UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

UDSM ndio chanzo cha mfubao wa Elimu Tz

Bin Maryam,

Huu umekuwa wimbo wangu miaka mingi kudai Kiswahili kitumike kufundishia mfumo mzima wa elimu yetu. Watu wanasahau kuwa kumfundisha mtu kwa lugha mama ni rahisi kupata matokeo bora kuliko lugha ngeni.

Wengi wetu hata tulipokwenda Form 6, kiingereza kilikuwa bado ni tata na shida bila kukimbilia kamusi kutafuta tafsiri.

Ni vipi tutaweza kuwa na waelimika wengi ikiwa twatumia lugha ngeni ambayo mpaka leo miaka 47 ya kujiendesha tunashindwa kuitumia?

Naafiki kabisa kama tungefundisha fizikia kwa kiswahili, ungepata wanafunzi wengi wenye utashi wa kusoma ili waelewe fizikia hivyo kuongeza watu wenye kuweza kutumia elimu kuboresha maarifa na vipaji.

Kiingereza ni muhimu kujifunza kama lugha kwa ajili ya mawasiliano na si kitu cha kuona aibu kama utachapia kimombo au kushindwa matamshi! Tunaona ni ufahari na kuwa tumeelimika tukizungumza na kutoa matamshi ya Kiingereza bila mshindo wa kilugha au kubabaika. Hayo ndio tunayaita maendeleo!

Rev, Kishoka:

Tunaweza kuendeleza mjadala wa kutumia kiswahili kwa miaka 100 inayokuja na bado kuna watu wengi watakaotaka kuendelea kutumia kiingereza.

Kwa maoni yangu tuache kiingereza kiendelee kutumika lakini wakati huohuo tuanze kuandika vitabu vya maana kwa kiswahili. Na wanaong'ang'ania kutumia kiingereza tunawataka watunge vitabu kwa kiingereza.

Wanaotaka kuendelea kutumia kiingereza tunataka watuonyeshe kazi za uandishi katika lugha hiyo na wasomaji wangapi wa kitanzania wenye kutumia kazi hizo.

Na wanaotaka kutumia kiswahili na waonyeshe kazi zao za uandishi katika lugha hiyo na jinsi gani wasomaji wa kiswahili wanavyotumia kazi hizo.
 
Bin Mariam, labda UDSM wataweza kutumia kiswahili, ila chuo kama SAUT itakuwa vigumu kwani vinawanafunzi kutoka zambia kenya uganda ghana africa ya kusini na malawi, isitoshe mwakahuu wanategemea kudahiri wanafunzi kutoka italy, uk na usa. Pia kina wahadhiri watawa kutoka Italy itakuwa vigumu kuwaambia wafundishe kwa kiswahili!

Tanzania ina university 32 UDSM wakitumia kiswahili poa tu! kwani hata china ujerumani UAE na urusi kuna vyuo vinatumia mitaala ya kiingereza kwa ajili ya local and international students.
 
Bin Mariam, labda UDSM wataweza kutumia kiswahili, ila chuo kama SAUT itakuwa vigumu kwani vinawanafunzi kutoka zambia kenya uganda ghana africa ya kusini na malawi, isitoshe mwakahuu wanategemea kudahiri wanafunzi kutoka italy, uk na usa. Pia kina wahadhiri watawa kutoka Italy itakuwa vigumu kuwaambia wafundishe kwa kiswahili!

Tanzania ina university 32 UDSM wakitumia kiswahili poa tu! kwani hata china ujerumani UAE na urusi kuna vyuo vinatumia mitaala ya kiingereza kwa ajili ya local and international students.

Lugha mama ya Tanzania ni lugha ipi? Si Kiswahili? Kwa nini tukimbilie kuwa na mfumo wa elimu ambao unatumia lugha ya pili au tatu ikitegemea kama unajua kilugha chenu kufundishia?

Ukienda kusoma Norway, Finland, China, Sweden, Russia, Libya, Spain, Portugal, UK, USA ni shurti ujue lugha mama ya nchi hizo.

Sasa kwa nini nasisi tusitumie nafasi hii kuikuza lugha yetu kupita mipaka ya Kenya na Uganda? Kwani kuna ubaya gani kwa Mnyanja au Mbemba wa Zambia au Mchwi kutoka Ghana kujifunza Kiswahili?

Nafikiri sisi tumejenga ile hisia ya unyonge (inferiority complex) katika lugha yetu na ndio maana tunakimbilia sana kukataa isiwe lugha kuu ya matumizi na kukimbilia eti Kiingereza kiwe ndio lugha ya mawasiliano ya kimataifa.

80% ya Watanzania hawajui Kiingereza na hata wakijua ni maneno mawili Yes, No au My friend! Kwa nini tunapoteza nafasi ya pekee ya kuijenga lugha yetu ambayo ndio kitambulisho chetu kikuu?

Nafikiri ni matokeo ya vidonda vya ukoloni ndio maana nchi zetu za Afrika tunaona sifa kubwa sana kukoroga "yai" huku hata lugha asili zinatushinda! Ndio yale ya "Zabibu Speaking"!
 
Bin Mariam, labda UDSM wataweza kutumia kiswahili, ila chuo kama SAUT itakuwa vigumu kwani vinawanafunzi kutoka zambia kenya uganda ghana africa ya kusini na malawi, isitoshe mwakahuu wanategemea kudahiri wanafunzi kutoka italy, uk na usa. Pia kina wahadhiri watawa kutoka Italy itakuwa vigumu kuwaambia wafundishe kwa kiswahili!

Tanzania ina university 32 UDSM wakitumia kiswahili poa tu! kwani hata china ujerumani UAE na urusi kuna vyuo vinatumia mitaala ya kiingereza kwa ajili ya local and international students.

Mimi sina matatizo ya watu kusoma kwa kiingereza. Matatizo yangu kwanini hakuna vitabu vya kiswahili vya taaluma mbalimbali.
 
Rev, Kishoka:

Tunaweza kuendeleza mjadala wa kutumia kiswahili kwa miaka 100 inayokuja na bado kuna watu wengi watakaotaka kuendelea kutumia kiingereza.

Kwa maoni yangu tuache kiingereza kiendelee kutumika lakini wakati huohuo tuanze kuandika vitabu vya maana kwa kiswahili. Na wanaong'ang'ania kutumia kiingereza tunawataka watunge vitabu kwa kiingereza.

Wanaotaka kuendelea kutumia kiingereza tunataka watuonyeshe kazi za uandishi katika lugha hiyo na wasomaji wangapi wa kitanzania wenye kutumia kazi hizo.

Na wanaotaka kutumia kiswahili na waonyeshe kazi zao za uandishi katika lugha hiyo na jinsi gani wasomaji wa kiswahili wanavyotumia kazi hizo.

Bin Maryam,

Nimenunua kutoka Barnes and Noble kitabu cha Prof. Shivji na Hamudi Majamba kinachoitwa "Constitutional and Legal systems of Tanzania" nikajiuliza je hawa ndugu hili chapisho lao linaweza kuwa katika lugha ya Kiswahili ili Watanzania wanufaike na si "wasomi" wenzao wa nje ?

Nafikiri ni wakati muafaka kuanza kuwasukuma wasomi wetu wanaoandika machapisho yao kutetea shahada zao waanze kuwandika nakala nyingine kwa Kiswahili ili zitumike hata kwa mwananchi wa kawaida ambaye hajui Kimombo.

Hichi kitabu cha Mifumo ya Katiba na Sheria Tanzania ni kizuri sana kufundishia hata shule za Msingi ili kuanza kujenga Taifa lenye mwamko wa kujua Katiba na Sheria zake na miundo yake kuanzia umri mdogo. Lakini kama hawana chapisho katika lugha ya Kiswahili, basi tunalinyima Taifa hazina kubwa ya kuweza kujua jinsi sheria na katiba zao zinavyoundwa na hivyo somo la Uraia linapotea machoni mwetu na kubakia kwa "wateule" wachache wanaokwenda Kidato cha Sita na Chuo Kikuu!
 
Bin Maryam,

Nimenunua kutoka Barnes and Noble kitabu cha Prof. Shivji na Hamudi Majamba kinachoitwa "Constitutional and Legal systems of Tanzania" nikajiuliza je hawa ndugu hili chapisho lao linaweza kuwa katika lugha ya Kiswahili ili Watanzania wanufaike na si "wasomi" wenzao wa nje ?

Nafikiri ni wakati muafaka kuanza kuwasukuma wasomi wetu wanaoandika machapisho yao kutetea shahada zao waanze kuwandika nakala nyingine kwa Kiswahili ili zitumike hata kwa mwananchi wa kawaida ambaye hajui Kimombo.

Hichi kitabu cha Mifumo ya Katiba na Sheria Tanzania ni kizuri sana kufundishia hata shule za Msingi ili kuanza kujenga Taifa lenye mwamko wa kujua Katiba na Sheria zake na miundo yake kuanzia umri mdogo. Lakini kama hawana chapisho katika lugha ya Kiswahili, basi tunalinyima Taifa hazina kubwa ya kuweza kujua jinsi sheria na katiba zao zinavyoundwa na hivyo somo la Uraia linapotea machoni mwetu na kubakia kwa "wateule" wachache wanaokwenda Kidato cha Sita na Chuo Kikuu!

Rev:

Kuna mchumi mmoja wa Bangladesh alipokea Noble kwa kuanzisha credit system nchini mwake. Na alitoa hoja kuwa ni makosa makubwa kumnyima mtu wa kawaida credit au mkopo kwa sababu ya umasikini wake.

Kwa upande wetu ni makosa makubwa kutotoa vitabu vya kitaaluma kwa lugha inayozungumzwa na watu wengi. Vitabu hivyo sio lazima vitumike kwenye mashule lakini vikitumika kwa kujisomea tu vitatoa mchango mkubwa.
 
Sijui kama Watanzania tumeshaamka kutoka usingizi wa Ujamaa na kutambua kuwa tupo kwnye Uchumi wa soko huria na ni lazima tuanze kuchangia kwenye elimu na afya. Nimeona hili bandiko kwenye gazeti la Mwananchi likidai kuwa kuongezeka kwa ada ni kudumaza maendeleo ya kitaaluma na eti wananchi hawana uwezo!

Ukikomaa kwa kudai kuwa wewe ni masikini huna uwezo, hakika utabakia masikini milele! Jamani si kuna bodi ya mikopo kwa ajili ya elimu? kwani ni tabu gani kwenda kukopa na kulipa hapo baadaye?

Ni mpaka lini tutaendelea kulilia dezo? Hivi huyu aliyeandika makala hii anatambua uwiano wa mapato na matumizi ya chuo hiki au anajisemea ovyo? kuna gharama nyingi sana kuendesha chuo; mishahara, bima za afya, bili za umeme, maji, chakula, utunzaji wa mali: majengo, magari na ardhi, ulinzi, vitabu, mitambo na samani nk. Sasa kama Serikali inasema inapunguza ruzuku, je pesa zitoke wapi? Zitoke kwenye fungu la MCA au tutadai zitokee EPA na Richmond?


Ada mpya Mlimani itakwamisha maendeleo ya kitaalumaCHUO Kikuu cha Dar es Salaam kinatarajia kupandisha ada kwa kozi zote zinazotolewa chuoni hapo kuanzia muhula wa masomo wa kuanzia Septemba, mwaka huu kwa wanafunzi wapya na wanaoendelea na masomo.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya Tume ya Uchunguzi juu ya Uendeshaji wa Vyuo Vikuu na Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa serikali, kwa wastani ada hiyo inatarajiwa kupanda kwa zaidi ya asilimia 40 ya viwango vya sasa kwa kozi zote zinazotolewa kwenye chuo hicho.

Kwa mfano mapendekezo hayo yanaonyesha kuwa kozi za Sayansi ya Jamii isipokuwa Uchumi na Elimu karo itapanda kutoka Sh722,000 kwa mwaka hadi zaidi ya Sh1 milioni kwa mwaka na kozi za sayansi, udaktari na uandishi wa habari kuwa Sh1,122,000 badala ya Sh922,000 huku wanaosoma sheria wakitakiwa kulipa Sh2.5 milioni.

Mchanganuo huo pia unaonyesha kuwa wanaoendelea na masomo watatakiwa kulipa kati ya Sh1.3 hadi 2.5 milioni kwa mwaka kutegemeana na kozi wanazosoma na kwamba ongezeko hilo ni kwa ajili ya ada ya masomo (tuition fee), bila gharama nyingine kama malazi, chakula, vitabu na mahitaji mengine muhimu ya kitaaluma.

Licha ya uongozi wa chuo kusema kuwa haya ni mapendekezo yanayowezakuidhinishwa au kukataliwa na serikali, ni dhahiri kwamba chuo kimepania kuongeza ada kwa kiwango hicho ambacho tunadhani kwamba utakuwa mzigo mkubwa kwa wanafunzi na wazazi.

Kuna fununu kwamba ongezeko hilo ni kama maandalizi kwa chuo hicho kujitegemea kutokana na maelekezo ya serikali kwamba vyuo vyote vinavyojiweza vianze kujiendesha bila kutegemea ruzuku.

Ni dhahiri kwamba ongezeko hilo likipitishwa litakuwa na madhara makubwa kwa wanafunzi na wazazi, kutokana na ukweli kwamba, gharama zitakuwa zimeongezeka kwa kiasi kikubwa.

Inawezekana uongozi wa chuo umeliangalia jambo hilo kwa mtazamo kwamba, itakuwa rahisi kupata fedha kutoka kwenye Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ambayo hutolewa na serikali kwa wanafunzi wanaotimiza masharti.

Hata hivyo, bado mzigo huo unawaelekea wanafunzi na wazazi kwa kuwa ndiyo watakaolipa mkopo huo baada ya kumaliza masomo na zaidi ya hapo, wanatakiwa kuchangia asilimia 40 ya fedha hizo, ambalo pia ni tatizo kutokana na wengi kutokuwa na uwezo.

Itakumbukwa kwamba, mwaka jana kulitokea mgomo chuoni hapo baada ya kufukuzwa wanafunzi walioshindwa kulipa asilimia 40 ya ada hiyo mpaka serikali ilipoingilia kati na kuwasaidia walioshindwa kabisa.

Si hivyo tu, kuna baadhi ya wanafunzi ambao hawana sifa zinazotakiwa kupata mkopo huo, lakini wana sifa za kusoma Chuo Kikuu, ambao hulipiwa na wazazi wao, kwa hiyo kuongezwa kwa karo unakuwa mzigo mzito unaoweza kusababisha baadhi yao kushindwa kuendelea na masomo na idadai ya wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho kupungua kwa kiasi kikubwa.

Tunashauri kwamba, kama suala hilo halijapelekwa serikalini uongozi wa chuo ufikirie upya juu ya viwango hivyo na kama kuna haja ya kuongeza, ongezeko lisizidi asilimia 20 ili wanafunzi waweze kusoma na taifa letu liendelee kupata idadi kubwa ya wasomi na wataalamu wanaohitajika sana kwa maendeleo ya taifa letu katika karne hii.

Hata kama mapendekezo hayo yamepelekwa, serikali ione umuhimu wa kushusha na badala yake vyuo vishauriwe vitafute njia mbadala ya kupata fedha badala ya kuwatwisha mzigo wanafunzi na wazazi. Tunaamini kwamba, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambacho kinaaminika kitaaluma, kina uwezo kwa kupata fedha kutoka kwenye miradi mbalimbali ya utafiti ambazo zinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kuziba upungufu utakaotokea endapo serikali itapunuguza ruzuku au fedha za uendeshaji wa chuo hicho bila kuongeza ada kwa asilimia kubwa.
 
Sijui kama Watanzania tumeshaamka kutoka usingizi wa Ujamaa na kutambua kuwa tupo kwnye Uchumi wa soko huria na ni lazima tuanze kuchangia kwenye elimu na afya. Nimeona hili bandiko kwenye gazeti la Mwananchi likidai kuwa kuongezeka kwa ada ni kudumaza maendeleo ya kitaaluma na eti wananchi hawana uwezo!

Ukikomaa kwa kudai kuwa wewe ni masikini huna uwezo, hakika utabakia masikini milele! Jamani si kuna bodi ya mikopo kwa ajili ya elimu? kwani ni tabu gani kwenda kukopa na kulipa hapo baadaye?

Ni mpaka lini tutaendelea kulilia dezo? Hivi huyu aliyeandika makala hii anatambua uwiano wa mapato na matumizi ya chuo hiki au anajisemea ovyo? kuna gharama nyingi sana kuendesha chuo; mishahara, bima za afya, bili za umeme, maji, chakula, utunzaji wa mali: majengo, magari na ardhi, ulinzi, vitabu, mitambo na samani nk. Sasa kama Serikali inasema inapunguza ruzuku, je pesa zitoke wapi? Zitoke kwenye fungu la MCA au tutadai zitokee EPA na Richmond?

Mimi sina tatizo za watoa hudumu kupandisha gharama za huduma zao. Tatizo hapa nyumbani ni viwango vya upandishaji. Si ajabu kuamka na kuambiwa kuwa bei imepandishwa kwa asilimia 50, mara dufu au zaidi! Sasa hata kama unania ya kulipa, utapata wapi hizo pesa kwa ghafla hivyo? Watoa huduma kwenye soko huria huwa kupandisha bei ni hatua ya mwisho, wanaangalia kwanza uwezekano wa kupunguza gharama za uzalishaji. Ndiyo maana lay-offs haziishi. Kwetu tunakimbilia kupandisha bei. Kwa hawa wasomi wameangalia kwa mfano kiasi gani wanaweza kupunguza bili za umeme kwa kutukia balbu bora zaidi, vyombo efficient zidi n.k? Kwenye magari, kuna hata siku moja wenzetu wameangalia fuel consumption ya gari? Umetaja chakula, kwani bado wanatoa chakula bure? Mimi nadhani wangeanza huku kwanza kabla ya kufikiria kupandisha bei. Pengine wataona hawana haja ya kupandisha kwa kiasi kikubwa vile.
 
Hiki Chuo Kinaongozwa Na Waadhili Amboa Wana Mtandio(veil) ( Not Mtindio) Wa Ubongo Mimi Huwa Nawaita Fool Sorry Full Professors. Walirithi Kasumba Ambayo Mabya Sana Ambayo Tuliachiwa Na Wazungu Kwamba Prof Is An Enemy To A Student Not A Friend. Inovation ,invertion And Creations Ya Vipaji Inahitaji Utulivu Na Uwezezaji Wa Mawazo Ya Vizazi Vipya Katika Kurahisisha Shughuli Za Kila Siku Za Mwanadamu. Lakini Hawa Ma Prof Wetu They Are To Rigig Beyond Reparing.kilicho Nisikitisha Kuliko Vyote Walipinga Sana Kuanzishwa Kwa Kwa Vyuo Vingine. Hawajui Kwamba Elimu Inapatika Na Kwa Vitabu Na Sio Kwenye Jengo Linaloitwa Chuo. Pia Elimu Yote Sio Kwa Sababu Ya Chuo Zumuni Lakwe Ni Kumsaidia Mwananchi Wa Kawaida Kwa Hiyo Huko Chini Kwa Mwananchi Wa Kawaida Ndio Mwisho Na Chanzo Cha Elimu.
 
Hiki Chuo Kinaongozwa Na Waadhili Amboa Wana Mtandio(veil) ( Not Mtindio) Wa Ubongo Mimi Huwa Nawaita Fool Sorry Full Professors. Walirithi Kasumba Ambayo Mabya Sana Ambayo Tuliachiwa Na Wazungu Kwamba Prof Is An Enemy To A Student Not A Friend. Inovation ,invertion And Creations Ya Vipaji Inahitaji Utulivu Na Uwezezaji Wa Mawazo Ya Vizazi Vipya Katika Kurahisisha Shughuli Za Kila Siku Za Mwanadamu. Lakini Hawa Ma Prof Wetu They Are To Rigig Beyond Reparing.kilicho Nisikitisha Kuliko Vyote Walipinga Sana Kuanzishwa Kwa Kwa Vyuo Vingine. Hawajui Kwamba Elimu Inapatika Na Kwa Vitabu Na Sio Kwenye Jengo Linaloitwa Chuo. Pia Elimu Yote Sio Kwa Sababu Ya Chuo Zumuni Lakwe Ni Kumsaidia Mwananchi Wa Kawaida Kwa Hiyo Huko Chini Kwa Mwananchi Wa Kawaida Ndio Mwisho Na Chanzo Cha Elimu.

Sawa mkuu
huo u enemy wa prof na mzungu kutuachia duuuuuuuu
Mbona hawa ma prof wa kizungu wapo friendly sana

Bin Maryam umefikia wapi? Mbona kimya?????
 
Mkamap na wengine naomba tafsiri za maneno haya:

All pages
Articles with the fewest revisions
Articles with the most categories
Articles with the most revisions
Book sources
Broken redirects
Categories
Dead-end pages
Disambiguation pages
Double redirects
Export pages
File list
Gallery of new files
List of blocked IP addresses and usernames
List redirects
Log in / create account
Logs
Long pages
MIME search
Most linked to categories
Most linked to images
Most linked to pages
Most linked-to templates
My watchlist
New pages
Oldest pages
Orphaned pages
Pages without language links
Popular pages
Preferences
Prefix index
Protected pages
Random redirect
Short pages
Statistics
System messages
Uncategorized categories
Uncategorized images
Uncategorized pages
Uncategorized templates
Unused categories
Unused files
Unused templates
Upload file
User contributions
User list
Version
Wanted categories
Wanted pages
 
Huu Ulikuwa Mtindo Wa Miaka Ya Sabini Na Earlier 80s. Sasa Hivi Kwa Wazungu Unapata Plastic Smiles
 
Hiki Chuo Kinaongozwa Na Waadhili Amboa Wana Mtandio(veil) ( Not Mtindio) Wa Ubongo Mimi Huwa Nawaita Fool Sorry Full Professors. Walirithi Kasumba Ambayo Mabya Sana Ambayo Tuliachiwa Na Wazungu Kwamba Prof Is An Enemy To A Student Not A Friend. Inovation ,invertion And Creations Ya Vipaji Inahitaji Utulivu Na Uwezezaji Wa Mawazo Ya Vizazi Vipya Katika Kurahisisha Shughuli Za Kila Siku Za Mwanadamu. Lakini Hawa Ma Prof Wetu They Are To Rigig Beyond Reparing.kilicho Nisikitisha Kuliko Vyote Walipinga Sana Kuanzishwa Kwa Kwa Vyuo Vingine. Hawajui Kwamba Elimu Inapatika Na Kwa Vitabu Na Sio Kwenye Jengo Linaloitwa Chuo. Pia Elimu Yote Sio Kwa Sababu Ya Chuo Zumuni Lakwe Ni Kumsaidia Mwananchi Wa Kawaida Kwa Hiyo Huko Chini Kwa Mwananchi Wa Kawaida Ndio Mwisho Na Chanzo Cha Elimu.

Well said mkuu!
Ila naomba nirekebishe kidogo nafikiri hii kasumba ya u-enemy na students wamerithishana wenyewe cos hata wazungu hawako ivo.
Kingine ni kwamba most of the lecturers hapa bongo wako ktk competiton na students! Bahati nzuri au mbaya na mimi nimepata kufundishwa na hawa malecturer wa UDSM kwa kweli it's like they are taking everything done by students to be personal.
Mfano mdogo ni kuwepo hata misemo kwamba ukiwa mwanafunzi wa Engineering unatakiwa uwe tofauti na wengine usipande kutoka, usiwe mtanashati, na kwa wale wenye Dreadlocks (Rastafarians) kile kitivo sio mahala pao...utajikuta unapigwa sup za kufa mtu na ghafla tu unakuwa discontinued usipozikata rasta na kubadilisha tabia > hii ni true story niliiona wakati niko pale miaka ya nyuma.
The truth of the matter these guys need to change or be taken through CHANGE MANAGEMENT TRAINING ili mitizamo yao iwe +ve!
 
Si kila chuo kiliundwa kuwa chuo kikuu mimi navyojua, hivyo suala la vyuo kukua na kuwa vyuo vikuu mi binafsi siliafiki kwa sana pamoja na uchache wa vyuo tulivo navyo....
Bora kuanzisha vyuo vikuu vipya, kwa style hiyo hata Tambaza iatendelea kukua toka Sekondary ya kawaida, high school, mwisho Ka DIT then Mlimani si ndivyo? evelolution hiyo sijui ka iko powa.
Unajua way back compition ilikuwa kali,,.walio zama mlimani walikuwa vichwa kikwelii compared ta walio enda kwa hizo institution zingine. Nisahihishe ka nakosea..ka ulikuwepo bila shaka ndoto ya kuzama mlimani ulikuwa nayo.

Point clear, si UDSM bali ni wizara husika kutokuwa na mipango endelevu ya kuwa na vyuo vikuu vingi. Maproff si shida toka nje wangeweza ajiriwa maana UDSM mpaka sasa wako wanao toka nje.

Nimebahitika kuwa mbeya wantime kuna kampasi ya MU, wako wanafunzi wansoma sheria,degree na diploma. Ukiuliza kuna maproff wangapi ni kituko, dogo kamaliza last year MU main campus kaja hapa nae lecturer, na test antunga mpak U.E, sasa huyo si mmoja wako wengi tu, Niambie quality ya hawa wanasheria itakuwa vp? au uzoefu wa mtaa ndo utawatoa?
....nakuja
 
Jamani wazazi tuamkeni, suala sio mtoto kusoma taaluma tu pia anahitajika kulelewa kimaadili, kuna chuo kama SUZA na Tumaini makumira cumpas pamoja na masomo ya taaluma vijana hupewa elimu ya kiroho na maadili ya maisha.

lakini udsm sijui prof.mkandara anaswali msikiti upi? pia keshakuwa masanja wa tvt atakaa saangapi kufuatilia taaluma, watoto nao kila wikiendi wanakata viuno majukwaani wakiwania free airtime za tigo!
 
Si kila chuo kiliundwa kuwa chuo kikuu mimi navyojua, hivyo suala la vyuo kukua na kuwa vyuo vikuu mi binafsi siliafiki kwa sana pamoja na uchache wa vyuo tulivo navyo....
Bora kuanzisha vyuo vikuu vipya, kwa style hiyo hata Tambaza iatendelea kukua toka Sekondary ya kawaida, high school, mwisho Ka DIT then Mlimani si ndivyo? evelolution hiyo sijui ka iko powa.
Unajua way back compition ilikuwa kali,,.walio zama mlimani walikuwa vichwa kikwelii compared ta walio enda kwa hizo institution zingine. Nisahihishe ka nakosea..ka ulikuwepo bila shaka ndoto ya kuzama mlimani ulikuwa nayo.

Point clear, si UDSM bali ni wizara husika kutokuwa na mipango endelevu ya kuwa na vyuo vikuu vingi. Maproff si shida toka nje wangeweza ajiriwa maana UDSM mpaka sasa wako wanao toka nje.

Nimebahitika kuwa mbeya wantime kuna kampasi ya MU, wako wanafunzi wansoma sheria,degree na diploma. Ukiuliza kuna maproff wangapi ni kituko, dogo kamaliza last year MU main campus kaja hapa nae lecturer, na test antunga mpak U.E, sasa huyo si mmoja wako wengi tu, Niambie quality ya hawa wanasheria itakuwa vp? au uzoefu wa mtaa ndo utawatoa?
....nakuja

ukisoma threads za nyuma tayari tulishayaongelea na sasa tuko hatua nyingine. haya yaliongelewa karibia threads tatu hivi. sasa heshima yako mkuu, hatua tuliopo sio tena kwenye background of the problem bali tumeisha vuka hata kwenye findings, na sasa mbele yetu ni solution na recommendation, ambapo tuko tunaandaa dismentaling nzima ya Lugha ya pili kama sehemu ya kufundishia. tuendelee bin mariam. leo ninachukua haya maneno uliyoweka kwa vijana wangu ili wanitafsirie.
 
Si kila chuo kiliundwa kuwa chuo kikuu mimi navyojua, hivyo suala la vyuo kukua na kuwa vyuo vikuu mi binafsi siliafiki kwa sana pamoja na uchache wa vyuo tulivo navyo....
Bora kuanzisha vyuo vikuu vipya, kwa style hiyo hata Tambaza iatendelea kukua toka Sekondary ya kawaida, high school, mwisho Ka DIT then Mlimani si ndivyo? evelolution hiyo sijui ka iko powa.
Unajua way back compition ilikuwa kali,,.walio zama mlimani walikuwa vichwa kikwelii compared ta walio enda kwa hizo institution zingine. Nisahihishe ka nakosea..ka ulikuwepo bila shaka ndoto ya kuzama mlimani ulikuwa nayo.

Point clear, si UDSM bali ni wizara husika kutokuwa na mipango endelevu ya kuwa na vyuo vikuu vingi. Maproff si shida toka nje wangeweza ajiriwa maana UDSM mpaka sasa wako wanao toka nje.

Nimebahitika kuwa mbeya wantime kuna kampasi ya MU, wako wanafunzi wansoma sheria,degree na diploma. Ukiuliza kuna maproff wangapi ni kituko, dogo kamaliza last year MU main campus kaja hapa nae lecturer, na test antunga mpak U.E, sasa huyo si mmoja wako wengi tu, Niambie quality ya hawa wanasheria itakuwa vp? au uzoefu wa mtaa ndo utawatoa?
....nakuja

karibu sana ndugu yetu. tumesema swala la prof sio kigezo cha chuo kuwa bora. tuliongelea angalia threads za hapa hapa. kuwa tunahitaji watu wa kubadili mchanga kuwa sambusa.

pili nilipata kuambiwa kuwa huyo Inocent wa mzumbe mbeya campus, alienda pale na kujiita lecturer jambo ambalo lilichukkulia wanafunzi kumkatalia hata test yake aliyokuwa tayari ameisha itunga.

hata hivyo, tunahitaji marekebisho makubwa sana katika vyuo vikuu vyetu, wala sio kuonyesha kuwa chuo fulani ni afadhali ya kingine.
 
karibu sana ndugu yetu. tumesema swala la prof sio kigezo cha chuo kuwa bora. tuliongelea angalia threads za hapa hapa. kuwa tunahitaji watu wa kubadili mchanga kuwa sambusa.

pili nilipata kuambiwa kuwa huyo Inocent wa mzumbe mbeya campus, alienda pale na kujiita lecturer jambo ambalo lilichukkulia wanafunzi kumkatalia hata test yake aliyokuwa tayari ameisha itunga.

hata hivyo, tunahitaji marekebisho makubwa sana katika vyuo vikuu vyetu, wala sio kuonyesha kuwa chuo fulani ni afadhali ya kingine.

Ebwana Bin Maryam unaendelea je?
Mushombosi pia umefikia wapi? pia na wengine wote mmefikia wapi?
 
Back
Top Bottom