Uhusiano wa Franco na Mobutu

Uhusiano wa Franco na Mobutu

Ninachokiona hapa kwenye bandko lako Mkuu,Franco alikuwa akicheza na akili za Mobutu Seseseko Wa Nzabanga na alifanikiwa!
Simaro ameeleza kuhusu hawa watu wawili. Mobutu alikuwa fanatik (shabiki) wa Franco na OK Jazz hivyo alipopata uraisi aliendelea kutumia fursa hiyo na sherehe zake nyingi alitumbuizwa na Franco. Franco nae alitumia fursa hiyo ipasavyo. Ni kweli pia bendi nyingi zilipata fursa kama hiyo lakini OK Jazz walikuwa mbele zaidi.
 
Franco alikuwa rafiki wa Mobutu lkn walikuwa wanakosana na kupatana
pia kuna kisa kimoja mwaka 1973 Franco na mdg wake walikuwa wanagombnia demu sasa mdg wa Franco akaamua kusafiri na huyo demu ktk gari mdg wa franco akaamua kuangusha gari maksud ili wafe wote lkn huyo demu alivunjka mguu ila Jamaa akafariki
Siongo Bavon Marie Marie alifariki 1970. Alipata ajali baada ya kuto kuelewana na Kaka yake. Kwa uhakika wa kifo cha huyu bwana muulizeni Papa Chimanga Assosa wa Bana Marquiz (rafiki yake marehemu Bavon) mwanamuziki wa Zamani wa Negro Success kupitia RTD FM kipindi cha Kavasha Time yuko kila Jumamosi na Mtangazaji Nguli Mbazigwa Hassan. Hapo pia utapata taarifa nyingi na muziki wa zamani wa DRC. Si kweli kwamba Bavon alitaka kujiua.
 
Franco alipata ukimwi miaka ya 1980's na hawara yake alikuwa mwanamuzk ktk bendi ya okk jazz alieitwa mpongo love
Watu wanamlengesha Mpongo Love kwa OK Jazz- nijuavyo hakuwa mwanamuziki wa OK Jazz bali alikuwa na uhusiano mkubwa na bendi hiyo. Le Professor Empopo Deyes Loway (Saxaphonist OK Jazz) ndo alikuwa mentor mkubwa wa Mpongo Love. Alishirikiana na Mayaula Mayoni (Ndaya), Simaro Lutumba. Kwenye album yake moja back up voice ilikuwa ya Wuta Mayi (OK Jazz).
Kwa mara ya kwanza kuwa Mpongo Love alikuwa hawara wa Franco nausikia hapa-sidhani kama ni kweli.
 
labda umesahau,hebu fwatilia historia ya mpongo love,mwaka 1977 Franco alimsajili mpongo ktk band alikaa miaka miwili okk jazz,hata wimbo wake "ndaya"aliutunga kwa msaada wa Franco,hebu fwatilia
mpongo love alifariki 1994
Mwimbaji aliyekaa muda mfupi ni Jollie Detta : massu
 
Mimi huwa zinanichanganya hizi Congo mbili, Brazzaville na Congo Kinshasa, hebu nipeni itofauti hapo, hawa wanamuziki kina Koffi, Werrason n.k wanaishi Congo ipi? Kabila anaongoza Congo ipi? Congo ipi ni maarufu kuliko nyingine na kwa nini?
 
M'pongo Love hajawahi kuimbia O.K. Jazz, ubishi wa nini? Ndaya ni wimbo wa Mayaula Mayoni, aliutunga na kumpa Mpongo aimbe katika bendi yake (bendi ya M'pongo).
Kuhusu huo wimbo uko sahihi kabisa ulitungwa na Mayaula lakini ulipigwa na Tp OK jazz.
 
Nijuavyo Tabu ley alikuwa akishirikiana na Dr Nico Kasanda wakiwa na bendi ijulikanayo African Fiesta kabla ya Tabu ley kujitenga na kuanzisha Afrisa international
Tabu Ley Rochereau alianza muziki African Jazz ambako alikutana na Dr Nico, Dechaud Mwamba kaka wa Dr Nico na Tino Baroza (Mjomba wa Dr Nico). Walipomkimbia Grand Kalle ndo wakaanzisha African Fiesta, walipotengana na Dr Nico ,Ley akunda African Fiesta Le People baadae akaiita Afrisa International na Dr Nico akaja na African Fiesta Sukisa. Ley hajawahi kuwa mwana OK Jazz.
 
1991-07-09_Lola-Aime-Josky-Ndombe-Diatho.jpeg
 
Vipi Josky Kiambukuta, yeye hakuwa generation ya Franco. Kuna wimbo niliona kaimba na madilu alikuwepo ndani unaitwa kitu kama 'Chandra'
Jo Sex , Le Commandant de Bord Josky Kiambukuta alizaliwa 1949 na kuanza muziki 1969 African Fiesta Sukisa chini ya Dr Nico, alipotoka hapo akafadhiliwa kuanzisha L'Orchestre Continental na 1973 akaingia TP OK Jazz alikopelekwa na Simaro (mwenyewe alitaka kwenda kwa Tabu Ley). OK Jazz ilianzishwa 1956 Franco akiwa 18.
 
Sijawahi kuzipenda nyimbo za Franco hata kidogo; nilikuaga shabiki wa Pepe Kalle, Nyboma, mzee wa Nzawisa na kidogo hapo katikati ya miaka ya 90 yule jamaa aliywahi chezeaga Yanga na baadae kugeukia music (nimemsahau jina, wazee wenzangu nikumbusheni). Franco na kijana wake Madiluu Sysytem wala though baada ya Franco kufariki, Madiluu alikuja kutoa album yake kama solo artist, ilibamba sana; thanks for the nice history anyway brother.
Watoto zitafuteni nyimbo hizo YouTube mtazipata
 
Back
Top Bottom