Uhusiano wa Franco na Mobutu

Uhusiano wa Franco na Mobutu

Sijawahi kuzipenda nyimbo za Franco hata kidogo; nilikuaga shabiki wa Pepe Kalle, Nyboma, mzee wa Nzawisa na kidogo hapo katikati ya miaka ya 90 yule jamaa aliywahi chezeaga Yanga na baadae kugeukia music (nimemsahau jina, wazee wenzangu nikumbusheni). Franco na kijana wake Madiluu Sysytem wala though baada ya Franco kufariki, Madiluu alikuja kutoa album yake kama solo artist, ilibamba sana; thanks for the nice history anyway brother.
Watoto zitafuteni nyimbo hizo YouTube mtazipata
Sawa mkuu tuachie sisi tufurahie vitu adimu na midundo adimu. Franco was a genious hana mfano.
 
Wakuu habarini za muda huu,

View attachment 717548
View attachment 717549

Zimeanzishwa thread nyingi kuhusu Franco na Mobutu, historia ya Mobutu imeelezwa na ya Franco pia, leo naleta historia ya uhusiano wa watu hawa wenye majina makubwa Africa na ulimwenguni, mwanasiasa na gwiji la muziki.

View attachment 717532
View attachment 717529

KUNYONGWA KWA KINA EVARISTE KIMBA

Mnamo mwaka 1965 Mobutu anakua rais wa Zaire na kuagiza kunyongwa kwa watu zaidi ya 6 wengi wao wakiwa mawaziri wa serikali aliyoipindua katika eneo la matonge jijini Leopold Ville (Kinshasa) kwa kosa la uhaini, mamilioni ya watu wanashuhudia hadharani, mmoja wao ni Franco, baada ya hapo Franco akatunga nyimbo iitwayo Luvumbu Ndoki (Luvumbu mchawi) hii ni hadithi ya kikongo kuhusu Mfalme Luvumbu aliyeuwa ndugu zake wa karibu kwa ajili ya kujinufaisha.

Nyimbo hii inaonekana na mamlaka kama dhihaka kwa mobutu kutokana na kitendo chake cha kunyonga mawazili wale Franco anakamatwa na kuachiwa alafu anakimbilia Brazaville kwa miezi 6 mpaka pale mambo yalipokuwa shwari.

AUNTHENTICATION POLICY (Zairenisation)

Mnamo mwaka 1971 mobutu anabadili jina la Congo kuwa Zaire, sarafu kua Zaire, pamoja na miji kuitwa majina ya kiafrika, Leopoldville inakua Kinshasa, Elizabeth Ville inakua Kisangani na kadhalika, kutokana na sera ya uafrika mpaka majina ya watu yanabadilishwa.

Bendi ya Franco, Tp Ok jazz inaandamana na mobutu nchi nzima kueneza sera ya mobutu na kutoa album iitwayo belela unthenticite na congress ya mpira.

MALIPO YA KAZI

Mobutu anampa Franco eneo la ardhi pale Kinshasa, Franco anajenga night club iliyoitwa un Deux trois, pia Mobutu baada ya kubinafsisha kampuni za kigeni anampa Franco kampuni ya muziki iitwayo mazadi.

JACKY NA HELEINE(nyimbo za Franco)

Franco añatoa nyimbo mbili Jacky na heleine ambazo serikali iliziona hazina maadili na kumpa Franco kifungo cha miezi 6 jela, na bar yake kufungwa miezi 2, alivobisha kua hazina maadili mama yake alisikilizishwa, yote haya yalifanywa na Kengo wa Dondo aliyekua attorney general.

Mobutu anamtoa jela Franco baada ya week 3 na kumshusha cheo Kengo wa Dondo kua balozi wa Zaire nchini Ubelgiji, Franco anaimba nyimbo ya kumponda Kengo iitwayo trailleur (anasema fundi nguo akikinyanganya sindano utawachomaje watu? Yaani kengo kaporwa madaraka na Mobutu)

Franco anaimba lettre a mr le directeur general (barua kwa director general) nyimbo ambayo añawaponda viongozi wa serikali kwa rushwa na usimamizi mbovu, hii inachukuliwa na wengi kama diss song kwa Mobutu.

Mwka 1984 anaimba nyimbo ya kumsifu Mobutu iliyoitwa Candida na biso, wakati wa uchaguzi ambapo watu walitakiwa kujibu ndio au apana kama wanamtaka Mobutu, hakukua na wapinzani.

Mobutu alifadhili band nyingi kubwa za muziki nchini Zaire, ikiwemo TP OK JAZZ


KIFO CHA FRANCO

Franco anafariki jijini Ubelgiji mwka 1989, Mobutu akiwa Ufaransa ziarani,
Mobutu anatangaza siku 4 za maombolezo na radio zote kupiga nyimbo za Franco tu, mwili wa Franco unapelekwa Palais du people kuagwa
View attachment 717547

Mobutu aliporudi aliitembelea familia ya Franco pamoja na kaburi.

Kwa kiasi kikubwa Mobutu alimtumia Franco katika ku mobilize watu kwenye siasa zake na pia Franco alinufaika sana kwa kuendesha magari ya kifahari kama mercedes benz na kuishi vizuri, kuliko wanamuziki wengi wa Congo na nje ya Congo

Kwanz nikupongezee mkuuu kwamb wew nimfuatiliaj na mi napnda xan kujua histria ya huyu jmaaa mobutu vp naeza pata wapi maelezo zaid kuhuc huyu mobutuuuuu mkuuu????
 
Marehemu Thierry Mantuika Kobi huyu ndo alifundishwa ule upigaji gita la Luambo (Mi solo) hivyo nyimbo nyingi Franco alikuwa na hamsini zake kobi akipiga Mi Solo (gitaa chombezi). Mara nyingi alishirikiana na Marehemu Jerry Dialungana Kasi akiwa kwenye solo gitaa. Hawa waliingia OK Jazz kati ya 1976-1978. Wapigaji solo wengine wakati huo walikuwa Franco mwenyewe (Mi solo), Papa Noel (1978), Dizzy Mandjeku (1986 or 88).
 
Sawa mkuu tuachie sisi tufurahie vitu adimu na midundo adimu. Franco was a genious hana mfano.
Nakubaliana na wewe kabisa mkuu, unajua mambo ya music ni ya ajabu sana, ni kama mapenzi tu; demu unaye muona we mkali wenzio wanaona wa kawaida sana, miaka hiyo ya kina Franco ndio kina Michael Jackson nao walikua kwenye pick kimuziki, huwezi amini kaka, sijawahi kupenda nyimbo za kizungu kabisa except ule wa the Londoners baaasi, ila nyimbo za kina Pepe, Nyboma na wale wengine nimewataja hapo ju, aise ilikua lazima ninunue cassette zao, tena kaka uzi hu umenikumbusha ile studio ya kupiga copy ilikua mapipa pale inaitwa BINGO records, ilikua na kauri mbiu yake ya hivi, "muziki husahaulisha dhiki" Noma sana aise.
 
Marehemu Thierry Mantuika Kobi huyu ndo alifundishwa ule upigaji gita la Luambo (Mi solo) hivyo nyimbo nyingi Franco alikuwa na hamsini zake kobi akipiga Mi Solo (gitaa chombezi). Mara nyingi alishirikiana na Marehemu Jerry Dialungana Kasi akiwa kwenye solo gitaa. Hawa waliingia OK Jazz kati ya 1976-1978. Wapigaji solo wengine wakati huo walikuwa Franco mwenyewe (Mi solo), Papa Noel (1978), Dizzy Mandjeku (1986 or 88).
Kuna mwingine pia anaongezeka hapo kwenye solo anaitwa micherino Visi Mavatiku.
 
Michelino1.jpeg
 
Baadhi ya wanamuziki nyota wa OK Jazz. Kutoka kulia Simaro Lutumba (1961-1993) Rhythm guitar, Josky Kiambukuta 1973, Ntessa Daliensti (Muzi), Malage de Lugendo(1980's), Madillu (1980), Youlou Mabialla Mwana wa Luambo, Mwana wa OK Jazz (1966) ndo muimbaji peke yake ambaye bendi yake ya kwanza kuimba ni OK jazz wengine wote waliingia wakiwa wametoka kwenye bendi zinazofahamika, Mangwana (1972) Ndombe (1975?) wote hao waimbaji. Hao wa mwisho wawili ni Jerry Dialungana(solo ) na Thierry Mantuika (Mi Solo)
 
Baadhi ya wanamuziki nyota wa OK Jazz. Kutoka kulia Simaro Lutumba (1961-1993) Rhythm guitar, Josky Kiambukuta 1973, Ntessa Daliensti (Muzi), Malage de Lugendo(1980's), Madillu (1980), Youlou Mabialla Mwana wa Luambo, Mwana wa OK Jazz (1966) ndo muimbaji peke yake ambaye bendi yake ya kwanza kuimba ni OK jazz wengine wote waliingia wakiwa wametoka kwenye bendi zinazofahamika, Mangwana (1972) Ndombe (1975?) wote hao waimbaji. Hao wa mwisho wawili ni Jerry Dialungana(solo ) na Thierry Mantuika (Mi Solo)
Sasa mbona mnatuchanganya.... Jamaa hapo wanasema franco aliambukizwa ukimwi hawara yake .. wewe unakataaaa..
 
Yollou Mabiala ana sauti nzuri ya aina yake akikaa na Wuta Mayi utapenda.
 
Mavatiku alipoingia OK Jazz 1975 ndo Franco alipohamia kupiga Mi Solo na Mavatiku akawa anapiga solo gitaa. Jamaa mahiri sana. bahati mbaya kuna wakati Franco aliwahisi wanampamgo wa chini kwa chini kuanzisha bendi (mavatiku na ndombe) ndo ukawa mwisho wao. ndombe alikuja kurudi baadae. Mavatiku yeye alirudi kwenye project ya Lisanga ya Banganga (Franco, Ley na Mavatiku). Na josky alitupia sana hapo mavocal. Hao niliowataja hapo ukiacha Franco wote ni baada ya Mavatiku. Usimsahau Fan Fan na Bholen huko nyuma.
 
Sijawahi kuzipenda nyimbo za Franco hata kidogo; nilikuaga shabiki wa Pepe Kalle, Nyboma, mzee wa Nzawisa na kidogo hapo katikati ya miaka ya 90 yule jamaa aliywahi chezeaga Yanga na baadae kugeukia music (nimemsahau jina, wazee wenzangu nikumbusheni). Franco na kijana wake Madiluu Sysytem wala though baada ya Franco kufariki, Madiluu alikuja kutoa album yake kama solo artist, ilibamba sana; thanks for the nice history anyway brother.
Watoto zitafuteni nyimbo hizo YouTube mtazipata
Yule aliyechezea yanga anaitwa Mayaula Mayoni mzee wa Mbongo, namfagilia sana nyimbo zake slow flani hv lkn tamu sana.
 
Sijawahi kuzipenda nyimbo za Franco hata kidogo; nilikuaga shabiki wa Pepe Kalle, Nyboma, mzee wa Nzawisa na kidogo hapo katikati ya miaka ya 90 yule jamaa aliywahi chezeaga Yanga na baadae kugeukia music (nimemsahau jina, wazee wenzangu nikumbusheni). Franco na kijana wake Madiluu Sysytem wala though baada ya Franco kufariki, Madiluu alikuja kutoa album yake kama solo artist, ilibamba sana; thanks for the nice history anyway brother.
Watoto zitafuteni nyimbo hizo YouTube mtazipata
kama hukuwahi kupenda Mziki wa Franco basi hujawahi penda muziki kabisa ndugu yangu
 
Pepe Ndombe yeye alikuwa mzuri sana kwenye kuimba peke yake.
Uimbaji wa pekee sijui nani alikuwa zaidi fikiria Mangwana (mabele), Djo Mpoyi, malage, Carlyto na Madilu. Ndombe nafikiri aiimba mwimbo wake tu wa Voyage du Bandundu. Ndombe, Josky na Ntessa nafikiri hawa walikuwa ndo wakali wa nyimbo za kuita na kuitikia. Hapo hatujawazungumzia waimbaji wazamani (Vicky, Edo, Boyibanda, Youlou, Kwany, Mujos etc)
 
Back
Top Bottom