Uchawi upo, usidanganywe

Uchawi upo, usidanganywe

Hakuna uchawi narudia tena hakuna uchawi.uchawi ni imani uchawi umejaa upotoshwaji zaidi kiliko ukweli lakini naomba nikilii nguvu hii ipo hoja ya msingi hapa inatendaje kaz?na kwa nini wengine hurogeka na wangine hawarogeki ukweli ni kwamba wanao rogeka ni wale wasio jiamini ni wale wanao ishi kwa mashaka ni wale wenye hofu,unadhani kwa nini watu wengi wanao sali sana wanao jiita wapendwa huutaja zaidi uchawi kwa kutojiamini kwao hudhani uchawi wanaujua kweli ukweli bado hawaujui.0756805540 niulize cho2te kuhusu uchawi nitakufungua utakua huru

Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante, na wewe umeshautaja uchawi!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, story nliyoandika mimi sio hearsay, ni habari ya kweli nliyoshuhudia kwa macho

Mkuu nilikua sijsoma story yako nikiamini, kama story zingine zote za uchawi, huwa zinaacha loopholes and surely enough yako pia was no exception to this. Kwanza ni kawaida kwa waganga wa jadi kusema mbaya wako ni jirani yako au ndugu yako kama hujui hili hadi leo basi siwezi kushangaa kwanini unaamini uchawi upo.

Pili, kuuwawa na tembo au wanyama maeneo ya karibu na mbugani ni jambo la kawaida, sawa na mtu wa mjini kugongwa na gari. Nadiriki kusema ilikua coincidence tu na pengine huyo mtu asingekufa mganga angekuja na sababu zingine kama kawaida yao.

Nitakupa kisa kidogo, Juma alimwambia Obedi leo usiku utanikoma baada ya kukorofishana, Obedi usiku ule aligongwa na gari na kufariki pale pale unadhani Juma ni mchawi? Kwanini isiwe conicidence? Unaweza muongelea mtu mabaya bila kumaanisha na jambo baya likampata ila hiyo sio ithibati ya kuonyesha wewe ni mchawi.

Hizi ndo kasoro za story za uchawi, ni story za hearsay na mara nyingi zina loopholes ambazo watu hukimbilia kusema ni uchawi wakati zinaweza kujibika kwa njia zingine.

HAKUNA UCHAWI.
 
Mkuu nilikua sijsoma story yako nikiamini, kama story zingine zote za uchawi, huwa zinaacha loopholes and surely enough yako pia was no exception to this. Kwanza ni kawaida kwa waganga wa jadi kusema mbaya wako ni jirani yako au ndugu yako kama hujui hili hadi leo basi siwezi kushangaa kwanini unaamini uchawi upo.

Pili, kuuwawa na tembo au wanyama maeneo ya karibu na mbugani ni jambo la kawaida, sawa na mtu wa mjini kugongwa na gari. Nadiriki kusema ilikua coincidence tu na pengine huyo mtu asingekufa mganga angekuja na sababu zingine kama kawaida yao.

Nitakupa kisa kidogo, Juma alimwambia Obedi leo usiku utanikoma baada ya kukorofishana, Obedi usiku ule aligongwa na gari na kufariki pale pale unadhani Juma ni mchawi? Kwanini isiwe conicidence? Unaweza muongelea mtu mabaya bila kumaanisha na jambo baya likampata ila hiyo sio ithibati ya kuonyesha wewe ni mchawi.

Hizi ndo kasoro za story za uchawi, ni story za hearsay na mara nyingi zina loopholes ambazo watu hukimbilia kusema ni uchawi wakati zinaweza kujibika kwa njia zingine.

HAKUNA UCHAWI.
Wewe nakushusha ngiri kwanza halafu nakunyoa nywele huko huko uliko ili ujue uchawi upo.
Utatuambia mwenyewe na kuomba msamaha
 
Wewe nakushusha ngiri kwanza halafu nakunyoa nywele huko huko uliko ili ujue uchawi upo.
Utatuambia mwenyewe na kuomba msamaha

Tafadhali fanya hivyo, nikupe hadi lini?
 
Hiki ni kisa cha kweli kilichotokea kwenye familia yetu miaka 18 iliyopita.

Ilikuwa mwaka 2000, wakati huo nikiwa na miaka 12. Familia yetu ilikuwa inaishi huko Tarime vijijini kwenye eneo (plot) ambayo haikuwa yetu ila ya jirani yetu ambaye tulikuwa tunaishi naye kama majirani japo kulikuwa na mgogoro wa chini chini a.k.a vita baridi . Back 1999 mdogo wangu alifariki akiwa mchanga kama mwezi m1 na ilisemekana kuwa yule jirani yetu amehusika na kifo chake kichawi. Mwaka 2000 katikati, mdogo wangu wa pili akaanza kuugua. Aliugua sana na kufariki kama miezi 4 baadaye, kwa kuwa yule dogo alikuwa amerithi jina la babu yetu,basi kaka zake baba wakasema hawawezi kukubali baba yao auwawe kirahisi hivyo, wakaamua kufuatilia kupata ukweli wa kifo cha yule dogo.

Wakiwa wamejidhatiti kutaka kujua ukweli juu ya kifo cha yule bwana mdogo waliangukia mikononi mwa mganga mmoja wa kienyeji maeneo ya Nyamongo(sitamtaja jina ila namkumbuka). Walipoeleza shida yao waliulizwa kama wanataka kujua chanzo cha kifo cha yule dogo ili iweje. Wakasema wanataka kama kuna binadamu awaye yote amehusika, NAYE AFE. Wakakubaliana kuwa hata kama ni mmoja kati ya wanafamilia au mmoja kati ya wale walioenda kwa mganga, AFE TU. Mganga akafanya mambo yake na akamtambua aliyehusika na kifo cha dogo na akawatajia kuwa ni yule jirani yetu. Akawaeleza kuwa kuna siku yule bwana mdogo alienda kuchunga pamoja na mtoto mkubwa wa yule jirani yetu kwa mtindo maarufu kule ukuryani wa kuchanganya mifugo, na ndipo yule jamaa aliwapelekea kinywaji a.k.a togwa almaarufu kama OBOSARA kule machungani na kwenye kikombe cha yule bwana mdogo kuliwekwa sumu iliyotafuna ini lake na kupelekea mauti yake. wazee wakiwa na hasira wakakazia kuwa AFE TU. Basi mganga akawaomba zana za kazi ili akamilishe kazi yake chap. Zana zenyewe zilizohitajika ni KINYESI CHA TEMBO na mizizi ya miti kadha wa kadha... Kwa kuwa wazee hawakuwa wataalamu wa mambo waka-opt kutoa pesa watafutiwe zana. Wakatoa keshi laki na ishiirini tii shilings na kazi ikaanza baada ya mganga kumtuma kjana wake ambaye ndiye alikuwa msaidizi wake kwenda porini Serengeti kusaka zana za kazi. Wakaahidiana kuwa baada ya wiki mbili mganga atafika nyumbani kwetu kukamilisha kazi.

Kweli baada ya wiki mbili mganga alitua maskani kwetu usiku wa manane, wakachinja kuku mkubwa jogoo na mganga akapiga na ugali wa mhogo uliochanganywa na mtama akalala. Kesho yake tukaamka na mganga akaanza show kwa kupiga tambiko moja kali sana pale maskani. Tambiko liliambatana na kafara kadha wa kadha na utabiri juu ya maisha yetu pale nyumbani kwa mtu mmoja mmoja. Binafsi mganga alinisimulia kuhusu habari zangu za shule na jinsi nlivyokuwa mkorofi na mgomvi shuleni Kumwika Primary school.
Usiku huo mganga alitia timu kibabe nyumbani kwa yule jirani yetu na kufanya vitu kadha wa kadha bila kuonekana na akapotea kama watu wasiojulikana.

Mganga aliondoka siku iliyofuata kwa ahadi kuwa tutapata majibu ndani ya siku chache..

Baada ya wiki kama mbili, siku moja alfajiri sana mama yangu pamoja na kaka na dada zangu wawili waliamka na kwenda kufuata majani ya kuezekea nyumba eneo la kama kilomita tatu kutoka nyumbani. Asubuhi sana mimi na baba tukaenda kulima kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe pale pale jirani na nyumbani. Eneo tulilokuwa tunalima lilikuwa ni kwenye mpaka kabisa wa eneo letu na eneo la yule jirani yetu. Kitu cha ajabu ni kwamba ng'ombe walikuwa hawafiki mwisho wa shamba, walikuwa kama wanaogopa hivi na wakikaribia mwisho wanakimbia kama wameona kitu cha kutisha. Mara ghafla tukasikia mlio mkali sana kutoka vichakani jirani kabisa na pale tulipokuwa tunalima na ni jirani na makazi ya mke mdogo wa yule jirani yetu. Kufumba na kufumbua tukaona tembo mkubwa na mkonga wake akitoka mle vichakani na kuondoka kwa kasi kelekea Serengeti porini.

NINI KILIKUWA KIMETOKEA?
Ni kwamba kuamkia siku ile, yule jirani yetu alilala kwa mke wake mkubwa na kwa sababu mifugo yake ilikuwa inalala kwa mke wake mdogo ambaye ndiye alikuwa anaishi karibu sana na nyumbani kwetu, ilibidi asubuhi sana jamaa awahi kwa mke mdogo apige zake bangi (alikuwa mvutaji wa bangi ya kiko) na kufunga ng'ombe kwa ajili ya kwenda shamba kulima. Alipofika nyumbani aligonga mlango na kumsisitiza bi mdogo amfungulie mlango maana ana kiu ya jani sana na asichelewe shambani. Yule bi mdogo alikasirika sana kuamshwa mapema vile kwa sababu tu eti jamaa anataka kula mmea. Akamjibu kwa jeuri kuwa ''Kwani huko ulikotoka hakuna bangi?, mi sifungui mlango alfajiri yote hii".
Jamaa kwa hasira akaondoka kwenda kichakani kukata (alikuwa na sime yake) fimbo ama mjeledi ama kiboko kwa ajili ya kuja kumshikisha adabu yule mwanamke. Akamuahidi kuwa anarudi na atapata tabu sana. Inasemekana kuwa jamaa alipofika kule vichakani alijisikia kama anahitaji kuachia mzigo almaarufu kama kujisaidia, na alipochuchumaa kukata gogo ghafla bin vuu alitokea tembo mbele yake na ndipo jamaa aliposimama kwa taharuki. Yule tembo alim-mwaga utumbo baada ya kumpiga na jino lake maeneo ya mbele. Kama kawaida tembo huwa ni mstaarabu, alikata majani kadhaa akamfunika na kukojoa juu yake kisha akatoa mlio ule tuliousikia kama taarifa kuwa kazi imeisha. Tembo akachikichia serengeti akipita vijiji kadha wa kadha huku nyuma akiacha msiba mzito kitongojini na kwenye familia ya yule ndugu. Tembo hakusababisha madhara zaidi katika safari yake ya kuelekea porini..

Kama unaaminishwa na sayansi kuwa uchawi sio real, endelea tu mpaka utakapopigiwa show kali ya kibabe na wazee wa kilingeni..

Dunamist
Made in Tanzania
tapatalk_1533702179059.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahah... Nilichoelewa ni kwamba una miaka 30.. Kwamujibu wa hadith yako tumeona jamaa ameuliwa na tembo. Na kama mlimkuta ameshakufa mlijuaje kama alienda kwa mke mdogo kuvuta bangi? Mlijuaje alienda kwenye kichaka kukata fimbo akamchape mkewe? Mlijuaje alihisi kunya alipofika kichakani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wao ndio walitega mtego na hii INA maana walienda pata feedback kwa mtega Bomu.naunganisha sentensi tu.
 
Nimegundua uhusiano wa tembo na kinyesi kilichotumika kwa mganga..huenda kingetumika cha simba angeuliwa na simba,, aya bna,, pia mtoa mada ni 30+ aged
 
Mkuu nilikua sijsoma story yako nikiamini, kama story zingine zote za uchawi, huwa zinaacha loopholes and surely enough yako pia was no exception to this. Kwanza ni kawaida kwa waganga wa jadi kusema mbaya wako ni jirani yako au ndugu yako kama hujui hili hadi leo basi siwezi kushangaa kwanini unaamini uchawi upo.

Pili, kuuwawa na tembo au wanyama maeneo ya karibu na mbugani ni jambo la kawaida, sawa na mtu wa mjini kugongwa na gari. Nadiriki kusema ilikua coincidence tu na pengine huyo mtu asingekufa mganga angekuja na sababu zingine kama kawaida yao.

Nitakupa kisa kidogo, Juma alimwambia Obedi leo usiku utanikoma baada ya kukorofishana, Obedi usiku ule aligongwa na gari na kufariki pale pale unadhani Juma ni mchawi? Kwanini isiwe conicidence? Unaweza muongelea mtu mabaya bila kumaanisha na jambo baya likampata ila hiyo sio ithibati ya kuonyesha wewe ni mchawi.

Hizi ndo kasoro za story za uchawi, ni story za hearsay na mara nyingi zina loopholes ambazo watu hukimbilia kusema ni uchawi wakati zinaweza kujibika kwa njia zingine.

HAKUNA UCHAWI.
Kukimbilia kujibu na hujasoma inadhihirisha loophole mahali fulani upstairs.
Hivi unajua hata Isack Newton hakwenda kukaa chini ya ule mti wa Apple akiwa kwenye research ya gravitational force? Ilikuwa coincidence tu, kama unavyoamini wewe. Lakini haiondoi ukweli kwamba alichogundua kinathibitika. Unadhani hakuna mtu aliyekuwa amewahi kuona kitu kinaanguka kutoka juu kwenda chini na kisirudi juu? Pengine waliamini ni coincidence kama unavyoamini wewe..
 
Kukimbilia kujibu na hujasoma inadhihirisha loophole mahali fulani upstairs.
Hivi unajua hata Isack Newton hakwenda kukaa chini ya ule mti wa Apple akiwa kwenye research ya gravitational force? Ilikuwa coincidence tu, kama unavyoamini wewe. Lakini haiondoi ukweli kwamba alichogundua kinathibitika. Unadhani hakuna mtu aliyekuwa amewahi kuona kitu kinaanguka kutoka juu kwenda chini na kisirudi juu? Pengine waliamini ni coincidence kama unavyoamini wewe..
Huoni aibu kujibu story za kusadikika kwa mifano hai inayothibitika. Leo Kuna ndege, rockets nk kwa kutumia gravitational force, uchawi zaidi ya story za kitoto za kusimuliana vitu visivyomake any sense hauthibitiki.

Mtu kauwawa na tembo mbugani cha ajabu nini hapo au ulitaka agongwe na meli Serengeti! Badala useme mganga aliwapiga hela kumbe wewe pamoja na kukua akili imeganda pale pale.

Waafrika kuendelea bado sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huoni aibu kujibu story za kusadikika kwa mifano hai inayothibitika. Leo Kuna ndege, rockets nk kwa kutumia gravitational force, uchawi zaidi ya story za kitoto za kusimuliana vitu visivyomake any sense hauthibitiki.

Mtu kauwawa na tembo mbugani cha ajabu nini hapo au ulitaka agongwe na meli Serengeti! Badala useme mganga aliwapiga hela kumbe wewe pamoja na kukua akili imeganda pale pale.

Waafrika kuendelea bado sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahah! Umejibu vyema, Leo kuna ndege na rocket kwa coincidence ya apple kuanguka kutoka juu kwenda chini. Lakini pia leo yule jamaa hayupo kwa coincidence ya yule tembo. OVA
 
Hahahahah! Umejibu vyema, Leo kuna ndege na rocket kwa coincidence ya apple kuanguka kutoka juu kwenda chini. Lakini pia leo yule jamaa hayupo kwa coincidence ya yule tembo. OVA
Ndege bado zinaruka vp huyo mganga wako bado anaua watu kwa tembo? Anaweza niua mimi nikiwa posta kwa tembo? Hata kama sio huyo unaweza tafuta mganga yoyote aniue kwa njia yoyote ya kichawi. Huwa mkifika hapa mnaruka mita laki

Nimejaribu sana kurogwa bila mafanikio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndege bado zinaruka vp huyo mganga wako bado anaua watu kwa tembo? Anaweza niua mimi nikiwa posta kwa tembo? Hata kama sio huyo unaweza tafuta mganga yoyote aniue kwa njia yoyote ya kichawi. Huwa mkifika hapa mnaruka mita laki

Nimejaribu sana kurogwa bila mafanikio.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, kwanza sijasema mahali popote kuwa mimi ni mchawi. Nimekusimulia kisa nlichoshuhudia 18yrs back. Ila pamoja na yote hayo hata kama ningekuwa mchawi nisingeweza kukuthibitishia kwa njia rahisi unayoitaka wewe. Hivi kwa kuamini sayansi, wewe leo unaweza kutengeneza rocket au ndege? Si unatumia zilizopo kama uthibitisho wake?
 
Back
Top Bottom