Mkuu nilikua sijsoma story yako nikiamini, kama story zingine zote za uchawi, huwa zinaacha loopholes and surely enough yako pia was no exception to this. Kwanza ni kawaida kwa waganga wa jadi kusema mbaya wako ni jirani yako au ndugu yako kama hujui hili hadi leo basi siwezi kushangaa kwanini unaamini uchawi upo.
Pili, kuuwawa na tembo au wanyama maeneo ya karibu na mbugani ni jambo la kawaida, sawa na mtu wa mjini kugongwa na gari. Nadiriki kusema ilikua coincidence tu na pengine huyo mtu asingekufa mganga angekuja na sababu zingine kama kawaida yao.
Nitakupa kisa kidogo, Juma alimwambia Obedi leo usiku utanikoma baada ya kukorofishana, Obedi usiku ule aligongwa na gari na kufariki pale pale unadhani Juma ni mchawi? Kwanini isiwe conicidence? Unaweza muongelea mtu mabaya bila kumaanisha na jambo baya likampata ila hiyo sio ithibati ya kuonyesha wewe ni mchawi.
Hizi ndo kasoro za story za uchawi, ni story za hearsay na mara nyingi zina loopholes ambazo watu hukimbilia kusema ni uchawi wakati zinaweza kujibika kwa njia zingine.
HAKUNA UCHAWI.