UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

Hili sio suala la dini. Na kama lawama za Nyerere zinakuja, zije kwa siasa zake katika masuala ya elimu.

Shule zilizotaifishwa nyingi zilikuwa za dini lakini sehemu kubwa ya funding ilikuwa inatoka serikalini. Hivyo Nyerere alifanya vizuri kutaifisha shule. Nyerere alisomeshwa kwa schoolarship ya serikali lakini kazi alipangiwa katika shule ya dini. Na haya yalikuwa mapungufu makubwa ya serikali ya mkoloni.

Pamoja na kutaifisha hizo shule na kuzifanya kuwa za taifa, sera zake za kuendeleza elimu zilikuwa mbovu sana. Mpango wa UPE ambao ulikuza literacy rates ulikuwa ni mbovu. Wataalamu wa mambo ya elimu walitoa mapendekezo yao kuwa ili UPE iwe na mafanikio bila kupunguza kiwango cha elimu, ni lazime mpango uwe wa miaka 20 (long term). Mapendekezo hayo aliyakataa na kusema UPE inaweza kufanyika kwa mpango wa miaka 7 tu. Na katika mpango wake huo akatumia walimu wasio na mafunzo. Na matokeo mabovu ya mfumo mzima yalianza kuonekana kabla ya yeye kuondoka madarakani. Na kama mipango yake ingekuwa mizuri katika UPE, serikali ya Mkapa isingerudia kufanya mpango uliofanana na UPE miaka michache iliyopita.

Pamoja na kuongeza shule nyingi wakati wa mpango wa UPE bajeti ya elimu haikuongezeka kukidhi mahitaji ya wizara hiyo. Hivyo kuwa na sera na kutotoa pesa za kusaidia sera hizo ni sawa na kutokuwa na sera zenyewe.

Pia alikuwa nyuma sana katika sera za elimu ya juu. Model yake ilikuwa kwa watu wengi kuwa na elimu ya darasa la saba. Baada ya kundi hilo kuwe na kundi watu waliomaliza vyuo vya kati ambao watakuwa kama viranja. Na baada ya kundi hilo liwepo kundi la wachache wenye elimu ya juu watakaongoza wenzao.

Mfumo huu ulizungumzwa kwanza na William Edward Burghardt DuBois (mmoja wa waanzilishi wa Pan Africanism). Yeye alisema kuwa hili watu weusi waendelee ni lazima wawe na talented ten (asilimia kumi ya wenye vipaji).

Matalajio yalikuwa ni kutoa watu wenye vipaji kuendeleza jumuia zao. Siku za mwisho wa maisha ya DuBois alisema hawa talented ten wamekuwa ni dissapointment kwa jumuia za watu weusi. Badala ya kutumikia jumuia zao wamekuwa Bourgeoisie na mchango wao ni mdogo katika maendeleo ya mtu mweusi.

Watanzania wengi wanapoteza muda katika vyuo vya kati. Kwa maoni yangu vyuo vya kati vifanyiwe marekebisho hili viwe vyuo vinavyotoa digrii. Na wataalamu wa ngazi za kati (Viranja) wawe ni watu wenye digrii na sio diploma. Wahitimu wenye digrii wafanye kazi kama viranja katika miaka mitatu mpaka mitano ya mwanzo (Entry and Junior level). Na baada ya miaka hiyo waweze kushika senior position, lakini hizo senior position zitegemee performance yao ya miaka iliyopita.

Ukiajiri wanafunzi kutoka shule na darasa moja, bado kutakuwa na tofauti kati yao. Ukichukua wanafunzi kutoka shule moja campus tofauti, bado kutakuwa na tofauti. Na vile vile tofauti kati ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali ni kitu cha kutegemewa lakini sio cha kufanya chuo moja kuwa bora zaidi ya kingine. Mwajiri anapotoa ajira kwa wahitimu wapya ni lazima kutoa mafundisho ya utamaduni wa sehemu yake ya kazi, matarajio ya mwajiri na baadaye atumie angalau mwaka kuona ni jinsi gani mwajiriwa anafanya kazi yake vizuri.

Mpaka sasa utasikia wanasiasa wetu au wenye elimu ya juu Tanzania wanasema kutoa digrii kwa watu wengi kutawafanya wahitimu kuwa madreva wa taksi kama ilivyo Nigeria au Ghana. Kwa maoni yangu msimamo huu ni PURE CRAP. Watu wasinyimwe elimu kwa sababu ya ukosefu wa kazi. Mwenye digrii akiwa dreva wa taksi anafanya kazi hiyo kama stepping stone na lazima atakuwa na shughuli zingine za kuendeleza maisha. Mwenye elimu ndogo akiwa dreva wa taksi atafanya kazi hiyo kama way of life.

Mkuu Zomba,
Bado nasisitiza kwamba hujatenda haki kuleta malumbano ya kidini katika mada hii. Utatuhaibia mtiririko!

Unajua nilicheka pale wasomi wetu na Walimu wao, walipopelekwa DIAMOND JUBILEE wakavaa sale za CCM, na kuanza kuimba kidumu chama cha mapinduzi. waliporudi kwenye account zao wakakuta hela hamna na wakaanza kuandamana haikuchelewa wakatimuliwa mkuku. huku walimu wao walioenda nao wakiwatetea. nilipomuuliza jamaa mmoja aliyekuwepo kwenye DIAMOND kwa nini alienda akaambiwa alidhani wangeongezewa hela. nilimwambia haki inadaiwa na haibembelezwi. tuendelee kukata shule.
 
Unajua nilicheka pale wasomi wetu na Walimu wao, walipopelekwa DIAMOND JUBILEE wakavaa sale za CCM, na kuanza kuimba kidumu chama cha mapinduzi. waliporudi kwenye account zao wakakuta hela hamna na wakaanza kuandamana haikuchelewa wakatimuliwa mkuku. huku walimu wao walioenda nao wakiwatetea. nilipomuuliza jamaa mmoja aliyekuwepo kwenye DIAMOND kwa nini alienda akaambiwa alidhani wangeongezewa hela. nilimwambia haki inadaiwa na haibembelezwi. tuendelee kukata shule.

Mheshimiwa Mushobozi,
Kabla hujaendelea na stori za hao madenti na walimu wao, turudishe kwenye mada ya Mkamap.
 
mkamap said:
Lakini Nyerere alifanya juhudi za makusudi kutoa mtu singida na kumpeleka uchagani,kumtoa mtu bagamoyo na kumpeleka uhayani maana huko ndiko kulikua na shule.

Mkamap,

..mfumo wa elimu ambapo wanafunzi wana-move toka eneo moja kwenda lingine haukuanzishwa na Mwalimu Nyerere. Mfumo huo ulikuwepo tangu enzi za Mkoloni.

..Ndiyo maana basi unakuta Prof.Mmari,CJ Ramadhani,na Joseph Butiko, wote wamesomea Tabora, lakini si wazaliwa wa hapo. Ben Mkapa naye amesoma Pugu lakini si mzaliwa wa mkoa wa Pwani.

..Mimi naamini uchache wa mashule ndiyo uliolazimisha wanafunzi waende kusoma maeneo ya mbali na walikozaliwa. Napenda ifike mahali ubora na sifa za mashule uwavutie wanafunzi kuhama toka walikozaliwa. Kwa mfano kama shule ya Minaki ndiyo bora ktk PCB basi wanafunzi toka Musoma au Mtwara wawe na shauku ya kujiunga nayo.

..Mashamba ya masettler pia yalikuwa yana recruitment center mbali toka maeneo yalipo. Ndiyo maana utakuta kuna wamakonde wamelowea Tanga.

..Nyerere aliondoa ukabila ktk elimu, mbona ameshindwa kuuondoa jeshini? kwanini askari wengi wanatokea mkoa wa Mara?

NB:

..samahani kwa kutoka nje ya topic.
 
Mkamap,

..mfumo wa elimu ambapo wanafunzi wana-move toka eneo moja kwenda lingine haukuanzishwa na Mwalimu Nyerere. Mfumo huo ulikuwepo tangu enzi za Mkoloni.

..Ndiyo maana basi unakuta Prof.Mmari,CJ Ramadhani,na Joseph Butiko, wote wamesomea Tabora, lakini si wazaliwa wa hapo. Ben Mkapa naye amesoma Pugu lakini si mzaliwa wa mkoa wa Pwani.

..Mimi naamini uchache wa mashule ndiyo uliolazimisha wanafunzi waende kusoma maeneo ya mbali na walikozaliwa. Napenda ifike mahali ubora na sifa za mashule uwavutie wanafunzi kuhama toka walikozaliwa. Kwa mfano kama shule ya Minaki ndiyo bora ktk PCB basi wanafunzi toka Musoma au Mtwara wawe na shauku ya kujiunga nayo.

..Mashamba ya masettler pia yalikuwa yana recruitment center mbali toka maeneo yalipo. Ndiyo maana utakuta kuna wamakonde wamelowea Tanga.

..Nyerere aliondoa ukabila ktk elimu, mbona ameshindwa kuuondoa jeshini? kwanini askari wengi wanatokea mkoa wa Mara?

NB:

..samahani kwa kutoka nje ya topic.


No comment
 
Ndiyo maana nakwambia Zomba, chuki yako inakupa upofu. Hiyo Islamic University inahusiana nini na University College of Dar es Salaam? Haya University mlizuiwa na Mwalimu, hizo shule jee? Mbona mliishia na kinondoni? Mnatafuta uonevu hata pale pasipo na uonevu! Soma hapa chini kuhusu upande mwingine wa hiyo picha! Sasa mchawi nani kama siyo wenyewe. Hicho Chuo Kikuu unachozungumzia kilikuwa kijengwe Mombasa au Zanzibar lakini ilishindikana. Sasa UDSM wapi na wapi? Halafu soma jinsi waislamu wenzako walivyofurahia kutaifishwa kwa mashule mwaka 1968 kwa vile waliona kuwa wangepata nafasi ya kupata usawa katika elimu.Hiyo ni miaka arobaini iliyopita na usawa bado haujapatikana. Nani sasa alaumiwe, yule aliyefungua milango au yule aliyekataa kuingia. Udini wala Nyerere hawana nafasi katika mada hii.



Tuwaache hawa wenzetu waliopitia huko na sehemu nyingine kama hizo waichambue mada. Mimi na wewe tuliokwepa umande tukae pembeni!

Fundi Mchundo na Zomba:

Mnaingiza mada katika udini. Pamoja na hayo nimejaribu kufanya utafiti baada ya kusoma posti zenu. Tanzania ilikuwa na makabila au makundi manne ambayo yangeweza kufanya vitu vingi ikiwemo na kujenga vyuo vikuu. Makundi hayo ni yafuatayo:

Wachagga
Wahaya
Wanyakyusa
Na Waislamu wa mijini.

Haya makundi yalikuwa well organized na yalikuwa na institutions zao. WaIslamu wa mijini walikuwa na viongozi waliosoma, taasisi na connection za kuweza kujenga university. Mivutano yao na serikali ilifanya viongozi wao kutiwa ndani, vyombo vya kuvunja na serikali kuunda Bakwata ambayo iliongozwa na Mambumbu. Hivyo viongozi wa mwanzo wangekuwepo kile chuo cha Chang'ombe kingesimama.

Nimeishi kanda ya ziwa. Na shule niliyosoma ilikuwa wanafunzi kutoka Kagera, Mwanza, Shinyanga na Mara. Resource wise, watu kutoka Kagera walikuwa mbali sana. Na wangeachiwa wafanye wanavyotaka wangekuwa na vyuo vikuu tena sio kimoja, hiyo ni fact.

Mazingira ya wachagga na Wanyakyusa hayatofautiani sana na wahaya na uwezo wa wao kujenga vyuo ulikuwepo.

Tatizo linalokuja ni kuwa je hawa watu wangeachiwa kufanya mipango yao, je nchi ingekuwa wapi?
 
Fundi Mchundo na Zomba:

Mnaingiza mada katika udini. Pamoja na hayo nimejaribu kufanya utafiti baada ya kusoma posti zenu. Tanzania ilikuwa na makabila au makundi manne ambayo yangeweza kufanya vitu vingi ikiwemo na kujenga vyuo vikuu. Makundi hayo ni yafuatayo:

Wachagga
Wahaya
Wanyakyusa
Na Waislamu wa mijini.

Haya makundi yalikuwa well organized na yalikuwa na institutions zao. WaIslamu wa mijini walikuwa na viongozi waliosoma, taasisi na connection za kuweza kujenga university. Mivutano yao na serikali ilifanya viongozi wao kutiwa ndani, vyombo vya kuvunja na serikali kuunda Bakwata ambayo iliongozwa na Mambumbu. Hivyo viongozi wa mwanzo wangekuwepo kile chuo cha Chang'ombe kingesimama.

Nimeishi kanda ya ziwa. Na shule niliyosoma ilikuwa wanafunzi kutoka Kagera, Mwanza, Shinyanga na Mara. Resource wise, watu kutoka Kagera walikuwa mbali sana. Na wangeachiwa wafanye wanavyotaka wangekuwa na vyuo vikuu tena sio kimoja, hiyo ni fact.

Mazingira ya wachagga na Wanyakyusa hayatofautiani sana na wahaya na uwezo wa wao kujenga vyuo ulikuwepo.

Tatizo linalokuja ni kuwa je hawa watu wangeachiwa kufanya mipango yao, je nchi ingekuwa wapi?

Bin Maryam, kila sehemu katika jamii inaweza kutoa hadithi za namna zilivyonyanyaswa na utawala uliokuwepo wakati ule. Mimi siwezi kudai kuwa mwalimu alikuwa malaika, la hasha. Alifanya makosa mengi. Ninachokataa ni kuangalia kila kitu kwa kutumia darubini la udini au ukabila. Hatuna kabila la waislamu wa mjini. Kwani hao wakristu, wahindu ( Hindu Mandal, Azania Secongary, Jangwani sekondari) walionyang'anywa shule zao, kubanwa katika uendeshaji wa mahospitali yao hawana haki ya kulalamika? Ni siasa zilizofanywa kwa makusudi kujaribu ku'level' uwanja wa michezo. Pengine hawa watu wangeachiwa mipango yao nchi ingeendelea sana. Lakini pengine tabaka na tofauti zilizoanza kujitokeza wakati ule zingejikita zaidi na tungekuwa kama majirani zetu tukiji'identify' zaidi kutokana na kabila zetu, rangi zetu au dini zetu? Tungejuana vipi kama tungeendelea kusoma katika shule na kutibiwa kulingana na dini zetu?

Cha kujiuliza tumefanya nini toka wakati ule? Tumefanyia nini zile rasilimali zilizojengwa wakati ule? Tulicentralise kila kitu wakati ule ili kuhakikisha mgawanyo sawa katika jamii. Ndiyo moja ya sababu ya kuwa na Chuo Kikuu kimoja. Sasa dhana hii haitoshelezi mahitaji yetu na tumefungua vyuo vingi tu vya watu binafsi, vinavyoendesha na jumuia za kidini na vile ambavyo zamani vilichukuliwa kama vijichuo kwa wale ambao hawakuweza kuingia Chuo Kikuu. Kinachoongelewa katika mada hii ni nafasi ya hicho chuo mama UDSM katika mazingira na mahitaji ya elimu ya hivi sasa. Hiki Chuo, ambacho hakuna anayepinga nafasi yake katika jamii, je kinatekeleza wajibu (kama wengine wanavyoona) wa kuwahakikisha kuwa hivi vyuo vingine vinakuwa'nurtured' ili na vyenyewe viweze kutoa mchango wao au ndio kinaviona kama ni tishio katika himaya yake na kufanya jitihada kuhakikisha kuwa havifurukuti? Hatuzungumzii wachagaa, wahaya, wanyakyusa, wahindi, waarabu au wakristu, waislamu, singasinga, budhists, wahindu, rastafarians, atheists, wanaofuata imani za kiasili n.k. na nini hawa katika nafasi zao wamefanya katika hili suala la elimu. Hiyo ina nafasi yake sehemu nyingine lakini si katika mada hii!

Mimi niliingilia nilipoona mwenzangu anataka kulipeleka kusiko kwa kuingiza suala la nafasi ya uislamu katika kuanzisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hii niliona haina budi kukemewa. Mimi sijasoma katika hivyo vyuo vinavyozungumziwa hapa na ndio maana mchango wangu ulikuwa ni wa kusimuliwa. Si nia yangu kuingiza dini katika mada hii. Mniwie radhi kama mlinielewa hivyo.
 
Bin Maryam, kila sehemu katika jamii inaweza kutoa hadithi za namna zilivyonyanyaswa na utawala uliokuwepo wakati ule. Mimi siwezi kudai kuwa mwalimu alikuwa malaika, la hasha. Alifanya makosa mengi. Ninachokataa ni kuangalia kila kitu kwa kutumia darubini la udini au ukabila. Hatuna kabila la waislamu wa mjini. Kwani hao wakristu, wahindu ( Hindu Mandal, Azania Secongary, Jangwani sekondari) walionyang'anywa shule zao, kubanwa katika uendeshaji wa mahospitali yao hawana haki ya kulalamika? Ni siasa zilizofanywa kwa makusudi kujaribu ku'level' uwanja wa michezo. Pengine hawa watu wangeachiwa mipango yao nchi ingeendelea sana. Lakini pengine tabaka na tofauti zilizoanza kujitokeza wakati ule zingejikita zaidi na tungekuwa kama majirani zetu tukiji'identify' zaidi kutokana na kabila zetu, rangi zetu au dini zetu? Tungejuana vipi kama tungeendelea kusoma katika shule na kutibiwa kulingana na dini zetu?

Cha kujiuliza tumefanya nini toka wakati ule? Tumefanyia nini zile rasilimali zilizojengwa wakati ule? Tulicentralise kila kitu wakati ule ili kuhakikisha mgawanyo sawa katika jamii. Ndiyo moja ya sababu ya kuwa na Chuo Kikuu kimoja. Sasa dhana hii haitoshelezi mahitaji yetu na tumefungua vyuo vingi tu vya watu binafsi, vinavyoendesha na jumuia za kidini na vile ambavyo zamani vilichukuliwa kama vijichuo kwa wale ambao hawakuweza kuingia Chuo Kikuu. Kinachoongelewa katika mada hii ni nafasi ya hicho chuo mama UDSM katika mazingira na mahitaji ya elimu ya hivi sasa. Hiki Chuo, ambacho hakuna anayepinga nafasi yake katika jamii, je kinatekeleza wajibu (kama wengine wanavyoona) wa kuwahakikisha kuwa hivi vyuo vingine vinakuwa'nurtured' ili na vyenyewe viweze kutoa mchango wao au ndio kinaviona kama ni tishio katika himaya yake na kufanya jitihada kuhakikisha kuwa havifurukuti? Hatuzungumzii wachagaa, wahaya, wanyakyusa, wahindi, waarabu au wakristu, waislamu, singasinga, budhists, wahindu, rastafarians, atheists, wanaofuata imani za kiasili n.k. na nini hawa katika nafasi zao wamefanya katika hili suala la elimu. Hiyo ina nafasi yake sehemu nyingine lakini si katika mada hii!

Mimi niliingilia nilipoona mwenzangu anataka kulipeleka kusiko kwa kuingiza suala la nafasi ya uislamu katika kuanzisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hii niliona haina budi kukemewa. Mimi sijasoma katika hivyo vyuo vinavyozungumziwa hapa na ndio maana mchango wangu ulikuwa ni wa kusimuliwa. Si nia yangu kuingiza dini katika mada hii. Mniwie radhi kama mlinielewa hivyo.


Fundi Mchundo:

Mimi naamini kuwa mambo ya usomi ni pure talent. Na hizi talent ziko distributed equally katika jamii.

Katika jamii kama ya Tanzania ukiona kabila moja au dini moja imesoma sana ni bahati ya resources lakini sio kubalikiwa kwa talents kama inavyoweza kuwepo kwenye mawazo ya baadhi yetu.

Kwa sehemu kubwa elimu imechukuliwa kama sehemu ya kupata kazi nzuri. Na wasomi wachache sana wa Tanzania walioweza kumaliza shule na kutumia elimu yao kuanzisha shughuli zinazotoa ajira kwa watanzania wenzao au kufanya uvumbuzi wenye kusaidia jamii zao.

Na kama tutatumia kigezo hiki cha kuwa elimu ni lazima itumike kuleta mabadiliko yatakayosaidia jamii kuendelea mbele, basi tunaweza kusema kuwa nchi yetu haina wasomi kwa sababu hata wanaojiita wasomi wameshindwa kutumia elimu yao na kama serikali itaacha kutoa ajira kuna uwezekano wasomi wengi kurudia kufanya kazi za kijima zilizokuwa zinafanywa na mababu zao.

Kwa mtaji niliosema juu kazi ya kupata wasomi katika nchi yetu ndio kwanza imeaanza. Na UDSM inatakiwa kuwa mstari wa mbele au sio kikwazo.
 
Fundi Mchundo:

Mimi naamini kuwa mambo ya usomi ni pure talent. Na hizi talent ziko distributed equally katika jamii.

Katika jamii kama ya Tanzania ukiona kabila moja au dini moja imesoma sana ni bahati ya resources lakini sio kubalikiwa kwa talents kama inavyoweza kuwepo kwenye mawazo ya baadhi yetu.

Kwa sehemu kubwa elimu imechukuliwa kama sehemu ya kupata kazi nzuri. Na wasomi wachache sana wa Tanzania walioweza kumaliza shule na kutumia elimu yao kuanzisha shughuli zinazotoa ajira kwa watanzania wenzao au kufanya uvumbuzi wenye kusaidia jamii zao.

Na kama tutatumia kigezo hiki cha kuwa elimu ni lazima itumike kuleta mabadiliko yatakayosaidia jamii kuendelea mbele, basi tunaweza kusema kuwa nchi yetu haina wasomi kwa sababu hata wanaojiita wasomi wameshindwa kutumia elimu yao na kama serikali itaacha kutoa ajira kuna uwezekano wasomi wengi kurudia kufanya kazi za kijima zilizokuwa zinafanywa na mababu zao.

Kwa mtaji niliosema juu kazi ya kupata wasomi katika nchi yetu ndio kwanza imeaanza. Na UDSM inatakiwa kuwa mstari wa mbele au sio kikwazo.


Sasa ndio tunaongea. Hii ndiyo mada haswa tunayotakiwa kuchangia. Asante, fundi mwenzangu!
 
Sasa ndio tunaongea. Hii ndiyo mada haswa tunayotakiwa kuchangia. Asante, fundi mwenzangu!

Habari zenu za leo
Nimatumaini yangu wote mu wazima wa afya tele na poleni kwa kashi kashi lilopelekea kuyumba kwa jitihada maridadi tulizokua tunaendelea nazo, hii adha iliyotokea ni ya kusikitisha pia kufuruhahisha .
ktk upande wa kufurahisha ni kua imekua moja ya kichochezi saidizi ya juhudi zetu ktk kuutazama mfumo wa elimu yetu.

Hii imeonyesha jinsi gani mfumo wetu wa elimu ya juu ulivyofeli na kutoa wataalamu butu anayeamka na kukurupuka kwa kutoa maamuzi butu na kufanya uchumi butu.

Ni hii elimu yetu ya juu ilivyofeli hadi kufikia wasomi wetu kuhangaika na jambo forum kwa kuwatia korokoroni pia kuwafungulia mashitaka baadhi ya memba na kuwaacha watu waliochota mabilioni ya fedha IPTL,BOT,RICHMOND wakipeta.

Hakika elimu ya juu imefungamana mkabala na uchumi wa nchi,hivyo kufeli kwa uchumi nimatokeo ambayo yametokana na kufeli kwa elimu ya juu kunakopelekea wataalamu wake wanaoongoza nchi kutoa maamuzi ya ajabu ajabu .

Karibuni tuendelee na maada hii baada ya kukosa mawasiliano kwa mda wa siku kadhaa baada ya JF kukumbana na kimbunga kikali lakini jf kwa ujasili na u mamajusi(wise people) wake imepata kukishinda kimbunga.
 
Habari zenu za leo
Nimatumaini yangu wote mu wazima wa afya tele na poleni kwa kashi kashi lilopelekea kuyumba kwa jitihada maridadi tulizokua tunaendelea nazo, hii adha iliyotokea ni ya kusikitisha pia kufuruhahisha .
ktk upande wa kufurahisha ni kua imekua moja ya kichochezi saidizi ya juhudi zetu ktk kuutazama mfumo wa elimu yetu.

Hii imeonyesha jinsi gani mfumo wetu wa elimu ya juu ulivyofeli na kutoa wataalamu butu anayeamka na kukurupuka kwa kutoa maamuzi butu na kufanya uchumi butu.

Ni hii elimu yetu ya juu ilivyofeli hadi kufikia wasomi wetu kuhangaika na jambo forum kwa kuwatia korokoroni pia kuwafungulia mashitaka baadhi ya memba na kuwaacha watu waliochota mabilioni ya fedha IPTL,BOT,RICHMOND wakipeta.

Hakika elimu ya juu imefungamana mkabala na uchumi wa nchi,hivyo kufeli kwa uchumi nimatokeo ambayo yametokana na kufeli kwa elimu ya juu kunakopelekea wataalamu wake wanaoongoza nchi kutoa maamuzi ya ajabu ajabu .

Karibuni tuendelee na maada hii baada ya kukosa mawasiliano kwa mda wa siku kadhaa baada ya JF kukumbana na kimbunga kikali lakini jf kwa ujasili na u mamajusi(wise people) wake imepata kukishinda kimbunga.


Mkamap:

Hapa Marekani kuna vyuo vya namna mbili. Vyuo vya umma (public university) na vyuo binafsi (private university). Vyuo vya umma ambavyo vingi viko chini ya serikali za majimbo ni vya bei nafuu lakini havitoi schoolarship nyingi kwa watu wasio wakazi wa majimbo husika.

Vyuo vya binafsi vinatoa schoolarship kwa mtu wanayemtaka. Na mwanafunzi mzuri aliyepo sehemu yoyote duniani anaweza kupata nafasi ya kujiunga na vyuo hivyo kwa schoolarship iwapo uwezo wake ni wa juu au akiwa na bahati. Na vyuo hivi vimetoa watu wazuri na mchango mkubwa kwa taifa lao katika fani nyingi.

Kwanini na sisi tusianzishe vyuo binafsi visivyo na mwelekeo wa kidini au kikabila na kutoa nafasi kwa watanzania bila kutegemea misaada ya serikali?
 
Mkamap:

Hapa Marekani kuna vyuo vya namna mbili. Vyuo vya umma (public university) na vyuo binafsi (private university). Vyuo vya umma ambavyo vingi viko chini ya serikali za majimbo ni vya bei nafuu lakini havitoi schoolarship nyingi kwa watu wasio wakazi wa majimbo husika.

Vyuo vya binafsi vinatoa schoolarship kwa mtu wanayemtaka. Na mwanafunzi mzuri aliyepo sehemu yoyote duniani anaweza kupata nafasi ya kujiunga na vyuo hivyo kwa schoolarship iwapo uwezo wake ni wa juu au akiwa na bahati. Na vyuo hivi vimetoa watu wazuri na mchango mkubwa kwa taifa lao katika fani nyingi.

Kwanini na sisi tusianzishe vyuo binafsi visivyo na mwelekeo wa kidini au kikabila na kutoa nafasi kwa watanzania bila kutegemea misaada ya serikali?

Bin maryam
Heshima mbele
Mimi naungana na wewe kwa asilimia zote na unayoongea nami ndio mtazamo wangu tangu awali.
Bin maryam kama ulisoma maada zangu tafauti na hii mimi mara nyingi nimekua nikishitumu kua tanzania hatuna walioelimika(wasomi)na kama wapo niwachache sana ila hua kuna na midadi ya upinzani mkubwa ktk hilo .

Ni kweli kabisa tunahitaji vyuo vingi vilivyo ktk mitiririko wa aina tofauti tofauti vinavyotoa elimu ya juu angalau ktk kila mkoa tuwe navyo vyuo viwili viwe vya serikali ama private na Hili tu linafanikiwa ikiwa kama kuna waelewa(wasomi) vinginevyo ndiyo hivyo kubaki na chuo kimoja udsm.

Sasa tufanye je ili tupate hivyo vyuo vingi ni kazi yako wewe ,yule na mimi.
 
Tusiwalaumu UDSM pekee, kada nzima ya usomi haina mchango kwa mustakabali wa nchi, wasomi wote wamegeuka kuwa mafisadi wakubwa, ama kwa kuwasaidia walioko madarakani kuiba na kufifisha bongo za Watanzania. Ni ufusdi mtupu huku wakipewa nafasi za uongozi. Nao wanaokosa nafasi wanaona kazi hiyo ni bomu, hawafundishi, kwa sasa wanafuga na kuandika papers tu kwa ajili ya matumbo tyao, hawafai ni wauaji wa Tanzania yetu.
Mfubao wa elimu unatokana na ufisadi tu, hakuna kingine, tukikomesha ufisadi na kujenga mizizi ya utaifa, hakika elimu yetu itapanuka na kuwa yenye msaada mkubwa.
 
Tusiwalaumu UDSM pekee, kada nzima ya usomi haina mchango kwa mustakabali wa nchi, wasomi wote wamegeuka kuwa mafisadi wakubwa, ama kwa kuwasaidia walioko madarakani kuiba na kufifisha bongo za Watanzania. Ni ufusdi mtupu huku wakipewa nafasi za uongozi. Nao wanaokosa nafasi wanaona kazi hiyo ni bomu, hawafundishi, kwa sasa wanafuga na kuandika papers tu kwa ajili ya matumbo tyao, hawafai ni wauaji wa Tanzania yetu.
Mfubao wa elimu unatokana na ufisadi tu, hakuna kingine, tukikomesha ufisadi na kujenga mizizi ya utaifa, hakika elimu yetu itapanuka na kuwa yenye msaada mkubwa.

Kamanda
Ni kweli ni wasomi wanaoongoza nchi na wanaoongoza nchi ndio wamegeka mafisadi hiyo ni kweli.
sasa basi ktk hilo udhani ni chuo gani ambacho kimesababisha kalaa hilo??
 
Bin maryam
Heshima mbele
Mimi naungana na wewe kwa asilimia zote na unayoongea nami ndio mtazamo wangu tangu awali.
Bin maryam kama ulisoma maada zangu tafauti na hii mimi mara nyingi nimekua nikishitumu kua tanzania hatuna walioelimika(wasomi)na kama wapo niwachache sana ila hua kuna na midadi ya upinzani mkubwa ktk hilo .

Ni kweli kabisa tunahitaji vyuo vingi vilivyo ktk mitiririko wa aina tofauti tofauti vinavyotoa elimu ya juu angalau ktk kila mkoa tuwe navyo vyuo viwili viwe vya serikali ama private na Hili tu linafanikiwa ikiwa kama kuna waelewa(wasomi) vinginevyo ndiyo hivyo kubaki na chuo kimoja udsm.

Sasa tufanye je ili tupate hivyo vyuo vingi ni kazi yako wewe ,yule na mimi.

Mimi ni mwanahistoria wa ridhaa. Nitakupa mifano michache. Ugiriki na Rumi ziliendelea sana katika masuala ya kisayansi kabla ya Utawala wa Papa kushika hatamu. Lakini utawala wa kidini ulikataza sana mambo ya kisayansi. Kwa sababu enzi hizo fani za sayansi na uchawi zilikuwa bado hazina tofauti kubwa. Hivyo maendeleo yote ya wagiriki na warumi yalikaa kwa karne nyingi bila kufanyiwa kazi kwa sababu za kidini.

Waislamu waliagizwa na Mtume wao kwenda katika nchi zozote kutafuta elimu. Na maendeleo yoyote ambayo hayaendi kinyume na maagizo ya Mungu ni halali kusoma. Wasomi wengi wa mwanzo wa himaya za kiislamu walitumia maarifa kutoka jamii zingine. Walipofika Misri walichukua vitabu vya kigiriki na kuvitasfri kwa kiarabu.

Nchi za Ulaya ziliona mabadiliko hayo. Na wao walianzisha Renaissance. Walichukua kilichoandikwa na warumi, wagiriki na waarabu na kuendeleza kwa kutumia mazingira yao. Na wakaachana kwa kiasi kikubwa na tafsiri za kidini zilizo literal.

Na elimu wa Wagiriki imetokana na wao kuiga yale yalioanza Misri. Na Misri nao walianza kwa kuiga Axum iliyopo Ethiopia.

Kwa maoni yangu elimu ni matokeo ya kuiga. Tatizo letu tupo Superficial katika kuiga. Na haya yanaonekana katika huu mjadala.
Kwanini uonyeshe maarifa yako kwa kutumia kiingereza wakati mada yenye hipo kwa kiswahili?

Bongo flava, miss Tanzania ni Superficial. Haitufikishi mahali popote hata kama tutajitahidi kwa njia zote.

Ningeomba serikali, taasisi au wakundi ya watu wachapishe vitabu vya taaluma mbalimbali kwa kiswahili na waachie watu wasome katika maktaba au mashuleni. Nina imani kubwa hiyo elimu ya chuo kikuu watu wanayosoma kwa miaka mitatu au minne, kuna vichwa vitaisoma kwa mwaka mmoja au miwili.

Ni lazima tuanzishe Renaissance. Hile elimu ya High school Tanzania ni elimu ya mwaka wa kwanza wa chuo kikuu. Na kwa nchi zingine ni elimu ya mwaka wa pili. Lakini kwa sababu inatolewa kwa watu wasio na mwamko, ni lazima mhitimu wa elimu hiyo apewe mafunzo mengine hili aweze kufanya kazi.
 
Mimi ni mwanahistoria wa ridhaa. Nitakupa mifano michache. Ugiriki na Rumi ziliendelea sana katika masuala ya kisayansi kabla ya Utawala wa Papa kushika hatamu. Lakini utawala wa kidini ulikataza sana mambo ya kisayansi. Kwa sababu enzi hizo fani za sayansi na uchawi zilikuwa bado hazina tofauti kubwa. Hivyo maendeleo yote ya wagiriki na warumi yalikaa kwa karne nyingi bila kufanyiwa kazi kwa sababu za kidini.

Waislamu waliagizwa na Mtume wao kwenda katika nchi zozote kutafuta elimu. Na maendeleo yoyote ambayo hayaendi kinyume na maagizo ya Mungu ni halali kusoma. Wasomi wengi wa mwanzo wa himaya za kiislamu walitumia maarifa kutoka jamii zingine. Walipofika Misri walichukua vitabu vya kigiriki na kuvitasfri kwa kiarabu.

Nchi za Ulaya ziliona mabadiliko hayo. Na wao walianzisha Renaissance. Walichukua kilichoandikwa na warumi, wagiriki na waarabu na kuendeleza kwa kutumia mazingira yao. Na wakaachana kwa kiasi kikubwa na tafsiri za kidini zilizo literal.

Na elimu wa Wagiriki imetokana na wao kuiga yale yalioanza Misri. Na Misri nao walianza kwa kuiga Axum iliyopo Ethiopia.

Kwa maoni yangu elimu ni matokeo ya kuiga. Tatizo letu tupo Superficial katika kuiga. Na haya yanaonekana katika huu mjadala.
Kwanini uonyeshe maarifa yako kwa kutumia kiingereza wakati mada yenye hipo kwa kiswahili?

Bongo flava, miss Tanzania ni Superficial. Haitufikishi mahali popote hata kama tutajitahidi kwa njia zote.

Ningeomba serikali, taasisi au wakundi ya watu wachapishe vitabu vya taaluma mbalimbali kwa kiswahili na waachie watu wasome katika maktaba au mashuleni. Nina imani kubwa hiyo elimu ya chuo kikuu watu wanayosoma kwa miaka mitatu au minne, kuna vichwa vitaisoma kwa mwaka mmoja au miwili.

Ni lazima tuanzishe Renaissance. Hile elimu ya High school Tanzania ni elimu ya mwaka wa kwanza wa chuo kikuu. Na kwa nchi zingine ni elimu ya mwaka wa pili. Lakini kwa sababu inatolewa kwa watu wasio na mwamko, ni lazima mhitimu wa elimu hiyo apewe mafunzo mengine hili aweze kufanya kazi.

Duh.
Sijakutana na maoni ya namna hii kwa muda mrefu sana, hongera sana mkuu. Kulikuwa na mjadala unaendelea kuhusu matumizi ya lugha ya kiswahili katika kufundishia vyuoni, sijajua umeishia wapi hadi leo. Kama una taarifa muhimu naomba uzimwage hapa.
Vinginevyo asante sana kwa kumbukumbu hizi.
Idimi
 
Duh.
Sijakutana na maoni ya namna hii kwa muda mrefu sana, hongera sana mkuu. Kulikuwa na mjadala unaendelea kuhusu matumizi ya lugha ya kiswahili katika kufundishia vyuoni, sijajua umeishia wapi hadi leo. Kama una taarifa muhimu naomba uzimwage hapa.
Vinginevyo asante sana kwa kumbukumbu hizi.
Idimi

Ufundishaji wa Kiswahili katika vyuo vikuu vitaleta mjadala mkubwa. Ninachoomba mimi ni utunzi wa vitabu vya maarifa mbalimbali kwa kiswahili.

Latin ilikuwa ni lugha ya mashule wakati Sir. Isaac Newton anaandika master piece yake Philosophiæ Naturalis Principia Mathematica 1686.

Mwaka 1726 kazi yake ilikuwa tayari hiko kwa kiingereza Mathematical Principles of Natural Philosophy.

Matumizi ya kiingereza yaendelee lakini kushindwa kutafsiri vitabu katika lugha yetu wenyewe huo ni upumbavu ulikomaa.
 
Ufundishaji wa Kiswahili katika vyuo vikuu vitaleta mjadala mkubwa. Ninachoomba mimi ni utunzi wa vitabu vya maarifa mbalimbali kwa kiswahili.

Latin ilikuwa ni lugha ya mashule wakati Sir. Isaac Newton anaandika master piece yake Philosophiæ Naturalis Principia Mathematica 1686.

Mwaka 1726 kazi yake ilikuwa tayari hiko kwa kiingereza Mathematical Principles of Natural Philosophy.

Matumizi ya kiingereza yaendelee lakini kushindwa kutafsiri vitabu katika lugha yetu wenyewe huo ni upumbavu ulikomaa.

wewe na mimi tuandike hivyo vitabu
sasa tuanze kama mfano tuunganishe nguvu tuandike vitabu kwa kiswahili au una sema je?
 
wewe na mimi tuandike hivyo vitabu
sasa tuanze kama mfano tuunganishe nguvu tuandike vitabu kwa kiswahili au una sema je?


Mimi nipo tayari na mpango huo nilikuwa nao. Kuna Mwi-Ethiopia mmoja katoa kazi zake za theory of relativity kwa lugha yao.
 
Ufundishaji wa Kiswahili katika vyuo vikuu vitaleta mjadala mkubwa. Ninachoomba mimi ni utunzi wa vitabu vya maarifa mbalimbali kwa kiswahili.

Latin ilikuwa ni lugha ya mashule wakati Sir. Isaac Newton anaandika master piece yake Philosophiæ Naturalis Principia Mathematica 1686.

Mwaka 1726 kazi yake ilikuwa tayari hiko kwa kiingereza Mathematical Principles of Natural Philosophy.

Matumizi ya kiingereza yaendelee lakini kushindwa kutafsiri vitabu katika lugha yetu wenyewe huo ni upumbavu ulikomaa.


Katika mitaala ya VETA na vyuo vingi vya ufundi stadi, vitabu vingi viko kwa kiswahili. Shida iko katika ngazi za juu.
Huko ndiko kunakohitaji marekebisho makubwa sana.
 
Back
Top Bottom