simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,409
- 9,183
Upigaji kura unaendelea huko Igunga. Watu wengi wamejitokeza na kura zinaendelea katika hali ya amani na utulivu.
Waliojitokeza kwa wingi ni wazee na kina mama.
-------------------
05:24 PM - Mbowe on Channel 10: Tumeripoti vitendo vingi vya rushwa na ukiukwaji wa taratibu lakini vyombo vya dola havichukui hatua
05: 10 PM
Mwigulu Nchemba on Channel 10: Ktk kata ya Nhongo (Igunga) kuna mwanamke kapewa karatasi ya kura huku ikiwa imetikiwa sehemu ya mgombea wa CHADEMA
05:04 PM
05:00PM - KURA SASA ZINAHESABIWA KATIKA VITUO
Waliojitokeza kwa wingi ni wazee na kina mama.
-------------------
CLOSED: KUPATA MATOKEO FUATILIA THREAD HII - MATOKEO YA UCHAGUZI MDOGO IGUNGA
05:24 PM - Mbowe on Channel 10: Tumeripoti vitendo vingi vya rushwa na ukiukwaji wa taratibu lakini vyombo vya dola havichukui hatua
05: 10 PM
Mwigulu Nchemba on Channel 10: Ktk kata ya Nhongo (Igunga) kuna mwanamke kapewa karatasi ya kura huku ikiwa imetikiwa sehemu ya mgombea wa CHADEMA
Meneja wa kampeni wa CCM (Mwigulu) anasema ameshitushwa na habari kwamba kuna mama kapewa karatasi imeshawekewa tiki kwenye mgombea wa CHADEMA. Na habari hiyo wamepeleka katika tume ya uchaguzi na msimamizi wa uchaguzi kahojiwa.
Kuhusu hela zilizokuwa zinagawiwa na mbunge wao si rushwa bali ni hela walizokuwa wanagawa kwa mawakala wake.
05:04 PM
Dr. Slaa anaongea Channel 10:
Anasema watu Igunga wamejitokeza wachache, form namba 17 hazipo na zilizopo hazitumiwi ipaswavyo.
Kasema kuna vurugu zimetokea Tarime na mabomu yamepigwa na DC kaingilia uchaguzi, vurugu nyingine zimetokea Shinyanga kata ya Ndara na huko Njombe.
Kuhusu kukamatwa kwa gari la mbunge likiwa na mil 20 - ni kweli na mbunge wa CCM kaenda kutoa taarifa polisi eti kaibiwa gari na mil 20.
Hivyo wale vijana waliowakamata wafuasi wa CCM na mbunge wao wakigawana hela wamewekwa selo!
05:00PM - KURA SASA ZINAHESABIWA KATIKA VITUO
14.16pm - ITV/Radio One wameripoti kuwa kuna watu wamekamatwa kwenye kituo wakiwa na shahada halisi za watu wengine pamoja na photocopies.
Pia kuna vituo feki (hewa) vimeripotiwa.
Inasuburiwa neno la polisi katika mkutano na waandishi baada ya muda.
Tumemkamata mgambo akiwa kwenye foleni ya kupiga kura huku akitoa rushwa ya shs 5,000/= kata ya Swingizi, baada ya kumweka chini ya ulinzi, tukamkuta na shs laki saba, kwa sasa anashikiliwa na polisi, anasema alitumwa na viongozi wa CCM.
Nchemba anapita kila kituo anamwita msimamizi na kumpa hela, kwa sasa amedhibitiwa na vijana wetu
Habari za hivi punde kutoka Igunga zinasema vijana walinzi wawili wa CDM wanashikiliwa na polisi mjini Igunga kwa kile polisi wanachodai kuwa walitaka kuliteka gari la wafuasi wa CCM ambalo nalo polisi wanalishikilia.
Walinzi hao walifika eneo la Simbo na kukuta kundi dogo la wafuasi wa CCM wakigawa fedha karibu na zahanati ya Simbo.
Baada ya vijana hao kuwashtukia pale ghafla wale watu wa CCM waliamua kutimua mbio na kuliacha gari lao na vijana wa CDM wakaamua kulichukua na kuliendesha hadi kituo cha polisi.
Baada ya upekuzi polisi walikuta mfuko wa plastiki (Rambo) ndani yake mkiwa Sh 20 milioni ambazo ndizo zilikuwa zinagawaiwa kwa watu au wafuasi wa CCM.
Hivyo vijana hao wamegeuziwa kibao na polisi kama kawaida yao na hivyo wameambiwa wameliteka nyara hilo gari.
Kashindye (ambaye ni mgombea wa CHADEMA) kahojiwa sasa hivi ITV baada ya yeye kupiga kura na kusema kwa hapo alipo hali ni shwari ila atapata uhakika zaidi ya mwenendo wa uchaguzi baada ya kutembelea vituo zaidi ya kumi.
Amesema yupo postive na matokeo yoyote yatakayotoka lakini ana uhakika wa yeye kufanya vizuri na kuibuka kidedea.
Abdala Tilata wa StarTV anaongea
Ametembelea vituo 10 hali ni nzuri, usumbufu kidogo.
Askari aliyepotelewa na shahada ya kura aruhusiwa kupiga kura.
Mzee mmoja kaibiwa kadi na mkewe, kafanya kama afande alivofanya hapo juu na karuhusiwa kupiga kura. Mzee kaapa atampa likizo ya unyumba mkewe kwa siku kadhaa kuanzia leo.
Tundu Lissu amekubali hali ni shwari.
Tilata anasifia polisi.
Esta Bulaya live MTV.
Anasifia polisi.
Anasema kinamama, wazee wamejitokeza kwa wingi.
anaulizwa kuhusu mwamko wa vijana.
Anajibu, ati kwamba amekuwa sapraizdi kwamba vijana hawajajitokeza kwa wingi.
Live Mlimani TV: Heche.
mwanahabari: hali ikoje?
heche: ni nzuri, kuna hujuma, shahada zimenunuliwa na mabalozi, vijana wanakamatwa sana, lakini hali ni shwari.
mwanahabari: mahudhurio ya vijana na wazee:
heche: watu mchanganyiko wamejitokeza, vijana ni wengi, watu wazima pia, vijana wanakamatwa, mawakala wanazuiwa kuingia kwenye vituo ati si wakazi wa igunga, wakati sheria haisemi kama wakala lazima awe mkazi.
heche: hao wazee wanaosemwa na esther bulaya na wao wamechoka na maisha magumu, na hawapigii kura ccm.
TBC imeripoti zoezi la kupiga kura Igunga na kumwonyesha mwanamke anayejipambanua kuwa ni wa CHADEMA ambaye amesema balozi mmoja wa nyumba kumi kareport kuwa yeye kafariki dunia ili asipige kura kwa kuwa alikataa kuiunga mkono CCM.
Mlezi wa vyama vya siasa Mh. Tendwa, hajakerwa na wanasiasa (Mbunge Aden Rage) "kupanda na silaha jukwaani" wakati wa kampeini (maana hakutaja kama hilo lilimkera) bali amekerwa na tukio la Mkuu wa wilaya kufanyiwa fujo, kijana kumwagiwa tindikali, na tukio la kurushiana risasi.
Ameyasema haya wakati akihojiwa na Mtangazaji wa TBC1 kuhusu ni mambo gani yalimkera katika uchaguzi mdogo wa Igunga
source: TBC1 saa saba mchana leo.