UDSM mwaka huu kuna nini?

UDSM mwaka huu kuna nini?

Qualifications za kusoma kozi yoyote UDSM ni D mbili tu. Sasa kama capacity ni kudahili wanafunzi 100 na waombaji ni 1000 utawachuja vipi hao ubaki na 100?
Kwanza mtoa mada alitakiwa adadavue kwa kina kozi hizo za engineering zilizopo na capacity yake kwa kila moja

Huenda ni kweli unakuta kozi moja wanahitaji watu 150 na waombaji ni wengi sasa matokeo yake wanakosa wengi bila kujali ana one au nini bado wengi watakosa tu hapo.

Swala sio entry qualification ni capacity tu .

Waende vyuo vingine sio lazima udsm
 
Ukweli ni kwamba 1 ya 3 au 4 sio issue anymore kila mtu amefaulu marahi elimu yetu haina thamani tena ilisha ingiliwa na siasa .
Huu ndio ukweli sasa

Miaka ya zamani ilikuwa mtu kupata one anawekewa sherehe na shule inamtambua kama mwanafunzi bora.

Lakini saizi one imekuwa kitu cha kawaida sana, unaweza ukapata na mzazi hata asishtuke.
 
Ufauli wake O'Level upoje? Na je alisoma shule ya Technical?. Huyo mtu hata akiwa na 1 ya 3 kama O'level hakusoma masomo au shule yenye mrengo wa hiyo fani jua hawezi mchomoa mtu mwenye 1 ya 4 ambaye O'level alisoma shule na masomo ya mrengo wa hiyo fani.

Ufaulu wa A'level ni moja ya vigezo ila sio kigezo pekee.
 
Competition ni kubwa but form six leavers wengi wanaotaka engineering dit ni bora zaidi kuliko udsm .

Kwa sababu udsm wanatao bachelor of science in engineering , alafu dit wanatoa bachelor of engineering kwa hiyo wangetakiwa kuelewa hicho

Pia Udsm kwa tanzania hii siyo chuo bora kwa engineering labda ni chuo bora kwa mazingira mazuri.

Ni chuo kikuu kikongwe hapa bongo lakn siyo chuo bora kwa engineering .

Kama kuna kuna mwenye hoja alete hapa hoja zake kutetea udsm
DIT ni chuo kizur sana.. nilisoma pale koz flan hivi..

Wale jamaa wapo vzr..
 
Competition ni kubwa but form six leavers wengi wanaotaka engineering dit ni bora zaidi kuliko udsm .

Kwa sababu udsm wanatao bachelor of science in engineering , alafu dit wanatoa bachelor of engineering kwa hiyo wangetakiwa kuelewa hicho

Pia Udsm kwa tanzania hii siyo chuo bora kwa engineering labda ni chuo bora kwa mazingira mazuri.

Ni chuo kikuu kikongwe hapa bongo lakn siyo chuo bora kwa engineering .

Kama kuna kuna mwenye hoja alete hapa hoja zake kutetea udsm
Tofauti ya hizo degree mbili ni nini kwani, ivyo Bora duniani ni ya dit ama udsm
 
Tangu kupata uhuru sidhani Kama Kuna changes za maana zimefanyika kwenye mfumo wa elimu.

Anyways sio kesi kwa mwaka huu ufaulu ni mkubwa na hio sio UDSM tu hata MZUMBE kwa upande wa LAW wamechukua 3-5, wengine wote wamebehuliwa nje

Ajaribu kuapply na mburahati😂 ,(jokes)
 
UDSM wanafanya mambo ya kizamani sana.

Wasichojua ni juwa dunia ya sasa ufaulu unaongezeka sana one zipo kibao sawa ila sasa sio nyingi kama inavyosemwa

Wote hawawezi kusoma hapo sawa ila hata huyo mwenye 1.5 kweli?? Anakosa??
Kwa mfano chuo kina nafasi ya wanafunzi 100 wa kozi husika.
Wameomba watu 200 wa 1 ya 3&4, 150 wa 1 ya 5.
Wawachukue wote 350? Watasomea wapi wakati facilities zipo za watu 100?
Mnataka wachukue wote kisha mlete malalamiko watu wanarundikana hawasomi kwa utulivu, wanakosa vifaa vya kufundishiwa?
 
Habarini wana jukwaa.

Nimeona nije hapa jukwaani nitoe hili jambo, huenda nitapata ufafanuzi.

Nimekuwa nikikutana na malalamiko ya wanafunzi waliomaliza form 6 mwaka huu, wanaotarajia kujiunga na vyuo hivi karibuni. Wengi wao wanalalamika kuwa kila waombapo nafasi UDSM wanakataliwa, na wengine wanadiriki kusema kuwa vigezo sahihi wamekidhi kulingana takwa husika.

Sio mtaani wala mtandaoni ni malalamiko juu ya vijana na mabinti wanaotarajia kujiunga na Elimu ya Juu. Kuhusu Kukataliwa kuwa admitted hapo UDSM.

kuna huyu jirani yangu, yeye alisoma Ilboru Sec mchepuo wa PCM, kapata 1 ya 5, kachagua Udsm Course ya Civil Engineering, kakosa, bas analalama kila muda, hapa hata mie nimeshanga, huyu vigezo amekidhi kabisa, au labda huu mwaka 1 ya 3 na 4 ziko nyingi, hivyo inafanya wenye 5 na kuendelea wakose nafasi hapo COET?

Na Malalamiko ni kwa kila kada wanalalama mno, huku wakiwa na 1 zao nzuri, shida nn? Au utaratibu umebadilika hapo siku hizi? Kulikoniii?

Najua hapa kuna wafanyakazi, wana taaluma, wahadhiri, kutoka hapo UDSM, hebu mje mtoe ufafanuzi kutuondolea sintofahamu hii, maana huku uraiani hali ni mbaya watoto wanavurugwa vibaya, wakati ndoto zao ni kuwa hapo Mlimani main campus.

Tujuzweee kulikoniiiii?
Huyu wa engineering aende DIT palee.... Msulichuma
 
Back
Top Bottom