Kajunjumele BA
JF-Expert Member
- Jan 3, 2012
- 673
- 351
Inashangaza kuona vichwa mbalimbali vya habari vikishabikia sakata la akina Zitto Kabwe kama ndio anguko au mpasuko ndani ya CHADEMA. Binafsi sioni kama kuna mpasuko wala vipande ndani ya CHADEMA ila naona kinazidi kuimarika baada ya kugundua mbinu za usaliti na hujuma ambazo zingefanikiwa zingechangia kukivuruga chama.
Ndugu yangu amakyasa, nakubaliana nawewe kwamba huo Mpasuko unaonekana na hao wa "handisi" wa habari lakini "waandishi" wa habari wanajua kabisa kwamba CHADEMA imewajibisha pandikizi na kimsingi waandishi wa habari ni wachache sana wengi ni "WAHANDISI" wa habari.
Akili zao ndo ziko vipandevipande kwani zimegawanyika upande maslahi binafsi,upande ajira na upande Taaluma hivyo zina shindwa kuona jambo kwa uhalisia wake wanaishia kuona maluweluwe na vipandevipande kutegemeana na akili na utashi wake umeathiriwa vipi na rushwa ,ukabila wake ,udini na ujinga wa kujitakia.
Si unakumbuka hata Mkapa wakati wa kipindi chake alisema Tanzania haina waandishi wa habari anaoweza kuhojiana nao kwani uwezo wao wakuelewa uko chini sana. Lakini na sisitiza kwamba kwa mtazamo wangu simaanishi waandishi wote kwamba wana silika ya namna hii ila wengi sana ni "kanjanja" kiasi ya kwamba wanawafunika waandishi waadilifu.