Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
nachokionaga mimi tu kwa wa TZ wengi ngoja niseme sasa ukweli....sehem ambayo yupo Muislam ndo utaona kuna maneno sanaaa ya udini au uteuzi wa JK akiwa Muislam utaskia kuna udini hii ni mbegu mbaya sana tunayoipanda.
 
Tuspoteze muda
Wakristu uchaguzi unakuja,chagua mkristu mwenzako,hii ndiyo njia ya kuyaua hayo mashetani.
 
Tuspoteze muda
Wakristu uchaguzi unakuja,chagua mkristu mwenzako,hii ndiyo njia ya kuyaua hayo mashetani.
shetani ni wewe unaetaka kuleta uovu nchini, maneno yako tu yanaonesha wewe ni mpumbavu flani kama basterd hivi ambae huna muelekeo
ngurue tasa wewe pumbav
yani waweza kutoa ushauri kama huo kwa wa TZ?
 
Wana JF mimi sioni hoja ya msingi hapa ya kuingiza issue za udini katika chama. Mjumbe akichaguliwa kidemokrasia usiangalie udini wake kwani dini inahusu nini na mambo ya siasa? Mjumbe aliyechaguliwa ni mjumbe tu tuachane na kutafuta kabila lake wala dini yake mambo haya hayatatufikisha popote. Tusipandikize mbegu za chuki!!!
 
Tuspoteze muda
Wakristu uchaguzi unakuja,chagua mkristu mwenzako,hii ndiyo njia ya kuyaua hayo mashetani.

inawezekana husomi habari za dunia wala kusikiliza redio. ila ninaimani kwa akili yako invyoonekana unaangalia tv. Ushauri: badala ya kuangalia vipindi kama mizingwe na mapishi tu, angalia na taarifa za habari ujuwe hiko unachoshabikia kitaleta nini kwa baba , mama na mke/mume wako.
 
Tuspoteze muda
Wakristu uchaguzi unakuja,chagua mkristu mwenzako,hii ndiyo njia ya kuyaua hayo mashetani.

Naamini kabisa mkristo mwenye imani yake ya dini hawezi tamka maneno kama haya ... Wewe ndio shetani mwenyewe sasa!!Dah Tanzania ina Raia wa ajabu sana
Tanzania huwa hatuangalii dini sisi ... ingekuwa hivyo enzi za mwalimu na sokoine watu wangelalalamika sana eti.Hebu rudisha busara kidogo (kama uliwahi kuwa nayo)
 
Watu wanaoleta malumbano ya kidini inaonyesha mdidimio wao wa kiakili. it doen't matter kiongozi kuwa muislamu ama mkristo, tunachotaka ni kiongozi bora na sio mkristo bora wala muislam bora na ndiyo maana hatuchagui askofu au shekhe, tunachangua viongozi. Leteni mada zenye tija mtandaoni na acheni hizi fikra finyu. Lete changamoto yenye kuijenga nchi tuijadili na si kuanza kusema waislamu wangapi wakristo wangapi wahindu wangapi, n.k. Hoja yoyote ya kidini ni mufilisi na anayeleta naye ni mufilisi...
 
Tuspoteze muda
Wakristu uchaguzi unakuja,chagua mkristu mwenzako,hii ndiyo njia ya kuyaua hayo mashetani.

Hata mtoto mdogo ukimuuliza shetani ni nani atakujibu kwani kauli yako tu inaonyesha Ushetani wako na wote wenye mawazo kama yako.
 
Jamani tuache kuendekeza mambo ya UDINI!!!! Tuhoji tu tutapoona mtu anachaguliwa kwa dini yake na si vigezo vingine vya kiuongozi.

Ni ujinga na uzuzu mtupu mtu kusema eti chama fulani ni cha kidini kwasababu viongoziwe wengi ni wa dini fulani bila kuangalia sababu za msingi kwanza!! eti serikali ni ya kikristu etu tu kwasababu viongozi wengi ni wakristu !! Chaa! hamuoni kuwa wengi wao wameenda shule??!!

Kuendekeza mambo hayo mwishowe mtakuwa si watu wa DINI tena bali watu DUNI!!!

Haya ni mawazo yaliyopitwa na wakati. Hiyo sababu imepitwa na wakati kama kulitumika ujanja huo ili kuwapatia nafasi nyingi za uongozi na sehemu nyeti sasa tunaelekea kuuumaliza siku si nyingi
 
Mswahili,

Kama umefuatilia posting zangu hapa kuanzia nijoin rasm JF, nimekuwa napinga sana suala la udini na niliweka post kibao tu nikimpinga mchambuzi na skam yake ya kutaka rais ajaye Tz lazima awe mkristo.

Sijali kama viongozi wote wakati wa mkapa walikuwa wakristo au kama Dr Bilali alinyimwa kura na wakristo. Ukweli I dont give a damn about it.

Tanzania ni moja na ccm ni chama ambacho kipo bara na visiwani. Kama ccm waliendesha propaganda kupondea cuf kuwa ni chama cha waislam bila kujali hiyo sababu unayoiweka hapa kuwa zanzibar wengi ni waislam, then ccm nao lazima waangaliwe kwa ujumla wao kote kote bara na visiwani.

So far, viongozi wa juu 4, NEC, na CC ya ccm ina waislam zaidi ya asilimia 75%. Hawa ndio watoa maamuzi na sera za ccm. Sijali kuwa makatibu kata wa ccm wengi ni wakristo au kuwa wakati wa Mkapa waliokuwa wengi ni wakristo. I am talking about leo hii na wala sio longo longo zingine.

CCM wakiendelea na mchezo wao mchafu wa kuchafua vyama vingine kuwa vya kidini au vya kikabila, basi wategemee the same bullet ikituma back to them loud and clear.

KWA SASA, CCM INA VIONGOZI WENGI SANA WAISLAM. KWA STANDARD YA PROPAGANDA ZA CCM DHIDI YA CUF, CCM PIA NI CHAMA CHA WAISLAM.

Kwahiyo wakati wa mkapa kilikuwa chama cha WAKRISTOOO!!!!
 
Si afadhali hata Chadema top 4 leaders are from different ethnic backgrounds,nooow hebu tucheki CCM top 4 leaders,3/4 ni wa dini moja.m/kiti muislam,katibu muislam,makamu m/kiti Zanzibar muislam,makamu bara ndiye mkristo tu.Lakini tukisema ile dini ya ufisadi nadhani 100% au 4/4 wote ni wa dini moja.Sasa hapa si ndio udini ata its best? kaazi kweli kweli

Wakati wa Mkapa je? au wakiwa waislamu tu inakuwa udini lakini wakiwa wakristo ni haki yao?! Na ufisadi ulianzia wakati huo. List: MKAPA, SUMAE, MANGULA, MALECHELA, JACKSON MSOME, MSEKWA. TAFAKARI kabla ya kusema. SIKU HIZI 'HATUDANGANYIKI'
 
Kuna mtu aliwahi kusema hapa kuwa kuna makubaliano ndani ya ccm kuwa na uwakilishi sawa wa dini kubwa nchini za uislam na ukristo. Matokeo ya uchaguzi dodoma yanaonyesha kuwa waislam sasa wana-nafasi asilimia 75 ya uongozi wa ccm.

Ilivyokuwa CUF na viongozi wengi waislam watu waliita cuf, chama cha waislam. Sijui kama ccm itaitwa the same name? Viongozi wakuu wanne, Kikwete, Karume, Msekwa, na Makamba; ratio inaonekana tayari. Kwa kamati kuu (cc), ratio ipo wazi, cha ajabu hata NEC, ni the same trend.

Haya ni makubaliano ndani ya ccm au ni mabadiliko ya yale makubaliano ya awali? Naomba kuwasilisha

Tumekuwa wepesi wa kusahau au kijisahaulisha au kujifanya hatuoni. Wakati wa Mkapa mbona safu yote 100% ya juuu ilikuwa ni Wakristo?! watu hawakusema au dini ni Uislamu tu labda tukubaliane hapo kwanza.
 
kweli kabis kuna mambo mengi sana ya kuanga sasa sio kuanza mambo ya kidini hapa kila mtu ana dini yake na aheshimu dini ya mwenzake sio masula ya kuitana mashetani na nguruwe sisi ni wote wa tz
BR
 
Hata mtoto mdogo ukimuuliza shetani ni nani atakujibu kwani kauli yako tu inaonyesha Ushetani wako na wote wenye mawazo kama yako.
Jamani ngoja nimtetee huyu mtu...yeye si shetani hata kidogo...tunapomwita shetani tunamnyima fursa ya kutoa maoni yake...he is entitled to his opinions...hivi ndivo anavoona yeye, njia ya kuondoa udini ni wakiriso wote wamchague mkiristo mwenzake popote alipo. hivi ndivo walivo wakiristo wengi wa nchi hii hata wale ambao hawasemi...

Historia inaonesha kuwa Nyerere akiwa mkiristo pekee alipewa fursa ya kushirikiana na waisilamu wengi sana...wao hawakutanguliza udini bali maslahi ya taifa ya kudai uhuru...lakini hawa wa sasa ukiristo kwanza halafu utaifa baadaye...huyu bila shaka anataka kiongozi atakayechaguliwa awe anawapendelea wakiristo wenziwe...

PUNDE TUTAWAJUA WANAMAPINDUZI WA KWELI NA WADINI
 
maisha ya kulalamika yamesababisha watu wengi wasifanye sehemu yao kwa ajili ya kuondoa umaskini.wengi tunapoteza muda kwa kuangalia mambo yasioleta maendeleo.
wakristu wengi hawapendi kugombea uongozi sasa unategemea inakuwaje? hata kama mfumo wa uongozi unaubinafsi sisi tuo tunaweza kubadilisha. muhimu tusiukubali udini katika mambo yasiyo na msingi. lakini tubaki na dini zetu tuzieshimu na tusizitumie vinginevyo. tuungane tuondoe umaskini bila kuangalia wangapi wako wengi.tusiwe wanafki wakristo tumekuwa kwenye uongozi kwa muda mrefu ni muda wetu wa kwenda atua nyingine huku wengine wakiingia kwenye utawala
 
dah!!ni vipi jamani mambo ya dini tena!!Tz sio nchi ya ubaguzi, tuachane na wendawazimu huu!!
bro/sis uliyeandika hii thread, nenda ka-regroup kidogo!! kwani wakiwa waislamu kuna nini kama wanatenda kazi sawa na jinsi wangevyotendo wakristo!mi mkristo ila hata sina muda wa kupoteza kufikiria udini kwenye jamii!!
 
Tumekuwa wepesi wa kusahau au kijisahaulisha au kujifanya hatuoni. Wakati wa Mkapa mbona safu yote 100% ya juuu ilikuwa ni Wakristo?! watu hawakusema au dini ni Uislamu tu labda tukubaliane hapo kwanza.

wakati wa mkapa pia ccm kilikuwa chama chenye waislam wengi kwenye safu yake ya juu ya uongozi - kamati kuu na halmashauri kuu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom