Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Uchaguzi una kushinda na kushindwa...

Huyu Nape angekuwa muungwana angeipongeza Chadema.

Amekiri kushindwa lakini ameshindwa kwenda mbele zaidi.

ccm wachache sana waungwana, huyu si alisema CDM wamejilipua ili waonewe huruma...na bi kiroboto hata hakuliongelea swala hili bungeni na akaendesha bunge kana kwamba nothing had happened!

Na ajabu zaidi, wabunge wote wa ccm na wake zao kafu (waliokuwepo bungeni) hakuna mmoja hata aliyeomba mwongozo kuhusu janga kubwa lililotokea siku hiyo huko Arusha. Badala yake wakawa wanafanya mzaha as if sio watanzania walofariki.

Viongozi wa ccm ni wana roho mbaya saaana.
 
Hivi tuliposhindwa Arumeru tulikataa kumbe?

Hata Arumeru mlikubali na Nape ulitoa pongezi kwa Chadema, mimi ninaamini kama chama hakuna tatizo, isipokuwa Mwigulu. Huyu anatamani kupasuka. Roho ya nape ni tofauti na ya mwigulu, hata hivyo anayo nafasi ya kujifunza!
 
Tatizo lako unageukageuka ndani ya dk chache kuhusu ukweli wa siasa za vyama vingi tanzania
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

si mngepata hata kata moja best?? Punguzeni kutegemea polisi, A town tumezowea mabomu
 
Tunamshukuru Mwigulu kwani siasa zake zinatusaidia CHADEMA, naomba kama kuna kitengo kingine tupu ndani ya CCM aongezewe ili viwe viwili.
 
Last edited by a moderator:
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).

kiukweli mimi ni cdm lakini ninamkubali nape maana siasa zake hana hafekti kwa raiya yeyote wala hana kashfa yoyote iliyosababishwa na yeye hata mtu kufa,
nitofauti sana na mwigulu ambaye ndani yake ana roho ya uuaji hana tofauti na shetani,
hongera nape,
 
Kuna watu wameulizza sana juu ya matokeo ya uchaguzi Arusha, but jibu la harakaharaka katika kila uchaguzi kuna kushinda na kushindwa, na mshindani wa kweli lazima ajiandae kwa yote maana asiyekubali kushindwa si mshindani.(kama mabo yote yamekwenda sawa).


Teh teh teh huwezi kuutia Mtindi majani ya Chai...
Pale ndo Arusha Mjini sheikh...
 
hahaha na hawa mashosti vip?


images

green guard.
 
ccm wachache sana waungwana, huyu si alisema CDM wamejilipua ili waonewe huruma...na bi kiroboto hata hakuliongelea swala hili bungeni na akaendesha bunge kana kwamba nothing had happened!

Na ajabu zaidi, wabunge wote wa ccm na wake zao kafu /(waliokuwepo bungeni) hakuna mmoja hata aliyeomba mwongozo kuhusu janga kubwa lililotokea siku hiyo huko Arusha. Badala yake wakawa wanafanya mzaha as if sio watanzania walofariki.

-
Viongozi wa ccm ni wana roho mbaya saaana.

Here the swahili saying goes;"Mungu analipa hapahapa Duniani".)
CCM wamepata malipo halali kwa unyama waliowatendea wana wa Arusha na Bomu la Soweto!This is the price CCM have to pay.
 
kiukweli mimi ni cdm lakini ninamkubali nape maana siasa zake hana hafekti kwa raiya yeyote wala hana kashfa yoyote iliyosababishwa na yeye hata mtu kufa,
nitofauti sana na mwigulu ambaye ndani yake ana roho ya uuaji hana tofauti na shetani,
hongera nape,
Furaha ya ushindi imeanza kuwalevya, Nape anashinda anamwita dr Slaa majina mengi tu ya kuudhi na kupandikiza maneno ya ubaguzi wa kikabila na udini kwa haka kapost mnataka tumweke kundi la watu wastaarabu! Acheni utani
 
kiukweli mimi ni cdm lakini ninamkubali nape maana siasa zake hana hafekti kwa raiya yeyote wala hana kashfa yoyote iliyosababishwa na yeye hata mtu kufa,
nitofauti sana na mwigulu ambaye ndani yake ana roho ya uuaji hana tofauti na shetani,
hongera nape,
Furaha ya ushindi imeanza kuwalevya, Nape huyu anaemwita dr Slaa majina mengi tu ya kuudhi na kupandikiza maneno ya ubaguzi wa kikabila na udini eti leo kwa haka kapost ka kukubali ushindi wa cdm mnataka tumweke kwenye kundi la watu wastaarabu! Acheni utani
 
Hisia zako hazinihusu!....

Nikupongeze leo kwa kuja na mada ambayo inaonyesha ukomavu kisiasa. Binafsi nilikwisha acha kusoma mabandiko yako hapa Jukwaani

Ushauri kuna mbegu mbaya imepandwa na akina Mwigulu,Medeye na Mulongo. Ukabila! Hawa jamaa zako wameacha wamechafua hali ya hewa kati ya Waarusha dhidi ya Wachagga na makabila mengine.

Sitashangaa kama mbegu hii mbaya iliyopandwa itakua mwiba mkali kwa wagombea wa kabila la Waarusha kuaminika kwa wapiga kura wa makabila mengine jijini Arusha ktk chaguzi zijazo. Mmeharibu sana.
 
sijawahi kumsikia Nape akibong'a ung'eng'e tangu nizaliwe. Hivi anaijuwa kweli hii lugha ya kibiashara?
 
Nape hongera kwa kukubali, heshima Yang kwako nitairudisha kidogo, usiwe mropokaji kama mwenzio mwigulu!
 
Linganisha kauli ya leo ya Nape na ile ya tarehe 17/06/2013 juu ya hali ya kisiasa Arusha.\


KAULI YA NAPE 17/06/2013

Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22) kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.

Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.
Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka. Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.

Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.

CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.

Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwani kuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.

Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.

CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi. Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.

Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.


CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.

Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013
 
Nape kwa kauli yako ninaweza kukufikiria kukurudishia heshima yako, il a naombaa maelezo mstati wako was mwisho kwenye SMS yako!
 
Thenki yuu vere machi Arusha, Mwigulu Jembe, tunaomba sana CCM Mwigulu awe katibu mkuu maana babu Mangula kupata dogo dogo amesahau hata ile miezi sita aliyotoa kwa wala rushwa..
 
Back
Top Bottom