Uchumi wa nchi nyingi za Afrika utaendelea kukua kutokana na kuimarika kwa biashara kati ya China na Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111197953576.jpg

Fadhili Mpunji

Kila mkutano wa bunge la umma la China unapomalizika, utekelezaji wa mipango mipya ya serikali ya China huwa unaanza. Pamoja na kuwa mambo mengi yanayojadiliwa ni mambo ya ndani, mambo hayo pia huwa yanahusiana moja kwa moja na nchi za nje na yanahusu sera ya kidiplomasia ya China. Mkutano wa safari hii wa bunge la umma la China umefanyika wakati athari za janga la COVID-19 kwa uchumi wa dunia zikiwa zinapungua na shughuli za uchumi zikianza kufufuka.

Mwanzoni mwa mwaka 2020, biashara kati ya China na Afrika ilitetereka kidogo kutokana na janga la COVID-19, lakini kabla ya kutetereka huko kulikuwa na ongezeko zuri lililoendelea kwa muda mrefu. Kuendelea huko kulitokana na utekelezaji madhubuti wa ushirikiano kati ya pande mbili kati ya China na nchi za Afrika chini ya mpango wa “ukanda mmoja, njia moja”, na ushirikiano chini ya mpango wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC.

Kwa watu wanaofuatilia kwa karibu uhusiano kati ya China na Afrika, kupungua kwa biashara kati ya China na Afrika wakati wa janga la COVID-19, huku pande hizo zikiwa na wigo mpana wa ushirikiano kama huo, lilikuwa ni jambo la kushangaza kidogo. Lakini pia takwimu zilizotolewa hivi na wizara ya biashara ya China zinaonyesha kuwa hali ya kuongezeka kwa biashara kati ya China na Afrika, imerudi kwa kasi na kuleta matumaini zaidi.

Kulingana na takwimu zilizotolewa hivi karibuni na Idara ya Forodha ya China, mwaka 2021 kiwango cha biashara kati ya China na Afrika kiliongezeka kwa 35% ikilinganishwa na mwaka uliotangulia, na kufikia dola za Kimarekani bilioni 254.3, kiasi ambacho kimezidi kile cha kabla ya kutokea kwa janga la COVID-19 na kuweka rekodi mpya ya kihistoria. Uuzaji bidhaa nje za Afrika kwa China ulifikia dola za Kimarekani bilioni 105.9, ikiwa ni ongezeko la 43.7% kutoka mwaka 2020.

Pamoja na ukweli kwamba China imekuwa ni mshirika mkubwa zaidi wa biashara kwa nchi za Afrika katika kipindi cha miaka 20 iliyopita, kipindi cha miaka mitano iliyopita kimekuwa kipindi chenye manufaa makubwa kwa nchi za Afrika. Ni kipindi ambacho serikali ya China imetekeleza sera mbalimbali za makusudi kuhakikisha urari wa biashara kati ya China na nchi za Afrika unaboreshwa. Hii ni kutokana na utekelezaji wa makubaliano ya kuruhusu asilimia 97 ya bidhaa za kilimo kutoka nchi 33 za Afrika kuingia kwenye soko la China bila ushuru, kuzipatia nchi za Afrika uwezo wa uzalishaji na kuuza bidhaa nje, na hata kutumia mtandao wa internet kutangaza bidhaa moja kwa moja kwenye soko la China.

Kwa muda wa muongo mmoja na zaidi sasa uchumi wa nchi mbalimbali za Afrika kusini mwa sahara umekuwa na ongezeko, na ongezeko hili kwa kiasi kikubwa limekuwa na uhusiano na mchango wa China. Iwe ni kwenye kujenga miundombinu wezeshi, iwe ni kwenye kwa waafrika kununua bidhaa za mtaji za bei nafuu kutoka China na kuongeza uzalishaji, au iwe ni kwa kutoa soko kwa bidhaa za kilimo kutoka nchi za Afrika.

Wakati vyombo vya habari vya nchi za magharibi vimekuwa vikiendelea kutafuta dosari ndogo ndogo zinazojitokeza kwenye uhusiano kati ya China na nchi za Afrika, na kutumia dosari hizo kuipaka matope China, picha kubwa ya uhusiano kati ya China na Afrika ni bora zaidi kuliko inavyotajwa, na takwimu kutoka wizara ya biashara ya China, Idara ya forodha ya China, takwimu za uchumi kutoka nchi za Afrika, na hata hali halisi ya maisha ya waafrika wa kawaida, vinaonesha kuwa kuna mabadiliko chanya kwenye uhusiano kati ya pande hizi mbili.
 
Back
Top Bottom