Uhusiano wa namba hizi na majini,Shetani ....

Uhusiano wa namba hizi na majini,Shetani ....

Inaonekana hujasoma nilichoandika na kama umesoma hujaelewa

Hoja yangu sio wahusika wa utengenezaji wa uumbaji,bali hoja yangu ni kwenye kanuni amazi tayari zimewekwa kama zinahusika kumpangia mambo mtumiaji au hazihusiki

Kama hata hili umeshindwa kilielewa au umeshindwa kuchora line between wawekaji kanuni na kanuni zenyewe utapata dhida sana kuelewa mambo ya Mungu

Kwa kukusaidia soma swali lake la kwanza lililozaa jibu langu,ukichemka na hapo sitakuwa na namna ya kukusaidia dada yangu!

Kanuni na wawekaji kanuni ni separate entinty? Kwahiyo hizo kanuni nani anazi govern?
 
Kaka mara nyingi skype numbers ndo zinakua hivyo au other associated VOIP services, mfano mie naweza kuamua ni customize number gani ila by default zinakua hivyo.
 
Wakuu,

Sina kawaida ya kudharau jambo hata kama linaonekana ni la kijinga na nimeshapata faida kubwa kutokana na mtazamo wangu huu,nimeshafanikiwa kwenye mambo mengi ambayo watu waliyaona ni ya kijinga na wengine walijifunza kupitia hili

Leo naomba niwashirikishe jambo hili ambalo ni mewauliza watu kadhaa na wameonekana kunishangaa mtu kama mimi ni kwanini hasa nimeamua kulifuatilia hili,lakini najua kupitia hili naweza kujifunza kitu ambac ho sikua nakijua au nikajikuta napoteza muda wangu,yote haya ni matokeo na nimejiandaa kwa yote

Kuna namba watu wamekuwa wakidai kuwa kama unataka kuzungumza na Shetani au majini basi unaweza kuzipiga,kuna jamaa yangu aliwahi kuzipiga nikiwa nae na simu iliita na ikapokelewa halafu aliulizwa shida yake na alisema lakini aliepokea simu alimuambia kuwa "huwezi wewe na usitusumbue"

Kuna jamaa yangu mwingine alipiga nae simu ilipokelewa na aliambiwa kuwa wapo busy hivyo hawahitaji usumbufu

Ukiangalia namba hizi hazina namba kiunganishi ili ujue hata location ya namba hizi,kitu hiki kimenifanya nijiulize sana kama hii inakubalila kwa mamlaka husika za mawasiliano

Sina ufahamu hasa wa mambo ya mawasiliano na nadhani hapa kuna watu wengi wanaweza kunipa maelezo ya kutosha na nikaridhika kuhusiana na dhana hii kuwa namba hizi ukipiga unazungumza na shetani au majini,sidhani kama jambo hili halina maelezo kwa wale ambao wanajua kuhusu mawasiliano na ndio maana nikaamua kuja kuuliza hapa ili jambo hili niachane nalo

Namba zenyewe ni 11111111111 na 999999999 nadhani zipo na zingine,hebu wakuu nisaidieni hapo ili niweze kujua

Nikwanini hakuna namba kiunganishi lakini simu inaita?
Je ni akina nani wanaopokea simu hizi?

Karibuni ....

Mkuu juve2012 hebu sogea pan de hizi tuendelee kujifunza mambo haya,karibuni na wengine pia .....!!

111 ni free crime stopper ya vodacom. Usitishike na uwingi wa hizo namba maana mtandao unaishia kutambua kwenye idadi ya tarakimu za kimtandao. Mfano chukua simu nyingine andika namba yako kwa usahihi kisha ongeza namba kwa uwingi unaoutaka mbele yake na kupiga, utaona ikiita kwako. Mfano namba yako ni 0702878282 waweza andika 0702878282826782865432 na bado ikaita kwako.
 
Last edited by a moderator:
Ana uwezo wote, anajua yote na yupo kila mahali. Sijui kama unaelewa ipasavyo tafsiri na depth ya haya maneno

Inaonekana huelewi swali langu ...

Chukulia tu sijui maana ya hayo maneno,sasa nakuuliza,kuweza yote,kujua yote,kuwepo kila mahali kunahusikaje na kumpangia binadamu yale ambayo anafanya kila uchao?

Nahitaji ufafanuzi hapo ili tuone nani ambae haelewi hapa kati yetu wawili!
 
Kanuni na wawekaji kanuni ni separate entinty? Kwahiyo hizo kanuni nani anazi govern?

Kanuni na wawekaji wanaweza kuwa sio separate lakini unaweza kujadili kimoja bila kuhusisha kingine

Watu wameshajadili kanuni ya uvutano bila hata kumjua aliyeiweka [kwamujibu wa sayansi]

Kusimamia kanuni na kanuni kuhusika kwa mtumiaji kwenye suala la kumuamulia cha kufanya ni mambo mawili tofauti

Hapo ndipo ambapo mnashindwa kuelewa ...!!
 
111 ni free crime stopper ya vodacom. Usitishike na uwingi wa hizo namba maana mtandao unaishia kutambua kwenye idadi ya tarakimu za kimtandao. Mfano chukua simu nyingine andika namba yako kwa usahihi kisha ongeza namba kwa uwingi unaoutaka mbele yake na kupiga, utaona ikiita kwako. Mfano namba yako ni 0702878282 waweza andika 0702878282826782865432 na bado ikaita kwako.

Nakushauri mkuu rudia kusoma nilichoandika halafu u-comment tena!
 
1. Kuna mtu mwingine anaezijua hizi namba?
2. Kuna mtu mwingine amewahi kuzipiga hizo namba?
3. kuna mtu anaejua gharama za kupiga hizo simu??
4. Ni kweli anaejibu ni shetani au ni watu wenye mashetani??
5. Wanatoa huduma gani hasa??
Nadhani haya ndio maswali ya kujadili badala ya kupotezeana muda.
 
Nakushauri mkuu rudia kusoma nilichoandika halafu u-comment tena!

Nadhani pia hujaelewa nilichokiandiaka. Kwa ufupi ni kwamba 111111111 ukipiga (to be specific kwa mtandao wa vodacom) itakuunganisha na free crime stopper ambayo wameipa special number 111.

Hivyo hakuna uhusiano wowote wa majini/shetani na namba 111111111 kwa mtandao wa vodacom.
 
Nadhani pia hujaelewa nilichokiandiaka. Kwa ufupi ni kwamba 111111111 ukipiga (to be specific kwa mtandao wa vodacom) itakuunganisha na free crime stopper ambayo wameipa special number 111.

Hivyo hakuna uhusiano wowote wa majini/shetani na namba 111111111 kwa mtandao wa vodacom.

Ndio maana nikakuambia urudie kusoma mkuu kwasababu haya maelezo yako yamejibiwa kwenye maelezo ya mada pamoja na baadhi ya wachangiaji

Hebu soma mada halafu soma na maoni ya wachangiaji halafu utaona!
 
Ndio maana nikakuambia urudie kusoma mkuu kwasababu haya maelezo yako yamejibiwa kwenye maelezo ya mada pamoja na baadhi ya wachangiaji

Hebu soma mada halafu soma na maoni ya wachangiaji halafu utaona!

Mkuu mimi nimesoma post yako na kujibu maswali yako mawili ya mwisho wa post. Au labda ujikumbushe ulichouliza halafu uone kama post zangu zimejibu au la!

I admit kuwa sijasoma majibu au hoja za wengine ila nilijikita moja kwa moja kwenye maswali uloyouliza.
 
Uzi ulikuwa mzuri,ila umeniacha na maswali mengi!
 
Back
Top Bottom