Uchawi upo, usidanganywe

Uchawi upo, usidanganywe

Mkuu pengine uko sahihi lakini pia unaweza ukawa hauko sahihi.

Mimi siyo muumini wa uchawi kwa maana ya kwamba sijawahi kushiriki na sina mpango wa kuja kushiriki katika mambo ya ushirikina/uchawi lakini naamini uchawi upo. Kwa hiyo nitakachokieleza hapa chini kisichukuliwe kama vile na mimi ni mshiriki katika uchawi.
1. Miaka ya nyuma nikiwa mdogo niliwahi kuishi kijijini. Pale kijijini kulikuwa na watu kadhaa waume kwa wake waliokuwa wanajulikana sana kwamba ni wachawi sana. Kati ya hilo kundi kubwa kulikuwa na wazee wa kiume wawili na wabibi wawili waliokuwa wakiaminika kwamba ni wachawi zaidi ya wale wengine wote.

Sasa siku moja jioni alikuja mzee mmoja kututembelea kibiashara akitokea mkoa mwingine mbali kabisa na nyumbani na hiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kabisa kufika pale kijijini. Huyo mzee kabla hata ya kuja tulikuwa tumeshapata habari zake kwamba ni "muike" yaani ambaye kachanjiwa, harogeki na anaweza kujua hata hatari iliyopo mbele yake. Basi yule mzee alipofika pale nyumbani jioni akalala hadi asubuhi. Nakumbuka tukiwa tumekaa nje kwenye kama saa nne hivi asubuhi na yule mzee mara kwa mbali kama mita 30 hivi akatokea mzee wa pale kijijini ambaye ni mmoja wa wale wanaume wawili wanaoaminika zaidi kwa uchawi wao. Ghafla yule mzee mgeni akiwa anatetemeka kidogo akasema kwa kilugha lakini akimaanisha "huyo mtu anaekuja ni mchawi sana!" Kumbuka hapo ni mara yake ya kwanza kufika kijijini na hamjui mtu yeyote pale kijijini zaidi ya sisi wenyeji wake lakini aliweza kumtambua huyo mzee mchawi.

2. Mwaka fulani nikiwa mjini usiku kuna jirani yetu aliingiliwa na majambazi. Ilidaiwa kwamba hao majambazi walikuwa ni watatu ila wawili waliwahi kukimbia na mmoja hakufanikiwa kukimbia baada ya mwenye nyumba yaani jirani yetu huyo kutoka na bunduki na majirani wengine kumzingira. Nakumbuka kuna watu walikuwa wanampiga yule jambazi kwa magongo makubwa makubwa lakini yule jambazi hakuonekana kushituka au kuumizwa na kipigo hicho. Yaani watu wananyanyua juu gongo na wenye roho ndogo tunageuza shingo ili tusishuhudie jinsi hilo gongo litakavyotua kichwani au mwilini mwa jambazi lakini kila linapotua jambazi wala haonyeshi kuumia chochote. Basi kuna wazee fulani na uzoefu wao wakawatonya pembeni wapigaji kwamba inavyoonekana yule jambazi haumii kwa kipigo kile cha magongo kwa sababu atakuwa na hirizi inayompa kinga ya kutosikia maumivu. Wakawashauri ili aweze kupata maumivu basi wachukue vitu laini kama nyasi au mabua ndiyo wampige nayo. Bahati nzuri hapo pembeni kulikuwa na mabua ya mahindi. Wananchi wakang'oa yale mabua na kuanza kumpiga nayo. Mara tu baada ya kupigwa na yale mabua yule jambazi akaaanza kupiga makelele ya kuumia huku damu zikianza kumtoka kila sehemu. Kufumba na kufumbua akawa kaloa damu mwili mzima. Bahati nzuri polisi walifika wakamchukua na kumpeleka kituoni lakini kesho yake tukapata taarifa kwamba amefariki kutokana na kile kipigo cha wananchi.

Kama hizo story mbili zinathibitisha kama kuna uchawi au la sina hakika juu yake.

Hazithibitishi chochote na kama ilivyo kawaida ya story za uchawi zote huwa ni hearsay, kama hiyo number moja, inawezekana huyo mzee mgeni kijijini, kama nyie, aliambiwa kwamba huyo mzee wa hapo ni mchawi sana.

Hiyo number mbili labda mwizi ana ustahimilivu mkubwa wa maumivu kama walivyo wezi wengi au pengine mwizi aliumizwa na magongo hayo mabua yalikuja kukamilisha kazi tu au labda kuna more into the story ambayo wewe kwa kujua au kutojua hukuona/hujaandika ukizingatia unasema mlikua mnageuza shingo kwa kuogopa kuona kipigo.

Story za kusadikika za uchawi zina trait moja sawia; zote huwa ni story za hearsay na hazithibitiki hata siku moja.
 
Hazithibitishi chochote na kama ilivyo kawaida ya story za uchawi zote huwa ni hearsay, kama hiyo number moja, inawezekana huyo mzee mgeni kijijini, kama nyie, aliambiwa kwamba huyo mzee wa hapo ni mchawi sana.

Hiyo number mbili labda mwizi ana ustahimilivu mkubwa wa maumivu kama walivyo wezi wengi au pengine mwizi aliumizwa na magongo hayo mabua yalikuja kukamilisha kazi tu au labda kuna more into the story ambayo wewe kwa kujua au kutojua hukuona/hujaandika ukizingatia unasema mlikua mnageuza shingo kwa kuogopa kuona kipigo.

Story za kusadikika za uchawi zina trait moja sawia; zote huwa ni story za hearsay na hazithibitiki hata siku moja.
Mkuu, story nliyoandika mimi sio hearsay, ni habari ya kweli nliyoshuhudia kwa macho
 
Story za uchawi, ushirikina, wanga na ulozi ni story za kusadikika zinazoaminiwa na wavivu wa kufikiri.
Story ndio zinaaminiwa na wavivu wa kufikiri, Nlichokiona kwa macho pengine ungekiona leo ungekuwa kwenye kundi hilo(la wavivu wa kufikiri)
 
Jomoni. Nipeni address au contact za mganga mmoja wa ukweli. Nimevunjiwa nyumba yangu. Nataka kuanza na dereva wa tingatinga. Boss wake na aliyetoa oda.
 
Ulivyotaja KUMWIKA S/Msingi umenikumbusha M/Mkuu aliyemfata Mwl.OBOGO anaitwa Mwl.MASHEBE wa hiyo shule alikuwa akipiga bakora za MOJA MZINGA au MBILI REJAREJA.
 
Ulivyotaja KUMWIKA S/Msingi umenikumbusha M/Mkuu aliyemfata Mwl.OBOGO anaitwa Mwl.MASHEBE wa hiyo shule alikuwa akipiga bakora za MOJA MZINGA au MBILI REJAREJA.
Hahah! Namkumbuka Obogo alikuwa anakaa kule Muriba... Na mwalimu Sererya, kina Meng'anyi. Duh! Kitambo.
 
Hazithibitishi chochote na kama ilivyo kawaida ya story za uchawi zote huwa ni hearsay, kama hiyo number moja, inawezekana huyo mzee mgeni kijijini, kama nyie, aliambiwa kwamba huyo mzee wa hapo ni mchawi sana.

Hiyo number mbili labda mwizi ana ustahimilivu mkubwa wa maumivu kama walivyo wezi wengi au pengine mwizi aliumizwa na magongo hayo mabua yalikuja kukamilisha kazi tu au labda kuna more into the story ambayo wewe kwa kujua au kutojua hukuona/hujaandika ukizingatia unasema mlikua mnageuza shingo kwa kuogopa kuona kipigo.

Story za kusadikika za uchawi zina trait moja sawia; zote huwa ni story za hearsay na hazithibitiki hata siku moja.
Bahati mbaya mambo ya kiroho hayaelezeki kwa maneno...unapewa picha tu ila huwez kuelewa moja kwa moja mpk ushiriki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiki ni kisa cha kweli kilichotokea kwenye familia yetu miaka 18 iliyopita.

Ilikuwa mwaka 2000, wakati huo nikiwa na miaka 12. Familia yetu ilikuwa inaishi huko Tarime vijijini kwenye eneo (plot) ambayo haikuwa yetu ila ya jirani yetu ambaye tulikuwa tunaishi naye kama majirani japo kulikuwa na mgogoro wa chini chini a.k.a vita baridi . Back 1999 mdogo wangu alifariki akiwa mchanga kama mwezi m1 na ilisemekana kuwa yule jirani yetu amehusika na kifo chake kichawi. Mwaka 2000 katikati, mdogo wangu wa pili akaanza kuugua. Aliugua sana na kufariki kama miezi 4 baadaye, kwa kuwa yule dogo alikuwa amerithi jina la babu yetu,basi kaka zake baba wakasema hawawezi kukubali baba yao auwawe kirahisi hivyo, wakaamua kufuatilia kupata ukweli wa kifo cha yule dogo.

Wakiwa wamejidhatiti kutaka kujua ukweli juu ya kifo cha yule bwana mdogo waliangukia mikononi mwa mganga mmoja wa kienyeji maeneo ya Nyamongo(sitamtaja jina ila namkumbuka). Walipoeleza shida yao waliulizwa kama wanataka kujua chanzo cha kifo cha yule dogo ili iweje. Wakasema wanataka kama kuna binadamu awaye yote amehusika, NAYE AFE. Wakakubaliana kuwa hata kama ni mmoja kati ya wanafamilia au mmoja kati ya wale walioenda kwa mganga, AFE TU. Mganga akafanya mambo yake na akamtambua aliyehusika na kifo cha dogo na akawatajia kuwa ni yule jirani yetu. Akawaeleza kuwa kuna siku yule bwana mdogo alienda kuchunga pamoja na mtoto mkubwa wa yule jirani yetu kwa mtindo maarufu kule ukuryani wa kuchanganya mifugo, na ndipo yule jamaa aliwapelekea kinywaji a.k.a togwa almaarufu kama OBOSARA kule machungani na kwenye kikombe cha yule bwana mdogo kuliwekwa sumu iliyotafuna ini lake na kupelekea mauti yake. wazee wakiwa na hasira wakakazia kuwa AFE TU. Basi mganga akawaomba zana za kazi ili akamilishe kazi yake chap. Zana zenyewe zilizohitajika ni KINYESI CHA TEMBO na mizizi ya miti kadha wa kadha... Kwa kuwa wazee hawakuwa wataalamu wa mambo waka-opt kutoa pesa watafutiwe zana. Wakatoa keshi laki na ishiirini tii shilings na kazi ikaanza baada ya mganga kumtuma kjana wake ambaye ndiye alikuwa msaidizi wake kwenda porini Serengeti kusaka zana za kazi. Wakaahidiana kuwa baada ya wiki mbili mganga atafika nyumbani kwetu kukamilisha kazi.

Kweli baada ya wiki mbili mganga alitua maskani kwetu usiku wa manane, wakachinja kuku mkubwa jogoo na mganga akapiga na ugali wa mhogo uliochanganywa na mtama akalala. Kesho yake tukaamka na mganga akaanza show kwa kupiga tambiko moja kali sana pale maskani. Tambiko liliambatana na kafara kadha wa kadha na utabiri juu ya maisha yetu pale nyumbani kwa mtu mmoja mmoja. Binafsi mganga alinisimulia kuhusu habari zangu za shule na jinsi nlivyokuwa mkorofi na mgomvi shuleni Kumwika Primary school.
Usiku huo mganga alitia timu kibabe nyumbani kwa yule jirani yetu na kufanya vitu kadha wa kadha bila kuonekana na akapotea kama watu wasiojulikana.

Mganga aliondoka siku iliyofuata kwa ahadi kuwa tutapata majibu ndani ya siku chache..

Baada ya wiki kama mbili, siku moja alfajiri sana mama yangu pamoja na kaka na dada zangu wawili waliamka na kwenda kufuata majani ya kuezekea nyumba eneo la kama kilomita tatu kutoka nyumbani. Asubuhi sana mimi na baba tukaenda kulima kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe pale pale jirani na nyumbani. Eneo tulilokuwa tunalima lilikuwa ni kwenye mpaka kabisa wa eneo letu na eneo la yule jirani yetu. Kitu cha ajabu ni kwamba ng'ombe walikuwa hawafiki mwisho wa shamba, walikuwa kama wanaogopa hivi na wakikaribia mwisho wanakimbia kama wameona kitu cha kutisha. Mara ghafla tukasikia mlio mkali sana kutoka vichakani jirani kabisa na pale tulipokuwa tunalima na ni jirani na makazi ya mke mdogo wa yule jirani yetu. Kufumba na kufumbua tukaona tembo mkubwa na mkonga wake akitoka mle vichakani na kuondoka kwa kasi kelekea Serengeti porini.

NINI KILIKUWA KIMETOKEA?
Ni kwamba kuamkia siku ile, yule jirani yetu alilala kwa mke wake mkubwa na kwa sababu mifugo yake ilikuwa inalala kwa mke wake mdogo ambaye ndiye alikuwa anaishi karibu sana na nyumbani kwetu, ilibidi asubuhi sana jamaa awahi kwa mke mdogo apige zake bangi (alikuwa mvutaji wa bangi ya kiko) na kufunga ng'ombe kwa ajili ya kwenda shamba kulima. Alipofika nyumbani aligonga mlango na kumsisitiza bi mdogo amfungulie mlango maana ana kiu ya jani sana na asichelewe shambani. Yule bi mdogo alikasirika sana kuamshwa mapema vile kwa sababu tu eti jamaa anataka kula mmea. Akamjibu kwa jeuri kuwa ''Kwani huko ulikotoka hakuna bangi?, mi sifungui mlango alfajiri yote hii".
Jamaa kwa hasira akaondoka kwenda kichakani kukata (alikuwa na sime yake) fimbo ama mjeledi ama kiboko kwa ajili ya kuja kumshikisha adabu yule mwanamke. Akamuahidi kuwa anarudi na atapata tabu sana. Inasemekana kuwa jamaa alipofika kule vichakani alijisikia kama anahitaji kuachia mzigo almaarufu kama kujisaidia, na alipochuchumaa kukata gogo ghafla bin vuu alitokea tembo mbele yake na ndipo jamaa aliposimama kwa taharuki. Yule tembo alim-mwaga utumbo baada ya kumpiga na jino lake maeneo ya mbele. Kama kawaida tembo huwa ni mstaarabu, alikata majani kadhaa akamfunika na kukojoa juu yake kisha akatoa mlio ule tuliousikia kama taarifa kuwa kazi imeisha. Tembo akachikichia serengeti akipita vijiji kadha wa kadha huku nyuma akiacha msiba mzito kitongojini na kwenye familia ya yule ndugu. Tembo hakusababisha madhara zaidi katika safari yake ya kuelekea porini..

Kama unaaminishwa na sayansi kuwa uchawi sio real, endelea tu mpaka utakapopigiwa show kali ya kibabe na wazee wa kilingeni..

Dunamist
duuuhh mkuu, hata mjin tembo anaweza kufika??!

*I shall kindly Knee to leave my Pride*
 
Hazithibitishi chochote na kama ilivyo kawaida ya story za uchawi zote huwa ni hearsay, kama hiyo number moja, inawezekana huyo mzee mgeni kijijini, kama nyie, aliambiwa kwamba huyo mzee wa hapo ni mchawi sana.

Hiyo number mbili labda mwizi ana ustahimilivu mkubwa wa maumivu kama walivyo wezi wengi au pengine mwizi aliumizwa na magongo hayo mabua yalikuja kukamilisha kazi tu au labda kuna more into the story ambayo wewe kwa kujua au kutojua hukuona/hujaandika ukizingatia unasema mlikua mnageuza shingo kwa kuogopa kuona kipigo.

Story za kusadikika za uchawi zina trait moja sawia; zote huwa ni story za hearsay na hazithibitiki hata siku moja.
Pengine uko sahihi mkuu siwezi kukupinga. Ila uzuri nimejitahidi sana kuelezea kwa kadri nilivyoweza kwenye post hiyo. Bahati nzuri nimeishi kotekote mjini na kijijini, ushuani na kwenye mbavu za mbwa. Hivyo nina uzoefu kwenye maeneo yote hayo.
 
Kweli uchawi upo
mimi mdogo wangu wa kike aliingia ndani kulala yeye na kabinti kengine walikuwa wanalala chumba kimoja..
Tulikuwa wengi hapo nje tunapiga stori baada ya kumaliza kula chakula cha usiku, wazazi pia walikuwepo hapo nje.
Ajabu dada yangu mkubwa kuingia ndani ya chumba kile alikuwa na shida HAKUMUONA mdogo wetu huyo kitandani ila mwenzie alikuwepo.. ndio akaleta taarifa huku nje na kuuliza kama amelala chumba kingine mule ndani..
Tukajua mzaha ktk kumtafuta kweli akawa haonekani.. Mwenzie akaamka akasema wameingia wote ndani na kweli kwa macho yetu wote tulishuhudia wakienda ndani kulala.
Tukatafuta vyumba vyote hadi uvunguni hakuna mtu.. Akina mama wakaanza kulia wakijua mtoto amepotea.. Ikabidi tumfate balozi akaja tukatafuta nae bila mafanikio.
Wakafatwa ndugu wa karibu usiku huo wakaja tukamulika pande zote huko nje hakuna..
BASI jamaa 1 akatoa wazo la kufungua chumba cha kuku na bata ambacho huwa kinawekwa kufuri mapema tu.. AJABU akakutwa mtoto huyo ameinama style ya kuswali kiislam.
 
Wengine tunaamini uchawi wa mabarabara, mifereji iliyofunikwa, treni zinazoenda sambamba na UDA, huduma za afya bora, ustawi wa jamii kwa yatima, wazee na watoto, elimu bora, kazi na uchumi bora, huu ndio uchawi..
 
Tulipomwamsha akawa amezubaa kama alikuwa mbali tena usingizini...
Watu hatukuamini sababu kile chumba nicha nje tena cha mifugo na kilikuwa na kufuri . Lakini ndimo tulifungua tukamkuta ktk hali ya ajabu sana.
Kuna maoni kabla mtoto hajapatika eti tukaripoti polisi usiku huo huku wengine tuendelee kumtafuta.. Hakuna ambae alikuwa anahitaji kulala bila kumpata mtoto huyo kwani tuliamini tukilala bila kumpata basi hatutamuona tena na kama ni nguvu za giza basi watakuwa wamefanikiwa kirahisi.
Baada ya kumpata tukalala kukacha .. Ndipo Kesho yake watu wakaja kwa wingi kumjulia hali anaendeleaje na yukoje.. kwa kweli hakuwa nafuraha alikuwa amepooza sana sio mchangamfu.
Baadae wazazi walienda kwa mganga IKAJULIKANA kuna mzee mmoja wa tena ndugu alitaka KUMBEBA KICHAWI mtoto yule.
Basi toka hapo mtoto yule alianza kuugua.. alisumbuka sana kwa waganga miaka mingi hadi ilifikia akawa anakimbia kama anataka kuwa mwehu.. mara majini.. mara azirai.
 
Aliteseka sana hadi kuna madarasa aliyasoma mara mbili kutokana na kuchukua muda mwingi kwa waganga wa kienyeji.. Alipofika secondary hali yake pia ilikuwa ya kubadilika mara iwe sawa mara awe mgonjwa tena.
Kuna muda alikuwa hawezi kuona maandishi ubaoni , akapimwa na akapewa miwani ya kusomea.. Anadai kuna muda alikuwa anawaona hadi wachawi wanaokuja usiku kuwanga.. Tena anawataja kwa majina na walikuwa wanamuogopa sjui tu walimfanyaje mtoto huyo akawa anawaongelesha kwa kuwatukana usiku huo hadi mnashangaa.
Kwa ufupi alipata mganga mwingine akiwa amemaliza elimu ya secondary ndie alimsaidia akapona kabisa hadi leo.. Yupo ni mzima japo hakupata post nzuri kwenye mtihani wake wa kidato cha 4.
 
Back
Top Bottom