UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

Quality guys!

Nafikiri UDSM are worried about mushrooming of tens of Universities in Tz without adequate equipment and staff!

Well sidhani kama ni wivu!

Way foward- MU, SUA, Dodoma, OUT, DIT wao wapublish na kuwa innovative na competitive kushinda hata UD- na kwa hiyo wapunguze kulia lia kama makinda ya ndege! Walishakuwa wakubwa tayari!


Napenda style aliyotumia kuelezea hii kitu huyu Mzelendohalisi. Hakuna haja ya kulialia. Work hard, prove them wrong!!! It has always worked for me... Tangu shule ya vidudu nimekuwa the odd-one na siku zote nime-prove them wrong.. Nilikuwa mdhaifu na nilitoka kwenye jamii ya dini na kabila ambamo watu hawaamini wanaweza kuwa wasomi wazuri. Hata walimu walinibeza. Mtaa nilikokuwa naishi pia watoto wasomi hawakuishi huko... Lakini nilipambana nikapita kwa flying colors kote wakabaki midomo wazi. Nilipofika colkege nikapata 1st class bachelor, ndio heshima ikasambaa rasmi. Sikutosheka, nilipofika kazini nikasema nataka kuwa tofauti na wale wasiopata 1st class. Basi ndani ya miezi mitatu jina juu!! Sasa nachagua kazi. Namshukuru Mungu kunipa ujasiri. Sisemi haya kwa kujidai/no-bragging lakini ili kuonyesha hakuna haja ya kupiga kelele kama makinda ya ndege. Piga msuli onyesha unaweza. Kama vyuo vinaona vinaweza ila wanahisi UD ni majungu, basi wathibitishe. Nchi ni yetu sote. Kama quality iko chini ni vijana wa kitanzania wataumia... hapo nadhani ndipo UD wanapoona uzalendo unahitajika, hasa wao wakiwa partiots wa higher educ in tanzania. Hii isiwe vita ya UD against UDOM, MU or whateva, ila vita ya quality education.Tusiwe watu wa kuogopa challange na kusema majungu. Quality ya educ ikiwa mbaya itaathiri kila mahala. Actually, hata UD yenyewe inahitaji mtu kuwapigia kelele wapandisha kiwango chake cha elimu, ila atakaepiga kelele inabidi awe amefikia kiwango fulani cha kujiamini.
Mungu ibariki Tanzania.
 
ni wangapi kila siku wanamaliza Udsm na kazi hajui/hawawezi!!!!!Udsm sio kitu na hakuna la kujivuni pale ni historia isiyo na mshiko kwa wakati tulio nao sasa!!!!!!!
 
Kuna kitu kimoja sikukipenda kabisa katika maisha yangu pale UDSM...malecturer walivyokuwa wakituchukulia watu tuliokuwa tunasma pale. Walijikweza mno na mara nyingine walikuwa kama wanalazimisha ionekane kama haiwezekani kusoma na kufaulu vizuri na kutoka na elimu ya uhakika.Badala yake walikuwa wanatuburuza tukawa tunashinda kusoma madesa tukavisahau vitabu maana ndo ilikuwa njia pekee ya kuwakimbia wasitukamate.
Sasa kazi ipo huku mtaani! Mtu ana cheti kinang'ara lakini anachofanya bwana, duuh. na ndio maana tunaogopa wakenya wakija watatufuruga tuchanganyikiwe.
Hivi kwanini hatupendi kujishusha maana naona ego zetu zinatukwaza sana sasa hatuwezi hata kujirekebisha, na hili ni tatizo la mfumo mzima tunaoupitia.
 
Nafikiri hii mada inatupa challenge tuone wapi pa kurekebisha na sio kama inawadhalilisha UDSM.Tunawahitaji wataalamu ila sio wasoma madesa kama ilivyokuwa miaka michache iliyopita, ambao hawana lolote ni ubabaishaji tu kwa kwenda mbele.
 
mkamap,

i am worried that you could be an individual who is emotionally charged to bring forth such accusations. None of your comments have any grounding whatsoever and seem more as a result of your disgust of a few individuals who want to seem superior to those studying in other institutions.

I am a graduate of udsm and graduated more than 10 years ago and never had such sentiments circulating on campus. I have taught at udsm for more than 5 years and i have never had such sentiments.

Now, i can understand your point of view from what is happening right now and i could say that i believe your emotionally charged comments and i can only associate your sentiments as a result of this recent proliferation of universities and affiliated colleges.

If i were you and anyone put in a compromising position as being inferior, i would work hard to prove these claims as wrong. Right now it is quite early for new universities and colleges to compete with an old university that is highly ranked among other african universities but time, commitment, diligence and integrity will prove that other new universities are forces to deal with.


My advice, hang in there, get a good degree - and when i say a good degree i mean 1st or upper 2nd class degree.

Please forgive me if i may sound patronizing but it is not my intention.

Good day.

nimeguswa na majibu yako mazuri sana kwa ndugu yetu....umedhihirisha kuwa wewe kweli ni product ya chuo kikuu cha dar es salaam "hekima ni uhuru"!
 
Niliingiaga pale nikijua ni masuala ya kubukua na malibrary kumbe full madesa na chain,Vitabu hamna,kalibrary kadogo lecture rooms ndogo (Nimesikia wamejenga nyingine) sidhani kama zinatosha,
Contact za walimu na dent ni ndogo au hamna kabisa ukienda kwa ofisi mlango umefungwa wako kwenye mishemishe,wengine Full ubabe kisa yeye ni Lecturer
Ni kweli UDSM nyodo nyingi,Vyuo vingine havipati sapoti toka juu kama ilivyokuwa kwake, sasa hawa jamaa attention yote iko UDOM baada ya muda tegemea katabia ka UD toka UDOM
Roho inauma kuona Nguvu nyingi iliyowekwa pale inapotezwa mchana kweupe
Serikali ndo wakulaumiwa kwa kubagua watu wake na kama alivyosema JK Nyerere....sisi wa zanzibara wao wa zanziberi...,,dhambi ya kula nyama ya mtu inaendelea...
 
napenda kuchangia thread ii kama ifuatavyo kwa kuchambua baadhi ya michangu ya wadau mbalimbali.

kwanza mimi napenda kujitambulisha kama mmoja wa waliomaliza udms-eng na prof.masuha happen to be my lecturer ktk kozi mbalimbali.

prof masuha ni ktk maprofessor wachache hapa nchini ambao huwezi ku question uwezo wako kitaaluma na kijamii, his outstanding cv can tell it all ila lawama za udsm kuonekana ni chuo pekee kinachotoa degree za ukweli na wanafunzi wake kujion superior zinatokana na mfumo.

kwa mfano, udsm wanachaguliwa cream ya wanafunzi kiasi cha kwamba vyuo vingine wanaoenda uko wanaonekana hawajiwezi ila ilimradi tu nao wasome na ukweli uko wazi enzi zetu nchi nzima waliopata div. 1 na 2 form 6 wote wanaenda udsm the rest wanaenda vyuo vingine ingawa kwa sasa mabadiliko yanaanza onekana kwa vyuo binafsi kuruhusiwa.

pili, mentality ya wanafunzi wenyewe kwa ambae hakubahatika kwenda udsm anajiona kama ki elimu amefeli kwa kwenda vyuo vingine ingawa kwa sasa hali inaanza badilika kwa vyuo binafsi kuruhusiwa.

mwisho kwa suala la dit, eng. udsm ki mfumo ilikua imetengwa kua pekee kutoa degree za engineering na dit kutoa technicians, kumlaumu prof masuha nadhan si sahihi, hata kimfumo naona yuko sawa kwani kama technical school zote zikiwa zinatoa engineers who will work as technicians? infact technicians wanatika wawe wengi kuliko engineers kustrike good balance.
 
mwisho kwa suala la dit, eng. udsm ki mfumo ilikua imetengwa kua pekee kutoa degree za engineering na dit kutoa technicians, kumlaumu prof masuha nadhan si sahihi, hata kimfumo naona yuko sawa kwani kama technical school zote zikiwa zinatoa engineers who will work as technicians? infact technicians wanatika wawe wengi kuliko engineers kustrike good balance.

Hivi chuo hakiwezi kutoa Technicians na Engineers? Are the two 'mutually exclusive'?
 
Ina semekana mfubao wa elimu nchi unasababishwa na wanaojiita wasomi wa UDSM kuwa na chuki za kipumbavu na mentality mfuu iliyojengeka vichwani mwao.

Mfano wasomi wa UDSM wamekuwa na tabia ya kuzibia vyuo vingi vilivyo nasababu pia nia ya kua vyuo vikuu mfano DIT, kutokana na kuwa na ma egineer wachache ilikuwa na nia siku nyingi ya kutoa digrii lakini ilipambana na mkono wa uzibe kutoka UDSM isipate wasaha huo mfano wa wazi ni pale kiongozi mwandamizi wa UDSM DR Masua alipoamua kusafiri mpaka ulaya ili kukisiriba chuo hicho kwa wadau ili kisipate hadhi hiyo.

Bado kuna mfano wa Mzumbe kikiandamwa na propaganda za wakuu wa adimizi wa UDSM.
SWALI LA KUJIULIZA!!! kwanini? UDSM ni wahasimu wakubwa wa vyuo vinavyotoa kozi zinazofanana na zile zinazotolewa UDSM.

Na juhudi zao zinapokwama hufanya kila mbinu ili chuo husika kiwe chuo kishiriki chao,habari zinapasha.

Na cha kusikitisha zaidi hawa wahadhiri wamekua mstari wa mbele kukebehi vyuo vingine mfano utasikia ukipata C udsm hii ni A mzumbe, na sivyo hivyo tu wamekua wakienda mbali kulaghai wanafunzi wao na kuwaaminisha vitu vya ajabu ajabu mfano hii digrii ya UDSM ni masters ya ulaya.

Cha ajabu wanafunzi hao nao wamekua wakiamini hayo bila kuhoji mbona hawa ma tutor wetu wengi wamezichukua hizo master ulaya? baada ya ya kuchukua digrii hapa kwanini hawakwenda moja kwa moja DR huko ulaya.habari zilizidi kupasha na kuongeza,

DESA za UDSM ndizo zimeua kabisa elimu ya Tanzania maana zimekuwa zikitoa wanafunzi mabigwa wa desa wasio na skills, chanzo kilipasha.

Na kama mfumo mzima wa elimu Tz kuangaliwa inabidi waanze na UDSM maana inasemekana ni chuo kiliojaa kinyongo, chuki ku-disco watu wenye uwezo kwa sababu za ma-prof binafsi, kupitisha wanafunzi wasio na uwezo kwa uwezo wao wa kuvua chupi.

Sijaona ukweli wowote! Mie ninavyojua ni kwamba UDSM ndio imesaidia vyuo vingine kufikia kutoa degree na sasa nasikia hata NIT wanatoa degree
 
all in all am inrolled in very ranked university than udsm.

Hata hivyo hiyo ranki ya university si kitu kwangu kwangu mie nini nilichonacho kichwani mwangu

Hizo mentality zenu za udsm zimepitwa na wakati you must reform your mentality
kama kuna tuhuma udsm lazima watu wakubali na wazifanyie tathmini na kupata marekebisho ili tupate wataalamu bora mambo ya kukumbatia uozo acheni msiwe kama ccm wamekumbatia mabomu mpaka yanaanza kuwaripukia.

Nani anabisha hapo udsm wasichana hawavui chupi ili wapite mitihani yao ??
Nani anabisha huyo dr sijui prof masua hakuchomewa gari lake DIT ni sababu zipi naomba mniambie??

Hiyo udsm wakati inaanzishwa ilikua na ma prof wangapi,dr ms wangapi??
kuanza siku nyingi si kigezo, mnajua kuna vyuo vilianza kabla hata ya yesu lakini leo vinazidiwa na vyuo ambavyo hata miaka 20 havina.
So far what udsm had has done cha kujivunia na kusema chuo hiki ni mahili????

Egypt(misri) ni kati ya nchi kongwe duniani na ni nchi ya kwanza kustaarabika ndio maana wengine tunakwenda karne ya 21 wakati wamisiri wapo karibu karne ya 70 lakini ukongwe wao bado wamezidiwa mbali mno na chi changa kama canada, usa nkn.
hivyo ukongwe wa udsm si hoja ,hoja nikuchukua mhitimu wa udsm na mzumbe na dit pia ifm na kuona nani mfanisi ktk shughuli.
You talk sense
 
napenda kuchangia thread ii kama ifuatavyo kwa kuchambua baadhi ya michangu ya wadau mbalimbali.

kwanza mimi napenda kujitambulisha kama mmoja wa waliomaliza udms-eng na prof.masuha happen to be my lecturer ktk kozi mbalimbali.

prof masuha ni ktk maprofessor wachache hapa nchini ambao huwezi ku question uwezo wako kitaaluma na kijamii, his outstanding cv can tell it all ila lawama za udsm kuonekana ni chuo pekee kinachotoa degree za ukweli na wanafunzi wake kujion superior zinatokana na mfumo.

kwa mfano, udsm wanachaguliwa cream ya wanafunzi kiasi cha kwamba vyuo vingine wanaoenda uko wanaonekana hawajiwezi ila ilimradi tu nao wasome na ukweli uko wazi enzi zetu nchi nzima waliopata div. 1 na 2 form 6 wote wanaenda udsm the rest wanaenda vyuo vingine ingawa kwa sasa mabadiliko yanaanza onekana kwa vyuo binafsi kuruhusiwa.

pili, mentality ya wanafunzi wenyewe kwa ambae hakubahatika kwenda udsm anajiona kama ki elimu amefeli kwa kwenda vyuo vingine ingawa kwa sasa hali inaanza badilika kwa vyuo binafsi kuruhusiwa.

mwisho kwa suala la dit, eng. udsm ki mfumo ilikua imetengwa kua pekee kutoa degree za engineering na dit kutoa technicians, kumlaumu prof masuha nadhan si sahihi, hata kimfumo naona yuko sawa kwani kama technical school zote zikiwa zinatoa engineers who will work as technicians? infact technicians wanatika wawe wengi kuliko engineers kustrike good balance.
I prove you wrong. I got division one but never went to UDSM but SUA
 
Nafikiri hii mada inatupa challenge tuone wapi pa kurekebisha na sio kama inawadhalilisha UDSM.Tunawahitaji wataalamu ila sio wasoma madesa kama ilivyokuwa miaka michache iliyopita, ambao hawana lolote ni ubabaishaji tu kwa kwenda mbele.
Pamoja na huo ukongwe kwani yale mashindano ya Zain huwa wanafurukuta?Je na waajiri Tanzania nafikiri ndo wang'amuzi wanasemaje?Are there significant defferences in performance compared to other gradunts?Na kama chuo mama viongozi wengi wametoka hapo Vipi ufanisi wao kuletea Tanzania maendeleo? Tecknologia ngapi zinazotumika Nchini ambazo zimetoka UDSM?
 
Mkamap:

Hapa Marekani kuna vyuo vya namna mbili. Vyuo vya umma (public university) na vyuo binafsi (private university). Vyuo vya umma ambavyo vingi viko chini ya serikali za majimbo ni vya bei nafuu lakini havitoi schoolarship nyingi kwa watu wasio wakazi wa majimbo husika.

Vyuo vya binafsi vinatoa schoolarship kwa mtu wanayemtaka. Na mwanafunzi mzuri aliyepo sehemu yoyote duniani anaweza kupata nafasi ya kujiunga na vyuo hivyo kwa schoolarship iwapo uwezo wake ni wa juu au akiwa na bahati. Na vyuo hivi vimetoa watu wazuri na mchango mkubwa kwa taifa lao katika fani nyingi.

Kwanini na sisi tusianzishe vyuo binafsi visivyo na mwelekeo wa kidini au kikabila na kutoa nafasi kwa watanzania bila kutegemea misaada ya serikali?
Men you are right.Vyuo hivyo vya private vinavyotoa scholarship kwa bright students biashara zao ni kuuza mawazo yatokanayo na research results kwa makampuni au taasisi mbalimbali. Ndio biashara yao.kwetu yakianzishwa yatahitaji ruzuku serikali. Kwetu huku mawazo yanakuwa generated ulaya,IMF,WB.wanahitaji ready made products.Hivyo vyuo vitakosa biashara.
 
kamanda
ni kweli ni wasomi wanaoongoza nchi na wanaoongoza nchi ndio wamegeka mafisadi hiyo ni kweli.
Sasa basi ktk hilo udhani ni chuo gani ambacho kimesababisha kalaa hilo??
udsm
 
Hili sio suala la dini. Na kama lawama za Nyerere zinakuja, zije kwa siasa zake katika masuala ya elimu.

Shule zilizotaifishwa nyingi zilikuwa za dini lakini sehemu kubwa ya funding ilikuwa inatoka serikalini. Hivyo Nyerere alifanya vizuri kutaifisha shule. Nyerere alisomeshwa kwa schoolarship ya serikali lakini kazi alipangiwa katika shule ya dini. Na haya yalikuwa mapungufu makubwa ya serikali ya mkoloni.

Pamoja na kutaifisha hizo shule na kuzifanya kuwa za taifa, sera zake za kuendeleza elimu zilikuwa mbovu sana. Mpango wa UPE ambao ulikuza literacy rates ulikuwa ni mbovu. Wataalamu wa mambo ya elimu walitoa mapendekezo yao kuwa ili UPE iwe na mafanikio bila kupunguza kiwango cha elimu, ni lazime mpango uwe wa miaka 20 (long term). Mapendekezo hayo aliyakataa na kusema UPE inaweza kufanyika kwa mpango wa miaka 7 tu. Na katika mpango wake huo akatumia walimu wasio na mafunzo. Na matokeo mabovu ya mfumo mzima yalianza kuonekana kabla ya yeye kuondoka madarakani. Na kama mipango yake ingekuwa mizuri katika UPE, serikali ya Mkapa isingerudia kufanya mpango uliofanana na UPE miaka michache iliyopita.

Pamoja na kuongeza shule nyingi wakati wa mpango wa UPE bajeti ya elimu haikuongezeka kukidhi mahitaji ya wizara hiyo. Hivyo kuwa na sera na kutotoa pesa za kusaidia sera hizo ni sawa na kutokuwa na sera zenyewe.

Pia alikuwa nyuma sana katika sera za elimu ya juu. Model yake ilikuwa kwa watu wengi kuwa na elimu ya darasa la saba. Baada ya kundi hilo kuwe na kundi watu waliomaliza vyuo vya kati ambao watakuwa kama viranja. Na baada ya kundi hilo liwepo kundi la wachache wenye elimu ya juu watakaongoza wenzao.

Mfumo huu ulizungumzwa kwanza na William Edward Burghardt DuBois (mmoja wa waanzilishi wa Pan Africanism). Yeye alisema kuwa hili watu weusi waendelee ni lazima wawe na talented ten (asilimia kumi ya wenye vipaji).

Matalajio yalikuwa ni kutoa watu wenye vipaji kuendeleza jumuia zao. Siku za mwisho wa maisha ya DuBois alisema hawa talented ten wamekuwa ni dissapointment kwa jumuia za watu weusi. Badala ya kutumikia jumuia zao wamekuwa Bourgeoisie na mchango wao ni mdogo katika maendeleo ya mtu mweusi.

Watanzania wengi wanapoteza muda katika vyuo vya kati. Kwa maoni yangu vyuo vya kati vifanyiwe marekebisho hili viwe vyuo vinavyotoa digrii. Na wataalamu wa ngazi za kati (Viranja) wawe ni watu wenye digrii na sio diploma. Wahitimu wenye digrii wafanye kazi kama viranja katika miaka mitatu mpaka mitano ya mwanzo (Entry and Junior level). Na baada ya miaka hiyo waweze kushika senior position, lakini hizo senior position zitegemee performance yao ya miaka iliyopita.

Ukiajiri wanafunzi kutoka shule na darasa moja, bado kutakuwa na tofauti kati yao. Ukichukua wanafunzi kutoka shule moja campus tofauti, bado kutakuwa na tofauti. Na vile vile tofauti kati ya wanafunzi wa vyuo mbalimbali ni kitu cha kutegemewa lakini sio cha kufanya chuo moja kuwa bora zaidi ya kingine. Mwajiri anapotoa ajira kwa wahitimu wapya ni lazima kutoa mafundisho ya utamaduni wa sehemu yake ya kazi, matarajio ya mwajiri na baadaye atumie angalau mwaka kuona ni jinsi gani mwajiriwa anafanya kazi yake vizuri.

Mpaka sasa utasikia wanasiasa wetu au wenye elimu ya juu Tanzania wanasema kutoa digrii kwa watu wengi kutawafanya wahitimu kuwa madreva wa taksi kama ilivyo Nigeria au Ghana. Kwa maoni yangu msimamo huu ni PURE CRAP. Watu wasinyimwe elimu kwa sababu ya ukosefu wa kazi. Mwenye digrii akiwa dreva wa taksi anafanya kazi hiyo kama stepping stone na lazima atakuwa na shughuli zingine za kuendeleza maisha. Mwenye elimu ndogo akiwa dreva wa taksi atafanya kazi hiyo kama way of life.
Nafikiri you not serious. Athari za UPE hadi leo?miaka mingapi imepita watu wana pHD hawakusoma wala kufundishwa na walimu wa UPE utaendelea kuiongelea athari ya UPE hadi lini?that possibly is a lame excuse.take note you might be discussing with people who were born after UPE and therefore they know nothing about that MDUDE.Tuambieni baada ya miaka ya themanini kwa nini hatuendelei. Isitoshe vyuo vikuu hakuna walimu wa UPE.
 
me nadhani tuangalie ni chuo gani kinachotoa watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi!!
 
Angalia umri wa UDSM,MAENDELEO YA KUTOA WATAALAM,KUFUNGUA MATAWI MENGINE YANAYOENDANA NA CHANGAMOTO,KUONGOZA VYUO VINGINE VIPYA,WANAOGRADUATE MASTERS NA PHD,LINGANISHA NA UMRI WA UDSM NA VYUO VIKUU VUKONGWE KAMA UDSM.AKIKA UDSM TUNAMPA 30% KI MAFANIKIO
 
Back
Top Bottom