Uchawà kazi kweli kweli.

Uchawà kazi kweli kweli.

Ni hali halisi. Kanzu ni nguo iliyokuwa na inayoendelea kuvaliwa sana Middle East na North Africa. Na huko kote wakristu na waislamu wakiarabu wanavaa kanzu. Wayahudi hawavai kwa sababu ni wahamiaji na wamerudi na tamaduni za walikotoka.

Mtanzania wa kawaida ana amini "Salaam Aleykhum" ni salamu ya kiislamu wakati ni " amani iwe kwako " kwa kiarabu.

Hata kwenye harusi za kihaya, wageni wengi hawavai kanzu. Ni vazi la kitamaduni lakini halitumiki sana.

Inawezekana. Lakini wanakosea kama vile siku hizi wanavyosalimia " As salam Aleykhum" pamoja na "Bwana Asifiwe" ambayo nayo inachukuliwa kama salam ya kikristu. Kwangu mimi sioni tatizo kwa wao kuvaa kanzu hata kama ni kwa ajili ya kuheshimu imani yake. Ni heshima tu, sio uchawa.

Ubaya wa hili jambo ni kuwa watu wanataka kuhusisha Mbowe kuvaa kanzu na unafik. Hiyo ni quite low.

Amandla....

..kusema Mbowe ni mnafiki kwasababu amevaa kanzu sio sawa.

..lakini hatutakosea tukisema Mbowe amevaa kanzu kwa nia ya kuheshimu dini ya KIISLAMU kwasababu kanzu ni vazi la dini hiyo.
 
Kanzu sio vazi la kiislamu wala kofia ,kama unabisha kaangalie wachaga zamani walikuwa wakivaa vikofia hivyo .

kanzu ni vazi la kihistoria sio kwa waislamu pekee.
 
Yaani katika vitu viongozi wa kikristo wanakwama ni huu upuuzi wa kuvaa mavazi ya kiisilamu kwenye hafla za waisilamu. Huwezi kuona muisilamu yoyote anavaa msalaba hata baba mtakafifu aje. Nikimuona tu kiongozi wa kikristo anavaa mavazi ya kiisilamu namdharau sana.
Hayo si mavazi ya kiislamu mzee.
Muache uvivu wa kusoma vitu vidogo kama historia ya mavazi.
 
..kusema Mbowe ni mnafiki kwasababu amevaa kanzu sio sawa.

..lakini hatutakosea tukisema Mbowe amevaa kanzu kwa nia ya kuheshimu dini ya KIISLAMU kwasababu kanzu ni vazi la dini hiyo.
Futa hili wazo la kishamba na dalili ya kukosa uelewa wa mambo
 
Mh! Uchawa na ushoga quite unrelated! Uchawa ni kujitoa akili, ufahamu, weledi pamoja na kuujua ukweli as long as unanufaika na ushenzi unaoufanya bila kujali athali kwa jamii inayokuzunguka au jamii yote.

Ushoga you do not harm anybody only unafanya matendo ya ngono kinyume na nature na amri ya Mungu ( kwa wanao amini uwepo wa MUNGU)..... something of that nature anyway..
Kwamba unaenda kuhani msiba na waandishi wa habar na unampigia magoti mfiwa? Ndiyo
 
Hivi ni lazima Mkristo kuvaa mavazi ya kiislam katika msiba wa Muislamu

Alternatively , waislamu mbona huwa hawavai misalaba wanapokwenda kuwafariji wakristo?
Ninayeandika hapa ni mkristo...

Mzee baba kanzu ni vazi la utamaduni wa Kiarabu ambalo waislamu wamerithi tu kwa sababu ya sitiri ya mwili, sio kwamba ni vazi la waislamu...

Ukitazama kuna jamii tofauti za waislamu lakini si wote wenye kuvaa kanzu., tazama waislamu wa Afghanstan, Iran, Iraq, Pakistan, zile nchi zilizomeguka toka USSR wote hao hawavai kanzu...

Kitu pekee kilichonishangaza kwa baadhi ya walioemda kuhani msiba ni suala la kupiga magoti, sijajua ni suala la utamaduni (sijui wa wapi), uoga, kuigana !!!
 
Mkuu ukiingia kanisani umevaa kanzu na barakhashea itaonekana umevaa vazi la heshima au la kiisilamu?
Hao waumini wa kikristu japo nao ni wakristu kwa majina watakuwa wanasumbuliwa na ukosefu wa taarifa sahihi au hawana exposure.

Kuna siku ibadani Padri mmoja alianza kusalisha sala ya Baba yetu uliye mbinguni kwa lugha ya kiarabuni na sikuona mtu akisema Padri anasalisha kiislamu.
 
Fine, utashi wa kijinga. Mbona wao hawana habari na imani yako, why wewe kiherehere? Uhayawani tu.
Bashungwa, one can say for sure, he is looking for a comeback!

UCHAWA
Na huyu pia ni chama?!
👇👇👇👇
 

Attachments

  • images(102).jpg
    images(102).jpg
    51.8 KB · Views: 1
Hao waumini wa kikristu japo nao ni wakristu kwa majina watakuwa wanasumbuliwa na ukosefu wa taarifa sahihi au hawana exposure.

Kuna siku ibadani Padri mmoja alianza kusalisha sala ya Baba yetu uliye mbinguni kwa lugha ya kiarabuni na sikuona mtu akisema Padri anasalisha kiislamu.
Mkuu naona umeanza kunipanga. Padre asalishe kwa lugha ya kiarabu?
 
Mkuu naona umeanza kunipanga. Padre asalishe kwa lugha ya kiarabu?
Umesoma vizuri nilichokiandika kweli?

Kwa kukuongezea tu , huyo Padri alikuwa anawatoa waumini wake tongotongo kwamba waache kuhusianisha uislamu na kiarabu kama ambavyo wengi wenu mnafanya. Akijitolea yeye mfano kwa kuendesha sehemu ya Ibada kwa lugha ya kiarabu.
Miaka ya zamani kwenye Makanisa ya Kikatoliki kulikuwa na matumizi makubwa sana ya lugha ya kilatini kwenye ibada kiasi cha baadhi ya waumini wenye uelewa mdogo kuanza kuhusianisha kilatini na lugha ya mbinguni
 
Ninayeandika hapa ni mkristo...

Mzee baba kanzu ni vazi la utamaduni wa Kiarabu ambalo waislamu wamerithi tu kwa sababu ya sitiri ya mwili, sio kwamba ni vazi la waislamu...

Ukitazama kuna jamii tofauti za waislamu lakini si wote wenye kuvaa kanzu., tazama waislamu wa Afghanstan, Iran, Iraq, Pakistan, zile nchi zilizomeguka toka USSR wote hao hawavai kanzu...

Kitu pekee kilichonishangaza kwa baadhi ya walioemda kuhani msiba ni suala la kupiga magoti, sijajua ni suala la utamaduni (sijui wa wapi), uoga, kuigana !!!


..uhalisia wa hapa kwetu ukoje?

..uhalisia na mapokeo yetu Watz Kanzu ni vazi la Kiislamu.
 
Ninayeandika hapa ni mkristo...

Mzee baba kanzu ni vazi la utamaduni wa Kiarabu ambalo waislamu wamerithi tu kwa sababu ya sitiri ya mwili, sio kwamba ni vazi la waislamu...

Ukitazama kuna jamii tofauti za waislamu lakini si wote wenye kuvaa kanzu., tazama waislamu wa Afghanstan, Iran, Iraq, Pakistan, zile nchi zilizomeguka toka USSR wote hao hawavai kanzu...

Kitu pekee kilichonishangaza kwa baadhi ya walioemda kuhani msiba ni suala la kupiga magoti, sijajua ni suala la utamaduni (sijui wa wapi), uoga, kuigana !!!
Hilo la kupiga magoti sio zuri. Tumekatazwa kumsujudia binadamu mwingine ingawa kuna kabila zinataka wanawake wawasujudie wanaume. Mimi hata hilo la mwanamke kumpigia magoti mwanaume ( dada mkubwa anampigia got mdogo wake wa kiume, mke anampigia got mume wake n.k.) sikubaliani nalo. Hili la mwanaume kumpigia goti binadamu mwenzake ( bila kujali jinsia) nalo sikubaliani nalo.

Ila hamna kinacho nishangaza siku hizi. Wanaume wanajigalagalaza kama ishara ya heshima. Wanaume wanakuna nazi kutafuta kura. Hamna kitu kitawashinda kufanya kwenye kutafuta cheo ikiwa pamoja na kumuita binadamu mwenzao Mungu. Kwa kweli inasikitisha.

Amandla....
 
Kazu sio vazi la kiislamu wala kofia ,kama unabisha kaangalie wachaga zamani walikuwa wakivaa vikofia hivyo .

kanzu ni vazi la kihistoria sio kwa waislamu pekee.

..usiangalie zamani kanzu ilikuwa vazi la kila nani.

..mambo huenda yakibadilika. Na leo hii ktk zama hizi tunazoishi Kanzu ni vazi la Waislamu.

..Na kanzu kuwa vazi la Waislamu si jambo baya. Kwanza ni vazi lenye staha.
 
Hivi ni lazima Mkristo kuvaa mavazi ya kiislam katika msiba wa Muislamu

Alternatively , waislamu mbona huwa hawavai misalaba wanapokwenda kuwafariji wakristo?
Ni heshima tu. Hata mimi nikienda kwenye shughuli za wenzangu waislamu wakinialika nakula zangu kanzu. Nna kanzu zangu tatu maridadi toka kanzu mall kwa shughuli
 
Hivi ni lazima Mkristo kuvaa mavazi ya kiislam katika msiba wa Muislamu

Alternatively , waislamu mbona huwa hawavai misalaba wanapokwenda kuwafariji wakristo?
Duh,
Njaa mbaya aisee,
Hii kasumba ya dume kupigia magoti mmama ni ya wapi hii??
 
Kiuhalisia hakuna vazi la kiislamu. Hizo kanzu na kofia ni mavazi ya kawaida sana na hayana nasaba na dini yoyote ile. Kwakuwa imezoeleka jamii za kiarabu na sehemu za Asia kuvaa hivyo ambapo ndipo chimbuko la uislamu basi wengi huchanganya mavazi hayo na dini hiyo.
Tujielimishe kuepusha kuchanganya habari
 
..uhalisia wa hapa kwetu ukoje?

..uhalisia na mapokeo yetu Watz Kanzu ni vazi la Kiislamu.

Mapokeo ya watanzania ni sahihi kwa sababu ya hulka yetu kutokuishughulisha sana akili lakini uhalisia si hivyo, dhana ya kuhusisha vazi na dini ni kutokana na Uislamu kusisitiza sitiri katika mavazi na vazi la kanzu ni kielelezo chepesi cha kutimiza huo msisitizo ...

Vazi la kanzu linaweza kuwa vazi la kitamaduni, vazi la watanzania wenye asili ya kiarabu pia...

Ndugu zetu wa Kagera kanzu ni vazi la kitamaduni, Rwanda pia wanaume wanavaa kanzu kama vazi la kiitamaduni n.k...

Screenshot_20260912_184905_Instagram.jpg
 
Ukiwaona kwenye familia zao, wanakuwa wababe, sasa watu wa dizain watakubali katiba mpya ngumu sana kukubali
 
Back
Top Bottom