Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

Tanzanianjema,
lakini zaidi ndugu zetu wa vyama pinzani hawajaweza kuonyesha kuwa ni best alternative ya CCM

Unajua ndugu yangu hapa kuna utata mmoja mkubwa sana.
Inawezekana kuwa kosa na ujinga ni wetu sisi wapiga kura kwa sababu chama huendeshwa na mrengo, sera zake na mwisho kiongozi.
Lakini tunaposimama hapa na kusema kwamba wapinzani hawajaweza kuonyesha kama ni best alternative nadhani itakuwa tunatazama uzuri wa mwanamke kwa umbile lake. tabia, maradhi na hata weusi wake ni kichefuchefu kwetu.
Mrengo na Sera za vyama vya Upinzani zipo wazi kabisa tena nadhani vimejieleza kwa uwazi kuliko CCM kwa sababu hilo neno Ujamaa na Kujitegemea halipo tena ktk kamusi yao na wengi wetu ni jinamizi ambalo tunashindwa kulipa tafsiri nyingineyo zaidi ya Ukomunisti.
Leo ktk pitapita yangu kurudia kutazama tovuti yao nimeona marekebisho ikiwa ni pamoja na lile lengo la chama -Kuhakikisha ushindi ktk chaguzi sikuweza kuliona tena. Na kama lipo bado jaribu kulisoma vizuri kisha jiulize mwenyewe hii lugha kweli ni lugha ya demokrasia ambayo inampa nafasi ya kwanza mwananchi kuchagua mshindi?..
Mawaziri wetu ndio hao wabunge wetu, Kamati kuu, Wawekeshaji wao wakijiita wajasiriamali na kupewa mikopo mikubwa kuliko fedha za JK kwa mkoa mzima wenye wakazi zaidi ya millioni 2. Wake zao ndio wanazidi kuyachukua majumba ya msajiri kwa kauli ya bwana tu. Na hawa ndio wenye mamlaka ya mwisho kuweka mikataba ya nchi wasiulizwe kitu...
Alternative gani kweli tunaihitaji kama sii kujidanganya wenyewe kuzitazama sura na maumbile ya viongozi wa vyama hivi. Ni ktk mtazamo huo pekee tumekuwa tukichagua viongozi na hata vyama vyetu yaani kwanza uwe na address wewe mtoto wa nani imekuwaje upo Upinzani hali mtu kama wewe ulitakiwa CCM. Kuna sura za watu wanaotakiwa kuwa CCM na wengine wote msiokuwa na address ndio mjipange ktk Upinzani.
Tutafika kweli mjomba?
 
Ni ktk mtazamo huo pekee tumekuwa tukichagua viongozi na hata vyama vyetu yaani kwanza uwe na address wewe mtoto wa nani imekuwaje upo Upinzani hali mtu kama wewe ulitakiwa CCM. Kuna sura za watu wanaotakiwa kuwa CCM na wengine wote msiokuwa na address ndio mjipange ktk Upinzani.
Tutafika kweli mjomba?

Hiki ndicho kilimfika makongoro Nyerere..wakamgeresha na ubunge wa kuteuliwa ili atoke upinzani, baada ya kumtoa upinzani wamem-bwaga kiaina, wana hakika hatarudi tena upinzani
Huu mtindo wa CCM kuua upinzani nao ni ishara ya kutojiamini katika ushindani wa haki..wanategemea sana wizi wa kura na wanajua bila huo nafasi yao ya kuchuana on merit itakuwa mashakani ndo maana wanahangaika kuwatoa wapinzani upepo ili magurudumu yao yasitembee
 
Mzee ES unasema mambo yako sawa CCM lakini habari kama hizi zinatupa picha tofauti. Anyway, labda utupe picha ya ndani!!

CCM mambo magumu

2007-08-01 08:46:49
Na Mary Edward, PST Dodoma


Kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM ambacho jana kilitarajiwa kutangaza majina ya wanachama wake watakaowania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho, kiliendelea hadi usiku huku kukiwa hakuna taarifa zozote za maana kuhusu walioteuliwa.

Hata hivyo, habari zilisema kuwa baadhi ya mawaziri waliokuwa wakigombea uwakilishi katika NEC majina yao yamekatwa, wakiwemo wenyeviti wa CCM wa mikoa.

`Ninaomba tu msubiri kesho taarifa rasmi, lakini ninachoweza kukudokezea ni kwamba kuna majina ya mawaziri yamekatwa pamoja na baadhi ya wenyeviti (wa CCM) wa mkoa, akiwemo wa Mtwara Lakini subirini tu kesho,` kilisema chanzo chetu.

Kikao hicho ambacho kilitanguliwa na kingine cha Kamati Kuu ya CCM tangu Julai 28, awali kilitarajiwa kumalizika Julai 30, mwaka huu, lakini kilisogezwa mbele hadi jana kutokana na baadhi ya ajenda, ikiwemo ya kuwateua wagombea wa nafasi hiyo, kutokamilika.

Wakati tunakwenda mitamboni jana usiku, wajumbe wa kikao hicho cha Halmashauri Kuu kilichokuwa chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, walikuwa wakitoka kuelekea katika viwanja vya Bunge ambako walikuwa na hafla.

Hata walipokuwa nje ya ukumbi huo, maarufu kama White House wa mjini hapa, wajumbe wengi walikataa ama kuwakimbia waandishi ili tu wasitaje majina ya watakaowania nafasi ya NEC ambayo ni ya juu kabisa kwa chama hicho.

Na katika hatua nyingine, hatimaye Kamati Kuu ya?CCM, imethibitisha kuwasimamisha uongozi viongozi wanne wa Jumuiya ya Wazazi akiwemo Mwenyekiti wa jumuiya hiyo Taifa, Bw. Abihud Maregesi kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za shule za sekondari za Wazazi na kutumia madaraka yao vibaya.

Uamuzi huo ulichukuliwa kufutia kikao cha Kamati cha siku tatu kilichofanyika mjini hapa chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete.

Taarifa iliyotolewa mjini hapa jana na kusainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Bw. Aggrey Mwanri, ilisema hatua ya kuwasimamisha viongozi hao imelenga kutoa nafasi kwa vyombo vinavyohusika kufanya uchunguzi juu ya tuhuma zinazowakabili.

Mbali ya Bw. Maregesi, wengine waliotajwa kusimamishwa katika taarifa hiyo ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Bw. Ramadhani Suleimani, Kaimu Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo, ?Bw. Cosmas Hinju na Bw. Babilas Mpemba ambaye ni ofisa makao makuu ya jumuiya hiyo.

Aidha, taarifa hiyo ilifafanua kuwa, viongozi hao wamesimamishwa uongozi kwa mujibu wa Katiba ya CCM, toleo la Mei 2005, kifungu cha 110 (7) na kwamba Bw. Mpemba amesimamishwa kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa chama na jumuiya zake.

Taarifa iliongeza kuwa, lengo la kuwasimamisha viongozi hao ni kutoa nafasi kwa vyombo? vinavyohusika kufanya uchunguzi ili kubaini ukweli wa tuhuma kabla ya uamuzi kamili juu yao kutolewa.

Na katika hatua nyingine, Kamati Kuu imeridhia uamuzi wa kuwafukuza uanachama madiwani?watano wa CCM wa Wilaya ya Tunduru kwa tuhuma za kukiuka maadili ya CCM.

Taarifa ilisema uamuzi?huo wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Ruvuma wa hivi karibuni wa kutoa adhabu ya kuwafukuza uanachama madiwani hao, ulikuwa sahihi.

Halmashauri Kuu ya CCM? Mkoa wa Ruvuma, iliwafukuza uanachama madiwani hao baada ya kuthibitika kuwa walikiuka maadili ya uongozi na ya uanachama ambapo taarifa hiyo ilisema kuwa walifukuzwa kwa mujibu wa kanuni na maadili toleo la Mei,? 2002 kifungu 8.2.9.

Aidha, taarifa hiyo iliwataja waliofukuzwa na kupoteza wadhifa wa uanachama na Udiwani kuwa ni? pamoja na aliyekuwa? Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru, Bw. Burhan Makonje, madiwani Zuhura Mafutari, Suleiman Shaibu, Aindi Bakari na Halima Luambano.

Mbali na hilo, katika siku ya kwanza, Kamati Kuu ya CCM? ilifanya uteuzi wa wana-CCM watatu wa kugombea nafasi ya Meya wa Manispaa ya Arusha.

Walioteuliwa kuwania nafasi hiyo kwa mujibu wa taarifa hiyo ni Bw. Anaelson Ole Joel, Laurence Heddi na Julius Sekayan.

?Madiwani hao watatu walioteuliwa kugombea watapigiwa kura na Kamati ya Madiwani? wote wa CCM? wa Manispaa ya Arusha na atakayeshinda jina lake litawasilishwa kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha kama mgombea wa?nafasi ya Meya wa Manispaa ya Arusha? kwa tiketi ya CCM, taarifa ilifafanua.

Nafasi ya Meya wa Arusha, imekuwa wazi baada ya aliyekuwa Meya wa Jiji hilo, Bw. Paul Laizer kujiuzulu.

Wakati huo huo, Kamati Kuu ya CCM, imewateua wanachama wake watatu kuwa Makatibu wa CCM wa Wilaya kujaza nafasi zilizokuwa? wazi kutokana na sababu mbalimbali.

Taarifa ya Kamati hiyo iliwataja walioteuliwa kuwa ni Bw. Zabron Msemwa, Bw.Othman Dunga na Bi. Mary Maziku ambapo kabla ya uteuzi huo, Bw. Msemwa alikuwa Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Kibondo.

Bw. Nduga alikuwa Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba Mjini na Bi. Maziku alikuwa Katibu Msaidizi na Mhasibu wa Wilaya ya Ilala.

Hali kadhalika, Kamati hiyo imemvua haki ya kuchaguliwa katika uongozi wa CCM, Bw. Thomas Nyimbo baada ya kuthibitika kuwa tabia na mwenendo wake vinamfanya asistahili kuwa na haki hiyo.

Taarifa ilisema Kamati Kuu?imechukua hatua ya kumpa adhabu? hiyo kwa mujibu wa?kanuni za uongozi? na maadili toleo la 2002, kifungu 8.2.4 na kwamba hatua hiyo? imezingatia ukweli kuwa, Bw. Nyimbo aliwahi kupewa?adhabu ya karipio kwa kuacha tabia na mwenendo huo alionao lakini amerudia tena hivyo atatumikia adhabu hiyo kwa miezi 24.

SOURCE: Nipashe
 
hata na mie nimetatizika huyu komandoo ES ndio yule yule Mzee Es au kulikoni?

kumbe unaweza kubadili jina? kama hivyo na mimi nnaomba nibadili niwe Mtu wa pwani
 
"lakini zaidi ndugu zetu wa vyama pinzani hawajaweza kuonyesha kuwa ni best alternative ya CCM.....Hii ndio challenge kubwa anayokumbana mpiga kura wa Tanzania."


End of the story na Full Stop!
 
Mtumwitu na Zero,

You got it right, jina limebadilika kutokana na times na mazingara, lakini mawe ni yale yale ya kumkoma nyani na mpaka ijulikane wasup!
 
sasa uzee basi umekuwa kijana na komandooo? duh sasa hii hatari, na mie hebu nibofyulie hii siri ya kubadili jina
 
sasa uzee basi umekuwa kijana na komandooo? duh sasa hii hatari, na mie hebu nibofyulie hii siri ya kubadili jina
Wapo wengine waliobadili; nenda kwenye profile yako, kwa mfano aliwahi kuwepo Mwanasiasa siku hizi anajiita Kitila.
 
mwendapole you are right ...nadhani mako bado angeweza kuwa mbunge mzuri tu kuliko wabunge wengi...wakati wa kampeni nakumbuka jk alienda kuomba baraka za mama maria na kupata wasaa binafsi kuomba kwenye kaburi la mwalimu hadi kufikia kugaragara kwa hisia ....
mama maria na hata mwalimu kabla hajafariki yupo busy na kusomesha wajukuu zake ..i was taken by emmotions walipokua wanamshukuru museveni mbele ya jk kwa kuwalipia wajukuu za mwalimiu ada kwenye nchi mbalimbali ..sijui na mandela labda...siku moja mmoja wao anaweza kurudi kawa atakuwa na uwezo atakuwa na kumbu kumbu ya kusomeshwa na museveni kama babu yao alivyomsomesha museveni....unajua mwalimu angetaka asingeshindwa kufanya tukawa na amani karume ,eyadema jr,joseph kabilla ets..so lazima tumuenzi ..especially jk lazima amuenzi kwa vitendo ..ikiwemo kuliendeleza jina la mwalimu kwenye siasa za tanzania ...kama alivyiofanya mkapa kwa angalao kumkumbuka mmoja wa vijana wake..ie mako..
 
"lakini zaidi ndugu zetu wa vyama pinzani hawajaweza kuonyesha kuwa ni best alternative ya CCM.....Hii ndio challenge kubwa anayokumbana mpiga kura wa Tanzania."


End of the story na Full Stop!

Hivi unataka waonyeshe nini?? Unafikiri upinzani wa TZ na nchi nyingine kama Zambia (Chiluba) na Malawi walipoingia madalakani unatofauti gani? CCM wenyewe hatuoni wanachokifanya zaidi ya kuuza nchi. Infact wanaturudisha nyuma. Sasa hivi tunataka mzalendo wa kweli ili atukomboe siyo Baby Face!!! Tatizo bongo tunachagua rais bila kuangalia uwezo na commitment utafikiri tunampeleka kwenye mashindano ya Mr. President.
 
"Tatizo bongo tunachagua rais bila kuangalia uwezo na commitment utafikiri tunampeleka kwenye mashindano ya Mr. President."


Mzee acha contradictions, kuhusu nani wa kulaumiwa kati ya sisi wananchi na ccm au upinzani, hebu rudia tena nani wa kulaumiwa? Maana at one point unalaumu ccm na hapa unalaumu wananchi, what is up?
 
Komandoo,

Of course CCM ndiyo walaumiwa number one kwa kuwaacha 80 % ya wananchi vijijini bila elimu ya maana ili waendeleze utawala wao (Nafikiri unanielewa). Wananchi nasi kwa kushindwa kutumia busara zetu. Kama tunataka mabadiliko inabidi yaanzie mijini especially Dar lakini TZ mabadilioko yanaanzia Tarime.

Kuhusu Baby face, just a joke kwa kuwa huku ughaibuni watu most of the guys wanamsifu kwa uzuri alafu wanadai rais kijana kumbe hawajui hata BWM 1995 alikuwa na umri huohuo wa JK ila kwa sababu ya sura ya kunyata watu walifikiri ni mzee!!!
 
Jamani mlio nyumbani hamna hata mmoja aliyepata nyeti za nani kapita nani kabwagwa?Mzee ES,tunasubiria breaking news kutoka kwako uliye jikoni.

PS.Najua heading yangu inaweza kumzuga mtu kudhani posting yangu ina majina.Sorry if it misled anybody,which is likely.
 
Malegesi, hakuwa mtandao lakini alisaidiwa sana na mtandao kuipata hiyo nafasi, maana the big enemy alikuwa Idd Simba, ambaye ilitakiwa atolewe by any means necessary, kwa sababu alikuwa ni mwiba kwa kambi zote zilizogombea urais uliopita, pamoja na close ties zake na Mkapa!

Kataraiya, between Bukoba na Mwanza, sasa kuna new kids on the block, (Mtandao) Diallo, Karimagi, Kamalla, Masha,(mkubwa na mtoto) ambao sasa wanashika hatamu huko kwa kuwaondoa Shija, Mugema, na Rwakatare, wao sasa ndio the new north block power, with political power ku-make na un-make anyone politically, victim wa kwanza alikuwa Shija, baadaye Mgema, na sasa Kataraiya, next atakuwa Luangisa kwenye umeya, then itakuwa mbunge Suedi! na the likes!


Sasa imefika saa ya mtandao kushika hatamu ndani ya CCM, umoja wa wazazi, kina mama, na vijana, ni vitengo muhimu sana ambavyo lazima viwe mikononi mwa mtandao, na sasa ni oficial kwamba the mighty and undisputed Nchimbi, is leading the charge, next on line ni Magufuli, Mramba, na Mwandosya!

Mgema alifariki dunia!
 
Mlalahoi,

Nilidhani una news, kumbe nawe unasubiri kama wengine tu!
 
Swala la nani wa kumlaumu kwa predicament tuliyonayo leo Tanzania, ni swali tete. wote tunahusika katika kuijenga na kuiendeleza hii hali. Wananchi na CCM kwa pamoja tunahusika. Wananchi, wafanyakazi na wakulima tumejifanya kama hatuoni madudu ya CCM...kila uchaguzi ukija tunawapa kura, na baada ya hapo ndo tunaanza kulaumu hali ngumu na matatizo mengineyo. Uchaguzi ukifika, matatizo yote TUNAJIFANYA KUYASAHAU na kuamua kujipa imani kwamba this time it will work, as a result inakuwa vicious circle ya umaskini na ulalamishi. Bila kufanya kinachotakiwa.

Vile vile CCM, wakija kuomba kura wanakuja na sera na maneno mazuri. Wananchi wanawaamini wanawapa miaka mingine mitano. wakishaingia madarakani, wanaangalia maslahi yao na ni namna gani watashinda uchaguzi ujao. Mwisho wake ni nini? vicious circle ya umaskini kwa walio wengi na utajiri wa kutupwa kwa walio wachache.

Kipi kifanyike. Ni wahusika wote CCM na wananchi tuamke tugundue kwamba hizi siasa za kudanganyana, hazitatufikisha popote. Kwani lazima tulijue hili..wana ccm, wanachadema, wanacuf na wengineo, tunaweza kutofautiana kisera na kimtizamo, lakini wote ni watanzania na aneyeumia ni mtanzania, haidhuru yuko chama gani, Usidhani kila mwana CCM ana neema, la hasha..wengi ni njaa tupu!. Swala kwamba wananchi hawajasoma kwa hiyo hawawezi kulielewa hili..ni utter nonsense! Nchi yetu ni jukumu letu sote. Hili halitafanywa na Mbowe wala Zitto ni mimi na wewe kupiga kura kwa kuamini kwamba tunahitaji kuleta mabadiliko. Hata Zambia na Kenya tunaowatolea mifano, ni WANANCHI period. Ndo waligundua kwamba wanachezewa sanaa. Na siamini kwamba Wazambia wana akili kuliko watz!

Ukiamini kwamba wapinzani hawajaiva kisiasa, je tuliowapa dhamana ya nchi na wako madarakani kwa miongo zaidi ya minne, wamefanya nini kuonyesha kwamba wamekomaa kisiasa? zaidi ya kutuweka katika lindi la umaskini? Mwenye Jukumu la kuibadirisha Tanzania ni mwananchi wa kawaida! Tusitegemee CCM au upinzani kubadilisha mambo. Katiba ni mbovu hilo halina ubishi..je kipi kifanyike? CCM hawatakubali kuibadilisha kwa sababu inawapa nafasi wao, kwa hiyo njia mbadala ni kuingia na kupiga KURA kwa viongozi/chama chenye mwelekeo wa kuongoza juhudi za wananchi kujikomboa. Na wananchi wanalijua hili. Na kikubwa ni elimu..vijana wengi wapiga kura sasa wana hata elimu ya std seven na form four, na hawa ndo hawana kazi, wameahidiwa ajira hewa millioni moja kila mwaka, wakigundua kwamba huu ujinga unaofanywa na watu wachache ndo unaturudisha nyuma, basi twaweza fika mbele. we ukiona watu wako ughaibuni, wanaanzisha matawi ya CCM, unadhani wanaipenda CCM? nagoma kuamini hivyo, ni OPPORTUNISTS wanaamini kwamba inabidi waingie kwenye system ya chama ndo wafanikiwe nyumbani, kitu ambacho wanafanya wasomi walio majuu, iweje alaumiwe babu yangu wa Sengerema kwa kukubali kuipigia kura CCM kwa doti ya khanga au shati? moja kwa moja hapa elimu ya wananchi wetu sio kikwazo kwani wabinafsi namba moja ni wasomi, mimi na wewe tunaokaa kwenye PC zetu na kuandika humu JF na kwingineko! Swala sio Elimu, swala ni kuacha unafiki na kuelewa priorities na changamoto zinazolikabili taifa. Lets try, its possible.

Kwa sasa usitegemee EL na JK kufanya mabadiliko yoyote. wanafikiria namna ya kushinda 2010. Tuamke, twende kupiga kura, taratibu mambo yatabadilika! wachache walio upinzani akina Zitto, ni kizazi ambacho kimeweka historia na Iam sure wengi humu tunalilia changes, lakini hata kuweka jina humu JF tunaogopa! kwa sababu system itatufuatilia...mbona Zitto ameweza? WHATS UNIQUE bout him? he knows the challenges facing our country and he is ready to sacrifice the smallest he has fo the good of his country. Mi na wewe je? wote hatuwezi kuingia siasa, lakini hakika tunaweza kuchangia pale tunapoweza.
 
"Mark Mgema alifariki dunia, lakini naye alikuwa Mtandao"

Mwenyekiti wa zamani wa CCM Mwanza, hakuwa mtandao bro angekuwa Cheyo (UDP) asingeshindwa uchaguzi mdogo wa bunge maana mtandao wote walikuwa wakimsaidia Cheyo, mpaka vigogo wazito!

Kama angelikuwa hai, alikuwa ndiye target namba moja, kuondolewa na mtandao! Ukienda kwenye thred za huko nyuma tulishayazungumza haya zamani sana bro!
 
Back
Top Bottom