Ugwadu! Kiboko ya mchawi

Ugwadu! Kiboko ya mchawi

Sawa sawa, lakini ni utafiti upi umeufanya mpaka kufikia kuthibitisha dai hilo? je utajuaje wachawi wamekuja ama hawakuja?
Umeambiwa dalili zakutembelewa na hao jamaa - wachawi kwamba ni pamoja na kuota unakula vitu viisivyoeleweka, kujitafuna wakati umelala ... ukiona hivyo ujue kuna jamaa wanakuchezea usiku .. kinga yao umepewa .. unauliza nini tena rafiki yangu?

Yapo mengi ambayo nimewahi kusumbuka nayo na nilipopewa kinga yake sikuyaona tena. Mfano nilipohamia nyumbani kwangu, ilipokuwa ikifika usiku mida ya saa 06 hivi nilikuwa nasikia mambo ya ajabu kwenye bati, nilipojaribu kuwaeleza jamaa zangu walinambia nitafute maji ya baraka ninyunyizie kila pembe ya nyumba na mengine nirushe juu ya bati ... sikusikia tena.

Sikuwa na imani na hayo mambo ya wachawi lakini nilipojaribiwa ndo nikaambiwa la kufanya ..
 
75c854470c3eb4d87e7f7d54f61847f9.jpg
Unaweza kuona ni kitu cha kufikirika au cha maskhara lakini mchawi na ndimu ni vitu viwili tofauti kabisa
Mchawi anapenda sana damu na damu kwenye ndimu inaganda fasta...pengine hiki ndio kisa kikuu
Ukiwa na mauzauza usiku ukiwa unaota ndoto za ajabu hasa kulishwa vitu na kujitafuna mdomo lala tu na kipande cha ndimu na kulamba pia !
Jamaa wakija tu kuna hiyo malighafi hawasogei au wataenda kujipanga upya. .....
47ae1e689511708025638d5f26237cd9.jpg
Ni imani yako. Ila Jina ya Yesu Kristu ndilo jina kuu.
 
Hapa tupate tofauti kati ya matunda haya:-
Ndimu,
Limao ..
Au vyote vinafanya kazi sawa?
Limao/limau kuna wakati huiva na kuwa tamu hivyo sio malighafi nzuri sana
 
  • Thanks
Reactions: MC7

Similar Discussions

Back
Top Bottom