nabiidaniel
JF-Expert Member
- Feb 25, 2014
- 2,087
- 2,855
Ivi jamani, mmeshasema ni namba ya shetani! Unaitaji nini kutoka kwa shetani???
Kuna watu wanamhitaji shetani mfano:
1. Wachawi kila siku kabla ya kuwanga lazima wakutane na MKUU WA GIZA atoe maelekezo ya wapi na ruhusa ya nani wa kumdhuru na aina ya madhara, pia watoe report ya jana yake, wanaokosea adhabu hapohapo ikiwemo kuuwawa
2. Waganga wa kienyeji (ambao sio matapeli) kabla ya kutibu lazima awasiliane na MKUU WA GIZA aelekezwe kuhusu dawa na masharti kwa mteja, na kwamba Shetani atapata nini kwa kusaidiwa huyo mteja, lazima shetani apate uhai wa ndugu (damu), au ampandikizie mabalaa mengine kwa familia au kizazi chake
3. Watafuta utajiri, hawa lazima wajisalimishe kwa wakuu wa giza na watoe UZIMA wao, simaanishi uhai wa mwili, la, ni uzima wa kiroho, kwamba wapewe utajiri lakini hawawezi kupata TOBA tena, yaani hata wakitubu vipi, wakawa viongozi wa dini wanauhakika wa kwenda jehanum. Baadhi yao huitwa freemasons, satanist nk
Katika kitabu cha Hesabu... LAKINI MTU AKIFANYA DHAMBI YOYOTE KUSUDI, HUYO AMTUKANA BWANA...