Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Hivi mlinzi akimkamata mwizi kuna haja ya kumpongeza?
mwalimu kamfunza mwanafunzi akafaulu yatupasa kumpongeza?
Mtu kwa kutimiza wajibu wake yafaa apongezwe?
haya maswali najiuliza.
mimi kwa fikra yangu ni kwamba ili mtu apongezwe ni lazima afanye jambo zaidi ya wajibu wake baada ya kutimiza wajibu huo kwa ufanishi kama ilivyopangwa. Hapo pongezi zinastahili.
Kwa JK bado hajafikia kupewa pongezi, maana hata kutimiza wajibu kwa ufanisi hajatimiza.
 
Hivi mlinzi akimkamata mwizi kuna haja ya kumpongeza?
mwalimu kamfunza mwanafunzi akafaulu yatupasa kumpongeza?
Mtu kwa kutimiza wajibu wake yafaa apongezwe?
haya maswali najiuliza.
mimi kwa fikra yangu ni kwamba ili mtu apongezwe ni lazima afanye jambo zaidi ya wajibu wake baada ya kutimiza wajibu huo kwa ufanishi kama ilivyopangwa. Hapo pongezi zinastahili.
Kwa JK bado hajafikia kupewa pongezi, maana hata kutimiza wajibu kwa ufanisi hajatimiza.

Watanzania matarajio yetu ni madogo mno, ndiyo maana baadhi yetu wanaona kuna haja ya kumpongeza JK pamoja na kuwa anatimiza wajibu wake wa kuomba Watanzania wamchague kama Rais kwa kipindi cha miaka mitano. Na kama walivyosema wengi bado JK ana safari ndefu sana ya kutimiza yale aliyotuahidi Watanzania wakati wa kampeni za 2005. Akiweza kuyafikia aliyotuahidi na labda kuyapita basi atastahili pongezi zetu, lakini kwa sasa mengi aliyotuahidi bado ni ndoto tu na miaka ndiyo inazidi kuyoyoma.
 
Pongezi zangu zitakuja pindi haya yakifanyika:-

1. Watuhumiwa WOTE wakifikishwa mbele ya sheria na sheria KUACHWA kuchukua mkondo wake (na si vinginevyo).

2. Wezi wetu wote (pamoja na hawa waliofikishwa Kisutu) wakitendewa sawa na walivyolitendea Taifa bila kujali ushkaji na kulindana. Yani ikiwezekana adhabu yao iwe ni kunyongwa (kumradhi kama nahukumu vibaya as I believe ndiyo adhabu nzuri kwao). Rostam, Karamagi, Mkapa, Lowassa na wenzao ambao wamekuwa wakitajwa na tena kuoneshwa kwa vithibitisho kadha wa kadha wakifanyiwa uchunguzi wa kina na watanzania wakafahamishwa kwa ukweli na uwazi ili heshima zao ziendelee kupanda na kama ni kushuka zifikie ZERO!

3. Katiba ya nchi itafanyiwa marekebisho na kipengele kinachoweza kuwa kinamlinda rais ama kiongozi yeyote fisadi kikaondolewa na wote waliotupeleka kusiko wakahukumiwa sawa na matendo yao.

4. Rais akikubaliana nasi kuwa taifa hili ni letu sote na kufikiria kuwa na baraza dogo la mawaziri lenye 'wazalendo' wa kweli na hata kuwa na kiongozi walau mmoja ama wawili toka vyama vya upinzani.

5. Rais akiweza kudhibiti mfumko wa bei na kuangalia uwezekano wa kutimiza "Maisha bora kwa kila mtanzania" kabla ya mwaka 2010.

Tofauti na haya matano (kwa uchache) nina imani kubwa kuwa 'uzembe' wowote unaoweza kutendeka na kupelekea viongozi ambao ni wazi watanzania HAWATAKI HATA KUSIKIA MAJINA YAO wakaonekana hawakuwa na hatia kwa upindishwaji wa namna yoyote iwayo wa sheria ama kulindwa basi kutatupeleka kusiko kabisa.

Ni mawazo yangu tu

Naungana na wewe na niko upande wako mkuu
 
Yaani mkipewa pipi tu!
mnasahau yote.
Ingekuwa ni mambo ya "malovelove" ningesema mmepewa "Rimbwata"

Jiulize haya
1.kafanya haya kwa hiari?
2.kwanini anabagua wahalifu(huyu akamatwe na huyu aachwe)
3.Ratio ya fedha zilizoibwa na za waliokamatwa ni sawa 100:0
Maana yake ni kwamba workdone ni zero.
 
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete,

Naomba nikubipu au niku page ili uje kuokoa mgonjwa Tanzania ambaye yuko taabani bin hoi.

Tayari tumeshampiga Eksirei, mashine za MRI, CTScan, EKG, Mkojo, Choo, damu, testi za chakula na aleji zimefanyika, tunakoumba utoe tiba baba ili mgonjwa apone.

Niko nyuma yako, niko tayari kukusaidia, safisha mikono, vaa scrubs, shika mkasi na kisu uanze upasuaji....
 
Mheshimiwa Mtukufu Rais Colonel Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.

Ingawa sikubaliani na mambo mengi yaliyojikita ndani ya chama chako katika kuongoza Taifa hili, ninakusapoti sana na nafurahishwa na wewe binafsi kwa jinsi ulivyoonyesha kuwa unaweza kuchukua hatua thabiti dhidi ya maovu ndani ya chama chako kwa manufaa ya taifa hili.

Mungu akusaidie uendelee na ujasiri huo wa kukabiliana na maovu hayo bila woga kwa faida ya nchi hii.


NB: Kuwa thabiti pia kwenye swala la Jumuia ya Afrika ya Mashariki tusipoteze identity yetu.
 
Ukichunguza, utagundu kansa ya Tanzania inaletwa na CCM!!

Najua kuna watakaoamka na kuanza kulalama aa Mchungaji mbona unakoromea CCM, lakini narudia nilichosdema siku nyingi kuwa ni CCM ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo.

Sasa namuomba Dr. Kikwete aanze kazi ya upasuaji. Mimi namuambia kuwa Mchungaji yuko nyuma yake kumsaidia.

Kwanza inabidi aanze kampeni ya kubadilisha Katiba ili ikidhi mahitaji ya Watanzania wote na hata kuondoa ule wigo na seng'enge ambayo imekuwa inatumika na CCM vibaya kulidumaza Taifa letu.

Pili inabidi azipe nguvu kisheria na kikatiba Bunge na Mahakama. Hii ni mihimili imara ambayo inabidi iwe na nguvu za kutosha bila kuogopa Serikali kuu.

Tatu, namuomba aanze kampeni mpya ya kulijenga Tiafa letu, liwe Taifa la watu waaminifu na wachapa kazi.

Nne, vita dhidi ya uhujumu si ya kurembeshewa macho au kuongozwa kwa upole. Inabidi Dr. Kikwete awe mkali sana!

Nitaendelea baadaye...
 
Jamani hapa mkuu wa kaya anastaili pongezi, mafisadi watapona kweli?





Baadhi ya pikipiki ambazo Rais Kikwete alikuwa azigawe jana
Zilitolewa na wafanyabiashara kwa CCM Arusha

Mussa Juma, Arusha


RAIS Jakaya Kikwete jana alikwepa kugawa pikipiki 19 zilizonunuliwa na wafanyabiashara na viongozi wa CCM wilaya ya Arusha kwa ajili ya watendaji wa chama hicho huku akiwataka wawe makini na misaada.


Kinyume na matarajio ya viongozi wa CCM Wilaya ya Arusha walioandaa hafla kubwa ya ugawaji wa pikipipiki hizo Kikwete aliwakatalia na kuwataka wazigawe wenyewe.


"Pikipiki ni zenu mnajua mlipozipata mimi nimezishuhudia…gawaneni wenyewe," alisema Rais Kikwete.


Hali hiyo ilijitokeza mara baada ya Rais Kikwete kufika katika ofisi za wilaya hiyo na kuonekana kubadilika sura na kutumia dakika tano tu katika hotuba yake na kuondoka.


Rais Kikwete mara kwa mara alikuwa akizungumza na Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mohamed Mbonde na Mwenyekiti wa mkoa, Onesmo ole Nangole ambao kwa mujibu wa ratiba hawakuwa wamepewa nafasi kuzungumza.


Baadaye baada ya majadiliano na meza kuu, ratiba hiyo ilibadilishwa na nafasi ya kumkaribisha Rais Kikwete ambayo awali ilikuwa ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha, Jubilate Kileo ilihamishiwa kwa Nangole


Katika hafla hiyo, wafanyabiashara mbalimbali wa mkoa wa Arusha walihudhuria akiwamo mmoja wa watuhumiwa wa wizi wa Fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA), (jina linahifadhiwa) ambaye alikuwa meza ya mbele, mkuu wa mkoa wa Arusha, Isdori Shirima na madiwani wa CCM.


Katika hotuba yake fupi, Kikwete aliwataka viongozi wa CCM kuwa makini na misaada ambayo wanapata kwa ajili ya chama chao.


"Ni kweli hatuwezi kujenga chama bila ya kuwa na rasilimali bora, lakini pia msitafute rasilimali zitakazowaletea matatizo," alisema Rais Kikwete bila ya kufafanua.


Alisema ameziona pikipiki hizo, lakini hatazigawa kwa kuwa hana muda kutokana na kuwahi uwanja wa ndege na akawaachia jukumu la kuzigawa viongozi wenyewe wa CCM wa Wilaya ya Arusha.


Rais Kikwete pia aliwataka wana CCM Wilaya ya Arusha kuanza kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa.


Mara baada ya maneno hayo, Rais Kikwete aliaga na kuondoka na kuwaacha wana CCM wakiwa wameduwaa.


Hata hivyo, katika hali ya kuonyesha kukerwa na alichokibaini Rais Kikwete, ilidaiwa baadaye kuwa aliwaita uwanja wa ndege Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha, Kileo na Katibu wake, Mohamed Nyawenga.


"Wameitwa uwanja wa ndege katibu na mwenyekiti hivyo sasa hatujui nani atagawa tena hizi pikipiki," alisema kiongozi mmoja wa CCM wilaya.


Kabla ya kuitwa uwanja wa ndege, Kileo alikuwa ameomba kukutana na wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya katika ofisi za chama jambo ambalo pia lilikwama.


Hadi saa 17:30 jioni hakuna kiongozi yoyote wa CCM ambaye alikubali kugawa pikipiki hizo na hivyo kuwaacha makatibu kata wa CCM waliotakiwa kuchukua pikipiki hizo wakihangaika kujichagulia kila mtu ya kwake.


Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Arusha, Semmy Kiondo ambaye alikuwa kiongozi pekee wa wilaya aliyebaki katika ofisi hiyo jana, alisema msemaji wa kilichotokea ni katibu wa wilaya.


"Mimi sio msemaji wa hili suala naomba uwasiliane na katibu wa wilaya ambaye kaondoka na mwenyekiti… na hizi pikipiki tutazigawa,"alisema Kiondo.


Awali, akisoma risala kwa Kikwete, Nyawenga alisema pikipiki hizo 19 zina thamani ya shilingi milioni 24.7 na zimetolewa ikiwa ni sehemu ya kuimarisha utendaji wa viongozi wa kata za CCM katika Wilaya ya Arusha.


Mara baada ya Rais Kikwete kuondoka watu walikusanyika katika makundi katika viwanja wa CCM na wengi walionekana kumpongeza Rais kwa kutojiingiza katika ugawaji wa pikipiki hizo.


"Rais wetu yupo makini hawezi kujiingiza katika hili suala lenye utata,"alisema

kiongozi mmoja.


Hata hivyo, wengi waliitafsiri hali hiyo na makundi ndani ya CCM Mkoa wa Arusha hasa yaliyotokana na uchaguzi mkuu ndani ya chama hicho mwaka jana, huku wengine wakisema ni sehemu ya juhudi za rais kupambana na vitendo vya ufisadi.


Tuma maoni kwa Mhariri






Contact Us DISCLAMER

Email:webmaster@mwananchi.co.tz © Mwananchi Communications Ltd 2006- 2009
 
Kama ze fisado alikuwepo meza kuu lazima astuke oohhh
 
Hongera ya nini kwenye hili!? 😕
 
wakuu naona hamkubali kwamba mkuu wa kaya kaanza kuwalia mingo mafisadi. Kukataa zawadi zao waziwazi ni dalili tosha kwamba Jakaya ametambua kwamba waliompigia kura wanataka afanye nini.
 
wakuu naona hamkubali kwamba mkuu wa kaya kaanza kuwalia mingo mafisadi. Kukataa zawadi zao waziwazi ni dalili tosha kwamba Jakaya ametambua kwamba waliompigia kura wanataka afanye nini.

Ningempa hongera kama angwasemea hovyo hovyo mafisadi na kutaka hizo zawadi zao zirudishwe badala ya kusema gawaneni wenyewe. Wenyewe ndiyo akina nani!? wakati yeye ndiye mwenyekiti wa CCM na alialikwa katika shughuli ile akakubali sasa kaona kuna fisadi meza kuu kaamua kukimbia!!!?
 
Kama mwenyekiti wa chama anapaswa kuchukua hatua badala ya kuzira.Kama atawaidhiria na jamaa wa EPA na Richmond kwamba wagawane wenyewe hali itakuwa mbaya sana.
 
double standards na zile million 40 za yule fisadi wa rada (Somaiya) alizozitoa kwa ajili ya kikao cha UV-CCM mbona hakuzikataa?
 
Ilibidi mtu akishachaguliwa raisi aachane na mambo ya siasa manake hapo hatujui kama alienda kwa maslahi ya kichama , serikali au ni vipi mambo yao ccm sisi hayatuhusu lazima tutenganishe
 
Tutajua kweli amejitoa mhanga kupambana na mafisadi pale atakapowapandisha kizimbani Lowassa ,karamagi, Msabaha na Rostam pamoja na Malegesi ; hizi nyingine ni fix zake tu.Yule jamaa wa EPA asingekuwa meza kuu muungwana angezigawa hizo pikipiki!!
 
Alisema ameziona pikipiki hizo, lakini hatazigawa kwa kuwa hana muda kutokana na kuwahi uwanja wa ndege na akawaachia jukumu la kuzigawa viongozi wenyewe wa CCM wa Wilaya ya Arusha.

Tatizo hapa ni muda tu na unaona amefanya delegation ya hilo jukumu, kama angekuwa amekerwa na lolote kwanini hakuliweka wazi hadharani kwenye hiyo hotuba yake fupi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom