Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,920
- Thread starter
- #181
Unamfananisha mtengeneza gari, ambaye hata chuma anachotumia kutengeneza b ari hakitengenezi na mungu aliyeumba vyote?
Kanuni ya kufananisha vitu inakutaka kufananisha vinavyofanana.
Kwa kumfananisha mtengeneza gari, ambaye hata chuma anachotumia kutengeneza gari hajakiumba from scratch na mungu ambaye mnadai kaumba kila kitu from scratch na ana ujuzi wote na uwezo wote unaonyesha kutoelewa kanuni za kufananisha vitu na hivyo kuchanganya mambo.
Hapo ndipo unapolosea.
Unaangalia ujuzi wa huyo unayemdai kuwa mungu, mjuzi wa yote na muweza yote kama unavyoangalia ujuzi wa binadamu, wakati binadamu hawezi yote na hajui yote.
Una tatizo la kimsingi kabisa katika fikara zako nzima kuhusu kumuelewa huyu mungu wako.
Kwa upande mmoja umempaza awe mjuzi wa yote na muweza yote, kwa upande mwingine umemshusha awe sawa na nwanadamu tu.
Chagua moja.
This is a contradiction.
Hapana,hakuna kujikinza kokote hapo;
Nilichokifanya nilitumia mantiki ya swali lako kukupa mfano wa kimantiki kuhusu mtengeneza gari na mwendeshaji,nilidhani kuwa unaweza kuling'amua hili kumbe huwezi,pole sana
Point ya msingi hapo ni namna ambavyo kanuni na tabia zote zilizoko ulimwenguni hazihusiki na maamuzi binafsi ya kila mmoja wetu bali zinafanya kazi kama zilivyo
Nilikuambia kuhusu kanuni ya mvuto vile ambavyo inakupa unachokihitaji kwa kufikiri,sijui kama ulioona hii au hata hukusoma
Kanuni zimewekwa kusimamia viumbe kupata vile ambavyo vitataka kwa hiyari yavyo na sio kuvipangia cha kupata kama vile ambavyo muendesha gari hapangiwi mahali pa kupita na mtengeneza gari!