Nimekuwa nafuatilia sana siasa za mageuzi ya nchi yetu!
SImfahamu sana Godbless Lema, lakini nilikiwa Arusha uchaguzi wa 2005, alishindwa kwa kura kadhaa,inaaminika kulikuwa na "zengwe", Mrema (kama sikosei, wa CCM akapita)....Hapo ndipo alipoibuka Godbless Lema! Kipindi kile hakuwa mtu mwenye vurugu kama nimjuaye leo.....
Tundu Lissu, nilikuwa namfahamu akiwa anatetea haki za watanganyika, mambo ya ardhi n.k, amekuwa mwanaharakati makini, amehudhuria na kutoa mada mbalimbali katika majukwaa ya kuelimisha umma n.k Kiukweli nilikuwa namuona ni msomi makini na mwerevu1
Hawa wanasiasa wawili wanafanana sana namna walivyoingia na kupat aumaarufu kwenye siasa...Tundu Lissu, na Godbless Lema wote wakaibuk atena 2010 kwa kushinda viti vya ubunge...wot ekwa mbinde!
Hivi karibuni nimekuwa nikifuatilia sana yanayotokea CDM, hawa jamaa wawili wapo katika usukani wa sakata lilnaloendelea CDM; Tundu Lissu (eti mwanasheria wa CDM) ametangaza kuwa "ZITO KABWE, MKUMBO NA M.KITI ARUSHA" eti "WAMEFUKUZWA"???
Godbless Lema ndiye mpika majungu wa M1, M2, M3 etc...waraka ambao hata uongozi wa CDM umesema hautambui!!
Sasa kama uongozi hauutambui huo waraka kina ZZK wamefukuzwaje?
Je CC ina mamlaka ya "kumfukuza" mwanachama? ama ni Baraza Kuu?
Mimi naona, CDM inakwisha, INAKUFA! WHY? Kwa sababu wanatumia siasa za majitaka za Lissu na Lema...na wengine wachache! Hata watu makini kama Mnyika na Kamanda Mbowe wanashawishika na siasa hizi?
CDM 2015 itrapoteza sana voti Bungeni, na what I see MBOWE, LEMA, LISSU, MNYIKA na MDEE watapoteza nafasi zao Bungeni.
CDM inapoteza muelekeo kwa kuwa imealika watu kwenye madaraka AMBAO SIYO WANASIASA!