoja huu haujihusishi na madawa ya kulevya , bali unatumia bishara hio kujificha , la tatu ambalo nakamilisha robo ya ukweli ambao unapaswa kuujua ni kwamba BIBTWAG ni sehemu ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA (U-97 )”
Nilijikuta nikipatwa na mshangao wa hali ya juu mno , nilishangaa zaidi na Zaidi na mpaka hpo nilijua sababu ya kijana Deusi kuwa na hali ya kujiamini katika kujitambulisha kama wakalawa UMOJA BAMBA TISINI NA SABA (U-97)
“ Kwa maelezo hayo nadhani mheshimiwa ushajua ni sababu ipi nipo ndani ya taifa la Tanzania , lakini pia kuweka mambo sawa ni kwamba mpaka sasa , mheshimiwa na wewe ni mwanachama wa U-97 “
“ Unamaanisha nini kusema mimi ni mwanachama wa huo umoja , sijawahi kujiunga katika hu umoja mimi “ niliongea na kijana yule hakuonesha papara kabisa , alionekana kujua kile anacho ongea na anacho kifanya na hio ilionesha katika uso wake kwanni hakuathiriwa na neno langu lolote lile .
“Mheshimiwa kwanza nikuambie tu kwamba hatua mbali mbali za wewe kuingia katika uanachama wa U-97 zilichukuliwa , bila shaka nadhani unaelewa kanuni nzima ya kila mtu anehudhuria kwenye mkutano wa BIBTWAG moja ya vigezo ni kuwa mfanya biashara mkubwa mwenye pesa , kitu ambacho wafanya biashara wengi ndani ya taifa hili wamekupita , lakini hawakuweza kupata mwaliko wa kwenda kwenye kusanyiko la BIBTWAG “
“ Kwa hilo naelewa n ahata mimi lilinishangaza mara Baada ya kupata mwaliko , lakini bado swala hilo halinifanyi kuwa mwanachama wa wa U-97 na kama ulivyosema umoja huu haujihishi na madawa ya kulevya kitu ambacho nilikuwa najua siwezi kuwa katika umoja huo ilihali sina ufahamu nao “
“ Ni kweli unayozungumza , lakini naamini ukiweza kufikiria kwa mambo yote ulio yaona ndani ya kusanyiko la BIBTWAG unaweza ukapata mwanga wa ukubwa wa U-97 fikiria matukio yote mheshimiwa uliokutana nayo ndani ya kusanyiko hilo kisha tuendelee na mazungumzo “ aliongea kijana Deusi na mimi nilijikuta nikkianza kuwaza kwanzia siku ya kwanza natoka hapa Tanzania kwenda chini Singapore kuhudhuria mkutanoo wa BIBTWAG mawazo hayakuniacha hapo tu yalinipeleka katika matukio yote niliokutana nayo na mengine nilioshiriki katika kuyafanya ,, lakini pia swala la kukutana na waziri mkuu pamoja na mheshimiwa raisi mstaafu lilipita ndani ya kichwa changu , na mpaka hapo swali likaibuka katika kichwa change , kwani kwa ninacyokumbuka mheshimiwa Ndalu na yeye alikuwa ni mwanachama wa U-97 na katika sakata zima la kutokomeza madawa ya kulevya alikuwepo kwenye kundi , lakini pia kumbukumbu zangu zilirudi siku alionifata nchini Kenya , niliwaza pia uwepo wa waziri mkuu ndani ya meli ile , mpaka hapo nilijikuta nikiwa na jibu moja kwamba waziri mkuu na yeye alikuwa ni mwanachama wa U-97 “
“ Nadhani mpaka hapo mheshimiwa ushajua namaanisha nini nilikuambia kuwa wewe ni mwanachama wa U-97 na bila kupoteza muda niende moja kwa moja katika pointi ya msingi ya swala lililonileta hapa nchini , kwanza kabisa nikupongeze kwa maamuzi ya kishujaa ulioyafanya , na kupitia maamuzi yako nipo hapa nchini kwa ajili ya kukamilisha zoezi la wewe kuingia ikulu , na kwanzia sasa nitakuwa mshirika wako wa karibu mno na kuna baadhi ya maelekezo kutoka kwa wakuu wangu utayapata kupitia mimi “
Nilijikuta nikiwa sina la kusema kwani mpaka hapo niliamini kabisa U-97 sio kama nilivyokuwa nikidhania , na sio mimi tu na hata kwa mheshimiwa Bendera niliamini alikuwa katika kiza kinene kabisa , kwani baadhi ya watu aliokuwa akaituamini tayari tulikuwa wanachama wa umoja huo .
Mazungumzo yangu na bwana Deusi yaliisha huku akiahidi kuonana na mimi mara kwa mara , nilimuomba anieleze ni mkakati gani unaenda kufanyika mpaka mimi kuingia ikulu lakini hakuweza kunikubalia kabisa huku akijitetea kwamba hilo sio jukumu lake la kuniambia na pia hakuwa na maamuzi nalo , na ilibidi nimkubalie , lakini swala lingine liliibuka katika kichwa changu ni kwanini hawa U-97 wanataka kuniweka madarakani , ni nini dhumuni lao haswa , ukizingiatia sikuwa nikiujua umoja huu kwa kina swala hilo lilizidi kunichanganya .
Basi baada ya siku kadhaa kupia nililerejea makao makuu ya nchi nikiwa na mke wangu Wema , japo nilikuwa nikijua mambo ya usaliti aliokuwa amenifanyia mke wangu lakini sikuacha kumpenda , hakika nilikuwa nikimpenda sana mke wangu , tabasamu lake lilinifanya kusahau kila jambo lililotokea .
Nilikutana na mheshimiwa Bendera ofisini kwake na tukaongea baadhi ya mambo ya safari yangu , lakini pia mambo ya kikazi na namna ambavyo tunaweza kuendelea kutatua changamoto za wananchi , niseme tu kwamba mheshimiwa raisi alikuwa ni moja ya watu wachapakazi mno , meza yake ilikuwa imechafuka mafaili kila kona na yote alionekana kuyafanyia kazi .
Basi baada ya siku kumi kupita nikiwa katika majukumu ya kazi alikuja moja ya kijana ambae nilikuwa nimempa kazi ya kumatilia mke wangu kwani sio mar azote mke wangu nilikuwa nikiwa nae , wakati nikiwa ofisini mara nyingi mke wangu huenda kwenye mizunguko yake ya kibishara , na jambo hilo kutokana na usaliti wake aliokuwa amenifanyia sikuwa nikimuamini sana , n ahata nilivyofika Dodoma niliamini kuna uwezekano wa mke wangu kutafuta nafasi ya kukutana na mheshimiwa raisi kwa ajili ya kuendeleza mapenzi yao , na swala hilo lilinifanya nimpe mtu kazi ya kumfatilia mke wangu kila mahali anapokuwa kwa siku nzima .
Basi siku hio kumi hatimae kijana niliempa kazi aliniletea taarifa ambayo ilinifikirisha sana , taairifa hio ilikuwa ni kwamba mke wangu wa siku hio ya asubuhi alienda ikulu kuonana na mehsimiwa Bendera , jambo ambalo kwa siku hio mke wangu hakuniambia kama ataenda kuonana na mheshimiwa raisi , kwani aliniaa asubuhi kwamba ataenda kwenye maswala yake ya kibiashara , nikukumbushe tu kwamba mpaka kwa wakati huo mke wangu hakuwa akijua chochote juu ya mimi kuujua ukweli kwamba mwanaume wake wa kwanza aliemtia usichana wake ni mheshimiwa Bendera na wala pia kwa bendera hakuwa akijua kwamba najua siri yao wote wawili .
Kwanza jambo la kwanza lilinifanya ni waze ni jambo gani mke wangu kaenda kuongea na mheshimiwa raisi kwa siku hio na kama ni jambo la kibishara kwanini hakuniaga , lakini pia kama ni swala la mapenzi sidhani kwamba wanaweza wakafanya kitendo cha kukutania ikulu kwani kwa ninavyojua mheshimiwa bendera ni moja ya watu ambao wanaheshimu sana wake zao kwa hio jambo la yeye kwenda pale ikulu halikuwa swala la kimapenzi na hilo nililipinga kwa asilimia mia moja , lakini kilichonifikirisha ni kwamba ni kipi ambacho walienda kuongea hapo ikulu kwani mke wangu hana biashara yoyote inayo endelea na mheshimiwa bendera .
Baada ya kupoteka taafira hio niliwaza sana na nikaamua moja kwa moja jioni nitakapo kutana na mke wangu nitajaribu kumsanifu nione kama ataniambia nini .
Mheshimiwa Henry anajikuta akishituliwa kutoka kwenye kumbukumbu yake hio ya miaka ya nyuma na mhudumu wa ndege kwa ajili ya kufunga mikanda , kwani ndege inakarbia kutua.
>>>>>
Merina aliendesha gari huku akiwa kama mtu ambae hakuwa akiamini kile kinacho mtokea katika maisha yake , hakuamini kabisa kwamba mtu ambae alikuwa akimuota usiku na mchana ndio mtu ambae yupo pembeni yake , kwake swala hilo lilikuwa ni kama ndoto , kuna muda alijikuta akigeuza macho upande ambao amekaa damiani kuhakikisha kama kweli ni yeye au ni picha yake , ama kamfananisha na mtu mwingine,,hata uendeshaji wake wa gari ulikuwa haupo katika umakini , mambo mengi yalikuwa yakipita katika kichwa chake .
Upande wa Damiani na yeye alikuwa ametulia na kila muda alikuwa akiangalia nyuma kuona kama kuna watu waliokuwa wanamfatilia , lakini mpaka wanakunja kuingia upande wa masaki hakuna gari alioitilia mashaka .
Haikuwachukua muda mrefu mpaka kufika sehemu ambayo alikuwa akiishi mlimbwende Merina , baada ya kuingiza gari mtu wa kwanza kutoka ni yeye na kisha aliefatia akawa ni Damiani , bila hata ya kujiuliza mara mbili mbili mara baada ya wote kutoka kwenye gari , Merina alimkumbatia Damiani palepale huku akiwa anatoka machozi , na wakati huo mdogo wake aliekuwa juu ya gorofa kwenye balconi alikuwa akiangalia kila kitu , na hakuamini kumuona dada yake akiwa katika hali kama ile .
Damiani na yeye alijikuta akipandwa na hisia za ajabu kutokana na kumbatio la mwanadada Merina , alikiri kwamba alikuwa na hisia juu ya mlimbwende huyo zilizojificha , alihisi machozi yakimdondokea katika bega lake na hapo ndipo alipo jua kuwa mwanamke huyo alikuwa akilia , baada ya kukaa katika hali yakukumbatiana kwa muda kidogo hatmae Damiani alimtoa merina akiwa amemshika mabega na kumuagnalia usoni , uso mzuri wa merina uliopambwa na machozi ulimpagawisha kijana damiani .
“ I am sorry merina , butu I have to go “ aliongea Damiani akimwabia naomba unisamehe lakini nataka kuondoka sasa .
“ Noo Damiani please “ hapana damiani tafadhari “
“Nitakuweka katika hali ya hatari Merina, ngoja niondoke nitatafuta namna nzuri ya mimi na wewe kuongea, naomba uniazime gari “
“Damiani please “ aliongea merina kwa hisia kali , lakini damiani hakutaka kubadilisha mawazo yake na kubaki ndani hapo ,alijua alikuwa akifatiliwa na kitendo cha kukaa hapo kingeweza kumuingiza merina katika matatizo .
Alimfuta machozi kwa mkono na kisha alichukua ufunguo wa gari na kisha aliingia na kuliwasha na geti lilifunguliwa na yeye alilitoa na kuondoka huku akimuacha merina akiwa amesimama huku akiwa haamini kwamba damiani kaondoka , alitamani kukaa nae japo kwa dakika kadhaa waongee , alitamani akae hata kwa dakika chache amwambie ni kwa kiasi gani alikuwa akimpenda na alikuwa akimsubiri kwa hamu lakini damiani alikuwa tayari ashaondoka , laity angejua damiani ndio stephano lamberk huenda kesho yake angemzukia mahali anapoishi .
Wakati akiwa amesimama alikuja kushituliwa na mdogo wake mage aliekuja kimbea kwa ajili ya kutaka kujua ile hali iliokuwa ikiendelea pale ndani , kwani alishuhudia kila kitu
“ Sista who is that guy ?”
“ Dada yule ni nani ?” aliuliza mage
Merina hakutaka kuongea kitu kingine Zaidi ya kuondoka na kuelekea ndani , na aliingia katika chumba chake na kujitupa kitandani huku machozi yakiendelea kumtoka , yalikuwa ni machozi yaliochangayika na furaha , japo damiani ameondoka , lakini hakuamini kama amemuona kwa mara nyingine , kwake jambo hilo hakulitegea kutokea mapema kwa kiasi hicho tena wakati ambao alikuwa akimuhitaji Zaidi , kwake aliona kama miujiza , kwani ni muda mchache tu ndio ametoka kuachana na Patrick , alijikuta furaha ikianza kurudi , Imani ya kwamba damiani atamuona tena ilirudi upya ,, moyo wake ulianza kujaa furaha , alijikuta akinyanyuka na kuruka ruka kama mtu aliechanganyiwa , wakati akiendelea hayo , mdogo wake mage alikuwa amesimama mlangoni akimwangalia dada yake huyo ambae alizidi kumshangaa , kwani japo kwa umri wake mdogo lakini aliweza kujua ni wakati gani n dada yake alikuwa na tatizo na wakati gani yuko sawa , mage alikuwa akijiuliza hali ya dada yake kwani alivyoingia ndani na alivyomkuta ni vitu viwili tofauti , lakini pia swala la kumuona kijana alieondoka na gari la dada yake pia lilizidi kumtia shauku kutaka kujua Zaidi , ni hali ambayo hakuwahi kumuona dada yake kuwa nayo hapo kabla, hali ya dada yake kuwa na furaha kiasi hicho .
Wakati Merina anaendelea kushangilia ,, simu yake iliokuwa ndani ya mkoba ilitoa mlio , na kukatisha kile alichokuwa akikifanya na kuuchukua mkoba wake uliokuwa kwenye kona ya kitanda na kisha alitoa simu yake na kuangalia nani anapiga , mara sura yake ilibadilika kutoka hali ya kawaida kwenda hali ya huzuni , mtu aliekuwa akipiga alikuwa ni Patirick , Merina alimuonea huruma mwanaume huyo kwani hakuwa na mapenzi nae kabisa na kwa jinsi mdada huyu alivyojielewa alielewa Patrick alikuwa akiumia juu yake , lakini aliamini pia hawezi kuwa na Patrick kwani hakuwa akimpenda na huenda angemsababishia maumivu mbeleni ..
Alipokea simu ile na kisha aliweka sikioni na kuanza kusikiliza kile ambacho kijana mtanashati patirick alitaka kumuambia mrembo huyo.
“ Merina mpenzi please naomba usinikatili namna hii , nimekuongojea muda mrefu ni kilihitaji penzi lako , kwanini lakini merina “ ilikuwa ni sauti upande wa pili ya kijana Patrick akionekana kulilia penzi la mrembo Merina , maneno yale ya Patrick yalimuingia kisawa sawa merina , na kujikuta hata machozi ya kimtoka , aliyajua maumivu ya mapenzi pale unapomsubilia mtu halafu mtu huyo kuonesha kutokupenda .
“ Am so sorry Patrick .. Damiani is back “
“ Nisamehe sana Patrick , Damiani kesharudi”
“ What ! are you sure Merina “
“ Nini ! una uhakika merina “.
“ Yess Patrick najua ni kiasi gani unaumia , lakini ni ukweli damiani kesharudi , hatuwezi kuendelea tena mimi na wewe , nisamehe , najua ni kiasi gani unanipenda , lakini hisia zangu kwakoo zimegoma sitaki kuja kukusababishia maumivu mbelen Patrick “.
“Merina najua yote hayo , lakini kwanini swala hili tusijipe muda , tumetoka kuongea muda mfupi uliopita ukiwa huna uhakika wa damiani kurudi , inawezekana vipi kuonana nae within that short of time , are you trying to avoid me Merina ?”.
“ Its hard to explain Patrick but trust me , he is back , nimekuja nae mpaka nyumbani , you can ask Mage”.( ni ngumu kuelezea Patrick , lakini ni kweli kesharudi , tena nimekuja nae mpaka nyumbani , unaweza kumuuliza Mage )
“ Tutaongea Merina kesho , nakupenda sana siamini kama kesharudi , na hata kama karudi siamini kama anakupenda kama ninavyokupenda mimi “
Aliongea Patrick na kisha alikata simu na wakati mazungumzo hayo yanaendelea Mage alikuwa akisikiliza na baada ya kusikia jina la Damiani alijikuta akitoa macho , na kumbukumbu za mtu aliemuona akiingia ndani hapo akiwa na dada yake zilimjaa upya , jinsi dada yake alivyomkumbatia yule mwanaume aliyakumbuka yote hayo , maneno ya dada yake aliokuwa akimwambia juu ya mwanume huyo mwenye jina la Damiani pia aliyakumbuka .
“ Ooh !! my god that was Damiani “ alijikuta akijisemea mtoto huyu wa miaka kumi na tano , alijikuta na yeye akiwa ni mwenye mshangao ( “ Mungu wangu kumbe ni Damiani )..
Alitoka hapo upande wa chumba cha dada yake akielekea upande wa chumba chake aliingia ndani na ni kama simu ilikuwa ikimsubiri kwani mara baada ya kuingia tu simu yake aina ya iphone ilianza kuita … aliisogea mpaka kwenye dressing table na kisha alinyanyua simu yake na kuangalia jina , na kukuta ni Patrick .
“ Yess bro “
“ Uko poa shem “.
“ Ndio niko poa shem “
“Nimekupigia Mage kuna swala nataka kukuuliza “
“Yes”
“ Your sister anataka tuvunje mahusiano , najua wewe na dada yako hamfichanagi , so I believe unamjua Damiani kama sio kumsikia “
“ Ndio namjua bro pat ,, and he was here just moment ago(alikuwa hapa ) “
“ Unasema kweli Mage ,, ni kweli damiani kesha rudi ?”
“ Ndio Shem ,, hali ya hapa nyumbani leo ilikuwa ya aina yake , mwanzoni sikufahamu kinacho endelea kwani kuna mkaka handsome alifika akiwa na sister , Am so sorry but they hugged so romantic , kusema ukweli bro kwa sister bora umuache tu , nakupenda sana shemu nilitamani uwe na sista lakini anampenda mtu mwingine , and for me napenda kumuona dada yangu akiwa na furaha “
“ Okey Mage “ na hapo hapo simu ilikatwa .
ITAENDELEA .

0687151346
 
Moja ya simulizi zangu bomba zaidi
2HOURS OF MEMORIES
weka oda mapema upate bei ya punguzo


Kesho jioni naweka mzigo wakjuu
LIJIKITABU-1.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom