Hakuna uchawi. Ni imani za watu zimejenga hofu kuwa kuna kitu kinaitwa uchawi. Siamini uchawi.
Nakubaliana na wewe 100%Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.
Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni mema/ mazuri.
Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.
Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni wema/ uzuri.
vipi na wale wazee wanaocheza bao kuanzia asubuhi mpaka jioni lakini huwaoni wakienda kujisaidia, ila sasa mtazamaji anayeangalia bao utaona kila baada ya muda anaenda haja kubwa au ndogo lakini wale wazee hawanyanyuki wanaendelea kucheza tu kumbe wanakupasia mizigo yao! Mimi ishanipata miaka ya nyuma pande za mwananyamala nilikuwa nazuga kwenye bao wakati namlia mingo dem flani, wewee si mchezo kila wakati wazee wananisakizia kupeleka mizigo yao, bahati kulikuwa na bar jirani nikawa najisevia kwenye toilet yao nilipokuja kushtukia mchezo washantesa sanaa! nikawa sikai tena nikawaacha wasakiziane mizigo yao wenyewe kwa wenyewe!
Hawadanganyi maana hata mie nimekaa na kushuhudia sana ndumba na mambo kama hayo.
Nakumbuka shule ya msingi niliyokua nasoma(jina nalihifadhi) ipo karibu kabisa na baharini, pembezoni mwa barabara ya kwenda Mombasa. Wakati wa usiku ilikua inageuka kuwa treni...sasa ole wako upande,unaenda okotwa huko Lamu umechizika.
Mwalimu gfsonwin sasa kwenye mpira enzi zile za African Sports na Coastal Union,ilikuwa balaa,kuna mechi moja mwaka 89,Yasini Napili alipiga shuti mpira umempita kipa halafu ukapasuka vipande viwili na vile vipande havikuvuka goal line kuamanisha kwamba sio goli,na mechi hiyo hiyo kulikuwa kuna babu alikuwa amepelekwa ufukweni mwa bahari wakati maji yamekupwa, wakawa kama wamemzika kwa kusimama isipokuwa kichwa na shingo ,baada ya mpira kwisha matokeo yalikuwa nunge, basi watu wakasahau kwenda kumfukua kule ufukweni mpaka maji yakawa yanajaa bahati nzuri wavuvi wakasikaa kelele alizokuwa anapiga ndio wakaenda eneo la tukio ndio wakamfukua.Nilikuwa kambini usiku kabla ya mechi hii basi vitu vingine siwezi simulia kwani huwezi amini mambo yaliyokuwa yanafanyika.Mungu alinisaidia niliacha mpira msimu uliofuata kwani nilikuwa nimechaguliwa kwenda form five toka Usagara Secondary,oops isije id ika.........Sarikoki sikjui kama ulikuwa kishazaliwa..... ha ha ha
mie sijasema tanga ndo kumejaa ila tu nimesema nloshuhudia tanga. BTW si ni kweli hasa chumba geni??
sijui wachezaji wa mpira wa miguu wa sasa. lakini wale wa miaka 1975 - 1985 cha moto walikiona.
masuala ya kulala makaburini, kuogeshwa maji ya ajabu ajabu tulikuwa tukisema "maji ya maiti" n.k ndio ilikuwa mpango mzima. ukikataa na mechi hupangwi!