MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 710
Hodi hodi naingia jamvini, malenga mnipokee
Ujumbe wangu kumpelekea, meneja uchaguzi CCM
Umfikie aliko, akiomboleza chama chake kushindwa uchaguzi
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Uchaguzi ndivyo ulivyo, kuna mshindi na mshindwa
CCM mlijiamini, tena mno kupita kiasi
Badala ya kutangaza sera, mkawatumia wajeshi
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Mkawatisha wananchi, kwa mitutu na mabomu
Hofu kuu ilitanda, Jiji la Arusha likazizima
Wakazi wakakimbizwa, vijana kukamatwa
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Ikawadia siku ya uchaguzi, wakapiga wachache mno
Ukweli ukabainika, wengi waliopiga ni wana-CCM
Wana-CCM hao wakaamua, CHADEMA kuichagua
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Kumbe mlipowapiga CHADEMA, wana-CCM nao walichoka
Ahadi kedekede mlitoa, chache sana mlitimiza
Hali ikawa mbaya, vijana kukosa ajira
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Mkatangaza mikopo, kwa akinamama na vijana
Kumbe mliwaandaa, maswahiba zenu kuwapa
Wananchi wakabaini, mkenge kuingizwa
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Tamati najongea, malenga nahitimisha
Najua hamu bado mnayo, shairi hili kulisoma
Japokuwa vina halina, bado laitwa shairi
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo
Natumai mmejifunza, wananchi kutowadharau
Mabomu kutowapiga, bure bilashi kuwaua
Mnapovunja haki zao, mwawatakia nini
Usiomboleze sana Mwigulu, uchaguzi ndivyo ulivyo