Tanzanianjema,
Unajua ndugu yangu hapa kuna utata mmoja mkubwa sana.
Inawezekana kuwa kosa na ujinga ni wetu sisi wapiga kura kwa sababu chama huendeshwa na mrengo, sera zake na mwisho kiongozi.
Lakini tunaposimama hapa na kusema kwamba wapinzani hawajaweza kuonyesha kama ni best alternative nadhani itakuwa tunatazama uzuri wa mwanamke kwa umbile lake. tabia, maradhi na hata weusi wake ni kichefuchefu kwetu.
Mrengo na Sera za vyama vya Upinzani zipo wazi kabisa tena nadhani vimejieleza kwa uwazi kuliko CCM kwa sababu hilo neno Ujamaa na Kujitegemea halipo tena ktk kamusi yao na wengi wetu ni jinamizi ambalo tunashindwa kulipa tafsiri nyingineyo zaidi ya Ukomunisti.
Leo ktk pitapita yangu kurudia kutazama tovuti yao nimeona marekebisho ikiwa ni pamoja na lile lengo la chama -Kuhakikisha ushindi ktk chaguzi sikuweza kuliona tena. Na kama lipo bado jaribu kulisoma vizuri kisha jiulize mwenyewe hii lugha kweli ni lugha ya demokrasia ambayo inampa nafasi ya kwanza mwananchi kuchagua mshindi?..
Mawaziri wetu ndio hao wabunge wetu, Kamati kuu, Wawekeshaji wao wakijiita wajasiriamali na kupewa mikopo mikubwa kuliko fedha za JK kwa mkoa mzima wenye wakazi zaidi ya millioni 2. Wake zao ndio wanazidi kuyachukua majumba ya msajiri kwa kauli ya bwana tu. Na hawa ndio wenye mamlaka ya mwisho kuweka mikataba ya nchi wasiulizwe kitu...
Alternative gani kweli tunaihitaji kama sii kujidanganya wenyewe kuzitazama sura na maumbile ya viongozi wa vyama hivi. Ni ktk mtazamo huo pekee tumekuwa tukichagua viongozi na hata vyama vyetu yaani kwanza uwe na address wewe mtoto wa nani imekuwaje upo Upinzani hali mtu kama wewe ulitakiwa CCM. Kuna sura za watu wanaotakiwa kuwa CCM na wengine wote msiokuwa na address ndio mjipange ktk Upinzani.
Tutafika kweli mjomba?
lakini zaidi ndugu zetu wa vyama pinzani hawajaweza kuonyesha kuwa ni best alternative ya CCM
Unajua ndugu yangu hapa kuna utata mmoja mkubwa sana.
Inawezekana kuwa kosa na ujinga ni wetu sisi wapiga kura kwa sababu chama huendeshwa na mrengo, sera zake na mwisho kiongozi.
Lakini tunaposimama hapa na kusema kwamba wapinzani hawajaweza kuonyesha kama ni best alternative nadhani itakuwa tunatazama uzuri wa mwanamke kwa umbile lake. tabia, maradhi na hata weusi wake ni kichefuchefu kwetu.
Mrengo na Sera za vyama vya Upinzani zipo wazi kabisa tena nadhani vimejieleza kwa uwazi kuliko CCM kwa sababu hilo neno Ujamaa na Kujitegemea halipo tena ktk kamusi yao na wengi wetu ni jinamizi ambalo tunashindwa kulipa tafsiri nyingineyo zaidi ya Ukomunisti.
Leo ktk pitapita yangu kurudia kutazama tovuti yao nimeona marekebisho ikiwa ni pamoja na lile lengo la chama -Kuhakikisha ushindi ktk chaguzi sikuweza kuliona tena. Na kama lipo bado jaribu kulisoma vizuri kisha jiulize mwenyewe hii lugha kweli ni lugha ya demokrasia ambayo inampa nafasi ya kwanza mwananchi kuchagua mshindi?..
Mawaziri wetu ndio hao wabunge wetu, Kamati kuu, Wawekeshaji wao wakijiita wajasiriamali na kupewa mikopo mikubwa kuliko fedha za JK kwa mkoa mzima wenye wakazi zaidi ya millioni 2. Wake zao ndio wanazidi kuyachukua majumba ya msajiri kwa kauli ya bwana tu. Na hawa ndio wenye mamlaka ya mwisho kuweka mikataba ya nchi wasiulizwe kitu...
Alternative gani kweli tunaihitaji kama sii kujidanganya wenyewe kuzitazama sura na maumbile ya viongozi wa vyama hivi. Ni ktk mtazamo huo pekee tumekuwa tukichagua viongozi na hata vyama vyetu yaani kwanza uwe na address wewe mtoto wa nani imekuwaje upo Upinzani hali mtu kama wewe ulitakiwa CCM. Kuna sura za watu wanaotakiwa kuwa CCM na wengine wote msiokuwa na address ndio mjipange ktk Upinzani.
Tutafika kweli mjomba?