Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Mwankijiji, mgaya ,Mkandara

Ule msamaha niliomba kule naufuta rasimi ulikua batili ,ni halali kutaja ID za watu na kama ninyi ni waungwana inabidi mniombe msamaha.

Kunifungia kama ule mkwara wenu mnaopenda kuupiga hautofanya kazi labda tu niamue mwenyewe.
Asanteni.
NB.Ila mkandara aliniambia kistaarabu si ki mkwara

Wewe nawe mbona unatisha tisha watu? kama unataka kutaja ID za watu wewe zitaje na kisha uone sheria za JF zinavyofanya kazi. Mambo ya kukaa hapa unatoa tuhuma za ajabu ajabu hayana msingi.

Kama unaweza kutaja ID we go ahead ila yakikukuta usiingie na jina lingine na kuanza kutoa vilio kuwa umeonewa. Kama kuna mtu mwingine ametaja ID za watu kwa nini usiwaambie Mods wamchukulie hatua? Kwani wewe si mmoja wa members wa forum hii?
 
Hii ni nafasi nyingine kwa Mwenyekiti wa ccm kuweka usawa kwenye chama kinachoongoza nchi yetu. Suala la kuwa na viongozi wengi wa kamati kuu ya ccm ambao ni kutoka dini moja linaleta picha ambayo haionyeshi usawa wa dini mbili kubwa Tanzania za Ukristo na Uislam.

Huu ni ushauri tu, ni muhimu sana kwa Kikwete kushawishi wanaccm kuwa na katiba ambayo itaweka usawa wa kidini kwenye chama tawala.

Majina haya yanaonyesha kile kinachoendelea CCM:

1. Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete - Mwenyekiti - Muslim
2. Ndugu Pius Msekwa - Makamu Mwenyekiti (Bara) -
3. Ndugu Amani Abeid Amani Karume - Makamu Mwenyekiti(Zanzibar) - Muslim
4. Ndugu Yussuf R. Makamba - Katibu Mkuu - Muslim
5. Capt. (mst) George Huruma Mkuchika - Naibu Katibu Mkuu (Bara)
6. Ndugu Salehe Ramadhan Ferouz - Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)- Muslim
7. Dr. Ali Mohamed Shein - Mjumbe - Muslim
8. Ndugu Mizengo Kayanza Peter Pinda - Mjumbe
9. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha - Mjumbe - Muslim
10. Alhaj Ali Hassan Mwinyi - Mjumbe - Muslim
11. Ndugu Benjamin William Mkapa - Mjumbe
12. Mzee Rashid Mfaume Kawawa - Mjumbe - Muslim
13. Dr. Salmin Amour - Mjumbe - Muslim
14. Ndugu John Samwel Malecela - Mjumbe
15. Capt. (mst) John Zefania Chiligati - Mjumbe
16. Ndugu Amos Gabriel Makala - Mjumbe
17. Ndugu Bernard Kamilius Membe - Mjumbe
18. Ndugu Kidawa Hamid Saleh - Mjumbe - Muslim
19. Ndugu Samwel John Sitta - Mjumbe
20. Ndugu Pandu Ameir Kificho - Mjumbe - Muslim
21. Ndugu Anna Abdallah - Mjumbe
22. Ndugu Rostum Aziz - Mjumbe - Muslim
23. Dr. Mohamed Gharib Bilal - Mjumbe - Muslim
24. Ndugu Pindi Hazara Chana - Mjumbe
25. Ndugu Andrew Chenge - Mjumbe
26. Dr. Maua Abeid Daftari - Mjumbe - Muslim
27. Ndugu Samia Suluhu Hassan - Mjumbe - Muslim
28. Ndugu Mohamed Seif Khatib - Mjumbe - Muslim
29. Ndugu Haji Omar Kheri - Mjumbe - Muslim
30. Dr. Abdallah Omari Kigoda - Mjumbe - Muslim
31. Ndugu Abdurahman Kinana - Mjumbe - Muslim
32. Ndugu Anne Semamba Makinda - Mjumbe -
33. Ndugu Fatuma Said Ali Mchumo - Mjumbe - Muslim
34. Ndugu Zakia Hamdan Meghji - Mjumbe - Muslim
35. Ndugu Omar Yussuf Mzee - Mjumbe - Muslim
36. Ndugu Emmanuel John Nchimbi - Mjumbe
37. Ndugu Ali Ameir Mohamed - Mjumbe - Muslim
38. Ndugu Yussuf Moh’d Yussuf - Mjumbe - Muslim

You are still playing the same game. What if all of them were muslims? What if all of them were christians? There is nothing wrong for CCM to have all of its leaders from the same faith, tribe or whatever. The same should be said of CUF, etc
 
Soma yaliyoandikwa hapa kijana, halafu uendelee na mjadala.


Kwa hiyo unakubaliana kuwa ccm ni chama cha kidini ila ni kwa sababu waanzilishi wake wa TAA na TANU+ASP walikuwa waislam? Je ni vizuri?
 
Ni bora hao wenye dini kuliko hao ambao inaonyesha huwajui wapo dini gani,mbona idadi ya kupishana sio kubwa ni kama wanne tu ikiwa sijakosea.
ndugu huwezi kuweka sawa kila kitu ,uwezo huo binadamu hatuna ,hivyo muhimu ni kufuata maadili na maamuzi yanayotolewa labda ungeleta hoja ya kuonyesha ni wapi walienda kufungua misikiti na vyuoi vya kiislamu kujengwa kwa wingi na nafasi nyeti kupendelewa kwa waislamu ,sasa tuwekee na Baraza la Mawaziri tuone na makatibu wao na wakubwa wa maidara na wizara.Hiyo hoja kama ungeileta Kitaifa labda ningekubaliana na wewe ikiwa tu utaambatanisha na utendaji na wapi upendeleo ulifanyika.
Nikiongeza Maraisi wote wamefungua wanaosemekana ni Waislamu(Hope you can seeve between Islam & Muslim) makanisa.
 
Mi sioni kama tatizo ni udini, inaonekana kuna Wazanzibar wengi ambao kama tunavyojua Wazanzibar 9 katika kumi ni waislamu.
 
This is very interesting, maana sasa yamekuwa haya?

FMES,

Kama viongozi 30 kati ya 38 wa kamati kuu ya ccm ni waislam katika nchi ambayo wakristo na waislam wako sawa kwa idadi, je unaweza kusemaje kuhusu mgawanyo huo?
 
Mwenzangu Ameshindwa kuondoa MAFISADI ambao ni hatari katika Maendeleo ya mtanzania halafu mnamletea mengine?

Ningeshauri tumuache tu apumzike maana mambo aliyonayo ni mengi na yanamzidi uwezo.
 
Ni bora hao wenye dini kuliko hao ambao inaonyesha huwajui wapo dini gani,mbona idadi ya kupishana sio kubwa ni kama wanne tu ikiwa sijakosea. ndugu huwezi kuweka sawa kila kitu ,uwezo huo binadamu hatuna ,hivyo muhimu ni kufuata maadili na maamuzi yanayotolewa labda ungeleta hoja ya kuonyesha ni wapi walienda kufungua misikiti na vyuoi vya kiislamu kujengwa kwa wingi na nafasi nyeti kupendelewa kwa waislamu ,sasa tuwekee na Baraza la Mawaziri tuone na makatibu wao na wakubwa wa maidara na wizara.Hiyo hoja kama ungeileta Kitaifa labda ningekubaliana na wewe ikiwa tu utaambatanisha na utendaji na wapi upendeleo ulifanyika.
Nikiongeza Maraisi wote wamefungua wanaosemekana ni Waislamu(Hope you can seeve between Islam & Muslim) makanisa.

Kweli umekosea. Kuna waislam 30 na wakristo 8. Tofauti ni 30-8 = 22
 
Halafu wacha kuchanganya Uislamu na waislamu hivyo ni vitu tuwili tofauti ,maana muislamu wa Uislamu hawezi kufungulia masoko ya manguruwe wala hawezi kujenga kiwanda cha Ulevi kama unazungumzia waislamu jina sawa endelea.
 
Halafu wacha kuchanganya Uislamu na waislamu hivyo ni vitu tuwili tofauti ,maana muislamu wa Uislamu hawezi kufungulia masoko ya manguruwe wala hawezi kujenga kiwanda cha Ulevi kama unazungumzia waislamu jina sawa endelea.

Kama wewe unawajua ambao sio waislam wa kwelikweli basi unaweza kuwataja. Wao wenyewe wanasema ni waislam na hili ni swala kubwa sana kwa ccm kuliangalia kama inataka kujenga usawa kwa dini kubwa Tanzania.
 
1) Mwanakijiji naona hapa unataka kulazimishia jambo. Ningekuona analytical zaidi kama jitihada uliyofanya kucalculate hii proportion ungefanya hivyo hivyo kujua asilimia ngapi ya wanachama wa CCM ni waislamu na ni asilimia ngapi ni wakristu. Ili hii proportionality principle yako iwe valid ni lazima ufanye hivyo. Nachojua kwa hesabu ya watu Tanzania waislamu wanazidi wakristu. Usijisingizie kuwa hujasema na kwamba umeuliza swali kwa sababu ya hii alama ya kuuliza. Maelezo yako wazi kuwa unatoa hoja na sio swali.

UFAFANUZI:

- Assume asilimia 70 ya wana CCM ni waislamu na asilimia 30 ni wakristu. Utafanya pia representation 50/50?

- Na kama asilimia 90 ni wakristu na asilimia 10 ni waislamu utafanya pia 50/50

So ili nikuamini nashauri utujulishe hili.

2) Mwanakijiji unaasume kwamba iwa CCM wanawakilisha maslahi ya dini. Hawa sio viongozi wa dini. Waislamu na wakristu si lazima wapingane kwenye sera hata kama zinahusu dini. Nakumbuka Mrema ni mkristu lakini anasaport anasupport Mahakama ya Kadhi.

3) Huwezi kujua wakristu na waislamu kwa kuangalia majina. Kuna wengine wana majina ya kiislamu lkn hawajui msikiti uko wapi, wengine majina ya kikristu lkn hawajui kanisa liko wapi. Wengine wanahudhuria matukio ya kidini km social ocassion tu na sio religious. Sasa unaweza kutuambia ni wangapi kati ya hao uliotaja ni practioners wa dini zao?

Kwa hiyo unataka kusema kuwa asilimia 70 ya wanaccm ni waislam kwa hiyo ndio maana viongozi wa ccm wengi ni waislam? Hivi kuna wanaccm wangapi visiwani ukilinganisha na Mwanza? Kwa nini kuna watu wengi wa visiwani kwenye kamati kuu kuliko wa kutoka mwanza.

Hesabu yako nayo ina matatizo. CCM kuna udini na inabidi waache udini na wawe fair kwa dini zingine na sio kupendelea waislam kuliko wakristo na dini zingine.
 
mwafrika.. very good.. finally Kuhani naye ameanza kuiona point yangu. Swali langu kuna viongozi wangapi Chadema (mtu asichukue sita tu na kugeneralize kwenye chama kizima). Then watuoneshe ni jinsi gani wamefikia suala hilo la Ukabila. Wangwe na wale wengine wenye kurudia masuala ya Ukabila wanajilimit kwenye namba ya wabunge sita tu na kuonesha generalization ya chama kizima na uongozi mzima wa Chadema.

Kuhani,

Of course najua Katiba ya CCM inasema (nikiwa nimelelewa ndani ya chama hicho). Najua jinsi gani viongozi wake wanapatikana, na ukirudi nyuma nimewahi kusema binafsi sijali sana nani ananiongoza as far as immutable characteristics are involved... Angalia definition yangu ya ukabila na udini ilivyo kwenye posti ya kwanza ili uelewe unachosema ndicho nimekijengea hoja, japo imekuchukua muda kufikia hapa.


Mwanakijiji,

Kama nilivyosema mwanzoni, ni bora watu waachane na hizi dividing lines. Mimi sioni tatizo kwa chadema kuwa na wabunge 5 kati ya 6 kutoka kabila moja kama vile ambavyo sioni tatizo kwa ccm kuwa na viongozi 30 kati ya 38 ambao ni waislam.

Dini na kabila visiwe vigezo vya kupima uongozi bali utendaji na ubora wa viongozi. Ukiangalia marekani, Bush alivyoingia ikulu, alikuja na timu karibu yote ya watu wa Texas kwenye kazi mbalimbali za ofisi yake. Sidhani kama kuna yeyote kutoka Montana amekuwa anapiga kelele kuwa ikulu imejaa watu wa Texas. Obama ameweka kampeni yake Chicago na kuna uwezekano kuwa wengi wanaofanya naye kampeni sasa hivi watapata kazi za utendaji ikulu kama Obama akishinda. SIdhani kama watu wa New Mexico wataanzisha makelele kuwa ikulu imejaa watu wa Chicago.

Hizi dividing lines zililetwa na wakoloni na mpaka leo zinaimaliza Afrika. Swali lako ni muhimu sana hapa, kama ni tatizo kuangalia ukabila Chadema, basi iwe tatizo pia kuangalia udini ccm. In the end, no body cares, mimi sina mtu yeyote wa kabila langu kwenye uongozi wa juu wa ccm lakini ninapata kila ninachohitaji. Haya mambo ya kungangania ukabila na udini yanatuponza.
 
Goosh,

Who cares if all of them were muslims?

Do you care if CUF has more muslims than christians? Do you care if UDP has more sukumas than other tribes? Do you care if CHADEMA has more chagga MPs than other tribes?

If you do, then I do care about 30 muslims out of 38 ccm leaders.
 
Do you care if CUF has more muslims than christians? Do you care if UDP has more sukumas than other tribes? Do you care if CHADEMA has more chagga MPs than other tribes?

If you do, the I do care about 30 muslims out of 38 ccm leaders.

If this is the case then, I dont think there is anything I can do to help you think beyond dividing lines. You are just doing the same thing CCM fanatics have been doing to other parties and yet you call yourself opposition!

Shame on you and all who care about tribes and religions.
 
Wewe nawe mbona unatisha tisha watu? kama unataka kutaja ID za watu wewe zitaje na kisha uone sheria za JF zinavyofanya kazi. Mambo ya kukaa hapa unatoa tuhuma za ajabu ajabu hayana msingi.

Kama unaweza kutaja ID we go ahead ila yakikukuta usiingie na jina lingine na kuanza kutoa vilio kuwa umeonewa. Kama kuna mtu mwingine ametaja ID za watu kwa nini usiwaambie Mods wamchukulie hatua? Kwani wewe si mmoja wa members wa forum hii?


si nilitaja ile ID na msamaha niliouomba nimeufuta nifungie basi
 
Jee ni kweli kuwa CCM ni chama cha wakatoliki pamoja na uwingi wa waislamu kwenye kamati kuu. is it true that CCM stands for christian church movement?

Jee Decision za kuendesha chama zinatolewa na waislamu au wakristo?
 
si nilitaja ile ID na msamaha niliouomba nimeufuta nifungie basi

mkamap, hasira za nini? sio mimi nafungia watu hapa. Wote mimi na wewe kama unapenda jamvi letu tunatakiwa kufuata taratibu zilizowekwa na mods ili kurahisisha kazi yao. Hasira na ugomvi vya nini? inasaidia nini kwenye hoja kutaja ID za watu?

Tusaidiane na tukumbushane tu kutunza sheria za forum. Mengine ya kutoa vitisho sio mazuri. Kama unataka kutaja ID za watu, wewe taja tu ila kumbuka kuwa ukifungiwa kwa kufanya hivyo, usianze kulalamika kuwa umeonewa.
 
Jee ni kweli kuwa CCM ni chama cha wakatoliki pamoja na uwingi wa waislamu kwenye kamati kuu. is it true that CCM stands for christian church movement?

Jee Decision za kuendesha chama zinatolewa na waislamu au wakristo?

Kama viongozi wakubwa watatu kati ya wanne wa ccm ni waislam, basi nadhani tayari umepata jibu la swali lako.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom