Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
MKAMATENI IDDI SIMBA KWANZA ALIYESHIRIKI KUKWAPUA PESA ZA EPA!
WAPI LUKAZA NA MALEGESI? NYIE ccm MNATUONA WATOTO?
NA CHADEMA JIBUNI HILI NIWAPE MAMBO!
YEYOTE ATAKAYEENDELEA KUWALISHA WANANCHI HUU UPUUZI..KAMA NI ccm NITAENDELEA KUTAJA NA WENGINEO...NASEMA NYIE MAFISADI ccm NATAKA MNIELEZE...HIZI NI MBINU ZA UCHAWI WENU ULIOSHINDWA HUKO BUNGENI!
NYIE CHADEMA PIA MNA MATATTIZO...WOTE HAPA NI KAMA MAFISI YANAYOGOMBEA MALI ZA WATANZANIA NA WAKATI HAKUNA ALIYEJIBU MASHTAKA YA KULIUZA TAIFA LETU!
KAMATENI MKAPA MARA MOJA!
 
Na Kama Kuna Wabunge Hapa...rudini Huko Bungeni Mkadai Ripoti Za Epa Na Madini..kuanzia Sasa Naaanda Majina Yote Ya Wale Waliohusika Na Wakati Mkiendelea Na Mambo Yenu Ya Dini Na Ukabila...na Mimi Nadondosha Majina Ya Dini Na Kabila La Ufisadi
MPO?
 
ISSUE SI ccm na chadema...ISSUES NI RIPOTI ZA MADINI,EPA NA WAHUSIKA WA MEREMETA NA KIWIRA KUKAMATWA MARA MOJA! WE ARE TIRED OF POLITICS NA HUU UCHAFU! WE NOW WANT FREEDOM...!AND WE MEAN IT! WE ARE DECISIVE AND WE SHALL NEVER WAVER!
WE WILL STAY STRONG....AND WE SHALL BE THE VICTORS...GOD WILLING...WE SHALL OVERCOME!
NB:chadema na ccm wote mmeguswa na UFISADI na wote ni mamluki wao!ACHENI HIZI PARAPANDA HAPA KWANI NI DHAMBI HATA KWA MUNGU KUMYIMA MNYONGE HAKI YAKE!
 
Wamiliki Wote Wa Bank M Ya Ocean Road Wakamatwe Mara Moja Tukianzia Na Mmiliki Wa Bora Apts...wote Hao Ni Wanachama Waaminifu Wa Chama Cha Mafisadi.
 
MJJ aanalyse uchaguzi au uteuzi wao, asitujie tu na statement za ki-pr - school kwa vile eti 65% ni wa dini moja wakati huo huo, dini ziko karibu 50% - 50% kwenye population ya TZ bara na 98% dini moja in ZNZ. Alikuwa wapi kwenye analysis ya ukabila ndani ya CHADEMA ambao ni obvious?

MJJ aliposema kuhusu dini nilistuka kwanza lakini baada ya kusoma hayo majina sioni cha ajabu kabisa, kwanza upande wa bara waislamu ni walewale wa siku zote, na huko ZNZ alitaka nani awe kama sio hao ni kweli kabisa ZNZ more than 98% ni waislam ni ngumu kupata wahusika sawa katika dini2. Tujadili utendaji wao na si swala la udini jamanikwani kama ni swala la dini basi CUF na CHADEMA wanaongoza adui mchukie sifa yake mpe
 
Na Kama Kuna Wabunge Hapa...rudini Huko Bungeni Mkadai Ripoti Za Epa Na Madini..kuanzia Sasa Naaanda Majina Yote Ya Wale Waliohusika Na Wakati Mkiendelea Na Mambo Yenu Ya Dini Na Ukabila...na Mimi Nadondosha Majina Ya Dini Na Kabila La Ufisadi
MPO?

Safiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii tunausbiri hili ndio la maana dini mambo gani, watu wako busy na UFISADI saangapi ataswali au kwenda kanisani
 
Halafu jambo jingine la kusikitisha kuhusu hawa watu wenye maslahi yao ya vyama...ccm na chadema wanachama wake wote wakijumlishwa pamoja hawafikii hata nusu ya wananchi wa TANZANIA AMBAO NI ZAIDI YA MILIONI 30 SASA!
Hivyo kupigania maslahi ya chama na kuyaacha yale ya watanzania ambayo ni uwajibishwaji kwa mafisadi ni DHAMBI KUBWA SANA TU!
Mkifanya hivyo mtapewa lawama!Watanzania tumeshajifunza sana na KAMWE HATUTARUDIA MAKOSA!
Tunataka pia muwape consideration wananchi ambao hawana vyama ambao ni wengi kuliko hata hao wenye vyama(ccm+chadema- MAFISADI!)=UHURU!
 
Kamati KUu ya CCM haijajaa UDINI labda useme imejaa waislam

UDINI
Udini ni khali ambyo inatokea kwa watu kuanza kubaguana na mwingine kwa kutumia Dini kwa lengo na madhumuni flani.Suala la Wananchama wa CCCM kuchagua Viongozi wao kwa kuangalia uwezo wao tu ni jukumu lao la msingi na ikumbukwe kuwa kamati kuu ya CCM inatoka pande mbali mbali ya Tanzania ni si rahisi kumwambia au kupanga kila mkoa uchague Mwislam.Hii imetokea tu na wala siyo kwamba RAis alipanga kuchagua waislam.Kwa hoja hii hakuna UDINI katika kamati kuu ya CCM na Mzee Mwanakijiji naomba uhitimishe hili.na wajumbe wa CCM ni wa KUCHAGULIWA.

UKABILA
Ukabila ni Tabia ya watu kutumia Kigezo ya ukabila kupeana madaraka kwa kufuata imani yao waliyo nayo ya UDINI,Udini ni Imani kabisa ya kuamini kwamba bila mtu mwenye kabila letu mambo hayataenda.Suala la Wangwe kusema kuna Ukabila CHADEMA ni suala amblo ni la kweli,Iweje Wabunge wote wa kuteuliwa wawe wachaga au wanatoka kadna ya Kaskazini.Kumbuka hawa ni KUTEULIWA.

Dhana ya KUTEULIWA na KUCHAGULIWA
Kuchagua mtu anaweza kuchaguliwa kwa kuangalia uwezo wake au pi akutokana na mambo ambayo yanaweza kuamuliwa na jamii aliyopo ,na inawezekana kwa ukabila,dini na jambo lingine ambalo litaamuliwa na wapiga kula hao na sehemu wanyotoka.Kuteuliwa huwa kunafanywa na mtu mmoja au wengi ili wanangalia Vigezo vilivyopo na mazingira waliyopo,Mfano CHADEMA waliangalia Vigezo vya ukabila na ukaribu wao na wateuliwa ila kuweza kurahisisha utendaji wao wa kazi,na hii inawezekana ilichangiwa na wazazi wao au wakwe zao kuchangia kiasi flani cha Pesa katika Kampeni,ambalo ni kweli na halina chembe ya ubishi.

HITIMISHO
Tusitumie Wangwe Doctrine kuhalalisha mambo ambayo hayana ukweli,Ukishindwa kwa hoja uslite vioja,ona tayari mlishaanza kuleta Vioja.Mpaka Kieleweke jenga hoja Nzuri ili kuweza kuweka uzito katika nia yenu.Kuanza kuonge ambao ambayo hamkuyaweka katika Ripoti yenu kwa umma hapa kwa kumpataka MAtope Wangwe Mnakosea

Gembe... kama ukabila ni idadi ya watu wa kabila moja au eneo moja kwenye nafasi fulani basi udini ni idadi ya watu wa dini moja mahali pamoja bila kujali maelezo yoyote yale. Hii ndiyo Wangwe Doctrine. Ingawa watu wako sensitive na udini watu hao hao hawaoni usensitive wowote kwenye madai ya ukabila. Kwangu vyote viwili ni sumu kali.

Je tunataka "Wangwe" atokee CCM na kusema kuna udini ndio tuangalie kama kuna dalili yoyote ya udini? Kwanini kati ya watu 6 tu halalishe Ukabila mkubwa lakini watu 28 tusione udini? Unless of course tuko biased kwa namna fulani na makabila?

Kipimi tunachopimia Chadema, ni kile kile kinachopimiwa CCM...
 
Jamani eeh!

Ukabila na UDINI NI BAADA YA RIPOTI KUSOMWA NA BUNGE!

KWASABABU MSIMAMO WA WATANZANIA NI HUU...

KAMA RIPOTI ZIKISOMWA NA KUGUNDULIKA KUWA HAO WAISLAM WALIO WENGI HUKO ccm HAWAKUHUSIKA NA UFISADI...THEN HAKUNA HAJA YA UDINI...

NA KAMA TUKIKUTA SI KABILA FLANI PEKEE,PIA TUSIFANYE UKABILA!

HIVI NA MIMI NIKIANZISHA THREAD NA KUSEMA WASUKUMA WOTE NI MAFISADI KWASABABU YA CHENGE MTAKUBALI?

VIPI KUHUSU MKAPA? HATUWEZI KULAUMU WATU FLANI FLANI KWA MAMBO YAO NA KU GENERALIZE!

KUNA chadema wasafi na wachafu,na pia kuna ccm wasafi na wachafu...

Kuna Waislam wasafi na wachafu..Kuna wakristo wasafi na wachafu na kuna wachaga wasafi na wachafu..The list goes on and on...! DHAMBI YA UFISADI HAIANGALII DINI,CHAMA,KABILA WALA RANGI...NI DHAMBI NA WASHIRIKA WAKE NI WASHIRIKA WA USHETANI NA UFEDHULI DHIDI YA MWANANDAMU!

RIPOTI ZETU NDIZO ZITAKAZOWAANIKA WOTE HAO!HAPA NINAOUNA KUNA MPANGO MAALUM KAMA ULE WA NCCR MAGEUZI!

UZURI MMOJA SASA TUNA JF NA KILA ISSUE INAPITA HAPA!

THEREFORE..HATUTAKUBALI THIS TIME!
 
Gembe... kama ukabila ni idadi ya watu wa kabila moja au eneo moja kwenye nafasi fulani basi udini ni idadi ya watu wa dini moja mahali pamoja bila kujali maelezo yoyote yale. Hii ndiyo Wangwe Doctrine. Ingawa watu wako sensitive na udini watu hao hao hawaoni usensitive wowote kwenye madai ya ukabila. Kwangu vyote viwili ni sumu kali.

Je tunataka "Wangwe" atokee CCM na kusema kuna udini ndio tuangalie kama kuna dalili yoyote ya udini? Kwanini kati ya watu 6 tu halalishe Ukabila mkubwa lakini watu 28 tusione udini? Unless of course tuko biased kwa namna fulani na makabila?

Kipimi tunachopimia Chadema, ni kile kile kinachopimiwa CCM...
Niliomba wakakuamshe,Naona umeshaaamka

Mzee Mwanakijiji,
Hoja si kwamba wangwe aje atokee CCM ili tuone kuna Udini,La hasah hoja ni kwamba Kamati kuu kuna Udini?Rejea wajumbe wa kamati kuu wanapatikana vipi?Je unadhani woete kuwa waislam ua wakistro huwa inapangwa na wajumbe wanaowapigia kura?Si kweli hii imetokea tu


Suala la CHADEMA kuchagua hao 6 lilipangwa na Viongozi wa juu wenye Maslahi yao Binafsi na hili.Na ndiyo hoja ya wangwe inapoonekana ina ukweli ndani yake na siyo maneno ambayo yanatolewa na Mpaka kieleweke kwamba alikutana na Rostama Pale Kempski.Je CHADEMA inakataza wanachama wake kuwasiliana na Mtu au kada wa chama Kingine?Mbona mie huw anakutana sana na Zitto(japo hajui mie ni member wa JF) na kuzungumza naye sana tu na watu wa chama changu wananiona ?au kwasabau mie siyo kiongozi mkubwa wa chama ila ni kiongozi wa kawaida??
 
Udini+Ukabila..... umeibuliwa "kufunika kombe" mwanaharamu apite..... Hapa moto mbele. Hakuna cha ukabila Chadema wala udini CCM na CUF.... Hoja hapa ni WEZI WA EPA wakamatwe, wezi wa MEREMETA wakamatwe. Mkapa na genge lake la kina Mramba, Chenge, Yona, wafikishwe mahakamani haraka iwezekanavyo. Wangwe tunajua toka mwanzo. Alipewa kazi ya kuzima soo la Buzwagi, akakuta haikua ajena ya Chadema na Zitto, ilikua ajenda ya WATANZANIA na sasa namwambia WANGWE na waliomtuma ajenda ya UFISADI si ajenda ya CHADEMA na Dk. Slaa ni ajenda ya Watanzania na kama ulimsikiliza Mzee J.S. Malecela, kwa makini alikua akiipigia mstari japo hakutaka kusema wazi, lakini kwa kusema kwake kwamba EPA ilianzishwa na Chegeni, angeweza kusema kwamba Buzwagi ilianzishwa na Lembeli, lakini CCM wenzake wakampuuza akaja Zitto akawasha moto. Sasa hapa si CCM wala Chadema watakaozima moto wa kuwabana mafisadi. NI HOJA YA UMMA.
 
Conclusion ni kwamba

Wapinzani wengi wa Tanzania njaa zinawasumbua.Leo ukimfuata Mbowe ukamuuliza ni kwanini anadhani yeye anafaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA hawezi kukupa jibu la kulidhisha.Hili ni tatizo la Viongozi wetu tulionano

Sijui wanasubiri nini kukubali ndivyo walivyo?
 
Watu hapa wanajaribu kuspin tuu lakini ukweli unajulikana . Kama tunataka kutumia standard tulizotumia Chadema basi standard hizo hizo zitumike CCM pia. Huu ni ujinga wa hali ya juu, Mimi naipinga hoja ya kusema watu wanapewa vyeo Chadema kutokana na kuwa ni wachaga , kwanza nataka mniambie tunazungumza Wachaga wa sehemu gani ? Kwani kwa kusema Wachaga tuu aitoshi ni too vague jamani .

Mkuu Rufiji,

Heshima mbele, sisi JF we have nothing to do na hizi kauli za ukabila huko Chadema, hayo ni maneno ya Wangwe, sisi tunajadili tu hapa ya kutoka huko ndani ya Chadema, sasa tusiingizwe kwenye mijadala ambayo sisi sio chanzo chake.

CCM tuna matatizo ya ufisadi na baadhi ya viongozi wabovu, lakini one thing hatuna ni matatizo ya ukabila na udini, sasa iweje hapa JF tuweze kuchambua ishus za ufisadi wa CCM zinazoibuliwa na viongozi wa CCM bila tatizo, lakini wananchi wakijaribu kujadili ishu ya ukabila iliyoibuliwa na Makamu wa Mwenyekiti wa Chadema iwe tatizo?

Nyinyi Chadema acheni hizi siasa za ubabe, sisi CCM tumekubali kuwa tuna matatizo ya ufisadi na tnyafanyia kazi, hatukuwalaumu Chadema kuwa ndio mnaoleta matatizo yetu, wakuu huko Chadema tatueni matatizo yenu yaliyoibiliwa na makamu wa mwenyekiti wenu Wangwe, lakini msitafute mchawi hapa na hizi nyepesi nyepesi!
 
The Citizen (Dar es Salaam) 3 July 2008 Posted to the web 3 July 2008

Joas Kaijage

Kagera Region members of the Chadema national governing council have challenged the recent suspension of party vice-chairman Chacha Wangwe which was approved by the party's national executive committee. The members, who vowed to vote against the decision during the forthcoming meeting of the council, said the suspension of Mr Wangwe was a result of deep-rooted problems among the party's top brass which should first get cleared instead of "victimising the critics within the leadership".

A governing council member who requested for anonymity said the suspension of Mr Wangwe was a result of machinations of some individuals "who were not ready to see any of the party's national leadership positions held by members hailing from regions other northern part of the country".

He said such ideologies were the very reasons behind the defection of the party's former vice-chairman, Dr Walid Amani Kaborou, who shifted to CCM, paving the way for Mr Wangwe to replace him.
 
Mzee ES.. madai ya Ukabila chadema kwa sababu ya namba hayakutuka kwa wangwe tu, yamewahi kutolewa huko nyuma na makada wa CCM. NI madai tu yanayoangalia namba. Binafsi siamini kuwa kuna Udini CCM kama vile nisivyoamini kuna Ukabila kwenye Chadema. Nikisikia mtu anasema kuna udini/ukabila mahali naraise standard of evidence very high.

Haiwezekani mtu aje na kusema kuwapo watu sita kwenye uongozi wa chama fulani ambao kwa na moja au nyingine wana husiana na mkoa mmoja basi ni ukabila. Katika kesi ya Chadema kwanini iwe ni ukabila na isiwe jambo jingine? Kilichotokea ni kuwa wanaangalia namba, na bahati mbaya namba hiyo inawahusisha wachagga.

Narudia tena nilichosema mwanzoni, madai ya Ukabila dhidi ya wachagga hayakuanzishwa leo. Tangu mara tu baada ya Uhuru madai ya ukabila wa Wachagga, Wanyakyusa na Wahaya yamekuwa yakitolewa. Mwalimu akalazimika kuunda tume ya Mang'enya. Na wakati anaangalia "Vitu vinavyotupasa kurekebisha" Mwalimu akarudi na kulifafanua hilo la ukabila wa namba. Akaelezea kwanini at the time kwenye civil service kuna watu wengi wa makabila hayo, na akawapa changamoto wanaodai Ukabila waangalia katika political positions waone kuna wahaya, wachagga, na wanyakyusa wangapi.

Lakini hilo halijakoma. Leo hii kuna watu ambao wanaamini kabisa kuwa Wachagga wana ukabila, wanashangaa jinsi wanavyosaidiana kibiashara au kuendeleza mambo ya familia. Wanashangaa wachagga walivyosambaa katika biashara sehemu mbalimbali za nchi na hata Afrika yetu. NIliwahi kwenda pale Karonga Malawi, miaka ya themanini kuna wachagga hapo utadhani moshi mjini! Binafsi nadhani kuna kitu kingine kinachowasukuma watu hawa wanaouona Ukabila wa wachagga. Sitakitaja kwa sasa kwani mtu yeyote mwenye kufikiria anaweza kukibunia na kupatia.

Angalieni kwenye vyuo vyetu vikuu, kuna wachagga wangapi, wahaya wangapi na wanyakyusa wangapi. Nenda hata nje ya nchi uone kuna maprofesa wangapi kutoka makabila hayo? Mtu anayeangalia namba tu bila kujaribu kuangalia historical reasons atapiga kelele Tanzania ina ukabila.

Suala la Chacha ni jambo muhimu sana nalo linahusu utaratibu. Utaratibu uliotumika kuwapata wabunge wa viti maalum ndani ya chama hicho haukuwa mzuri na ulionekana kuwa na upendeleleo au ulifungua mwanya wa watu kadhaa kupata nafasi hizo. Hoja hiyo imewahi kupelekwa na kuangaliwa. Je Chadema walihalalisha utaratibu uliotumika, je walifafanua walipataje wabunge hao sita?

Tumeona jinsi CCM inavyofanya uchaguzi wa wabunge wake wa viti maalumu. Kuna mfumo mzuri tu kiasi kwamba Mbunge wa kiti chochote maalum akiacha nafasi hiyo inajulikana wazi nani yuko kwenye "line" kumrithi. Je vyama vya upinzani ikiwamo Chadema wana utaratibu huo? Je walikuwa na utaratibu huo? So far kabla ya 2005 hawakuwa na utaratibu unaoeleweka. Hilo ndilo kosa kubwa zaidi ambalo watu ndani ya chama chochote wanapogundua matatizo yake wanalirekebisha.

Baada ya Uchaguzi wa 2005 na walipokaa kuangalia Katiba upya katika kile ambacho kilikuwa ni kama kukijenga chama upya, wakaamua kubadili Katiba na kuhakikisha kuwa utaratibu wa wabunge wa viti maalumu unaeleweka. Sijui ni kwa kiasi gani wamefanikiwa. Sasa hivi, Chadema wangeweza kujibu hoja za Wangwe kiurahisi tu bila kufikishana hapa:

"tumezisikiliza hoja za mhe. Wangwe na wajumbe wengine, tumetambua kuwa utaratibu uliotumika katika kuwapata wabunge wa viti maalumu haukuwa mzuri, wa wazi, na unaozingatia maslahi ya chama katika Taifa. Kimsingi hatukuwa na utaratibu uliowekwa wazi na unaofaa. Hili bila ya shaka limesababisha manung'uniko kwa watu (blah blah blah)

Kwa hiyo kwa kuzingatia mambo hayo Kamati Kuu ya Chadema inaomba radhi wanachama wake kwa kusababisha mtazamo huo na kuwafanya wahisi mambo ya kikabila ndani ya chama. Chadema haiwezi kuvumilia, kukaribisha au kufumbia macho madai ya ukabila kwani ni sumu isiyokoma.

Hivyo basi Mkutano Mkuu umefanya mabadiliko ya Katiba ili kuweka utaratibu wa kupata wabunge wa viti maalumu. Utaratibu huo utakuwa hivi na vile kuanzia uchaguzi ujao.

Tunamshukuru Bw. Wangwe na wanachama wengine kwa kulileta jambo hili mwangani katika kukikosoa chama na kusahihishana. Tusonge mbele. Asanteni"
Makofi .. na bao halali linakuwa limefungwa...

Na mambo mengine yangeweza kutatuliwa kiurahisi, lakini wao wanataka kushindana nani anaweza kumtuhumu mwingine zaidi!
 
CCM ni chama cha kiislam na huu ni ukweli usiopingika.

Udini uachwe ccm maana utaigawa nchi.
 
Hii ni nafasi nyingine kwa Mwenyekiti wa ccm kuweka usawa kwenye chama kinachoongoza nchi yetu. Suala la kuwa na viongozi wengi wa kamati kuu ya ccm ambao ni kutoka dini moja linaleta picha ambayo haionyeshi usawa wa dini mbili kubwa Tanzania za Ukristo na Uislam.

Huu ni ushauri tu, ni muhimu sana kwa Kikwete kushawishi wanaccm kuwa na katiba ambayo itaweka usawa wa kidini kwenye chama tawala.

Majina haya yanaonyesha kile kinachoendelea CCM:

1. Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete - Mwenyekiti - Muslim
2. Ndugu Pius Msekwa - Makamu Mwenyekiti (Bara) -
3. Ndugu Amani Abeid Amani Karume - Makamu Mwenyekiti(Zanzibar) - Muslim
4. Ndugu Yussuf R. Makamba - Katibu Mkuu - Muslim
5. Capt. (mst) George Huruma Mkuchika - Naibu Katibu Mkuu (Bara)
6. Ndugu Salehe Ramadhan Ferouz - Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)- Muslim
7. Dr. Ali Mohamed Shein - Mjumbe - Muslim
8. Ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda - Mjumbe
9. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe - Muslim
10. Alhaj Ali Hassan Mwinyi - Mjumbe - Muslim
11. Ndugu Benjamin William Mkapa - Mjumbe
12. Mzee Rashid Mfaume Kawawa - Mjumbe - Muslim
13. Dr. Salmin Amour - Mjumbe - Muslim
14. Ndugu John Samwel Malecela - Mjumbe
15. Capt. (mst) John Zefania Chiligati - Mjumbe
16. Ndugu Amos Gabriel Makala - Mjumbe
17. Ndugu Bernard Kamilius Membe - Mjumbe
18. Ndugu Kidawa Hamid Saleh - Mjumbe - Muslim
19. Ndugu Samwel John Sitta - Mjumbe
20. Ndugu Pandu Ameir Kificho - Mjumbe - Muslim
21. Ndugu Anna Abdallah - Mjumbe
22. Ndugu Rostum Aziz - Mjumbe - Muslim
23. Dr. Mohamed Gharib Bilal - Mjumbe - Muslim
24. Ndugu Pindi Hazara Chana - Mjumbe
25. Ndugu Andrew Chenge - Mjumbe
26. Dr. Maua Abeid Daftari - Mjumbe - Muslim
27. Ndugu Samia Suluhu Hassan - Mjumbe - Muslim
28. Ndugu Mohamed Seif Khatib - Mjumbe - Muslim
29. Ndugu Haji Omar Kheri - Mjumbe - Muslim
30. Dr. Abdallah Omari Kigoda - Mjumbe - Muslim
31. Ndugu Abdurahman Kinana - Mjumbe - Muslim
32. Ndugu Anne Semamba Makinda - Mjumbe -
33. Ndugu Fatuma Said Ali Mchumo - Mjumbe - Muslim
34. Ndugu Zakia Hamdan Meghji - Mjumbe - Muslim
35. Ndugu Omar Yussuf Mzee - Mjumbe - Muslim
36. Ndugu Emmanuel John Nchimbi - Mjumbe
37. Ndugu Ali Ameir Mohamed - Mjumbe - Muslim
38. Ndugu Yussuf Moh'd Yussuf - Mjumbe - Muslim
 
Mkuu MMJ,

Ni kweli kabisa kuhusu maneno yako, lakini at this point and time anayeliibua hili ishu la ukabila na mengineyo huko Chadema, ni huu utata wa makamu wa Chadema na sio CCM,

Tunachosema ni kwamba Chadema, ishughulikie hilo sasa kuliko kuja hapa na kujaribu kila njia mpaka zisizokuwa na heshima kwa taifa na sisi wananchi katika kujisafisha, wabunge sita wa chama kmoja cha siasa kama cha Chadema kutoka mkoa mmoja ni a valid political concern, ambayo ikiwa raised na makamu wa chama cha Chadema, dawa yake sio kuja JF na kujaribu kujisafisha dawa ni kujisafisha huko ndani kwanza,

JF tuna haki zote za kujadili any ishu inayoletwa hapa kwa sababu ndio hasa kazi yetu muhimu na kubwa kuliko zote, lakini kisiasa kujaribu ku-inject mjadala wa udini ndani ya CCM, kwa sababu hapa kuna tatizo la makamu wa mwenyekiti wa huko Chadema mwenye tatizo na ukabila ndani ya chama chake sio dawa ya kujibu hili tatizo huko Chadema,

Viongozi wa Chadema tumewaambia toka mwanzo kuwa hili tatizo mmelikosea sana toka mwanzo, na so far toka tuseme ninaona movemment nyingi sana hapa lakini please wakuu sisi ni watu wazima jaribuni kutu-treat with a respect angalau kidogo, naona maneno mengi sana tunahitaji matendo, malalamiko ya Wangwe yasemwe kama ni valid au sio, siamini kwamba Wangwe ni best kuwa makamu wa mwenyekiti huko, lakini kama ni chaguo la wananchi liheshimiwe, kama ana makosa aadhibiwe na tarehe ya mwisho wa adhabu yake isemwe wazi kusiwe na speculations!

Ahsante Mkuu
 
Soma yaliyoandikwa hapa kijana, halafu uendelee na mjadala.

Mkuu Mwanakijiji,

Maoni yako yamenipeleka mbali sana. Umenikumbusha enzi za TANU ilipoanza.
Waasisi wa TAA na baadae TANU walikuwa na idadi kubwa sana ya Waislamu. Hili halikuwa jambo la kushangaza kwa kuwa harakati hizi zilianzia Dar-Es-Salaam ambako wengi wa wakazi wake ni Waislamu. Kwa hiyo hata idadi ya wafuasi pia walikuwa wengi ni Waislamu.

Uhuru ulipokaribia, nafasi muhimu za uongozi ghafla zikaanza kuchukuliwa na waliokuwa Wakristo. Mmoja wa wazee waasisi Sheikh Suleiman Takadiri, katika mkutano wao pale ofisi za makao makuu ya TANU mtaa wa Lumumba, akamuuliza Mwalimu Julius Nyerere, imekuaje mbona ghafla hivi tunaona idadi ya Wakristo katika viti nyeti inazidi ya Waislamu na sisi ndio tuko wengi zaidi?

Mwalimu akamgeuzia kibao kwa kumwambia, wewe mdini sana. Umejuaje kuwa idadi ya Wakristo katika viti muhimu vya uongozi iko juu zaidi kuliko ile ya Waislamu. Bila shaka huo udini wako ndio uliokuacha wewe unahesabu watu na dini zao wakati sisi tunashughulikia harakati za kupata uhuru.


Mzee Mwanakijiji, ukianza kuhesabu watu kwa makundi hutaweza kujiridhisha wala kumridhisha mwingine. Wewe unahesabu uwiano wa watu kwa dini zao. Mimi labda nitaanza kuhesabu watu kwa umri wao. Na mwingine ataanza kuhesabu watu kwa jinsia zao. Labda kuna na mwenzetu mwingine ataanza kuhesabu watu kwa rangi na nywele zao. Kweli tutafika?

Kama chama kina watu wengi wa kabila moja au wa mkoa mmoja thautawatendea haki kama tutawazuia wengine wa kabila hilo au mkoa huo kuingia chama hicho kwa kuwa kina wanachama wengi wa kabila hilo au wa mkoa huo? Hali kadhalika dini, jinsia au umri?

Kwa mtaji huo huo, huwezi kuwazuia watu wa kabila fulani, mkoa fulani, umri fulani ( wazee kwa vijana) dini fulani au rangi fulani wasigombee nafasi za uongozi katika chama chochote, kwa sababu tu kuna viongozi wengi wanaofanana nao kikabila, kimkoa, kidini. kijinsia, kiumri au kirangi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom