Mzee ES.. madai ya Ukabila chadema kwa sababu ya namba hayakutuka kwa wangwe tu, yamewahi kutolewa huko nyuma na makada wa CCM. NI madai tu yanayoangalia namba. Binafsi siamini kuwa kuna Udini CCM kama vile nisivyoamini kuna Ukabila kwenye Chadema. Nikisikia mtu anasema kuna udini/ukabila mahali naraise standard of evidence very high.
Haiwezekani mtu aje na kusema kuwapo watu sita kwenye uongozi wa chama fulani ambao kwa na moja au nyingine wana husiana na mkoa mmoja basi ni ukabila. Katika kesi ya Chadema kwanini iwe ni ukabila na isiwe jambo jingine? Kilichotokea ni kuwa wanaangalia namba, na bahati mbaya namba hiyo inawahusisha wachagga.
Narudia tena nilichosema mwanzoni, madai ya Ukabila dhidi ya wachagga hayakuanzishwa leo. Tangu mara tu baada ya Uhuru madai ya ukabila wa Wachagga, Wanyakyusa na Wahaya yamekuwa yakitolewa. Mwalimu akalazimika kuunda tume ya Mang'enya. Na wakati anaangalia "Vitu vinavyotupasa kurekebisha" Mwalimu akarudi na kulifafanua hilo la ukabila wa namba. Akaelezea kwanini at the time kwenye civil service kuna watu wengi wa makabila hayo, na akawapa changamoto wanaodai Ukabila waangalia katika political positions waone kuna wahaya, wachagga, na wanyakyusa wangapi.
Lakini hilo halijakoma. Leo hii kuna watu ambao wanaamini kabisa kuwa Wachagga wana ukabila, wanashangaa jinsi wanavyosaidiana kibiashara au kuendeleza mambo ya familia. Wanashangaa wachagga walivyosambaa katika biashara sehemu mbalimbali za nchi na hata Afrika yetu. NIliwahi kwenda pale Karonga Malawi, miaka ya themanini kuna wachagga hapo utadhani moshi mjini! Binafsi nadhani kuna kitu kingine kinachowasukuma watu hawa wanaouona Ukabila wa wachagga. Sitakitaja kwa sasa kwani mtu yeyote mwenye kufikiria anaweza kukibunia na kupatia.
Angalieni kwenye vyuo vyetu vikuu, kuna wachagga wangapi, wahaya wangapi na wanyakyusa wangapi. Nenda hata nje ya nchi uone kuna maprofesa wangapi kutoka makabila hayo? Mtu anayeangalia namba tu bila kujaribu kuangalia historical reasons atapiga kelele Tanzania ina ukabila.
Suala la Chacha ni jambo muhimu sana nalo linahusu utaratibu. Utaratibu uliotumika kuwapata wabunge wa viti maalum ndani ya chama hicho haukuwa mzuri na ulionekana kuwa na upendeleleo au ulifungua mwanya wa watu kadhaa kupata nafasi hizo. Hoja hiyo imewahi kupelekwa na kuangaliwa. Je Chadema walihalalisha utaratibu uliotumika, je walifafanua walipataje wabunge hao sita?
Tumeona jinsi CCM inavyofanya uchaguzi wa wabunge wake wa viti maalumu. Kuna mfumo mzuri tu kiasi kwamba Mbunge wa kiti chochote maalum akiacha nafasi hiyo inajulikana wazi nani yuko kwenye "line" kumrithi. Je vyama vya upinzani ikiwamo Chadema wana utaratibu huo? Je walikuwa na utaratibu huo? So far kabla ya 2005 hawakuwa na utaratibu unaoeleweka. Hilo ndilo kosa kubwa zaidi ambalo watu ndani ya chama chochote wanapogundua matatizo yake wanalirekebisha.
Baada ya Uchaguzi wa 2005 na walipokaa kuangalia Katiba upya katika kile ambacho kilikuwa ni kama kukijenga chama upya, wakaamua kubadili Katiba na kuhakikisha kuwa utaratibu wa wabunge wa viti maalumu unaeleweka. Sijui ni kwa kiasi gani wamefanikiwa. Sasa hivi, Chadema wangeweza kujibu hoja za Wangwe kiurahisi tu bila kufikishana hapa:
"tumezisikiliza hoja za mhe. Wangwe na wajumbe wengine, tumetambua kuwa utaratibu uliotumika katika kuwapata wabunge wa viti maalumu haukuwa mzuri, wa wazi, na unaozingatia maslahi ya chama katika Taifa. Kimsingi hatukuwa na utaratibu uliowekwa wazi na unaofaa. Hili bila ya shaka limesababisha manung'uniko kwa watu (blah blah blah)
Kwa hiyo kwa kuzingatia mambo hayo Kamati Kuu ya Chadema inaomba radhi wanachama wake kwa kusababisha mtazamo huo na kuwafanya wahisi mambo ya kikabila ndani ya chama. Chadema haiwezi kuvumilia, kukaribisha au kufumbia macho madai ya ukabila kwani ni sumu isiyokoma.
Hivyo basi Mkutano Mkuu umefanya mabadiliko ya Katiba ili kuweka utaratibu wa kupata wabunge wa viti maalumu. Utaratibu huo utakuwa hivi na vile kuanzia uchaguzi ujao.
Tunamshukuru Bw. Wangwe na wanachama wengine kwa kulileta jambo hili mwangani katika kukikosoa chama na kusahihishana. Tusonge mbele. Asanteni"
Makofi .. na bao halali linakuwa limefungwa...
Na mambo mengine yangeweza kutatuliwa kiurahisi, lakini wao wanataka kushindana nani anaweza kumtuhumu mwingine zaidi!