Uchawà kazi kweli kweli.

Uchawà kazi kweli kweli.

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
52,093
Reaction score
101,981
Hivi ni lazima Mkristo kuvaa mavazi ya kiislam katika msiba wa Muislamu

Alternatively , waislamu mbona huwa hawavai misalaba wanapokwenda kuwafariji wakristo?
 

Attachments

  • IMG-20260911-WA0000.jpg
    IMG-20260911-WA0000.jpg
    143.1 KB · Views: 15
  • IMG-20260910-WA0047.jpg
    IMG-20260910-WA0047.jpg
    73 KB · Views: 12
Yaani katika vitu viongozi wa kikristo wanakwama ni huu upuuzi wa kuvaa mavazi ya kiisilamu kwenye hafla za waisilamu. Huwezi kuona muisilamu yoyote anavaa msalaba hata baba mtakafifu aje. Nikimuona tu kiongozi wa kikristo anavaa mavazi ya kiisilamu namdharau sana.
 
Yaani katika vitu viongozi wa kikristo wanakwama ni huu upuuzi wa kuvaa mavazi ya kiisilamu kwenye hafla za waisilamu. Huwezi kuona muisilamu yoyote anavaa msalaba hata baba mtakafifu aje. Nikimuona tu kiongozi wa kikristo anavaa mavazi ya kiisilamu namdharau sana.
Mkuu Tindo kanzu sio vazi la Waislam pekeyao. Kanzu ni vazi la heshima kwa watu wote na wakati wote kama ilivyo suti

Wahaya na Waganda kwa mfano kanzu huvaliwa na watu wote bila kujali dini zao likiwa ni vazi rasmi la heshima na taadhima kwao ambapo hata katika maharusi na misiba ya watu wa dini zote vazi hilo hutumika

Nigeria na baadhi ya nchi Afrika Magjaribi kanzu ni vazi la taifa katika nchi ambayo kuna zaidi ya Wakristo milion mia moja

Katika historia ya kale kanzu imetumika kwa watu wa imani zote na ipo katika maandiko karibia ya dini zote

Kwa hapa Tanzania kanzu pia imekua kama vazi la kitamaduni kwa watu wa Pwani ikiwemo Zanzibar. Kwa hiyo kwa maoni yangu mtu akivaa vazi hilo haina maana ameikana imani yake au amejipendekeza

Hilo ni vazi rasmi la heshima na la kitamaduni kwa waswahili na miongoni mwa mavazi yanayotambulika na kuruhusiwa ndani ya ukumbi wa Bunge pia

Tujaribu kuwa na fikra za kutuunganisha kama Taifa na jamii moja ya Watanzania kuliko kutugawa kwa ajili ya mavazi tu! Kwa hili tusichochee uasi wala tusikinukishe(I'm joking😀)
 
Hivi ni lazima Mkristo kuvaa mavazi ya kiislam katika msiba wa Muislamu

Alternatively , waislamu mbona huwa hawavai misalaba wanapokwenda kuwafariji wakristo?
Kanzu sio vazi la kiislamu. Ni vazi la kitamaduni. Kama ilivyo mtandio.

Kama ni hivyo, basi suti ni vazi la kikristu. Kwa hiyo ni kosa waislamu kuvaa suti wanapoenda kumfariji Mkristu.

Siku mkristu akibeba tasbih kwenda kutoa pole ndio tutamshangaa. Kama ambavyo tutamshangaa muislamu atakaye fanya hivyo huku kavaa msalaba.

Amandla...
 
Mkuu Tindo kanzu sio vazi la Waislam pekeyao. Kanzu ni vazi la heshima kwa watu wote na wakati wote kama ilivyo suti

Wahaya na Waganda kwa mfano kanzu huvaliwa na watu wote bila kujali dini zao likiwa ni vazi rasmi la heshima na taadhima kwao ambapo hata katika maharusi na misiba ya watu wa dini zote vazi hilo hutumika

Nigeria na baadhi ya nchi Afrika Magjaribi kanzu ni vazi la taifa katika nchi ambayo kuna zaidi ya Wakristo milion mia moja

Katika historia ya kale kanzu imetumika kwa watu wa imani zote na ipo katika maandiko karibia ya dini zote

Kwa hapa Tanzania kanzu pia imekua kama vazi la kitamaduni kwa watu wa Pwani ikiwemo Zanzibar. Kwa hiyo kwa maoni yangu mtu akivaa vazi hilo haina maana ameikana imani yake au amejipendekeza

Hilo ni vazi rasmi la heshima na la kitamaduni kwa waswahili na miongoni mwa mavazi yanayotambulika na kuruhusiwa ndani ya ukumbi wa Bunge pia

Tujaribu kuwa na fikra za kutuunganisha kama Taifa na jamii moja ya Watanzania kuliko kutugawa kwa ajili ya mavazi tu! Kwa hili tusichochee uasi wala tusikinukishe(I'm joking😀)
Waganda na wahaya waliiga vazi kutoka pwani kwa waarabu walioingia bara kufanya biashara.
West Africa walifanya modification ya kanzu ya waislamu. Suit ni vazi la Ulaya, Africans have adopted it likewise
 
Kanzu sio vazi la kiislamu. Ni vazi la kitamaduni. Kama ilivyo mtandio.

Kama ni hivyo, basi suti ni vazi la kikristu. Kwa hiyo ni kosa waislamu kuvaa suti wanapoenda kumfariji Mkristu.

Siku mkristu akibeba tasbih kwenda kutoa pole ndio tutamshangaa. Kama ambavyo tutamshangaa muislamu atakaye fanya hivyo huku kavaa msalaba.

Amandla...

..Kanzu ni vazi la Kitamaduni, lakini pia ni vazi la Waislamu.

..majority ya Waislamu huvaa kanzu mahsusi kwa ajili ya ibada na sikukuu za dini yao?

..hao wanaovaa kanzu kwenda kumpa pole Mama Abduli hudhani kama wanafanya hivyo kwa kuiga uvaaji wa Waislamu?

..Mama Abdul angekuwa Mkristo unadhani jamaa zetu wangevaa kanzu na kwenda kumpa pole?
 
Mkuu Tindo kanzu sio vazi la Waislam pekeyao. Kanzu ni vazi la heshima kwa watu wote na wakati wote kama ilivyo suti

Wahaya na Waganda kwa mfano kanzu huvaliwa na watu wote bila kujali dini zao likiwa ni vazi rasmi la heshima na taadhima kwao ambapo hata katika maharusi na misiba ya watu wa dini zote vazi hilo hutumika

Nigeria na baadhi ya nchi Afrika Magjaribi kanzu ni vazi la taifa katika nchi ambayo kuna zaidi ya Wakristo milion mia moja

Katika historia ya kale kanzu imetumika kwa watu wa imani zote na ipo katika maandiko karibia ya dini zote

Kwa hapa Tanzania kanzu pia imekua kama vazi la kitamaduni kwa watu wa Pwani ikiwemo Zanzibar. Kwa hiyo kwa maoni yangu mtu akivaa vazi hilo haina maana ameikana imani yake au amejipendekeza

Hilo ni vazi rasmi la heshima na la kitamaduni kwa waswahili na miongoni mwa mavazi yanayotambulika na kuruhusiwa ndani ya ukumbi wa Bunge pia

Tujaribu kuwa na fikra za kutuunganisha kama Taifa na jamii moja ya Watanzania kuliko kutugawa kwa ajili ya mavazi tu! Kwa hili tusichochee uasi wala tusikinukishe(I'm joking😀)
Mavazi huwa yanatafsiriwa hata kwa mazingira boss. Mazingira ya Tanzania kanzu ni vazi la waisilamu, na hata hawa wakristo wanaovaa hapa ni katika hafla za waisilamu, huu ni ukweli usioacha shaka. Hawa wakristo wanaovaa kanzu lengo lao ni kuwa impress waisilamu, na wala hawavai kama vazi la heshima. Sipingi maelezo yako maana una hoja za msingi, lakini uhalisia unakataa.

Kama huamini nisemacho mwambie mkristo avae kanzu aingie nayo kanisani kama hajazua taharuki. Suit ni vazi la heshima sana, lakini nikikukuta umevaa wakati unaogelea ama unalima Shambani, nitajua una walakini.
 
..Kanzu ni vazi la Kitamaduni, lakini pia ni vazi la Waislamu.
Wahaya wanavaa kanzu kama sehemu ya utamaduni wao. Watu wengi wa Middle East wanavaa kanzu bila kujali dini zao. Hata Yesu alivaa kanzu. Waislamu wetu wengi wanachanganya utamaduni wa kiarabu na uislamu. Siku hizi wanavaa mpaka Keffiyeh kama ishara ya uislamu.
..majority ya Waislamu huvaa kanzu mahsusi kwa ajili ya ibada na sikukuu za dini yao?
Majority misikitini wanakuwa wanavaa nguo za kawaida tu.
..hao wanaovaa kanzu kwenda kumpa pole Mama Abduli hudhani kama wanafanya hivyo kwa kuiga uvaaji wa Waislamu?
Wanavaa kuiga utamaduni wa wazanzibari. Na baadhi kweli wanavaa kwa sababu mfiwa ni muislamu. Wanawake wengi wanavaa mitandio wakienda kutoa pole kwa waislamu wenzao. Ni ishara ya heshima tu na sio kosa. Hata Nyerere alivaa sana Balaghashia ambao wengi waliiona kama kofia ya waislamu.
..Mama Abdul angekuwa Mkristo unadhani jamaa zetu wangevaa kanzu na kwenda kumpa pole?
Wasingevaa maana pasingekuwa na haja. Jamii yetu inaishi kwa heshimu tamaduni za wenzetu. Ndio maana wakristu wakitaka kuchinja wanamtafuta Abdallah awachinjie. Kufanya hivyo sio uchawa kwa waislamu bali heshima.

Hivi karibuni nimewaona Boni na Sugu wakiwa na virasta. Nao tuseme wanafanya hivyo kwa sababu ya uchawa?

Amandla...
 
Back
Top Bottom