Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Chadema sio saizi ya ccm...hii ni level nyingine.Nape na ccm yako chaliii,chezea kingine sio chadema.
M4C forever...aibu kwa magamba.
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).


Yaani pamoja na Mwigulu kumtembeza kijana wa Igunga ili kupata huruma ya Wana Arusha hakufanikiwa kupata hata kata?
Nilijua toka mwanzo kwa kampeni zile sidhani kama watu watamuelewa kwanza alikuwa ana mdhalilisha kijana wa watu. Labda Iramba pekee ndio wangemuonea huruma lakini sio kwingineko.
2015 ngoja tume ya uchaguzi oboreshe daftari la wapiga kura. Hela tutachukua za CCM lakini kura Chadema.
"We need change! whether good or bad"
 
Ushauri wa bure: Anza kujifunza kufunga mdomo maana kelele zako zinakudhalilisha zaidi toka ulipoanza na nyimbo za kuvua mapacha watatu magamba ukashindwa ukageukia mahubiri machafu ya udini, ukabila na ukanda. Madhara yake hayo yote yataleta mpasuko mkubwa sana ndani ya chama chako kwani UVCCM Bagamoyo walishatangaza kuwa rais 2015 CCM hatatoka kanda ya kaskazini. Huo sio ukanda? Badala ya kuangalia uwezo wa mtu mnaangalia anakotoka, jinsia na dini yake. Madhara ya mahubiri yako hayo utayaona zaidi ndani ya CCM kadiri tunavyelekea 2015. Sasa watu wa Mbeya wameanza kuhoji kuhusu madhara yanayowapata wao kwamba kunani? (Mwakyembe, Mwandosya, Ulimboka, Kibanda nk) Hawa nao ni wachagga? Haya ni matunda ya wahubiri kama wewe. Pamoja na onyo lako Lowassa anachanja mbuga na kampeni za urais 2015. Huna la kumfanya kwani hata bosi wako anamsapoti. Huwa unakuwa na busara zaidi ukinyamaza kuliko ukianza kupayuka mamabo ambayo huwezi kutekeleza. Bora hili la Arusha umeongea ki utu uzima. Nadhani umeanza kukua. Ila hilo la mahubiri yako ya udini, ukabila na ukanda nitaendelea kukusutu kila wakati kwani umepanda mbegu mbaya sana katika nchi yetu. Kwa akili yako ulidhani unaibomoa CHADEMA bila kujua kuwa ndiyo ulikuwa unaiimarisha zaidi kwani wananchi wamekupuuza. Sawa na mwenzako Mwigulu anahangaika na kutengeneza kesi za ugaidi lakini hazimsaidii badala yake CHADEMA inazidi kupaa. Wote wawili badala ya kufanya kazi za CCM mmekuwa busy na kuitangaza CHADEMA na Slaa. Matokeo yake CCM inazidi kupotea katika ramani. Baba wa Taifa Mwl Nyerere alisema dalili za mwanasiasa aliyefilisika ni kujitambulisha kwa udini, ukabila, ukanda na hata ujinsia. Kumbe alikuwa anakuzungumzia wewe na CCM yako. Sasa Lowassa anautaka uraisi kupitia CCM na anatoka kanda ya kaskazini na huko ndiko wewe unakokuchukia. Utafanyaje? Uwezo wa kumsimamisha huna, uwezo wa kumwadhibu kama ulivyosema huna. Huoni wakati umefika sasa wa wewe kufunga mdomo? Katika sekretarieti hii mpya mwenye nafuu ni Kinana peke yake. Wewe na Mwigulu ni wrong persons at the right place. Sekretarieti ya Makamba ilikuwa na nafuu mara mia kwani ilikuwa na watu wazima sio ninyi mnaoshughulika na ukabila, udini, ukanda na kutengeza kesi za ugaidi! Mnabahati mwenyekiti wenu naye ni kama mbwa kibogoyo!
 
Nape Kule ZNZ 1995, 2000, 2005 na 2010 zote mmeshindwa U Rais. Pia Jimbo la Mtoni nimemtumia Mpaka risasi. Pia, Igunga mabavu yametumika kuhakikisha ushindi lazima
 
Kwa hali inanipa iman kuwa CDM 2015 inaingia ikulu bila tabu, ama kweli sasa watz tumechoka na magamba!!!!
 
Huyo mbona tushamshtukia kama ni mamluki wa cdm? ametumwa kuja kutupeleleza

Kuna siku nlisema....vijana wa ccm wakanishambulia sana.....nliwauliza ivi mnavyoshabiakia hao vijana....mmewascreen vipi kujua ni double agent....au kwa kuwa wanamtukana slaa na mbowe basi wanaichukia CDM.....CCM tumieni akili
 
Hapo kwenye RED hapo,sio huyu tu,hata Juliana Shonza na Mtela Mwampamba mnawaona kama watu muhimu lakini mnawakatisha tamaa makada wenu wengine hasa vijana,lakini kumbukeni kama hawa vijana MTEla na shonza mliweza kuwarubuni wanaweza kurubunika pia,sio watu wazuri sana,jitahidini kutumia makada wenu mliokuwa nao,naamini matokeo haya yameipaisha sana CDM na kuwashusha wale wanazi wa siasa za mauaji na chuki.
......................Kuna siku nlisema....vijana wa ccm wakanishambulia sana.....nliwauliza ivi mnavyoshabiakia hao vijana....mmewascreen vipi kujua ni double agent....au kwa kuwa wanamtukana slaa na mbowe basi wanaichukia CDM.....
 
Hata wakibadili safu, ngoma bado inogile. Kwa ile falsafa yako ya kujivunia gamba badala ya kujivua hamna chenu tena. Imani kwa wananchi utarudi pale tu mtakapowanyonga mafisadi wa EPA, meremeta, iptl, anben, Richmond/symbion, ttcl vs celtel, kagoda, n.k. Ama muwahukumu kama wahujumu uchumi na kufirisi mali zao zote. Raia wanaona matendo machafu ya watawala huku wao wakiishi kwa mlo mmoja. Na kwa jeuri yenu mmeamua kuwaongezea na kodi ya kichwa (sim card) huku mkishindwa kukusanya kodi kwenye resource kuu mfano madini, gas, utalii. Raia wanachukia kuona wanyama wanasafirishwa bioa mtu hata mmoja kuwajibika, huku maelfu ya tembo wakiuwawa mchana kweupe. Askari wetu wamebaki smart kwenye eneo moja tu la kupiga na kugandamiza democrasia huku wakiwaacha mafisadi wakitanua mitaani. Na hakika kwenu nyinyiem haya hayarekebishiki kwa kuwa hakuna aliyemsafi. Kwa maana nyingine anguko lenu halina pingamizi.

True 100%
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

Ujue wananchi waliowengi wanajua kuwa polisi wanatumwa na CCM kuwapiga raia, kwahiyo hilo jambo linazisha chuki baina serikali na wananchi.
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

graph ya ccm kukubalika vs muda ikoje?-ve au +ve?mkuu safina linazama hilo angalia usiwe wa mwisho kutoka huko chama la zamani
 
Kwa mara ya kwanza tokea kuumbwa kwa Binaadamu ndio CCM mnakubali kushindwa. Sasa anzeni kufunga virago 2014 na 2015 ndio tunamaliza

Ndugu zanguni kumbukeni nilishapost taarifa hapa jamvini kwamba,sasa hivi watanzania waliowengi wameshaichoka ccm,kwa hiyo kilichofuata sasa ni kama ilivyotokea kule Kenya,kwamba chaguzi zinazokuja watanzania watapiga kura kwa hasira kutokana na matendo ya watawala kwa kutumia vyombo vya Dola vibaya.siku za ccm zinahesabika matendo yao sasa yanawahukumu,tumshukuru Nchemba na Nape kwa kuwafikisha ccm hapa ilipo waendelee kuiongoza ccm ili tuchukue nchi mikononi mwao........mfungo mwema
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

Kuna tetesi kua wewe umesababisha makusudi CCM ishindwe sababu ulikua unamkomoa Mwigulu Nchemba kwa kua anakuingilia majukumu yako.

Inasemekana mna ugomvi unaohusiana na uwepo wa kambi mbalimbali ndani ya CCM hivyo hata baadhi ya mbinu za ushindi ni wewe umewapa CDM
 
Last edited by a moderator:
Lazima ccm sisimu tuipeleke pale makumbusho iwe sehemu ya kivutio cha utalii hapa arusha,,,ushindi wa chadema ni ushindi wa haki
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

Ila Nape wewe najua ukipikwa na CDM unaweza kuwa mpambanaji wa kutosha na tukakomboa nchi ila shida bro njaa inakufanya ukose misimamo ila endelea kufanya kazi tuliyokutuma CCM ila kuwa makini mwigulu nasikia ameshitukia mpango wetu na amekurekodi unaninii ila usihofu tutamshinda mahakamani si unajua jembe Lisu yupo(CDM)
 
Ndugu watanzania wenzangu kuna siku mwigulu kwa niaba ya hao wenzake niliowataja hapo juu alisema Bungeni kuwa CCM ilikuwa inakaribia kuchukua viti 4 vya udiwani jijini arusha.Na ndio maana CDM wakaamua kulipua mabomu.Je hii ni kweli make leo hakuna mabomu na wamepigwa kipigo cha mbwa mwizi.Ebu athibitishe kauli yake.Huyu sio mchumi na msimwamini hata kidogo huyu ni zuzu.
inawezekana ni mchumi upande wa kitengo cha ulipuaji mabomu...
 
Nape hyo ndo siasa,na ulikua na hakiri sana zaman,baada ya kupewa dereva/v8/maiki na kibar cha kumtukana yeyote kama boss kasema/na pikipk ya kukusafishia njia ndo mwanzo wa shingo yako kuingia ndan....km mnataka mganga wa mkopo npo cz mnadaiwa na wale wazee wa pwan ndo maana ccm hoi
 
Nimeangalia kwenye column siwaoni christina lucas, msasa, hamida, zezeta macopolo, na wengineo. Leo buku Saba chungu!
 
Mwigulu kammwagia tindikali bwana Mussa Tesha, kama haitoshi akaanza kumuanika kwenye mikutano ya CCM huku akisema kuwa CHADEMA ndio waliomwagia! na bado kwenye uchaguzi wamemwagwa vibaya! kweli mwacheni mungu aitwe Mungu!
 
Back
Top Bottom